Ubalozi wa Marekani: Tumetiwa moyo na hakikisho la Rais Magufuli kwamba uchaguzi mkuu 2020 utakuwa huru, wa haki na wenye uwazi

Ubalozi wa Marekani: Tumetiwa moyo na hakikisho la Rais Magufuli kwamba uchaguzi mkuu 2020 utakuwa huru, wa haki na wenye uwazi

Na kwa kauli hiyo ya "Beberu mkuu" kumbe tume huru yaweza kuundwa muda huu kabla ya uchaguzi mkuu wa Octoba.
Kazi kwenu viongozi wote wa upinzani, kazi kwenu Wabunge na wananchi. Hapo ndio pa kukamatia na kwa kujitoa kwenu tutapata uchaguzi safi wa viongozi waliochaguliwa na wananchi wenyewe bila kujali ni wa chama gani.


Sent using Jamii Forums mobile app
Wapinzani wa sasa wamekaa kishamba sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hicho ni kipeperushi tu kama vipeperushi vingine!
Mimi nimeona 'kipeperushi' chenye 'background' ya mwewe kashikilia ngano kwenye mguu mmoja, na huo wa pili sijui kashika nini..., au ndio mkono unaotumika kuwarekebisha waliokengeuka?
 
Tamko hili ni kama agizo juu ya kauli aliyotoa Rais Magufuli juu ya uchaguzi mkuu wa 2020.

Hilo suala la Tume huru ya uchaguzi halijaingizwa hapo kwa bahati mbaya bali linaonyesha lina kusudio maalumu.

Haya US wamepiga kulia huku kushoto WB wametwanga kivingine.

Hakika mwaka huu kuna makubwa yaja tena yaja kisayansi kabisa.

View attachment 1341947

Sent using Jamii Forums mobile app


Ebu mkiwa na vichwa vyenu, muwe mnafikiri kabla ya kujazwa upepo upepo tu mtapasuka bure.. US yenyewe tume yao ni huru? Trump mwenyewe kaiba kura kielectroniki, so mambo ya kuwa mnatiana moyo kwa vitu vya kufikirika tu acheni. Kwa kazi kubwa ya kutukuka aliyofanya Mh. Rais Magufuli, hata umlete nani 2020 Mh. Rais atashinda kwa kura nyingi sana. Mm natabiri 90%+. Ila mambo ya kupewa matumaini sijui na ubalozi wa US, hiyo ni kiini macho, hivi kwanini mna vichwa kama vibuyu, you can't think deep kabisa.
 
Sio uongo hatuiwezi. Maana ukifurukuta hivi risasi, ukijigeuza kesi ya uhujumu, mkutano kidogo hata chumbani uchochezi!
Huku Muruto yuko na mbwa na virungu huku Mambosasa na bunduki hadi anaua wanafunzi kwenye mabasi!
Watu wafanyeje kama sio kumfuata Beberu na kumwambia mbona mbuzi "jike"wako anatumia pembe kujeruhi?

Sent using Jamii Forums mobile app
LOooh, hili jibu sidhani kama atakuwa na hamu ya kumeza chakula siku nzima leo.
 
Hatuwezi kuendelea kuongozwa kijuha namna hii.!!!
Naunga mkono tume huru ya uchaguzi ipatikane tu mapema.
Tumechoja! Tumechoka ! Tumechoka !




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na kuhusu WB, kwa nini tunang'ang'ania wakati tunawaita mabeberu, huku tukisema hizo taasisi zinatumika kutuumiza?

Kama tunavuka malengo ya makusanyo na tunafika trl 1 kila mwezi tangu awamu hii iingie madarakani huku tunabana matumizi, madaraja wafanyakazi hatupandishi, rushwa imedhibitiwa SASA kwanini tudhalilike tung'ang'anie mkopo wa trl 1? Hadi Bunge linalalamika sisi kukosa trl 1

Tunasema tunahela, matajiri lakini tunalilia trl 1 kwa ajili ya Elimu? Vipaumbele tuliweka nini? Ndege au Elimu?

mnaojiita Wazalendo inaingia akilini kweli?
Kama hata Marekani inadaiwa mikopo kutoka washitiri mbalimbali, nini cha ajabu kwa nchi ndogo km Tanzania kukop ama kudaiwa?
 
Kwa kazi kubwa ya kutukuka aliyofanya Mh. Rais Magufuli, hata umlete nani 2020 Mh. Rais atashinda kwa kura nyingi sana. Mm natabiri 90%+. Ila mambo ya kupewa matumaini sijui na ubalozi wa US, hiyo ni kiini macho, hivi kwanini mna vichwa kama vibuyu, you can't think deep kabisa.
Hii ndio sababu mhimu sana pawepo na tume huru ya uchaguzi; na nina hakika hata yeye Magufuli angefurahi sana kuupata ushindi wa aina hii usiokuwa na mawaa yoyote.

Lakini pamoja na kuwa na uhakika huo, hata wewe bado unahalalisha yasiyostahiri kama hapa chini
Ebu mkiwa na vichwa vyenu, muwe mnafikiri kabla ya kujazwa upepo upepo tu mtapasuka bure.. US yenyewe tume yao ni huru? Trump mwenyewe kaiba kura kielectroniki, so mambo ya kuwa mnatiana moyo kwa vitu vya kufikirika tu acheni.
Hata kama ingekuwa kweli kwamba Trump aliiba kura 'kielectronic', hakuna raia wake waliopigwa marungu/mabomu ya machozi; na kutishiwa uhai hadi wengine kuogopa kwenda kupiga kura!
 
M
Tamko hili ni kama agizo juu ya kauli aliyotoa Rais Magufuli juu ya uchaguzi mkuu wa 2020.

Hilo suala la Tume huru ya uchaguzi halijaingizwa hapo kwa bahati mbaya bali linaonyesha lina kusudio maalumu.

Haya US wamepiga kulia huku kushoto WB wametwanga kivingine.

Hakika mwaka huu kuna makubwa yaja tena yaja kisayansi kabisa.

View attachment 1341947

Sent using Jamii Forums mobile app
Mungu wabariki mabeberu.
 
Back
Top Bottom