Ubaguzi washika kasi ndani ya kanisa la Roma kama wa Afrika tufanye nini?

Sasa watu wasiofanana watakuwa vipi sawa,hata sisi tunaguana.
Wa masaki hawezi kaa meza moja na WA buza,wa mjini umuona wakuja mshamba
 
Hio video ubaguzi upo wapi hapo
 
Sasa watu wasiofanana watakuwa vipi sawa,hata sisi tunaguana.
Wa masaki hawezi kaa meza moja na WA buza,wa mjini umuona wakuja mshamba
Lakini hao hawajabaguana kwa rangi ya ngozi zao
 
Naam hapo umenena ✔️
 
Mtu mweusi ni duni kweli katika dunia hii kulinganisha na races zingine duniani

Ila kwanini wanajustify hilo?
 
Tangu zamani hizi dini nyemelezi za kigeni ni wabaguzi wawe wakristo au waislam. Nenda pwani uone waarabu wanavyooa binti zetu wazuri lakini wao wanawaficha wao arabuni wanapogeuza machangu kuliko kuolewa na waswahili. Sikumbuki Yesu kuwa na mfuasi mweusi japo aliponea Misri. Muhammad naye alikuwa na Bilal ambaye hakumgeuza swahaba bali kuku wa kuadhini. Ni ubaguzi mtupu.
 
Hujui usemalo. Tuliozalia watoto ulaya, watoto hawana hii kitu bali wazazi ndiyo wanaowagawanya kwa woga na unafiki wao. Hata waafrika tuna ubaguzi wa kulishwa. Mfano, muislam anambagua mkristo wakati wote ni wamakonde. Upuuzi na utumwa mtupu. Mchaga atakwambia yeye ni bora kuliko mpare. Mkurya ndo usiseme. Ushenzi mtupu. Mzaramo na wazenj ambao ni watoto wa watumwa waliotoka bara watakwambia wewe ni mbara utadhani waliandika maombi kuzaliwa pwani. Hivi kweli na kimanzichana ni pwani au kibaha? Hata kariakoo si pwani.
 
Tujilaumu wenyewe. Kwani hao wazungu ndiyo waliowafundisha waswahili kuvumilia ubaguzi wa kihindi na kiarabu nchini kwetu au utumwa wa akili na kujikana baada ya kupachikwa imani na majina yao?
 
Sawa tuliletewa dini, kwani kanisa katoliki kwa ukuu wake duniani ina maana halina mafundisho ya kupinga ubaguzi katika mahubiri yake ikiwa Mungu hana ubaguzi?
Kanisa halikuleta ushenzzziiii na utumwa tu bali lilikuja kupeleleza ili tutawaliwe na kunyakua ardhi yetu na kutufanya mataahira waliojikana na kila kitu chao. Huoni wanavyofiiiira watoto kila mahali duniani.
 
Uongo mkubwa
 
Ni kumfuata tu Yesu kristo ,tuachane kabisa na haya madhehebu ya kikristo yana ujinga mwingi sana
Huyo Yesu ndie mbaguzi nambari moja aliyesema hakuja kwa watu wengine bali kondoo waliopotea wa nyumba ya nani vileee? Malizia.

Kiufupi tunapokataa dini tunamaanisha kuwakataa mpaka hao Miungu wa uongo kama akina Yesu na baba yake mbingun huko wakina Yehova sjui nan na wakina Allah, hawa wote ni Miungu wa uongo waliotungwa na wazungu.

Ndiomaana dua zinazotegemea maombi ya hizi dini hazileti majibu sahihi tofauti na yale maombi walioomba babu zetu.

Ukimuomba Yesu magonjwa hayakomi, ukimuomba Allah mvua hainyeshi, ukimuomba Yehova huyu hasikii lolote kabisa utaumwa na kufa utakufa huyu Mungu mgeni hakusikii.

Hata hao wachungaji wenu wa uongo makanisani hawawaponyi kupitia huyo yesu wanaemuhubiri badala yake wana nguvu za kificho ambazo imebase kwenye mila za kiafrika tofauti na hayo maigizo wanayowahubiria.

Kiufupi mkatae Yesu na washirika wake na Mema ndipo yatakapo kujilia.
 
Suala la ubaguzi ni maamuzi ya mtu binafsi sio jamii nzima, mbona huyo nyuma anaefuatia kasalimiana na huyo mwafrika bila shida yoyote??
 
Wewe una matatizo. Kuna watu kama wanyarwanda ambao hukumbatiana na kuna watu kama watanzania huwa tunasalimiana kwa mikono. Tatizo lako ni kutaka kuharibu reputation aliyopata Kardinali Rugambwa na Kanisa katoliki. Ungejua ungenyamaza tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…