Tuwaombee Malawi hali yao kiuchumi ni mbaya sana

Tanzania tuko vizuri sanaa kuliko Malawi au ni yale yale kasoro watanzania wamezoea umasikini na ni wavumilivu, neenda vijijini ujionee umasikini wa Tanzania dar isukudanganye.
Hata huko dar maskini ni wengi
 
Sijui ni sababu ya nchi kuongozwa na upinzani au kitu gani.
Sababu HH wa Zambia anasema anajaribu kuziba matatizo yaliyo achwa na chama tawala ndio maana hali ngumu.
Au labda ndio siasa tu.

Sijui ni sababu ya nchi kuongozwa na upinzani au kitu gani.
Sababu HH wa Zambia anasema anajaribu kuziba matatizo yaliyo achwa na chama tawala ndio maana hali ngumu.
Au labda ndio siasa tu.
Siasa tu , mzigo wa duka sasa ukitaka chukua hapo malawi
 
Mi nadhani ungeanza na nchi yako kwanza...
Jana nimetoka mizungukoni nimewachukulia wanangu baadhi ya vitu wanapenda kula....nikaachana na daladala nikaingia kwa bajaji...kumbe Kuna zogo kati ya bajaji na daladala...mi nimo ndani wanarushiana maneno,nikamwambia tuondoke,anaondosha bajaji huku anaendelea na kamdomo....wakaanza kimbizia bajaji,dereva bajaji nae akaanza kukimbiza bajaji kama vile anakimbia kwa miguu,yaan ile unakimbia huku na kule ili usikamatwe...Mara ghafla kaparamiana na pikipiki iliyobeba trey za mayai....kibajaji kinataka kulala mi nikaruka...vitu vyangu vilisambaratika ...badala ya kusaidia watu wakaanza kuokota na kubugia bagia,wakaanza kuramba ubuyu....mayai wakazoa mpaka Ute wenye mchanga...bas ikabidi tujiinue sisi wenyewe🙌😔
 
Pole mkuu...hakuna majeraha ulipata?
 
Kila mtu ajiombee Kwa nafsi yake, Tanzania yenyewe Ina shida nyingi uanze kuiombea nchi nyingine kweli?
 
Huo ni umasikini au vinasaba vya wizi wa watanzania?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…