Dar ya Zamani ilikuwa ndogo ila mishe kibao,wajanja walikuwa wanapiga pesa Sana,serikali ilikuwa na mifumo dhaifu Sana.Wakati huo sera za uchumi wa serikali kuhodhi Mali zinakufa tunaingia uchumi wa soko huria watu walizipiga Sana.
Sent from my TECNO B1f using
JamiiForums mobile app
nakumbuka mwaka 2000 mpaka kuja 2005 kulikuwa na mabroo wanasukuma magari makubwa ya kutembelea ila kazi walizokuwa wanafanya hazieleweki kwa usahihi.
kuna broo mmoja ambaye kwa sasa ni marehemu(alijiua kwa kujipiga risasi na bastola), yeye alikuwa na kijiofisi chake cha ujanjaujanja kule nyuma ilipokuwa club billicanas
ndani ya kile kiofisi kulikuwa na meza moja, kiti chake cha kukalia, viti viwili vya wageni na desktop computer moja ndani ikiwa na OS ya window xp(ma IT technician wa zamani wanakumbuka).
huyu broo alikuwa anabadili gari za kutembelea mpaka mimi mwenyewe nikawa nashangaa, halafu gari zake zote kali zikiwa ktk condition nzuri unaweza dhani zimetoka moja kwa moja showroom.
wiki hii atakuja na pajero, baada ya wiki kadhaa utamuona na rav4, mara utamuona ana drive lexus nk. halafu yeye mwenyewe mda wote ni msafi. that was his lifestyle routine.
sijui ni akili ya utoto/ujana au nini,nikawa inspired na ile lifestyle yake, nikaamua kutafuta mbinu ya kumzoea maana jamaa alikuwa sio mtu wa mastori. akishuka tu kwenye gari, anazama ofisini.
pale ofisini kulikuwa na mpambe wake mmoja(siku hizi wanaitwa machawa) ambaye alikuwa anashinda mda mwingi.huyu mpambe na yeye kwa sasa ni marehemu.
nikamzoea huyu mpambe wake, halafu kila nikipata chance namuuliza kuhusu michongo anayopiga boss wake ili kama inawezekana aniajiri katika team yake.
yule mpambe akawa anacheka kwa dharau halafu ananiuliza "utaweza?". mimi kwa kujiamini nikawa namjibu ndio nitaweza. basi akaniambia ondoa shaka nitazungumza na broo ili tuone tunafanye.
baada ya kama mwez hivi,yule mpambe akaniambia tayari alishaongea na broo, twende ofisini nikakutambulishe.
tukafika, nikamsalimia, akaniambia dogo nimepata salamu zako, unataka nikupe kazi, nikamjibu ndio broo. akaniuliza swali lilelile nililoulizwa na mpambe wake, "utaweza?".
nikamjibu ndio nitaweza bro, halafu nikamuuliza kwani unataka kunipa kazi gani broo?. akanitazama kwa makini kama sikunde tano hivi, halafu akanijibu "kazi ya kusambaza unga".
roho yangu ikafanya paaa, wakati nikiwa kwenye mshtuko, yule broo akaendelea kuniambia anataka anipe kazi ya kusambaza unga ndani ya vitongoji vya jiji la dar, halafu niki improve atakuwa ananituma mikoani then niki improve zaidi atakuwa ananituma nje ya nchi.
those days nilikuwa bado chalii halafu mtoto wa kota, bado nipo home kwa baba na mama, sikuwa na knowledge kubwa kuhusu maisha.
lakini pia sikuwahi kuuona unga kwa macho wala kuuza, zaidi tu ya kusikia habari za madhara yake kwenye vyombo vya habari, kusikia mikasa mbalimbali ambayo wauza unga wanapitia na kuwaona mateja wakibembea ktk vichochoro vya kitaani kwetu.
hii ajira ambayo huyu broo alitaka kunipa kwa kweli ilinishtua sana,ni kitu kigeni kwangu. nikiwa kwenye mshtuko,akaniambia nenda kajifikirie,ukiwa tayari utanijulisha, ila usimwambie mtu, iwe siri yako.
ni kweli sikumshirikisha mtu, ila niliapa kutotafuta tena mazoea na yule bro. kila nikimuona ana park gari lake mimi namkwepa asinione.
yule mpambe wake kila mara alikuwa ananikumbusha kama bado najifikiria au vp. akawa ananiambia broo anasubiri jibu lako.
all in all, yule bro alikuwa ni ZUNGU LA UNGA wa level ya juu kabisa. may his soul continue to rest in peace.
sijataja jina lake kwa makusudi ili niwaachie
lesson wajanja wa zamani waunge dot vizuri. bila shaka watamjua.