Tusipoangalia kanda ya ziwa itatuletea tyranny of the majority

Typical CHADEMA rhetoric borrowed from German
 
Fikra
Fikra za ukanda kwa Tanzania zinajengwa na wanasiasa wajinga wajinga tu wasioona mbali kwa mustakabali mwema wa taifa.
Siasa za kujilimbikizia mali kwa njia haramu za kijima kwa kutumia mtaji wa ujinga wa wananchi walio wengi zitakoma muda si mrefu.
Watanzania walio wengi, wenye elimu, ujuzi na uchumi mzuri hawaishi kwenye kanda zao za asili. Hawa ndiyo watakaojenga Tanzania ya kesho, na ndiyo kundi lenye uwezo wa kuihami jamii na taifa katika ulimwengu huu wa utandawazi.
Changamoto itakayotupata watanzania kwa siasa za kikanda ni kwa kanda husika kutawaliwa na wahamiaji haramu huku wenyeji wakipambana na watanzania wengine kwenye siasa za kijima.
Tunahitaji kuifikiria Tanzania kama nchi, kiuchumi, kisiasa na kiutamaduni.
 
Yeah, ni kanda kubwa na ina watu wengi ambao ni turufu kwenye medani za siasa, biashara na uchumi. Lakini viongozi wake hawaleti maendeleo na wana ubinafsi. Kifupi viongozi hawana ushawishi serikalini kwenye kuleta maendeleo, ni Magu tu ndiyo akithubutu naye kwa sababu alikuwa kiongozi wa juu. Kanda ya ziwa unayoiona imejengwa na juhudi za sekta binafsi na siyo serikali. Kwa sasa kanda haina waziri hata mmoja, mawizri wote wamepurulwa. Siku ikitokea uchaguzi umefuata haki, wataamua rais awe nani!! Ipo siku nchi haitaamini kilichotokea. Watu wa kule hawana mapenzi na rais kutoka ccm kabisa.
 
Aliyeanza kutugawa ni Mwalimu Nyerere, miaka ya i930 tulikuwa na mkakati wa kujenga chuo kikuu WEST LAKE tulipopata uhuru mwalimu akatutaka tusubili kwanza kwa madai tulikuwa tumepiga hatua kubwa tulikuwa tunasomesha watoto kwa hela zetu za ushirika na mabo mengi tu tulikuwa mbele tuliendelea kusubili maendeleo hadi leo tuliminywa ili tuwasubili wenzetu waliokuwa na hali mbaya zaidi le hata makao makuu ya mkoa hayana stendi hayana hospitali tukiacha zile za kanisa, mbali na Barongo wakati wa mwalimu sikumbuki waziri aliyeteuliwa kutoka kagera tukiacha manaibu, wasomi wengi wa kanda ya ziwa walilazimika kwenda uhamishoni niite intellectual exile kwa sababu hawakutakiwa hawakupewa nafasi kwa hofu ya Mwalimu. sasa hivi ziara zote hizo za Paulo kuanzia huko ni kujaribu kufanya toba ya ukandamizaji wa maendeleo uliofanywa, bado kuna ukumgu mioyoni mwao na kuna hofu wanaweza kutoa adhabu kwa serikali, Makonda anaanza kanda ya ziwa kimkakati, Biteko ameteuliwa kimkakati. yetu macho tujiandae kuona mengi.
 
Hakuna shida, kwani, hawalipi Kodi? Mgao wa pesa ya maendeleo inabidi Uwe, mtu mmoja shilingi moja! Lakini katika kujenga viwanda na miundombinu, vigezo vya kisayansi ndio vitumike, sio idadi ya watu, na vigezo vingine vya kipuuzi.
Lakini kama unajenga hospitari,au vituo vya polisi, sehemu yenye wingi wa watu, inabidi ipate zaidi! Ni, simple math
 
Unaweza kulinganisha Maendeleo ya VUNJO na kisesa kwa Mpina?
Au Unaweza Kulinganisha GEITA VIJIJINI na Hai kwa Maendeleo?
Hai Kuna nini pale ? Mashina ya migomba kama mguu wa mbuzi. Vijiji vimechoka hakuna mzunguko wa fedha. Nenda Geita vijijini ukutane na trading Centers zilizochangamka kama Katoro, Nkome, Nzera, Lwamgasa, Nyarugusu na Bukoli. Usilinganishe Hai na Geita, huko Hai ni makaburini Tu. Koma kabisa.
 
Wanaozaliana Sana ni Kigoma, rukwa, ruvuma,Mtwara , mikoa ya Nagari ya Hindi , znz
 
- nimezungumzia GEITA VIJIJINI, kaangalie Maendeleo ya vijiji vya GEITA VIJIJINI na Vijiji vya Wilaya ya Hai
-Hai, ndio Wilaya yenye mabilionea wengi wa kichagga
 
- nimezungumzia GEITA VIJIJINI, kaangalie Maendeleo ya vijiji vya GEITA VIJIJINI na Vijiji vya Wilaya ya Hai
-Hai, ndio Wilaya yenye mabilionea wengi wa kichagga
Mara vijiji mara mji! Wewe na wenzako mnapenda sifa za kijanga tu! Wewe unadhani Geita vijijini watu hawajengi nyumba nzuri nyinyi ndo mnajua kujenga peke yenu? Kama unazungumzia Mabilionea wa hela za Kibongo njoo Katoro Geita vijijini uwaone!
 
Kanda ya ziwa wameshatushika pabaya kutokana na kuzaliana kwao kwa wingi. Hasa wasukuma. Hata Rais akitoka upande mwingine, kuna nafasi muhimu hazitaikwepa Kanda ya Ziwa ile ya Wasukuma na subtribes zake. Ujumbe ndani ya NEC ya imedhihirisha hilo. Na wamejua umuhimu wa kuja pamoja. Hatuna cha kufanya.
 

..hata Magufuli alikuwa mbinafsi.

..miradi aliyopeleka kanda ya ziwa ilikuwa ya kumpatia umaarufu binafsi na haikulenga kuwainua wananchi.
 
Makosa waliyafanya wale waliojidai wanawasema Sukima g ambayo haikuwepo, mdomo huo umewaumba na wao sasa wame gang up...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…