Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania watoa tahadhari ya uwepo wa tishio la shambulio la kigaidi

Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania watoa tahadhari ya uwepo wa tishio la shambulio la kigaidi

Binafsi tangu mikutano iruhusiwe nikawa nimekumbuka Yale mabomu ya mkutano wa chadema Arusha.

Ni kitu kili ni ijia kichwani.....

All in all Mungu ni mwema wakati wote
Wakati wote Mungu ni mwema
 
Mbona issue ya Garissa walionya na ikatick..... Tusipende ujuaji! wao Wana intelijensia kuliko nchi zetu maskini hizi sio sisi ikitokea mikutano ya Chadema ndio eti taarifa za intelijensia zinafanya kazi!!
Kwanini wasishirikiane na vyo7mbo vyetu vya usalama ili kudhibiti kuliko kuwatia wananchi hofu waishi bila furaha? Kauli zao tumesha zizoea, mfano Balozi wetu nchini Marekani atoe Taarifa kwa Watanzania na Raisa wa East Afrika wasitemblee Marekani kuna matishio ya watu kuuliwa kwa kupigwa Risasi unafkiri huyo Barozi wetu si angepewa Masaa 24 aondoke Marekani, Mabalozi kama awa ndiyo maana Magufuli alikuwa ana warudisha makwao uko.
 
Kwanini wasishirikiane na vyo7mbo vyetu vya usalama ili kudhibiti kuliko kuwatia wananchi hofu waishi bila furaha? Kauli zao tumesha zizoea...
Hiyo ni notice Kwa wazungu wenzao so ni kuwatahadharisha tu sio kwamba wamesema wasije.

Kushirikiana mbona kupo, si Kuna gaidi mwandamizi wa ISIS alipita Tz hapa ila TISS hawakumuona mpaka CIA ilipokuja kuwashtua.

So partnership ipo ila lazima alert itolewe watu wawe makini. Huku kwetu Kila kitu ni Siri maana wakitangaza wanaona ni kama wanakiri udhaifu hivi ila yakishatokea kama ya Hamza ndio tunaamka usingizini.
 
Crap.

Wenzio wana teknolojia ya kunasa mawasiliano yawe ya simu, internet, whatsap, etc.
kwani ni nani amekwambia hiyo teknolojia haipo hapa nyumbani komredi?! Mbona hayo mambo ni madogo sana kwa TISS Kiongozi?! Ongea vingine 😊
 
Ukuaji wa sayansi na teknolojia unatumiwa kiusalama vyema na wenzetu.

Kwa wenzetu uhai na usalama wa raia wao ndio kipaumbele cha kwanza, iwe ndani ya nchi zao au nnje ya nchi zao.
Ni vyema sana umemjibu huyo bwana kwa utu na uungwana... kuliko wenye kumshushua na kumbeza!

Mwenyezi mungu akubariki sana! 👊🏾👍🏾
 
Ukuaji wa sayansi na teknolojia unatumiwa kiusalama vyema na wenzetu.

Kwa wenzetu uhai na usalama wa raia wao ndio kipaumbele cha kwanza, iwe ndani ya nchi zao au nnje ya nchi zao.
Ni vyema sana umemjibu huyi bwana kwa utu na uungwana... kuliko wenye kumshushua na kumbeza!

Mwenyezi mungu akubariki sana!
Nilipo ni karibu na msikiti nikisikia ugaidi basi napataga mawazo sana na hawa maostadh hapa jirani
Hahaha! Gaidi sio maana yake hiyo iliyojengwa mawazoni mwako...

Gaidi ina maana yake. Soma na pekua usome kinagaubaga wa neno "terrorist" & "terrorism"

Linakuzwa kwa sababu ya chuki za kidini lakini si hao unaowaona wanajifanyia zao ibada ndo magaidi...hapana 😊
Soma! Chimbua maarifa... utapata mengi. 👍🏾
 
Watakuwa wali share hizo intel na vyombo vyetu kitambo, so magaidi kama bado wapo hai wafanye kuziaga familia zao kabisa, vyombo vyetu huwa havina mzaha kwenye ugaidi, ni risasi tu.
 
Ndugu neno security ni pana, unaweza kusoma wewe mpaka wajukuu zako na bado msimalize.
Kuna watu wanajua mpaka kilichopo akilini mwa watu wengine
Hapa umeongea la maana sana! Nakupa kongole

Ila kuna vijana wa hovyo ukiwaeleza hilo watakimbilia kusema umewadanganya... 😂😂😂
 
Hiyo ni notice Kwa wazungu wenzao so ni kuwatahadharisha tu sio kwamba wamesema wasije.

Kushirikiana mbona kupo, si Kuna gaidi mwandamizi wa ISIS alipita Tz hapa ila TISS hawakumuona mpaka CIA ilipokuja kuwashtua.

So partnership ipo ila lazima alert itolewe watu wawe makini. Huku kwetu Kila kitu ni Siri maana wakitangaza wanaona ni kama wanakiri udhaifu hivi ila yakishatokea kama ya Hamza ndio tunaamka usingizini.
Hamza ni nani na alifanya nini na sababu ya kufanya aliyoyafanya ilikuwa ni nini?!

Kumbe umekurupuka tu kuongea kwa mihemko... jibu hapo juu kuhusu Hamza na kwanini umemu-include hapa?!
 
Wacha wawabondee tujifunze, kama Uongoz mdhaifu hivi hata ulinzi lazma uwe dhaifu vile vile.

Hii nchi awamu hii tusipokuwa makin kuna mambo yatatokea na kuharibu maisha ya watu sababu ya uzembe wa uwajibikaji wa viongozi na wahusika.

Kuna mambo yanatokea nchin mpka mtu unajiuliza hivi wahusika wa kupambana na hizo issue huwa wanafanya kitu gani?

Ubalozi wa wamarekani kutoa hiyo alerts ni kwaajili ya kuwalinda raia wato tu, na sio wew mzawa, maana ilo ni jukumu lao , kila nchi kupitia balozi zake kuhakikisha maisha ya raia wa USA wako salama.

Hizo hizo ofisi za balozi wa USA huwa kama lango ama makao ya maafisa wa upelelezi wa USA, ambao kazi zao ni kukusanya taarifa wanazotaka kila nchi, kwa mfano baloz ya USA kwa TZ inaweza kuwa ina taarifa nying na za siri ambazo hata hao polisi wenu ama jeshi lenu halina why?

Sababu wao ndio wahusika wa technolojia zote za kiulinzi ikiwepo mawasiliano, pia taarifa za kila mienendo ya wageni wanaoingia na kutoka nchini hawa jamaa hujua, na ndiomaana mission zao nying hutiki.

Kutokea ama kutotokea kwa matukio hayo kutategemeana na reaction ya viongozi wetu na wahusika wa ulinzi wa taifa, na hivi tuna uongizi dhaifu basi tuombe sana uwajibikaji uwe mzuri, or otherwise imekula kwetu.

Hii nchi basi tu kuna mengi yanatendeka na kutokea kwakuwa ni siri basi acha ibaki kuwa siri, Vichwa panzi hawawezi kuelewa, maana wanapoona wanaamka salama na kuishi salama wanadhani na makusudi ama bahati kumbe kuna watu hawalali na ndio hao jasho lao na akili zao zinawafanya ama zinatufanya tuishi salama, hata wale wapumbavu wanaopenda kutukana Taasisi ya ulinzi nchini huwa nawaona washenzi maana hawajui mambo gan na mangapi yanazuiwa nchini, bila hivyo hii nchi ingekuwa makao ya wale wavaa mabomu na watetezi wa imani za hovyo hovyo kwa kuua raia kusingizia dini kumbe kuna milengo yao.

Tuweni macho.
 
Wacha wawabondee tujifunze, kama Uongoz mdhaifu hivi hata ulinzi lazma uwe dhaifu vile vile.

Hii nchi awamu hii tusipokuwa makin kuna mambo yatatokea na kuharibu maisha ya watu sababu ya uzembe wa uwajibikaji wa viongozi na wahusika...
Umesema:-
Wacha wawa bomoa, halafu mwisho umeandika - tuwe makini,-
Sijakuelewa!
 
Hawa USA kwenye kipengele hiki huwa hawakosei.....tukumbuke ya Kenya na Uganda
 
Back
Top Bottom