Ngongo
Platinum Member
- Sep 20, 2008
- 20,654
- 35,887
Heshima sana wanajamvi,
Mbio za ubunge katika jiji letu la Arusha sasa zipo wazi kabisa kiasi kwamba hata kipofu ni rahisi kujua na kufahamu nani atashinda ubunge.
Mara baada ya Mheshimiwa Mrisho Mashaka Gambo kupitishwa na kamati kuu kugombea ubunge Arusha Mjini kulikuwa na sintofahamu kubwa miongoni mwa wanaCCM kindakindaki. Wengi walijiuliza kulikoni kamati kuu kupitisha jina la mgombea ambae tayari alishasemwa hadhani na mheshimiwa Rais na hata Katibu Mkuu wa CCM Taifa Dr Bashiru.
WanaCCM wengi walikubaliana pengine kamati Kuu iliangalia nani mwenye uwezo wa kushinda nafasi ya ubunge na kuviweka vigezo vingine kando ikiwemo tuhuma za rushwa, uchonganishi (kiwanja cha Msikiti Mkuu Bondeni), kukwamisha ujenzi wa stand mpya, kuhujumu ujenzi wa shule mbali mbali kwa kisingizio cha udogo wa viwanja na nk.
CCM iliamini na kujiaminisha kwamba Mrisho Mashaka Gambo angewavusha salama katika uchaguzi mkuu, hapakuwemo mgombea mwingine wa kumzidi yeye.
Katika hali ya kushangaza sana kama si kusikitisha Mrisho Gambo Mashaka amepwaya kweli kweli, zile amri zake za ukuu wa Mkoa hazifui dafu katika kuomba kura. Mrisho bila ngoma,mdundiko na wacheza show hawezi kufanya mkutano,Mrisho bila kukusanya watu toka kata mbali mbali za wilaya ya Arusha Mjini,Arumeru hawezi kufanya mkutano, Mrisho Gambo bila usaidizi wa Mkuu wa Wilaya, Mkuu wa Mkoa hawezi kufanya mkutano. Mrisho Gambo yuko hoi bin taaban kisiasa na kiuchumi. Matajiri wengi wamejiweka kando na kampeni zake hawataki kutoa fedha tena wanamwangalia kama gari bovu.
Zipo tuhuma sijui zimetoka wapi, sijui nani kazianzisha zimesambaa kwa kasi ya ajabu juu ya kuungua soko la Samunge loooh hata kuandika naogopa soko la Samunge ni kaa la moto si mtaji tena wa Mrisho.
Update leo 17/09/2020.
Sasa ni dhahiri mpasuko mkubwa ndani ya CCM yapo makundi matatu makuu.
Kundi la Gambo ambalo linaungwa mkono na Mwenyekiti wa UWT na Mwenyekiti wa CCM Mkoa Kamanda Msatahafu Zelote Steven.Kundi hili lilihakikisha jina la Gambo linarudi pamoja na kugubikwa na tuhuma nyingi za rushwa na matumizi mabaya ya madaraka ikiwemo kuwaweka mfukoni aliyekuwakuwa Mkuu wa TAKUKURU na RPC.Wakuu hawa wa vyombo vya dola walikuwa wakisimamia kwa karibu harakati zote za ushindi za Gambo.
Kundi la pili linaongozwa na Monaban,Kundi hili liliumizwa sana na Gambo wakati akiwa RC ikiwemo kuporwa biashara zake za nafaka (National Milling) kwa kisingizio alikuwa mtu wa E N Lowassa.Kwa hakika hapa ndipo kwenye mzizi mkubwa wa fitina.Monaban ana kundi kubwa sana nyuma yake.Huyu hakubali ahadi za kitoto anataka Gambo atupiliwe mbali.
Kundi la tatu ni Msando huyu alijaribu kujitutumua akajikuta anaangukia kukaa sero masaa kadhaa kwa makosa ya kugawa barakoa.Msando mwanasheria ni kundi lililoingia chamani kuunga juhudi za Mheshimiwa sana.Alipewa kazi ya kuhakiki mali za chama kazi ambayo ilikuja kumwingiza Dr Bashiru katika nafasi ya Katibu Mkuu.Ilitegemea baada ya kazi nzuri basi nafasi ya ubunge ilikuwa halali yake.
Kikao cha Mwisho cha Waziri Mkuu mstaafu Mizengo bado hakijaleta muunganiko chamani.
Naomba kuwasilisha.
Ngongo safarini Bukoba kwasasa nipo Katerero sokoni.
Mbio za ubunge katika jiji letu la Arusha sasa zipo wazi kabisa kiasi kwamba hata kipofu ni rahisi kujua na kufahamu nani atashinda ubunge.
Mara baada ya Mheshimiwa Mrisho Mashaka Gambo kupitishwa na kamati kuu kugombea ubunge Arusha Mjini kulikuwa na sintofahamu kubwa miongoni mwa wanaCCM kindakindaki. Wengi walijiuliza kulikoni kamati kuu kupitisha jina la mgombea ambae tayari alishasemwa hadhani na mheshimiwa Rais na hata Katibu Mkuu wa CCM Taifa Dr Bashiru.
WanaCCM wengi walikubaliana pengine kamati Kuu iliangalia nani mwenye uwezo wa kushinda nafasi ya ubunge na kuviweka vigezo vingine kando ikiwemo tuhuma za rushwa, uchonganishi (kiwanja cha Msikiti Mkuu Bondeni), kukwamisha ujenzi wa stand mpya, kuhujumu ujenzi wa shule mbali mbali kwa kisingizio cha udogo wa viwanja na nk.
CCM iliamini na kujiaminisha kwamba Mrisho Mashaka Gambo angewavusha salama katika uchaguzi mkuu, hapakuwemo mgombea mwingine wa kumzidi yeye.
Katika hali ya kushangaza sana kama si kusikitisha Mrisho Gambo Mashaka amepwaya kweli kweli, zile amri zake za ukuu wa Mkoa hazifui dafu katika kuomba kura. Mrisho bila ngoma,mdundiko na wacheza show hawezi kufanya mkutano,Mrisho bila kukusanya watu toka kata mbali mbali za wilaya ya Arusha Mjini,Arumeru hawezi kufanya mkutano, Mrisho Gambo bila usaidizi wa Mkuu wa Wilaya, Mkuu wa Mkoa hawezi kufanya mkutano. Mrisho Gambo yuko hoi bin taaban kisiasa na kiuchumi. Matajiri wengi wamejiweka kando na kampeni zake hawataki kutoa fedha tena wanamwangalia kama gari bovu.
Zipo tuhuma sijui zimetoka wapi, sijui nani kazianzisha zimesambaa kwa kasi ya ajabu juu ya kuungua soko la Samunge loooh hata kuandika naogopa soko la Samunge ni kaa la moto si mtaji tena wa Mrisho.
Update leo 17/09/2020.
Sasa ni dhahiri mpasuko mkubwa ndani ya CCM yapo makundi matatu makuu.
Kundi la Gambo ambalo linaungwa mkono na Mwenyekiti wa UWT na Mwenyekiti wa CCM Mkoa Kamanda Msatahafu Zelote Steven.Kundi hili lilihakikisha jina la Gambo linarudi pamoja na kugubikwa na tuhuma nyingi za rushwa na matumizi mabaya ya madaraka ikiwemo kuwaweka mfukoni aliyekuwakuwa Mkuu wa TAKUKURU na RPC.Wakuu hawa wa vyombo vya dola walikuwa wakisimamia kwa karibu harakati zote za ushindi za Gambo.
Kundi la pili linaongozwa na Monaban,Kundi hili liliumizwa sana na Gambo wakati akiwa RC ikiwemo kuporwa biashara zake za nafaka (National Milling) kwa kisingizio alikuwa mtu wa E N Lowassa.Kwa hakika hapa ndipo kwenye mzizi mkubwa wa fitina.Monaban ana kundi kubwa sana nyuma yake.Huyu hakubali ahadi za kitoto anataka Gambo atupiliwe mbali.
Kundi la tatu ni Msando huyu alijaribu kujitutumua akajikuta anaangukia kukaa sero masaa kadhaa kwa makosa ya kugawa barakoa.Msando mwanasheria ni kundi lililoingia chamani kuunga juhudi za Mheshimiwa sana.Alipewa kazi ya kuhakiki mali za chama kazi ambayo ilikuja kumwingiza Dr Bashiru katika nafasi ya Katibu Mkuu.Ilitegemea baada ya kazi nzuri basi nafasi ya ubunge ilikuwa halali yake.
Kikao cha Mwisho cha Waziri Mkuu mstaafu Mizengo bado hakijaleta muunganiko chamani.
Naomba kuwasilisha.
Ngongo safarini Bukoba kwasasa nipo Katerero sokoni.