Uchaguzi KKKT: Askofu Malasusa achaguliwa kuwa Askofu Mkuu wa KKKT kuchukua nafasi ya Dkt. Fredrick Shoo

The so called mtu wa kitengo.
 
Nawashangaa sana hawa maaskofu wa KKKT kumchagua huyu kipenyo,mwaka 2018 KKKT ilitoa waraka wa jinsi mambo ya awamu ya tano yalivyokuwa ndiyo siyo na ikaamriwa usomwe kwenye makanisa yote ya KKKT lakini huyu kipenyo akazuia usisomwe kwenye Dayosisi ya Mashariki na Pwani aliyokuwa anaiongoza. Mtu ambaye alikwenda kinyume na maaskofu wenzake inakuwaje leo wamwani kuwaongoza? Ataiheshimu kweli Katiba ya KKKT? Naliona Kanisa hili likienda kupasuka. Au Jecha alifufuka akasimamia huo uchaguzi wao?
 

Siyo kweli, cheo cha Askofu Mkuu kipo ila ni kwa jimbo kuu anbalo ndani yake yanakuwepo majimbo mengine yenye maaskofu. Kwa kufupi Askofu Mkuu wa Jimbo la Katoliki kunakuwa na maaskofu wa majimbo ndani ya jimbo kuu, yaani yeye anakuwa ni dingi sawa na kuongoza kanda!
 
Hiki ni kifo cha KKKT labda Mungu aingilie kulinusuru Kanisa hili. Shame upon us watu wa KKKT
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…