Tusipotezeane muda! Ukweli ni kwamba 'Ulidanganywa' na 'Wanafiki' kuhusu Kabudi na Lukuvi, ila sasa 'Unatuzuga' na 'Kujikosha' tu Kwao

Kabudi na Lukuvi wameshushwa cheo yaani "Demotion" period.

Sawa wazee Kabudi na Lukuvi wamepewa nafasi mpya Ikulu ya kuwa washauri wa raisi.

Lakini kwa Kabudi ni kwamba ameondolewa pale Wizara ya katiba na sheria ili kufanya marekebisho ya sheria zote ambazo alizisimamia ziliporekebishwa wakati raisi akiwa John Magufuli.

Hii inamaanisha kwamba shinikizo la kutoka nje ni kwamba Kabudi ni "hardliner" na "ally" wa zamani wa JPM hivyo ni lazima aondoke hapo ili sheria hizo ziweze kufanyiwa mabadiliko.

Lengo kuu likiwa ni sheria kama madini ambazo zimekuwa "complex" kwa sasa na zahitaji watu wa nje ya wizara kusaidia kuzitafsiri na kuzibadili na uwepo wa Kabudi itakuwa ni kikwazo.

Kwa Lukuvi jambo la msingi ni kumdhibiti kada huyu mkongwe na anaeaminika ndani ya CCM na njia pekee ni kumweka karibu na raisi Samia ili iwe rahisi kufahamu nyendo zake.

Umri wa Lukuvi, uzoefu, na umahiri wa kazi unampa faida zaidi endapo angeendelea kuwa waziri kule Ardhi ambako angekuwa huru zaidi khas katika kipindi hiki hadi uchaguzi wa 2025.

Mtu ambae hatakuwa na wasiwasi sana ni Profesa Kitila Mkumbo ambae ameonekana kuwa si tishio na aweza tu kuendelea na u-backbencher bungeni.

Ila kwa Lukuvi na Kabudi ni wazi kuwa hii ni kushushwa cheo yaani "demotion" na kukaa ofisini kusoma gazeti tokea asubuhi hadi wamaliza kazi.

Kutokana na uzoefu wa kuwa karibu na watu waloshushwa cheo lakini bado waonekana ni tishio, uingiapo ofisini saa mbili au tatu asubuhi, kwanza ni kupata kikombe cha chai, kisha kama kuna kabrasha lolote basi laweza kukuchukua hadi saa tano walisoma tu na kama kuna cha kushughulikia basi waongea na katibu muktasi na atashughulikia hiki na kile.

Tatizo ni pale uingiapo ofisini asubuhi na kukuta hamna kabrasha siku hiyo isipokuwa magazeti yote upendayo kuanzia Daily News, Guardian, na Citizen ambayo kwa Kabudi ni cha mtoto, kisha kama wapenda ya kiswahili Nipashe na Habari leo hayakosi.

Mchana saa saba watoka kwa ruhusa au kujulisha wapi waendaa kwa "lunch" na saa nane lazima urudi na ujulishe, ni hatari sana.

Hali ni hiyohiyo kwa mzee Lukuvi na hali hii huweza kukufanya kukumbuka mambo mengi sana mazuri ambayo huenda wayakosa kwa kuendelea kuwepo hapo ofisini.

Wazee wengi ambao nimewahi kuwaona wengine waliishia kuacha kazi kwa kuchanganyikiwa na wengine kuanza hadi kutembea tu mabarabarani na kuishia kumaliza soli za viatu.

Lakini kwa Mzee Kabudi ni kheri akafikiria kuomba kurudi UDSM ili aendelee na kazi yake ya uhadhiri ambayo angalau itampa ukurasa mpya wa maisha nje ya baraza la mawaziri.

Kwa kuwa mzee Lukuvi ni "too late" kurudi kuwa mwalimu lakini aweza kuomba tu kuendelea kuwa mbunge wa kawaida kama Profesa Mkumbo, isipokuwa kama analazimishwa kuwa msomaji magazeti Ikulu.

Ni aibu na udhalilishaji kwa mtu mzima kushushwa cheo halafu wapelekwa sehemu kusoma magazeti na kunywa chai.

Mimi ni mmoja wa watanzania ambao tunafuatilia kwa makini mambo ambayo yanaendelea nchini ambayo sasa yamekosa dhamana ya wananchi walo wengi na ambao wanashindwa kuelewa nini lengo kuu.
 
Naskitika kukwambia huna akili. Huyu huyu kabudi aliyemuita jpm mungu ana akadeclare kwamba ben saanane was killed!! You might be insane
Ww ndio insane hapa hoja ya mleta mada imenyooka nadhani ww ubongo wako hauna oxygen. Hatari sana!!
 
Huyu mama anguko lake litakuwa lakishindo sana. Pale anamtegemea mzee wa msoga tu. Je naye akiitwa mbele ya haki itakuwaje?!
Uzuzu na utegemezi wa kijinga kabisa.
Kweli mwerevu wa kisiasa waweza fikiria kumtoa mhehe ardhi na kumuingiza mwanasheria ambaye hajawahi hata kumtetea mwizi wa kuku au baiskeli??!!!!
 
Wanakazi yao hopo wizarani wanataka utulivu wakimaliza watawarejesha.
 
Aiseee mnachekesha yani raisi aanze kujikosha kwa kabudi na lukuvi kwa kuwa wao ni Akina nani[emoji3][emoji3][emoji3] mnahisi Huyu mama ni mpumbavu labda hyo maamuz kafanya akiwa kalewa....
Kwann awaongelee wao tu..huon kuna namna hapo
 
Kinachoshangaza ni kwamba kila anayepigwa chini ni mkristo !
Mbona katika Awamu ya Hayati Rais Dk. Magufuli Wakristo tulipokuwa Wengi katika Serikali yake hukuja hapa JamiiForums kulalamika kuwa Waislamu wamesahaulika katika Teuzi zake?

GENTAMYCINE ni Mkristo halisi tena kutokea Dhehebu Kubwa na lenye Ushawishi katika Imani ya Ukristo duniani la Katoliki ( Roman Catholic ) ila nachukia sana Wasomi ( Intellectuals ) tukiacha Kujadili Mambo ya maana ya Kuisaidia kuijenga Tanzania yetu na tunaanza Kukimbilia katika Udini.

Nimesikitika.......!!!!
 
Ndiyo 'Kiherehere' Mkuu katika Ushauri.
Haya mkuu, huenda lisemwalo lipo ila mie ni big tomaso, sioni sababu ya kumhusisha mzee wa Msoga kwenye any wrongdoing itayoendelea maana na wao wana akili zao. Ngoja niende jamii sports kukusoma juu ya Sakho na Chama kama umesema nini kule leo, maana siasa za bongo pasua kichwa.
 
Sio rahisi kukubaliwa kurudi mahali ulipopaita jalalani.
 
Mtu mweusi yupo "allergic" na mtu mwenye uwezo na akili, ni species za ajabu sana sisi, binafsi nilishangaa sn unatoaje watu wa namna hiyo kwenye utendaji? Tunapenda mambo ya kijinga kijinga sana, nakupa swali as a food for thought, kwann waafrika ndio watu hapa duniani tunaishi maisha very deplorable? Miaka 60 ya uhuru bado tuko hivi? Jibu linaweza kuwa jepesi sana ukifanya comparative analysis ...wenzetu wana thamini sana viongozi wenye akili sisi tupo allergic na watu wenye uwezo na akili...tutakuwa hivi hivi in the next 100 years or even worse... wakati wenzetu wapo angani huko exploring the universe.

Kwa akili za namna hii tutabaki kuwa consumers wa technology ya mzungu for generations to come. AKILI NI KILA KITU hata kama hauna resources za aina yoyote.
 
Nyinyi ukoo wa marehemu mtaacha lini kuseng'enyana, kufitinishana, kung'ong'ana?

Mwacheni hangaya acheze taarabu banaa chee!
 
Kwa haya Madini yako ya uhakika uliyoyaandika ( uliyoyashusha ) hapa naomba ruhusa yako Mkuu nikuite Genius / Einstein ( Mtu Mwerevu ) kwani Umemaliza kila Kitu na nimefurahi mpaka Malaika wa Mbinguni nao wametambua na Kufurahi pia.
 
Aiseee mnachekesha yani raisi aanze kujikosha kwa kabudi na lukuvi kwa kuwa wao ni Akina nani[emoji3][emoji3][emoji3] mnahisi Huyu mama ni mpumbavu labda hyo maamuz kafanya akiwa kalewa....
Ndivyo inavyo dhihilika.
 
Iko wazi kua kilichofanyika ni kuwatoa hao wazee ili waweke watu wao.Ndo maana nafsi ilianza kujieleza kabla ya maamuzi kufanyika.Tulianza kusikia kauli za kuna wanaoutaka urais, mbio za 2025 wakae pembeni wakajipange vizuri,wasioendana na kasi na badae baada ya maamuzi ya mabadiliko kufanyika zikaja hizi kauli,hawa nawapa kazi nyingine.Ukiunganisha dot unaona kabisa kua nafsi inasuta.Tunajua kua mheshimiwa anaweza kubadilisha kiongozi muda wowote anaoutaka ila hiki likilofanyika sasa sicho kilichokusudiwa ndo maana ilianza kutafutwa sababu.Alikua na uwezo wakusema:Nitafanya badiliko la baraza bila kutanguliza sababu yoyote na angeeleweka na kusingekua na maswali mengi.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Viongozi wanaofanya ivyo ni wale ambao hawana uwezo wakuongoza.Ndo maana mara nyingi wanatumia nguvu kuzima hoja kinzani.Lakini bado hilo halijawai kusaidia nchi yoyote kwasababu watu tunapita ila hoja na mawazo yanaishi na kila leo zinazaliwa fikra mpya.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…