#COVID19 Tutegemee nini baada ya Rais Samia kusema 'Gwajiboy oyee Tunachanja, hatuchanji' mbele ya Askofu Gwajima?

#COVID19 Tutegemee nini baada ya Rais Samia kusema 'Gwajiboy oyee Tunachanja, hatuchanji' mbele ya Askofu Gwajima?

Sasa swali langu lilikuwa kama si Magufuli kupotosha je watanzania wengi wangekubali kuchanjwa? lakini kumbe hata Magufuli asingepotosha bado ingehitajika nguvu kubwa ili kuwashawishi watanzania wengi kukubali kuchanjwa,
Kama Magufuli asingepotosha nguvu ambayo ingetumika isingekuwa kubwa sana ukilinganisha na Magufuli alipopotosha kwa sababu kumbuka kushawishi watu wasahau ule upotoshaji mkubwa wa Magufuli ndipo nguvu kubwa ya kushawishi watu inapohitajika.
sasa nachokiona sasa hivi sioni nguvu kubwa kutumika kuwashawishi watu kuchanjwa bali naona watu wanatumia muda mwingi kumlaumu Magufuli kuwa ndio sababu ya watu kukataa kuchanjwa kana kwamba imetumika kila jitihada vya kutosha kuwashawishi na kuwaelimisha ikashindikana au kwamba kama si Magufuli basi ingekuwa rahisi tu kwamba watanzania wengi wangekubali kuchanjwa wenyewe tu.
Kama siyo Magufuli ni kweli ingekuwa rahisi tu kushawishi watu sasa hivi na kukubali kuchanja.Kumbuka Magufuli alikuwa ni mwanasiasa ambae ni populist.Huwa ni kazi ngumu sana kuneutralize na kufuta anachosema populist kwa sababu populist huwa wana ushawishi na nguvu nyingi sana katika jamii.Wanaomlaumu Magufuli katika hili wapo sahihi.
 
Leo wakati Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akielekea Bagamoyo kurecord filamu ya kutangaza utalii wa Tanzania alisimama kwenye jimbo la Kawe ili kusalimia wananchi.

Rais alimsimamisha Mbunge wa Kawe ili kutoa neno lakini kabla ya kumsimamisha aliwauliza wananchi wa Kawe kama watachanja au la kama video inavyoonyesha hapa chini.Katika hali ya kustaajabisha na ya kushangaza wananchi walimwambia Rais bila ya kupepesa macho kuwa hawatachanja kama video hii inavyoonyesha hapa chini.

Nimejiuliza maswali mengi sana.Kwa nini Rais aulize swali hilo kwenye jimbo ambalo mbunge wake hakubaliani na mambo ya chanjo?Ina maana Rais hajui kwamba kazi kubwa ambayo walifanya katika awamu ya tano ya kupinga chanjo ilifanikiwa sana hasa ukizingatia kuwa kazi hiyo ilifanyika katika Taifa lenye umasikini mkubwa sana wa akili?

My take:
Kwa sasa hivi serikali ya CCM inapata shida sana kula matapishi yake yenyewe ambayo waliyatapika katika awamu ya tano.Ni vyema serikali ikiri mbele ya wananchi kuwa Rais Magufuli hakuwa sahihi na alipotosha sana uma ili wananchi waanze upya kuelimishwa juu ya gonjwa la Corona na chanjo.

Mleta mada inaonekana ww ndio una umaskini mkubwa wa akili.Kwa umaskini wako mkubwa wa akili unaona Kawe tu ndio wanapinga chanjo.Nenda ulaya,USA,kote kuna ambao hawataki chanjo.Mpaka Rais wa USA alitoa bonus ya uds 200ili wachanjwe.Je nao wanaumasikini wa akili au bogas www ndio maskini mkubwa wa akili.Aidha ukichanjwa bado upo kwenye hatari mkubwa ya kuambukizwa na kuambukiza.Wanaochanjwa waheshimiwe na wasiochanjwa waheshimiwe.Watu msio na ufahamu wa hivi vitu mnyamaze.
 
Wananch sio wajinga wewe

Nenda makanisani mfano ya katoliki yaliyojaa wasomi wakubwa unakuta ni padri tu ndie kavaa barakoa ina maana waumini wote hawajielewi kasoro huyo padri tu? Wote hawajasoma na wana uelewa mdogo kasoro padri tu?

Ina maana wasomi wote wanaojazana makanisani na misikitini bila barakoa uelewa wao hawana?

Wananchi wanajielewa sana kuliko viongozi


Unapoona kiongozi wa dini yeye peke yake ndie kavaa barakoa waumini hawajavaa ujue kuwa waumini wana imani kwa Mungu kuliko kiongozi wao!!!! Kiongozi anaamini kuwa akiwa kanisani kwenye nyumba ya Mungu MUNGU ANAWEZA MTUPIA CORONA WAKATI WAUMINI HAWAAMINI HILO

Mungu ni wa dunia nzima, makao makuu yake hayapo Tanzania
 
Leo wakati Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akielekea Bagamoyo kurecord filamu ya kutangaza utalii wa Tanzania alisimama kwenye jimbo la Kawe ili kusalimia wananchi.

Rais alimsimamisha Mbunge wa Kawe ili kutoa neno lakini kabla ya kumsimamisha aliwauliza wananchi wa Kawe kama watachanja au la kama video inavyoonyesha hapa chini.Katika hali ya kustaajabisha na ya kushangaza wananchi walimwambia Rais bila ya kupepesa macho kuwa hawatachanja kama video hii inavyoonyesha hapa chini.

Nimejiuliza maswali mengi sana.Kwa nini Rais aulize swali hilo kwenye jimbo ambalo mbunge wake hakubaliani na mambo ya chanjo?Ina maana Rais hajui kwamba kazi kubwa ambayo walifanya katika awamu ya tano ya kupinga chanjo ilifanikiwa sana hasa ukizingatia kuwa kazi hiyo ilifanyika katika Taifa lenye umasikini mkubwa sana wa akili?

My take:
Kwa sasa hivi serikali ya CCM inapata shida sana kula matapishi yake yenyewe ambayo waliyatapika katika awamu ya tano.Ni vyema serikali ikiri mbele ya wananchi kuwa Rais Magufuli hakuwa sahihi na alipotosha sana uma ili wananchi waanze upya kuelimishwa juu ya gonjwa la Corona na chanjo.

Na kwa taarifa yako MagufuliJP was very right. Na ccm wasijaribu kufanya kosa hilo. Sasa hivi mambo mengi sana hayaendi na wanakumbuka MagufuliJP. Ukisema chochote cha kumnanga MagufuliJP you will test the heat [emoji91] of stone. Acha ujinga.

Kwa study iliyo fanyika Israel walio ugua corona wanakuwa na kinga kubwa dhidi ya virusi vya aina zote vya corona. Ambacho ndo hicho MagufuliJP alisema. Tuache usambae ili tupate kinga. Na sisi ukiangalia hatujapata Madhara makubwa kama nchi nyingine. Watu wanakufa sana baada ya kupata chanjo. Tuna madaktari kama 5 wamekufa baada ya chanjo. Nina rafiki zangu wanne wamekufa baada ya chanjo.
 
Na kwa taarifa yako MagufuliJP was very right. Na ccm wasijaribu kufanya kosa hilo. Sasa hivi mambo mengi sana hayaendi na wanakumbuka MagufuliJP. Ukisema chochote cha kumnanga MagufuliJP you will test the heat [emoji91] of stone. Acha ujinga.

Kwa study iliyo fanyika Israel walio ugua corona wanakuwa na kinga kubwa dhidi ya virusi vya aina zote vya corona. Ambacho ndo hicho MagufuliJP alisema. Tuache usambae ili tupate kinga. Na sisi ukiangalia hatujapata Madhara makubwa kama nchi nyingine. Watu wanakufa sana baada ya kupata chanjo. Tuna madaktari kama 5 wamekufa baada ya chanjo. Nina rafiki zangu wanne wamekufa baada ya chanjo.
Duh,wachanje tu!
Magufuli alikuwa sahihi kabisa kwenye hili!
 
Mapema Leo wakati Rais Samia yupo Tegeta jimbo la Kawe kwa Mchungaji Gwajima akiongea na wananchi na wakazi wa Kawe waliojitokeza kumsikiliza ameongea mengi lakini kati ya hayo ni pale aliposema "Gwajiboy oyeee, tunachanja, hatuchanji? Haya mheshimiwa gwajima endelea"


Kwa kauli hii Spika na Waziri wa Afya wako na hali gani kwa sasa?

Je, tuendelee kutegemea hatua zozote kutoka kwenye chama (CCM) dhidi ya Gwajiboy?
Gwajiboy 3 Ndugai na Gwajigirl 0
 
Mleta mada inaonekana ww ndio una umaskini mkubwa wa akili.Kwa umaskini wako mkubwa wa akili unaona Kawe tu ndio wanapinga chanjo.Nenda ulaya,USA,kote kuna ambao hawataki chanjo.Mpaka Rais wa USA alitoa bonus ya uds 200ili wachanjwe.Je nao wanaumasikini wa akili au bogas www ndio maskini mkubwa wa akili.Aidha ukichanjwa bado upo kwenye hatari mkubwa ya kuambukizwa na kuambukiza.Wanaochanjwa waheshimiwe na wasiochanjwa waheshimiwe.Watu msio na ufahamu wa hivi vitu mnyamaze.
Yaani wabongo bwana!
Uko sahihi nimeona utube maandamano nchi za ulaya wanaopinga chanjo nashangaa hapa wanataka kutufanya tunaokataa kana kwamba hatuna elimu,masikini ,ulaya je?

Na nina mifano ya waliochanja wamekufa ukilinganisha ambao hawajachanja!

Ht tunaopinga chanjo tuheshimiwe!
 
Huyu atafeli mno katika utawala wake wa kurithi.
Analeta mambo ya Meko Meko kuongea ujinga kwenye majukwaa .

Sukuma gang wamemzidi nguvu sasa anapuyanga puyunga tu.

1.Mara tozo ziko palepale
2.Mara Wahisani hawaleti misaada wanataka tufanye BIASHARA...wakati kila siku anaomba misaada ya chanjo ,fedha za maendeleo na mikopo juu anapokea.
3.Kelele za mpangaji hazmzuii mwenye nyumba kulala
4.Mara tupige picha tupeleke meseji kuwa yanayosemwa sio yaliyopo
5.Mara Gwajiboy hoyeeee na kampandisha hadi kwenye gari lake
Ujinga mtupu
Anapuyanga puyanga.
 
Alitakiwa atumie nguvu nyingi kuelimisha.Kazi ya kiongozi ni kuelimisha na wala siyo kupotosha.Magufuli alikuwa anatumia nguvu nyingi kupotosha.

Dada yangu kule kijijini amekataa kuchanjwa, nilipomuuliza kwa nini hataki kuchanja ameniambia kuwa Magufuli alisema kwenye redio kuwa chanjo hazifai.

Mtu kama huyu angeelimishwa na kiongozi huyu wa nchi angekubali kuchanjwa.

Watanzania wengi hawana elimu kwa hiyo kile wanachoambiwa na viongozi wao wanapokea kama kilivyo.Watu hawa wanapaswa kuelimishwa badala ya kupotoshwa.
Magufuli hajawahi kupotosha,kwenye hili jambo I stand with him!alikuwa sahihi,na ilitusaidia kuondoa hofu na Mungu alituvusha salama bila lockdown wala chanjo!
Unaweza compare na nchi zilizokuwa na lockdown kwa vifo?,hebu muogopeni Mungu.
Hizi chanjo hata mataifa mengine zinapingwa sembuse Tanzania? Acheni kumuonea Magufuli!
Gwajima yuko sahihi,tusiotaka chanjo tuheshimiwe,tuna elimu,tuna uelewa nk na wala sio masikini! Nyie,kachanjeni tu!
 
Na viongozi wote wa makanisa makubwa hasa RC wametoa amri watumishi wao wote wachanje.

Hata hivyo Rais yuko wazi na hafanyi propaganda za kijinga kama za yule mpuuzi,ukitaka chanja hutaki acha ,ukifa ni wewe sasa.

Tutafika mahala kama ukibainika una covid na umepelekwa hospital huenda ukatengwa kivyako kwa sababu umejitakia ilhali chanjo ipo na waliochanja watahudumiwa .
Viongozi hawawezi toa amri sababu chanjo ni hiari,ila wameshauri usipotoshe!

Chanjo haizuii maambukizi!
Ukichanja lzm ufuate tahadhari zote!
Sasa chanjo ya nini?
 
Na kwa taarifa yako MagufuliJP was very right. Na ccm wasijaribu kufanya kosa hilo.
Magufuli alikuwa very right kwa sababu gani?Hoja yako ni ipi?
Sasa hivi mambo mengi sana hayaendi na wanakumbuka MagufuliJP. Ukisema chochote cha kumnanga MagufuliJP you will test the heat [emoji91] of stone. Acha ujinga.
Kwa ushahidi wa ile ripoti ya CAG ambayo ilikuwa ni chafu sana, Magufuli alikuwa ni kiongozi populist ambae alikuwa ni mwizi,fisadi na mzembe wa mali za uma aliekuwa anajificha kwenye chaka la siasa za propaganda ili kulaghai wajinga.
Kwa study iliyo fanyika Israel walio ugua corona wanakuwa na kinga kubwa dhidi ya virusi vya aina zote vya corona. Ambacho ndo hicho MagufuliJP alisema. Tuache usambae ili tupate kinga.
Ukisema kuwa tuache usambae ili tupate kinga maana yake ni kwamba unawatoa sadaka wazee pamoja na watu wenye magonjwa sugu kitu ambacho hakikubaliki hata kidogo.
Na sisi ukiangalia hatujapata Madhara makubwa kama nchi nyingine.
Umejuaje kuwa hatupati madhara kama nchi nyingine wakati hakuna takwimu zinazotolewa?Umefanya tafiti gani ya nchi nzima hadi ukajua kuwa hatujapata madhara kama nchi nyingine?Yaani umetumia kigezo gani kujua kuwa hatujapata madhara kama nchi nyingine?
Watu wanakufa sana baada ya kupata chanjo. Tuna madaktari kama 5 wamekufa baada ya chanjo. Nina rafiki zangu wanne wamekufa baada ya chanjo.
Watu kufa baada ya kupata chanjo ni jambo la kawaida kabisa na ni jambo lililothibitishwa kisayansi kwa sababu hizi chanjo zina efficacy.Kama efficacy ya chanjo ni asilimia 70 lazima kuna watu wengi tu watakufa baada ya kupata chanjo.Unaelewa maana halisi ya efficacy katika chanjo?
 
Viongozi hawawezi toa amri sababu chanjo ni hiari,ila wameshauri usipotoshe!

Chanjo haizuii maambukizi!
Ukichanja lzm ufuate tahadhari zote!
Sasa chanjo ya nini?
Amri ni kwa watumishi sio waumini hata serikali inaweza sema mtumishi wa umma chanzo lazima hutaki tupishe usituletee ugonjwa,imefanyika hivyo nchi nyingi tuu na ilianza kwa neno hiari.

Kimsingi huna hiari ya kuambukiza wengine nadhani ulimsikia na Spika aliwaambia hivyo hivyo wabunge.

Achaneni na ujinga wa imani za ujinga wa kina Gwajima,mafuta ya mwamposa na ushirikina.
 
Magufuli hajawahi kupotosha,kwenye hili jambo I stand with him!alikuwa sahihi,na ilitusaidia kuondoa hofu na Mungu alituvusha salama bila lockdown wala chanjo!
Unaweza compare na nchi zilizokuwa na lockdown kwa vifo?,
Mungu ametuvusha salama kivipi?Una takwimu za watu waliokufa kwa Corona Tanzania?Unavyosema kwamba madhara tuliyopata huwezi kulinganisha na madhara waliopata watu waliokuwa na lockdown kwani unayajua madhara ambayo Tanzania imepata?Una data/takwimu?Unatumia kigezo gani kujua kuwa Tanzania haijapata madhara makubwa?Umefanya tafiti nchi nzima ukajua kuwa waliokufa kwa Corona siyo wengi?Hoja yangu hapa ni kwamba umetumia kigezo gani kufikia conclusion uliofikia kuwa Tanzania haikupata madhara makubwa wakati hadi kutoa takwimu ilipigwa marufuku?
hebu muogopeni Mungu.
Hizi chanjo hata mataifa mengine zinapingwa sembuse Tanzania?
Chanjo kupingwa katika mataifa mengine haihalalishi kuwa chanjo kupingwa Tanzania ni sahihi.Kwani nchi nyingine hazina wajinga?Hizo nchi nyingine wanaishi miungu ambayo haiwezi kuwa wajinga?Si wanaishi tu binadamu kama Tanzania?
Acheni kumuonea Magufuli!
Gwajima yuko sahihi,tusiotaka chanjo tuheshimiwe,tuna elimu,tuna uelewa nk na wala sio masikini! Nyie,kachanjeni tu!
Gwajima hayupo sahihi kwa sababu ni mbumbumbu peke yake ndiye anaweza kupingana na sayansi.Wewe unazikataa chanjo kwa kigezo kipi?
 
Back
Top Bottom