Tusipofanya sasa, Tutajuta Milele, ni lazima Wamasai waondoke Ngorongoro

Upande wa pili mbuga ipi?? Taja hapa
Magharibi na kaskazini magharibi inapakana na Serengeti, kaskazini inapakana na Loliondo na inakwenda hadi Kenya na mashariki karatu na kusini mashariki Hifadhi ya Manyara
 

Nimeacha kusoma hutuba yako baada tu ya kusoma mistari michache. Nadhani ndugu zetu hamna taarifa zote za suali la kuondoshwa kwa kwa masai. Kutoka katika taarifa mbali mbali za vyombo vya habari vya nje ya nchi ni kuwa sehemu hiyo serikali imeliuza eneo hilo kwa kampuni yenye makao makuu yake UAE ili kuifanya sehemu hiyo kutumka kwa trophy kwa watalii!!!!!! Kwa maana nyengine itakuwa ni sehemu ambayo watu watatoka nchi zao za mbali kuja Tanzania kuuwa wanyama wetu na kujichukulia ngozi, vichwa na pembe na kuvipeleka kwao. Sio kuwa itakuwa sehemu ya watalii kuja kuona wanyama ambao hawana nchini kwao na ambao ni fahari kubwa ketu kuwa nao, la! Serikali inaruhusu wanyama wetu wawe wanauliwa sio kwa sababu yeyote ile bali ni kwa mchezo tu. Kwa ufupi serikali imeamua kuweka mbele pesa na iko tayari kupoteza treasure ya taifa. South africa wanajuta kuruhusu mchezo huu na sijui kwa nini tanzania tunaona kuwa hii idea nzuri!!!!!!
 
Magharibi na kaskazini magharibi inapakana na Serengeti, kaskazini inapakana na Loliondo na inakwenda hadi Kenya na mashariki karatu na kusini mashariki Hifadhi ya Manyara
Sasa wanahama kwenda Serengeti au Kenya? kupitia Loliond!!?? Fafanua ili ujibiwe sasa
 
Hizo habari zilizoandaliwa na wakenya wenye mission ya kuhakikisha Ngorongoro inakufa hazina mashiko
 
Hii sio nchi ya Mkoloni...amka wewe!
 
Hizo habari zilizoandaliwa na wakenya wenye mission ya kuhakikisha Ngorongoro inakufa hazina mashiko
Nope my friend. Taarifa zangu nimesoma kupita BBC world news na al jazeera news. Zote zimenukuu exactly nilichosema kampuni inayoitwa OBC (orttelo Business Corporation) ndio wanakodi/wananua hiyo sehemu kwa lengo la kuanzisha trophy hunting business!
 
Hivi kiuhalisia hamna sehemu nyingine ya kuishi zaidi ya kuishi pamoja na wanyama huko Ngorongoro?
 
Kama wewe ni mkenya kubali tu kuwa Tanzania imeamka. Lazima Ngorongoro tuilinde na maslahi ya Tanzania tuyalinde ili utalii uzidi kutuingizia fedha
Mimi wa hapahapa, Ila siendi kama zuzu ilimradi watu wana interest zao niunge mkono....
 
Mimi wa hapahapa, Ila siendi kama zuzu ilimradi watu wana interest zao niunge mkono....
Sasa kama wa hapahapa tetra maslahi ya Tanzania. Hadi wabunge wa Chadema waliopo Bungeni na waliostaafu kina Salome Makamba, Esther Matiko, Mchungaji Msingwa wamesimama na maslahi ya Tanzania pamoja na wabunge WAZALENDO wa CCM wewe kwa nini usisimamie maslahi ya Tanzania?
 
1. UKOLONI
Serikali ya sasa ina hadhi ya kufanya mabadiliko kama ambavyo serikali ya kikoloni ilikuwa nayo. Lakini swali ni je,
a. Je, maslahi ya wakazi wa pale yanazingatiwa?
b. Ardhi mbadala yenye hali ya hewa au tabia ya nchi kama pale iko wapi? Serikali ya kikoloni iliwahamishia eneo ambalo halikuwa tofauti na Serengeti hasa kwa shughuli yao ya ufugaji au uchungi wa mifugo kama msemavyo kwa kejeli.
c. Ni mabadiliko gani hayo ambayo mnasema serikali ya sasa ina haki ya kufanya? Serikali ya sasa inataka kufanya nini pale? Je, inataka kubadilisha kuwa national park? Mswada uko wapi?
Watanganyika msidangayike kirahisi.
2. NEGOTIATION
Serikali hii haikufuata utaratibu wa kawaida wa serikali inapotaka kuchukua eneo. Serikali imekuja kujump in baada ya NCAA kuwatumia vyombo uchwara vya habari kuwadhalilisha na kuwatweza utu wa wakazi wa eneo lile.
Ilishindikana nini kufuata utaratibu wa kawaida wa kubadilisha matumizi ya ardhi katika vijiji au miji?
3. ARDHI NDOGO
Inaonekana wewe unaangalia hii nchi kwa macho ukiwa kwenye basi au ndege au gari yako binafsi. Niambie wilaya ambapo kuna ardhi tu imekaa inayoweza kuaccomodate wakazi takriban laki moja watakaondolewa pale NCA.
Na isitoshe watu wanaondolewa na watu wanaohitaji ardhi kubwa kwa ajili ya kilimo na ufugaji.
Sisi hatujazoea kuishi kwenye viwanja vya 20 kwa 20 babu.
Hatujazoea kulima bustani.
Hatujazoea kukaa kwenye joto kama la Vigwaza Pale.
Wamaasai wa Ngorongoro ni tofauti sana na Wamaasai wa mikoa ya Pwani kama Tanga, Moro na Pwani.
Na sisi hatujazoea kukaa koo zetu mbali mbali.
Niambie kijiji gani kiko tayari kupokea idadi yote hiyo ya watu?
Nimesikia wanasema watawapeleka Kitwai kule Simanjiro. Kitwai ni mahali padogo sana kwetu na pia ina hali ya hewa tusioikubali. Bora tufe kuliko kwenda Kitwai.
Wengine wanasema Kilindi; Sisi tunaishi kijamaa. Yaani ng'ombe hawana mipaka ya ardhi kati ya kitongoji kimoja na kingine. Huko Kilindi, watu wanaishi kwa mipaka.
Mkitupeleka Kilindi, mnaenda kuchochea migogoro isiyoisha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…