ethiopia kuna vita upande ule wa tigrey, pia, nje ya nchi kuna waethiopia wengi sana wamefanikiwa, hao jamaa wapo vizuri sana kwenye maduka na mikahawa, hivyo wakifanikiwa kutoroka kufika huko south, na baadaye ulaya na america, huwa wanafikia kwa jamaa zao waliotangulia, na wanasaidiana kutafuta maisha. hao wanaokamatwa tanzania usijefikiri ni maskini sana, kutoka ethiopia hadi south unawezashangaa ametumia milion 5, hiyo sio hela ndogo kwa mwafrika, hivyo usione wanapita na marori hapa ukafikiri ni maskini saana, hapana, ni kama hawa wabongo wanaojiita midle class tu.
utamaduni wa kukimbila nchi nyingine kutafuta maisha haimaanishi nchini kwako kuna shida saana, angalia Nigeria, angalia south america wanavyokimbilia marekani hadi trump anajenga ukuta, wanatafuta maisha. watanzania ni mbumbumbu wanaamini maisha yapo hapa tu, huu ugumu wa kupata pesa ulipo bongo usifikiri nchi zingine zenye viongozi wenye akili kuna ugumu kama huu. kuna nchi zilishatengeneza miundombinu na fursa ukifika tu mwaka mrefu umeshasimama na unapata pesa ndefu kuliko ungepata hapa na unaanza kutuma nyumbani kujenga na kusaidia ndugu zako. na south africa ni njia tu kwa sababu pale wakikukamata unapata asylum, wana uzungu fulani wa kuheshimu haki za binadamu sio kama hapa bongo wanafungwa wakati wanapita tu hata hawana haja kukimbilia hapa bongo. onyesha muethiopia mmoja tu aliyezamia bongo, hakuna, wanapita tu hapa.
kwa waliowahi kusafiri, ukikutana na wasomali popote pale, utaamini kuondoka somalia kwenda huko kumewasaidia, wana maduka makubwa, mahoteli, mikahawa, na biashara kubwa, kwa sababu nchi hizo zingine watu hawafanyi kazi kwa bidii kama sisi, hapa unasota kwa jasho na hupati pesa, jasho hili unatumia hapa bongo ukienda kulitumia nchi zenye fursa unatajirika mapema.