Ubaguzi wa rangi ni mzizi wa umaskini wa Wamarekani wenye asili ya Afrika

Ubaguzi wa rangi ni mzizi wa umaskini wa Wamarekani wenye asili ya Afrika

ldleo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
1,116
Reaction score
1,121
VCG111316554657.jpg

Katika sehemu ya mashariki ya mji wa Detroit nchini Marekani, kupitia picha za satelaiti, tunaweza kuona ukuta unaotoka kaskazini hadi kusini na kupitia mitaa minne, ambapo umetenganisha sehemu ya watu weupe na sehemu ya watu weusi. Katika nchi hii ambayo siku zote inadai kutetea haki na usawa, kuna dunia mbili tofauti, dunia tajiri ya Wamarekani weupe, na dunia maskini ya Wamarekani Weusi. Wachambuzi wa Marekani wanasema chanzo cha umaskini wa Wamarekani wenye asili ya Afrika ndio ubaguzi wa rangi.

Ripoti ya kila mwaka kuhusu hali ya haki za binadamu ya Wamarekani wenye asili ya Afrika iliyotolewa hivi karibuni na Shirikisho la Miji la Marekani ilieleza kwamba, Wamarekani wenye asili ya Afrika wana “asilimia 73.9 tu ya fursa za wazungu”, na hawana haki sawa na watu weupe katika kupata utajiri, afya, elimu na mambo ya kisiasa. Data za uchunguzi kuhusu hali ya kifedha ya wateja nchini Marekani zinaonyesha kuwa, wastani wa mali za familia ya Wamarekani weupe ni mara nane kuliko familia ya Wamarekani weusi. Wastani wa mali za familia ya watu weupe ni dola 983,400 za kimarekani, huku wastani wa mali za familia ya watu weusi ukiwa dola 142,500 tu za kimarekani.

Suala la ardhi ni chanzo kingine muhimu cha umaskini wa Wamarekani wenye asili ya Afrika. Ripoti iliyotolewa tarehe 3 Mei na Shirika la Habari la Uingereza Reuters inasema, wakulima wenye asili ya Afrika nchini Marekani walipoteza takriban ardhi zenye thamani ya dola bilioni 326 za kimarekani katika karne ya 20 kutokana na sera za ubaguzi wa rangi. Kuanzia mwaka 1922 hadi 1997, mashamba ya kilimo ya wakulima weusi katika majimbo 17 nchini Marekani yalipungua kwa kiasi kikubwa kutokana na “vitendo vya kimabavu vilivyoungwa mkono na serikali”, pamoja na sera ya ubaguzi wa rangi ya mikopo na hatua ya kuwalazimisha watu weusi kuuza mashamba yao.

Takwimu za Sensa iliyofanywa na Wizara ya Kilimo ya Marekani zinaonesha kuwa, mwaka 1910, wakulima wenye asili ya Afrika nchini humo walikuwa wanamiliki mashamba zaidi ya ekari milioni 16, ikiwa ni asilimia 14 ya mashamba yote ya kilimo nchini Marekani. Lakini hadi kufikia mwaka 2017, wakulima weusi walikuwa wanamiliki mashamba ekari milioni 4.7 tu. Hivi leo ni asilimia 1 tu ya watu weusi wanaomiliki mashamba nchini Marekani, ambao wanamiliki asilimia 0.1 tu ya mashamba ya kilimo ya nchi hiyo.

Ubaguzi wa rangi ulioendelea kwa miaka mingi nchini Marekani umesababisha ukosefu wa haki katika nyanja mbalimbali na kuchangia umaskini wa Wamarekani wenye asili ya Afrika. Marekani siku zote inajidai ni mlinzi wa usawa na haki duniani, lakini kama haiwezi kuondoa ubaguzi wa rangi kwenye nchi yake yenyewe, haitaaminiwa na jumuiya ya kimataifa.
 
Nawaza tu, hizo Billions za dola Marekani waazowapa Ukraine zingeweza kufuta hali hii ya umaskini kwa raia wao weusi kwa kiwango kikubwa.
Wewe ongelea matumizi ya kodi yako unayotoa hapa nchini kwako kwani hapa wewe unaona kodi tunayolipa inatumika vizuri.

Kuna rais moja alisema wakazi wa Kimara wabomolewe nyumba zao bila kujali kwamba mahakama iliamuru ubomoaji usitishwe hadi kesi isikilizwe na wakati huo huo akiamuru watu wa Mwanza wasibomolewe kwani alidai walimpigia kura.

Je, huo haukuwa ubaguzi? Au kwa kuwa huyo rais hakuwa mzungu basi hiyo haipaswi kuitwa ubaguzi. Lazima tukubali ukweli kwamba sisi watu weusi hakuna sehemu tusipobaguliwa ktk dunia hii.

Lakini kibaya zaidi sisi wenyewe tunabaguana kuliko hata tunavyobaguliwa na watu weupe. Hapa hapa Tanzania ukijulikana kwamba wewe ni Chadema kuna haki nyingi huwezi kupata na kubambikiwa kesi ya uongo kwako ni jambo la kawaida kama sio kuuwawa kabisa.

Umefika wakati tuache unafiki, ubaguzi uko popote ila kwetu watu weusi imekuwa too much ila tu sisi tuna hulka ya unafiki sana.
 
Wewe ongelea matumizi ya kodi yako unayotoa hapa nchini kwako kwani hapa wewe unaona kodi tunayolipa inatumika vizuri.

Kuna rais moja alisema wakazi wa Kimara wabomolewe nyumba zao bila kujali kwamba mahakama iliamuru ubomoaji usitishwe hadi kesi isikilizwe na wakati huo huo akiamuru watu wa Mwanza wasibomolewe kwani alidai walimpigia kura.

Je, huo haukuwa ubaguzi? Au kwa kuwa huyo rais hakuwa mzungu basi hiyo haipaswi kuitwa ubaguzi. Lazima tukubali ukweli kwamba sisi watu weusi hakuna sehemu tusipobaguliwa ktk dunia hii.

Lakini kibaya zaidi sisi wenyewe tunabaguana kuliko hata tunavyobaguliwa na watu weupe. Hapa hapa Tanzania ukijulikana kwamba wewe ni Chadema kuna haki nyingi huwezi kupata na kubambikiwa kesi ya uongo kwako ni jambo la kawaida kama sio kuuwawa kabisa.

Imefika wakati tuache unafiki, ubaguzi uko popote ila kwetu watu weusi imekuwa too much ila tu sisi tuna hulka ya unafiki sana.
Acha povu toa hoja zinazo eleweka ameuliza kwann hela anazo tumia Marekani kuchochea vurugu duniani asizitumie kuboresha maisha ya raia wake wanao teseka na umasikini?

Sent from my TECNO BB4 using JamiiForums mobile app
 
Jamii zote duniani zingelikua kama waarabu tungefika mbali sana,,,watu hawa asikuambie mtu aise,,ni watu wa aina yao usiomithilika, ni watu wakarimu, wana imani, labda wachache tu wako tofauti, tena mmoja mmoja.

Na huwezi kuwaona waarabu wamewatupia miganda ya ndizi, chupa au kuwafananisha na sokwe,lakini pamoja na haya yote bado waarabu+waisilamu wanaonekana wabaya.

Chuki hazijengi bali zinabomoa

So,,Endeleeni kuwaabudu hao wazungu na mayahudi,,, mtajuta.
 
Aise bora ubaguliwe uko state na wazungu kuliko Hawa weusi wenzetu ccm wao ubaguzi wao ni kukuchuna Kila kitu ulichonacho imradi matumbo Yao yanashiba. Na shida ya tumbo halina aibu, leo linashiba kesho linataka Tena.
 
USA inaitwa land of the dreams, yani hata ukawa dereva wa Uber ama mfanyikazi McDonalds ni rahisi kutimiza ndoto zako. Tatizo la watu weusi USA ni uzembe, mihadarati na kukosa elimu, kila kitu kipo ila wamechagua hayo maisha wenyewe.
Alafu hao black Americans ni wabaguzi sana kwa waafrika kutoka barani, ukiwaona huko achana na wao kabisa wanaweza kukuua, Akon alipohamia huko kutoka Senegal alitengwa sana
 
Wewe ongelea matumizi ya kodi yako unayotoa hapa nchini kwako kwani hapa wewe unaona kodi tunayolipa inatumika vizuri.

Kuna rais moja alisema wakazi wa Kimara wabomolewe nyumba zao bila kujali kwamba mahakama iliamuru ubomoaji usitishwe hadi kesi isikilizwe na wakati huo huo akiamuru watu wa Mwanza wasibomolewe kwani alidai walimpigia kura.

Je, huo haukuwa ubaguzi? Au kwa kuwa huyo rais hakuwa mzungu basi hiyo haipaswi kuitwa ubaguzi. Lazima tukubali ukweli kwamba sisi watu weusi hakuna sehemu tusipobaguliwa ktk dunia hii.

Lakini kibaya zaidi sisi wenyewe tunabaguana kuliko hata tunavyobaguliwa na watu weupe. Hapa hapa Tanzania ukijulikana kwamba wewe ni Chadema kuna haki nyingi huwezi kupata na kubambikiwa kesi ya uongo kwako ni jambo la kawaida kama sio kuuwawa kabisa.

Imefika wakati tuache unafiki, ubaguzi uko popote ila kwetu watu weusi imekuwa too much ila tu sisi tuna hulka ya unafiki sana.
Ukipiga ugali mkubwa na dagaa hua toa maoni mazuri, tatizo ukiwa na njaa unaharibu.
 
Jamii zote duniani zingelikua kama waarabu tungefika mbali sana,,,watu hawa asikuambie mtu aise,,ni watu wa aina yao usiomithilika, ni watu wakarimu, wana imani, labda wachache tu wako tofauti, tena mmoja mmoja.

Na huwezi kuwaona waarabu wamewatupia miganda ya ndizi, chupa au kuwafananisha na sokwe,lakini pamoja na haya yote bado waarabu+waisilamu wanaonekana wabaya.

Chuki hazijengi bali zinabomoa

So,,Endeleeni kuwaabudu hao wazungu na mayahudi,,, mtajuta.
Wewe utakua umeolewa na waarabu..la wanakulisha.

#MaendeleoHayanaChama
 
Pia watu weusi huko wavivu sana wanachojua ni muziki,bata,vitu vya anasa cheni sijui nini..

Wazungu wajanja walipeleka watoto wao shule then waafrika weusi wakawasukumia kwenye basketball,muziki ili watoto wao waendelee kushika system huku waafrika wakiishia kwenye muziki wengine wanapata utajiri lakini anaishia kwenye madawa nk.
 
Acha povu toa hoja zinazo eleweka ameuliza kwann hela anazo tumia Marekani kuchochea vurugu duniani asizitumie kuboresha maisha ya raia wake wanao teseka na umasikini?

Sent from my TECNO BB4 using JamiiForums mobile app
Ndio nimesema ya Marekani yanakuhusu nini kwani nchini kwako hamna watu maskini.?
 
Kuwa fukara USA ni kujitakia nobody will tell me otherwise.

Bado ndo nchi yenye fursa kuliko nchi yeyote ile kwa mtu yeyote yule.

Naijua Detroit vizuri na viunga vyake hadi Benton Harbor kule South of Michigan kama navyoijua Mwanjelwa na Uyole tu. Ni kweli kuna baadhi ya maeneo yamechoka sana tu, Detroit has become a ghost city baada ya viwanda vya magari kuhama mji kama mnavyojua it was once a motor city ila bado hiyo haitoshi kukufanya mtu uwe maskini US.

Unemployment rate US sahizi ni 3.6% wakati huo huo makampuni yote sahizi yanatafuta wafanyakazi, kila sehemu ukipita kuna bango la "We're Hiring" from Google to Apple to Mcdonalds to kampuni za usafi na kutunza wabibi. Unakosaje kazi kwa mfano?

Kuwa fukara US ni kujitakia.

 
Pia watu weusi huko wavivu sana wanachojua ni muziki,bata,vitu vya anasa cheni sijui nini..

Wazungu wajanja walipeleka watoto wao shule then waafrika weusi wakawasukumia kwenye basketball,muziki ili watoto wao waendelee kushika system huku waafrika wakiishia kwenye muziki wengine wanapata utajiri lakini anaishia kwenye madawa nk.
Hata miye huwa nashangaaa aisee

Ni muziki,basketball,mihadarati na ugangstar tu
 
Pia watu weusi huko wavivu sana wanachojua ni muziki,bata,vitu vya anasa cheni sijui nini..

Wazungu wajanja walipeleka watoto wao shule then waafrika weusi wakawasukumia kwenye basketball,muziki ili watoto wao waendelee kushika system huku waafrika wakiishia kwenye muziki wengine wanapata utajiri lakini anaishia kwenye madawa nk.
Hujajua systematic racism mzee..ukishajua utajua hasa kwanini wanakua hivyo weusi na hawana option zaidi ya ulizotaja.
 
Nawaza tu, hizo Billions za dola Marekani waazowapa Ukraine zingeweza kufuta hali hii ya umaskini kwa raia wao weusi kwa kiwango kikubwa.
Marekani ameshaona fursa ya kuvuna fedha zaidi ukiona hivyo.
 
Back
Top Bottom