Twendeni msibani Monduli - Arusha: zaidi ya ng'ombe 100 watachinjwa na kuliwa nyama kwenye msiba wa Laigwananani Edward Ngoyai Lowassa

Twendeni msibani Monduli - Arusha: zaidi ya ng'ombe 100 watachinjwa na kuliwa nyama kwenye msiba wa Laigwananani Edward Ngoyai Lowassa

Hii ni kali kwelikweli, sijawahi ona ng'ombe wengi kiasi hiki (zaidi ya 100) kwenye msiba mmoja na wenye afya kama hawa wakichinjwa kuliwa nyama msibani..

Bila shaka Arusha, Manyara na Kilimanjaro yote inahamia Monduli kwenda kula nyama na kumwaga Mzee Edward Ngoyai Lowassa...
hakuna mtu atashangaa maana sehemu ulizotaja arusha moshi manyara kwakweli nyama ni kama jadi nenda kwa morombo na kisongo ukaone watu wanavyokula nyama
 
Jamaa angu tafuta hela uwe unakula nyama ya kutosha ,ukienda buchani kata kilo hivi virobo robo na mishikaki achana navyo.
 
Acha ulaku wewe utapigwa zongo kwa kuendekeza tumbo.
Zongo?
Ngumi tena hadharani uangukie huko ukiwa chali we nenda kapeleke kisabengo chako uchezee mambata, maana kuna watu mnajifanya vichwa vibovu pasipotaka utani mnaleta utani unakutana na mtu hapendi utani anakuchakaza
 
Yaan nauli from dsm to Arusha zaidi ya 40'000 plus kurudi ili kufata nyama??

R.i.p Lowassa
Eeh, unafuata nyama. Hata hivyo si tunaenda kuzika pia, au?

Na si unajua nyama za kushea, mnakula na wengi ni poa sana kuliko kula peke yako nyumbani?
 
Kama wangesema kila atayefika atapewa ngo'mbe wake mmoja, tungesafiri
Msibani huwa tunakwenda kufariji, kumzika marehemu, na baada ya hapo tunakula nyama na misosi mingine...

Msibani huwa hutuendi kugawiwa ng'ombe au bia au soda ili uende nazo nyumbani kwako jombaa!!
 
Umasikini ni kitu kibaya sana....kama katika maisha yako chakula ni kitu kinakusumbua Sana kupata au ukiona unaenda kwenye sherehe etc ili ule basi jitathimini sana kimaisha. Yaan hapo unaweza nunuliwa kwa ajili ya chakula..
Ndugu sportstore shida yako ni nini kwani?

Chakula cha msibani kina uhusiano gani na ishu ya umasikini unayoitaja hapa?

Please, don't be so naive to that extent..

Huo ni msiba. Kwa jadi ya Kitanzania, msibani huwa tunakula..

By the way, ng'ombe zaidi 100 kila mmoja akiwa na kilo zaidi ya 250 unafikiri zitaliwa na nani kama msipoenda?

Kama uko karibu na una nafasi nenda msibani wewe. P..

Acha fikra zako za kishamba hapa..!!
 
Hii ni kali kwelikweli, sijawahi ona ng'ombe wengi kiasi hiki (zaidi ya 100) kwenye msiba mmoja na wenye afya kama hawa wakichinjwa kuliwa nyama msibani..

Bila shaka Arusha, Manyara na Kilimanjaro yote inahamia Monduli kwenda kula nyama na kumwaga Mzee Edward Ngoyai Lowassa...
Mkae kwa kutulia msije pigwa ngumi ya mwendo kasi hahaha
 
Nyie hamjui, nyama ya msibani tamu sana.

Mimi sipendi Maharage Iła nikiyakuta msibani nayala vizuri sana
 
Hii ni kali kwelikweli, sijawahi ona ng'ombe wengi kiasi hiki (zaidi ya 100) kwenye msiba mmoja na wenye afya kama hawa wakichinjwa kuliwa nyama msibani..

Bila shaka Arusha, Manyara na Kilimanjaro yote inahamia Monduli kwenda kula nyama na kumwaga Mzee Edward Ngoyai Lowassa...
Aisee! Twende kisa kuna Ng'ombe 100 wanachinjwa? Anayekwenda kwenye msiba aende kwa lengo la msiba na kwasababu kuna nyama
 
Msibani huwa tunakwenda kufariji, kumzika marehemu, na baada ya hapo tunakula nyama na misosi mingine...

Msibani huwa hutuendi kugawiwa ng'ombe au bia au soda ili uende nazo nyumbani kwako jombaa!!
🤣 unakua serious sana, hoja iliyotolewa kuna ngo'mbe kama 100 watachinjwa, so watu wa mikoa jirani watamiminika
 
Hii ni kali kwelikweli, sijawahi ona ng'ombe wengi kiasi hiki (zaidi ya 100) kwenye msiba mmoja na wenye afya kama hawa wakichinjwa kuliwa nyama msibani..

Bila shaka Arusha, Manyara na Kilimanjaro yote inahamia Monduli kwenda kula nyama na kumwaga Mzee Edward Ngoyai Lowassa...
Wamechinjwa na nani isije ikaleta taharuki tena kama miaka fulani hapo nyuma
 
Back
Top Bottom