Tuwaepuke wanasiasa wanataka kutuletea ukabila kupitia uChifu

Tuwaepuke wanasiasa wanataka kutuletea ukabila kupitia uChifu

Hawa wameibuka kutoka wapi?
Na je wana impact gani katika maisha yetu kwa ujumla?
Sijawahi kusikia Chifu anatoa neno lolote kwenye jumuiya yetu
Hata kusifu au kukemea kitu ila ghafla tunasikia chifu wa huku na kupewa uchifu sijui nini
Mkuu hii ndio asili ya Africa ndiko babu zetu walipotoka kabla ya kutekwa akili na mzungu aliedhulumu haki yako..
 
Nawasalimu kwa jina la Jamuhuri ya muungano wa Tanzania.

Hizi siasa za Uchifu sio siasa salama kwa mustakabali wa nchi.

Kwanza yale maguo yenye ngozi za chui sijui wameyatoa wapi!

Niseme tu kwamba, Tanzania hakujawahi kuwa na machifu kwa muktadha wa uongozi wa kitaifa.

Machifu wa Tanzania walikuwa ni tawala chache tu ambazo zilikuwa huko kwa watu wa iringa zamani hizo.

Baadae wakoloni walipokuja, wakaunda vikundi vya wahuni wachache miongoni mwa watanzania kisha wakawavika uchifu for the benefit of white man. Hawa ndio waliohusika kuwauza wenzao utumwani.

Huu uchifu wa sasa wa Samia, sio uchifu haswa. Ni vikundi vya wachawi wanaomsimika Hangaya kwa kumpa mamlaka na utii. Ni power transfer ama alama ya utii katika mamlaka za wachawi.

Wachawi hawa wako nchi nzima. Wamejivika uchifu bandia ili kuficha sura zao halisi.

Kila mahali Rais anapopita wanamvika maguo ya kichawi.

Jamani, nchi hii inamuhitaji Mungu. Tuache kutegemea viumbe dhaifu kama mizimu.

Mungu wetu ni Mungu mwenye nguvu sana, lakini anahitaji watu wanyoofu.

Shida yenu nyinyi ni majizi na watu wa konakona, ndio maana mmemkimbia Mungu mkajikabidhi kwa viumbe wachafu na dhaifu kama majini na mizimu.

Mrudieni Mungu mwenye nguvu na mamlaka, mzitii amri zake na yeye awafanye kuwa wake.

Hayo maguo ya mizimu hayawezi kuwasaidia lolote. Mnajidaganya.
Kila jambo huwa na kiasi, linapozidi huweza kubadili maana au kuharibu kabisa. Mfano, pete, ikizidi itakuwa Bangili.

Utamaduni ni jambo tofauti kabisa na uchifu. Uchifu unaweza kuwepo ndani ya utamaduni. Hapa ipo siku tutachanganyiwa mambo
 
Mkuu hii ndio asili ya Africa ndiko babu zetu walipotoka kabla ya kutekwa akili na mzungu aliedhulumu haki yako..
Hakuna kitu kama asili ya Afrika.

Kwanza neno lenyewe tu ni la Kiingereza CHIEF.

Chiefs ni watu waliosimikwa na mkoloni kwa ajili ya utawala wa kikoloni. Divide and rule tactics.

Waafrika walikuwa na viongozi wao lakini sio CHIFU. Hii CHIEF ni ya mzungu.

Na samia kaja na wachawi wake anaiwaita ati MACHIFU.
 
Kabisaaa nakazia hapa!
Ushirikina,uchawi kabisaa,kuabudu miungu
Ona machawi yalivyojipanga...
FB_IMG_16428741027400401.jpg
 
Ukiongelea uchifu unaongelea asili yetu..tamadunj..mila na miiko bila kusahau imani..wewe mlokole na mfia dini ambaye uliondolewa akili na utu wako kisa dini za wazungu na waarabu..ili wakutawale kuanzia akili na mali..unaona upuuzi kuenzi mila zako.

Bure kabisa..wewe.

#MaendeleoHayanaChama
 
Ukiongelea uchifu unaongelea asili yetu..tamadunj..mila na miiko bila kusahau imani..wewe mlokole na mfia dini ambaye uliondolewa akili na utu wako kisa dini za wazungu na waarabu..ili wakutawale kuanzia akili na mali..unaona upuuzi kuenzi mila zako.

Bure kabisa..wewe.

#MaendeleoHayanaChama
Kwanza uelewe kwamba CHEIF ni neno la kizungu.

Pili MACHIFU ni viongozi wa kiafrika waliowekwa na wazungu kwa ajili ya kazi za kikoloni.

Afrika haijawahi kuwa na CHEIF. Hii CHIEF ni invention ya mkoloni.

Hawa wa sasa hivi wanaoitwa MACHIFU ni wachawi wa samia.

Hakuna kitu kama CHEIF. Haya ni machawi tu yaliyotafuta chaka zuri la kujifichia.
 
Mkuu hii ndio asili ya Africa ndiko babu zetu walipotoka kabla ya kutekwa akili na mzungu aliedhulumu haki yako..

Sawa ni asili yetu lakini swali bado liko palepale mbona hatuwasikii kwenye jamii ?
Naomba unielewe hoja yangu
Kwanini hawana nguvu kwenye jamii yetu au ndio wamekuwa wale wa kuabudu mizimu tu
 
Wasaidizi wa Rais naona wanaendelea kumpoteza tu kwa kila namna, walianza kwenye zile teuzi anateau leo kesho anatengua, naona mpaka sasa bado Rais anakosea mambo mengi, nadhani nae binafsi anastahili kubeba lawama.

Anatakiwa awe anajiuliza kama hayo anayokwenda kuyafanya yana maslahi kwa taifa au ndio yataligawa taifa, hilo jina chief Hangaya alipewa akalipokea naona amenogewa sasa anataka kuendeleza hiyo tabia kwa mikoa yote Tanzania.

Haya mambo hayana maana, tuna wakuu wa mikoa, wilaya, wakurugenzi nk hawa machifu wanaolazimishwa kuwepo sasa kazi yao ni ipi? au ni urembo tu, kwamba wanatambuliwa uwepo wao japo hawana kazi? mikoa ya Tanzania ina mchanganyiko wa makabila mengi sasa hivi, hii biashara anayoleta Rais ni kuturudisha nyuma tu kifikra wakati tulishatoka huko zamani.
Kuna baadhi ya makabila mengi tu hapa Tanzania wakati wa ukoloni yalikuwa na machief (waliowekwa na wakoloni sehemu za pwani waliwata maakida, maliwali nak). Lakini baada ya uhuru Nyerere aka-mute haya mambo ya uchief (whether wa asili au wa kupewa na wakoloni). Sasa kama tukianza kuupa heshima sana hawa machief na kuufufua uchief kutoka makabulini ulikozikwa miaka 60 iliyopita tutaamsha dude moja baya saya huko mbeleni la ukabila na umajimbo.
 
Uchawi na CCM ni kitu kimoja.
Chama cha Michawi.

Inaamini eti mwenge unaleta amani, kwanii kipindi cha vita ya Kagera walipeleka vijana wetu vitani ambako walikufa kwa wingi, hawakuupeleka mwenge ambao kila siku wanausifi kwamba unaleta amani palipo na chuki?
CCM ni wakala wa shetani.
Hilo anayepinga na apinge,lakini ukweli unajulikana.
 
Huu uchifu wa sasa wa Samia, sio uchifu haswa. Ni vikundi vya wachawi wanaomsimika Hangaya kwa kumpa mamlaka na utii. Ni power transfer ama alama ya utii katika mamlaka za wachawi.
...Duh!....hizi ni siasa tu wakuu zisiwatishe... Tanzania yetu haiwezi kurudishwa kwenye Uchifu.
 
Nyerere aliwadanganya na kuwabrainwash msahau mila na tamaduni zenu ili awatawale bila usumbufu. Pia alipiga marufuku upinzani wa siasa kwa sababu hiyo hiyo. Mmefikia sehemu mnazikana na kuzikashifu jadi na tamaduni zenu.
 
Kama wameweka tegemeo lao kwa uganga, uchawi, ulozi, mizimu, matunguli na mauchafu kama hayo.........usitegemee jambo la kinyume chake. Kukimbiza tu moto unaoitwa mwenge ni ibada kamili ya kishetani, itakuwa kwenda kuzindikwa mauchawi na hao wanaoitwa machifu...........
 
Back
Top Bottom