Tuwatumie wafungwa/Magereza kuzalisha chakula cha wanafunzi na chakula kiwe bure kwa shule zote

Tuwatumie wafungwa/Magereza kuzalisha chakula cha wanafunzi na chakula kiwe bure kwa shule zote

MC RAS PAROKO

JF-Expert Member
Joined
Feb 14, 2013
Posts
623
Reaction score
606
Nitaandika kwa kifupi sana kwa kuwa hii ni hoja isiyo hitaji maelezo mengi. Hoja yangu ya msingi ni hii Badala ya serikali kuwafungia ndani wafungwa na kuwatumia kufanya usafi mara moja kwa wiki tuwatumie wafungwa hawa kuzalisha chakula cha wanafunzi mashuleni na kitolewe bure pia, kwa wanafunzi wote.

Serikali itenge mashamba ya shule kila wilaya Nchi nzima na mashamba hayo yahudumiwe na magereza yaliyopo katika wilaya husika.

Hii itasaidia kupatikana kwa chakula cha uhakika kwa wanafunzi wanaosoma katika shule za kutwa katika wilaya husika na kuwaondolea wanafunzi adha ya kurudi nyumbani kula mchana au kushinda na njaa shuleni kwa sababu kama tujuavyo sote ukiwa na njaa ni ngumu kuweza kutuliza akili uelewe unachofundishwa.

Pia wazazi wanaotozwa pesa kwa ajili ya chakula cha watoto wao katika baadhi ya shule watakua wamesaidika na wataweza kukidhi mahitaji mengine ya kielimu kwa watoto wao kama vitabu n.k

Kwa upande wa magereza itawasaidia kuongeza uwajibikaji na pia kuwasaidia kujifunza kushirikiana na wenzao na pia njia bora za kilimo ambazo zitawasaidia pindi warudipo uraiani wajue nini cha kufanya ili wabaki kuwa raia wema kwa kipindi chote cha maisha yao.

Na mwisho wa yote JAMII nzima itakua imefanikiwa kwa kuwa watoto watafanya vizuri shuleni,wazazi watapunguziwa gharama za kuwasomesha watoto wao na serikali itakua imewalisha wanafunzi bila gharama yeyote kubwa.

Ni aibu leo mfungwa anauhakika wa milo mitatu kwa siku huku mwanafunzi tunayeamini ndo future yetu hawana uhakika wa kupata milo mitatu. Yaani tunawajali wafungwa zaidi ya kizazi cha kesho.
 
Umewahi kupata nafasi ya kuwa mfungwa

Je umewahi kukaa hata mahabusu ukajua mateso ya kukaa sehemu moja?

Usije ukawa hujawai hata kuhojiwa na police
 
Ni Jambo jema ukishika jembe wewe uliyehuru huru kwaajili ya matumbo ya watoto wetu.

Kama sisi tulio huru huku uraiani tunashindwa kuwalisha Hawa watoto Basi hakuna sababu ya msingi ya kuwapa mzigo huu wafungwa.
 
Umewahi kupata nafasi ya kuwa mfungwa

Je umewahi kukaa hata mahabusu ukajua mateso ya kukaa sehemu moja?

Usije ukawa hujawai hata kuhojiwa na police
Nadhani ili kuwapunguzia wafungwa hayo mateso ya kukaa sehemu moja hii itakua zaidi ya activity kwao kwa sababu watakua wanatoka kwenda mashambani.
 
Kuwa tu mfungwa ni adhabu tosha, kutaka kuwageuza wafungwa ma tractor sio uugwana
 
Ni Jambo jema ukishika jembe wewe uliyehuru huru kwaajili ya matumbo ya watoto wetu.

Kama sisi tulio huru huku uraiani tunashindwa kuwalisha Hawa watoto Basi hakuna sababu ya msingi ya kuwapa mzigo huu wafungwa.
Ukishika jembe wewe uliye uraiani na mfungwa akishika kwa upande wake uzalishaji utakua x2
 
Kuwa tu mfungwa ni adhabu tosha, kutaka kuwageuza wafungwa ma tractor sio uugwana
Nakubaliana na wewe ila sikuwa na lengo la wao watumike kama tractor.. Ni kulima kama wanavyofanya vijana wakiwa JKT.
 
Adhabu wanazopewa zinawatosha.

Unless otherwise una lako jambo.
Hizo adhabu ni mateso tu wanapewa na hazina msaada wowote kwa jamii.. pia sina lengo la kuwaumiza ila ni katika hali ya kutaka wawe na mchango chanya ktk jamii.
 
Nadhani ili kuwapunguzia wafungwa hayo mateso ya kukaa sehemu moja hii itakua zaidi ya activity kwao kwa sababu watakua wanatoka kwenda mashambani.
Mkuu kuna wakati unaweza kuona wafungwa ni binadamu tofauti na wewe ila nao hawapendi kuwa ile sehemu

Kuwatumia sio mbaya ila sio kwa unavyo fikiria
 
Kila mfungwa apewe shamba lake alitunze mpaka mavuno, mavuno wagawane yeye na magereza kwa uwiano unaofaa. Sehemu ya mavuno yake iuzwe hela zao wawekewe kwenye account zao zitawasidia cku wakitoka
 
Nitaandika kwa kifupi sana kwa kuwa hii ni hoja isiyo hitaji maelezo mengi. Hoja yangu ya msingi ni hii Badala ya serikali kuwafungia ndani wafungwa na kuwatumia kufanya usafi mara moja kwa wiki tuwatumie wafungwa hawa kuzalisha chakula cha wanafunzi mashuleni na kitolewe bure pia, kwa wanafunzi wote.

Serikali itenge mashamba ya shule kila wilaya Nchi nzima na mashamba hayo yahudumiwe na magereza yaliyopo katika wilaya husika.

Hii itasaidia kupatikana kwa chakula cha uhakika kwa wanafunzi wanaosoma katika shule za kutwa katika wilaya husika na kuwaondolea wanafunzi adha ya kurudi nyumbani kula mchana au kushinda na njaa shuleni kwa sababu kama tujuavyo sote ukiwa na njaa ni ngumu kuweza kutuliza akili uelewe unachofundishwa.

Pia wazazi wanaotozwa pesa kwa ajili ya chakula cha watoto wao katika baadhi ya shule watakua wamesaidika na wataweza kukidhi mahitaji mengine ya kielimu kwa watoto wao kama vitabu n.k

Kwa upande wa magereza itawasaidia kuongeza uwajibikaji na pia kuwasaidia kujifunza kushirikiana na wenzao na pia njia bora za kilimo ambazo zitawasaidia pindi warudipo uraiani wajue nini cha kufanya ili wabaki kuwa raia wema kwa kipindi chote cha maisha yao.

Na mwisho wa yote JAMII nzima itakua imefanikiwa kwa kuwa watoto watafanya vizuri shuleni,wazazi watapunguziwa gharama za kuwasomesha watoto wao na serikali itakua imewalisha wanafunzi bila gharama yeyote kubwa.

Ni aibu leo mfungwa anauhakika wa milo mitatu kwa siku huku mwanafunzi tunayeamini ndo future yetu hawana uhakika wa kupata milo mitatu. Yaani tunawajali wafungwa zaidi ya kizazi cha kesho.
Tungewatumia tu wabunge mana mishahara yao na marupurupu hayana kodi.
 
Nakubaliana na wewe ila sikuwa na lengo la wao watumike kama tractor.. Ni kulima kama wanavyofanya vijana wakiwa JKT.
Sidhani Kama unafahamu unachokisema!nani aliekuambia wafungwa wanakula Milo mitatu?afu unajua sasa hivi magereza inajilisha !wafungwa wanafanya kazi Kama mashine
 
Mkuu umewaza vyema ila jiulize swali dogo tu, kama wafungwa watalima na mazao baada ya kuvunwa yanapelekwa mashuleni unafikiri chakula chao watapata wapi. Namaanisha chakula cha wafungwa kitatoka wapi ?.

Yaani mtoto wako asome shule lakini unataka wajibu wa kupatikana chakula chake afanye mtu mwingine, tena umeenda mbali na kugusa wafungwa kabisa.

Learn to have some consideration about what people are experiencing, don 't leer what others are experiencing
 
Back
Top Bottom