Tuzo za Muziki Tanzania 2021, Bado tuna safari ndefu sana

Tuzo za Muziki Tanzania 2021, Bado tuna safari ndefu sana

Mama ndio kawapa nafasi ya kupumuwa sasa hivi kinakukera nini?

Lile hibirisi la Chato ndio ulikuwa unalipenda?
Sio kila mtu atampenda huyo bibi yako, kama ambavyo wewe unamchukia yule ibilisi ndovyo jinsi ambayo wengine wanamchukia huyo changu.
 
wasanii wengi wana uchumi mdogo sana hii imewafanya kuishi maisha ya kinafiki na kujipendekeza, kwa akili ya kawaida tu kuna vitu vingi tu walitakiwa kuvikataa/gomea kuhusu hizo tuzo.

Nawapongeza wasanii waliozigoea hizi tuzo, waliozikataa na wale waliojaribu walau kutoa constructive criticisms waziwazi, ujue kuna muda mtu unafigt battle lako gumu halafu mtu mwingine anataka kukuhusisha kwenye ujinga ujinga wake.

Kusema kweli nimewaelewa walio gomea hizi tuzo kwakweli hizi ntuzo kuanzia maandalizi au sherehe ya utoaji haikuwa nzuri kabisa kabisa hivi kweli ile sherehe kwanini iligeuzwa ukumbi wa siasa na mapambio? Hivi kulikuwa na ulazima wa kuwa na tunzo nne za heshima?

Ukumbi uliochaguliwa haukuendana na tukio husika kimsingi ilibidi sherehe ifanyike mlimani city kulingana na design ya ukumbi ulo wa jana ulifaa sherehe ya mabadiliko ya katibu au kongamano!

Watu wa vyombo hawakujipanga kabisa kabisa!


Kwakweli pamoja zimerudi ila zilikuwa mbaya hazina mvuto!
 
Nadhani issue kupoa ni mpangilio mzima wa event haswa peformance, celebrities walikuwa wachache hasa powerful names kama wema ambao wangewatumia kugawa Tuzo ingekuwa na vibe zaidi

Kuhusu WCB sidhani kama wangeleta kitu kikubwa sanaaaaaa, nakumbuka last year kulikuwa na miss East Africa na wenyewe ndio walikaa mbele na major peformer alikuwa mbosso lakini issue mzima ilibuma.

Kikubwa nadhani labda wangeongeza msisimko Tu hasa kama Zuchu angeingia maana this year kafanya vizuri sana, labda na Diamond na Mbosso. The rest sidhani kama wangeleta impact kubwa sana kuzidi uwepo wa Ali kiba, Marioo, Konde na Mbosso
Uwepo wa Diamond na Rayvanny bila hata ya kuwa na ngoma ungeongeza kitu kikubwa sana, Zuchu angebadilisha sana matokeo ya awards na Diamond pia.
 
Ni Tanzania Pekeee Ambako Serikali Inaandaa Tuzo [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23].

Hizi ni Kazi za Makampuni Mbali mbali Ya mziki, Taasisi Mbalimbali zisizo za kiserikali.

Wizara Kuandaa Tuzo ni Kukosa Ubunifu, Uelewa wa Viongozi, Na Kutokuwa na Viongozi wenye Akili.

Hii ni Kukurupuka Kuona Unatuzo Nchi kwako Kumbe sio. Toka Lini Serikali Ikaandaa Tuzo zake kama Walivyo Fanya Tanzania?

Mwisho wa siki wanasahau kilicho wapeleka wanafanya Siasa Kuliko Mziki Wenyewee

Ni Kama Siku Ya Ufunguaji Kampeni tuuu

Tanzania Tuna Makampuni Makubwa ambayo yangeweza kuandaa hizi tuzo.

Wizara ilipaswa kwenda kuzungumza na haya Makampuni Ambayo Wasanii wanatangaza kuona namna wanavyoweza kuandaa Tuzo mbalimbali na kuwapa Heshima Vijana wetu lakini sio Serikali kuchukua kila kitu na Kukifanya, Hapo Hela za Walipa Kodi Zitarudi Vipi?

Pamoja na Vitu Kupanda Bei bado serikali inachukua kidogo tulicho Nacho Kwenda Kuweka kwenye tuzo ambako hakuna Return Yake, Badala ya Kampuni Binafsi kufanya hili na kupata Airtime.

Hii Wizara Ime Fail Big Time. Tanzania Tuna Viongozi wa Ajabu sanaaaa walio Jaaa Ubinafsiiiiiii na Ubinafsi wa Viongozi Wa Tanzania Unatokana na Ugumu wa maisha walio lelewa wakiwa watoto na umaskini waliokulia kuamini kuwa ukiwa mbinafsi una Save for future kumbe ujinga Tuuuu. Hakukua Na Haja ya Wizara kushikilia Bango hili kazi ya wizara ilikuwa ni kutafuta wadau wanao weza kuendesha hizi tuzo na zingine nyingiii, Ipo Siku Wizara itadhamini Ligi Kuu Tanzania Tunako Elekea.
 
Tuzo ni heshima, ukiangalia hata profile ya msanii ili ujue alikuwa mkubwa kiasi gani wanaangalia mauzo ya album na Tuzo. Pia Kuna pesa huwa inatolewa kwa kila category
Kwahiyo mabeyo na sasha watalipwa?
 
Back
Top Bottom