Tusipokubaliana na mtazamo wa Godbless Lema, CCM itaendelea kutawala na katiba ya Sitta itapita

 
Wizi na mbinu chafu za ccm zinajulikana wala hazihitaji nguvu kung'amua,tatizo majeshi yote mawili ccm wana hisa huko.
 
Kwa aya ya mwanzo tu' kichefuchefu! Unavutiwa na matusi yake kwa raisi? Halima Mdee Vs Esta Bulaya, Wewe Vs Lema now. Timizeni zile ndoto za ndoa za jinsia moja anazozitetea Lema.

kichefuchefu tena basi utakuwa mjamzito tena mimba changa...
 

maombi yangu yanaweza kuwa yamejibiwa .
 
Hahahahahaaaaaaa! Naona machadema yanajifariji. Mkuu aweda, unatafuta Uben Saanane nini?

Unakenenua kama umeliwa, kama tunajifarij kwann tulichukua kata zote 5 arusha? Si unacheka cheka tu hapa angalia utaliwa!!!
 
Hivi kuna mtu muoga kama Lema, sijui kama unakumbuka kipindi cha mkutano wa Chadema Arusha, Lema aliwakimbia polisi akaenda kujificha kwenye meza ya kuuzia nguruwe akiwaogopa polisi.
 
MwanaDiwani
Mkuu MwanaDiwani, kwanza asante kwa hii, ila pia ni kweli CCM haiwezi tena kushinda Arusha, na sio Arusha tuu, hata Arumeru zote mbili, ile ya Ole Medeye mwisho wa CCM ni 2015!.

Pia ni kweli Watanzania ni waoga, hivyo wanaichagua CCM kwa uoga tuu, kuwa Wapinzani ni vyama vya vurugu!.

Ni kweli pia kuwa Godbless Lema ni jasiri, na anaungwa mkono sana na machalii wengi wa Arachuga!, kwa sababu ni chalii mwenzao, ni mtoto wa kijiweni, hivyo kuendesha siasa za kijiweni!.

Kitakachomfanya Lema ashinde tena Arusha sio uwezo wake kuhamasisha maendeleo bali ni hiki Mtazamo: Kanda ya Kaskazini, CCM imechokwa mpaka basi!


Ila pia naomba usiwabeze Chadema kushindwa Kalenga!, ile ni ngome ya CCM!, kama lilivyo jimbo la Moshi mjini ni ngome ya Chadema!.

Kuna baadhi ya majimbo, Chedema wameshinda sio kwa sababu wamawasimamisha wagombea makini, no!, Chadema wameshinda kwa sababu CCM imechokwa mpaka basi, kiasi kwamba hata Chadema wangesimamisha jiwe, jiwe lingepita!.
Tatizo la Chadema ni dogo tuu na hapa nimelieleza!, CCM Imechokwa; CHADEMA Haijajipanga!


Uchaguzi wa 2010, kuna baadhi ya maeneo, Chadema imesimamisha wagombea "viazi" na wakashinda!, miongoni mwa majimbo haya ni Arusha!. Nilitaraji, uongozi wa Chadema, baada ya kupata "viazi" hivi, kipindi hiki cha miaka 5, pia wangefanya juhudi za makusudi, kuwajengea uwezo, wa kuwapunguzia huo "ukiazi" wao, ili watakaposimama tena 2015, wasimame wakiwa ni bora zaidi na sio na "ukiazi" ule ule wa 2010!. Hili halikufanyika!. Wananchi wa Arusha, wamechagua "kiazi!", wamevumilia miaka 5 ya maendeleo hasi, kwa excuse ya "ushujaa" na "kuondoa uoga!", halafu 2015, waletewe tena "kiazi" kile kile bila mabadiliko yoyote!, labda kama wapiga kura ni machalii pekee!, lakini watu makini wote!, hawatakubali!. Kama Chadema hakitajitathmini na kuwatia wana Arusha mtu makini!, at the same time CCM, wakarekebisha makosa yao ya 2010!, jimbo la Arusha litarudi CCM kiulaini kama kumsukuma mlevi!.

Pasco.
 
Last edited by a moderator:
Mikael P Aweda

Usitusemee wana - Arusha mjini.
Hakuna anayetaka kumchagua tena LEMA. Ujinga ujinga wake wananchi wa Arusha wameshauchoka.
Ila hapo Mwisho umeandika ukweli!
 
Last edited by a moderator:
Hivi kuna mtu muoga kama Lema, sijui kama unakumbuka kipindi cha mkutano wa Chadema Arusha, Lema aliwakimbia polisi akaenda kujificha kwenye meza ya kuuzia nguruwe akiwaogopa polisi.

Teh teh teh ...

Hata siku ile pale chuo cha uhasibu, polisi walipoanza kazi yao, LEMA aliruka fensi ya mchongoma na kutokomea huku akiacha 'shangingi' lake!

LEMA mwoga sana sijui ni ujasiri gani anawafundisha vijana wake!
 
Kuna viongozi wa Chadema they are the best kwenye kuhamasisha maandamano, kuchochea fujo na vurugu!, halamu they do nothing kuhamasisha maendeleo!. Watu wananaka maendeleo na sio maandamano!.
Pasco

Ngosha, unaweza kunifafanulia maana ya kuhamasisha maendeleo? Maendeleo yanapaswa kuhamasishwa vipi na mbunge?

Kwa upande mwingine, kuna maeneo hapa TZ, hayana hizo "fujo na maandamano" (mf. maeneo ya mikoa ya Dodoma, Singida, Lindi n.k.), je hali ya maendeleo huko ipoje?

Naomba unijibu ngosha.
 
Pasco
Ndugu Pasco,
Ninashukuru kwa hoja yako ambayo inafikirisha kwa wale wapevu wa fikra.

Naomba uelewe kuwa CCM ni chama ambacho kina uwezo wa kujitathmini, kugundua makosa na kujisahihisha.

Uwezo huo umekiwezesha/unakiwezesha kurudisha Majimbo ambayo kilipokonywa na wapinzani.

Naomba uelewe kuwa, CCM ilishalishawahi kulichukua tena jimbo Arusha Mjini kutoka kwa Makongoro Nyerere. Vile vile kuna majimbo mengi tu ambayo CCM ilipoamua kuyarudisha, iliyarudisha. Baadhi yake ni kama Kigoma Mjini ya Dr Walid Kaborou (CHADEMA) ambaye alidodoshwa na Peter Serukamba. Jimbo la Temeke kutoka kwa Mrema, Mwibara kutoka kwa Mutamwega, Ubungo kutoka kwa Lamwai, Siha kutoka kwa Makidara Mosi, Kyerwa kutoka kwa Benedicto Mtungurehi. Etcetera, etcetera

CCM imejipanga tena kurudisha majimbo kama Arusha Mjini, Vunjo, etc.

Ni kweli kuna maeneo mengi ambayo CCM iliwapa majimbo wapinzani kutokana na makosa na udhaifu wake wa kiuongozi. Mchakato wa kuchagua wagombea na uwepo wa makundi ulikidhoofisha chama wakati wa kampeni za kitaifa.

Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Kikwete alishawahi kugusia matatizo yaliyokifanya chama kupoteza majimbo mbali mbali.

Mwenyekiti alisema,"Kama kiongozi unatosha kwenye mchakato wa chaguzi za ndani utapita na kama hautoshi huwezi kupita. CCM inaweza kuingia madarakani mwaka 2015 iwapo uteuzi wa wagombea utafanyika vizuri bila dhuluma, kuoneana na kukasirisha watu. Tusifanye makosa haya tena kwa kuwa siku hizi watu wana chaguo mbadala, wanaodhani kila anayeteuliwa na CCM atashinda, hawako dunia hii kwani kuna maeneo tulifanya makosa tukaona adhabu yake.

"Tusiwaonee watu katika uchaguzi, tusiwadhulumu na kuwasukuma ukutani bila sababu, kama ipo tuwaeleze ukweli. Tusiifikishe CCM mahali sipo, ambapo tutakuja kujuta, itafika mahali tutapata Rais halafu tukawa na wabunge wengi wa upinzani, au Rais akawa wa upinzani wabunge wengi wakawa wa CCM, itakuwa ni hatari, tutaendesha vipi Serikali,"

Mwenyekiti wa Chama aliendelea kusema, "Ikifika mahali CCM ina wanachama milioni sita, lakini wakati wa uchaguzi kura za mgombea wa CCM na za mgombea wa upinzani ukijumlisha kwa pamoja zote hazifikii idadi hiyo, basi viongozi mmeshindwa kuongoza wanachama wenu,".

Usishangae kwa nini viongozi wa CCM tokea Mkutano Mkuu umalizike wako sehemu mbali mbali wakiwatembelea wananchi achilia mbali mikakati mengine ambayo haiwekwi kwenye public domain.

Wahenga walisema, kufanya kosa siyo kosa bali kurudia kosa ndiyo kosa!
 
Last edited by a moderator:
Hivi huu Uoga wa wabongo ni laana iloyotokea wapi? Kila siku huwa nashangaa. Lakini hii ni kama kuingia bafuni kuoga maji ya baridi. Uoga upo kwenye kopo la kwanza tu. Kopo la kwanza likishaingia mwilini, mengine yanapita bila wasiwasi. Fisiemu walitambue hilo. Wasiruhusu Wabongo wafikie kujimwagia kopo la kwanza.
 
Pasco

Unajichanganya mara useme arusha ccm imechokwa mpaka basi mara useme itashinda ebu acha kuwa popo
 
Last edited by a moderator:
Pasco
Nahisi unaugomvi binafsi na Lema
 
Last edited by a moderator:
Lema Arusha anabebwa na Wachagga wenzake.. Siasa za Arusha zimejaa ukabila na udini

Hii kitu ya kuwafanya wachaga kama sio raia wa nchi hii lazima itabackfire. Naamin wachaga ni watu wenye kuona mbali sana nawengi ni wasomi wazuri as compared to wengine na as of now wanawaangalia tu kama hawapo na wala hawaoni mnavyowasimanga lakini nda utakuja hii kitu kula kwenu bigtime..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…