Uchaguzi mkuu kiti cha Rais 2025 (video): Unabii waweka wazi kuwa ni Samia S. Hassan (CCM) vs Bishop Josephat Gwajima (CHADEMA)...

Hapo ujumbe Si mashindano.

Ujumbe ni kuwa,

Ajaye ni Gwajima,

CCM wakimteua, anakuwa Rais.

CHADEMA wakimteua, anakuwa Rais.
 
Hata katika logic ya kawaida , Mungu hataruhusu mwanamke atawale . Mungu alitaka mwanamke awe msaidizi wa mwanaume toka mwanzo wakati dunia inaumbwa .
 
Ngoja tufanye kunukuu tu, kwa matumizi ya baadaye...

Nina swali, mbona Gwajima jimbo limemshinda? Ataweza nchi kweli!!!
Jimbo limemshindaje Josephat Gwajima ndugu Watu8?

Kama serikali haitaki au haipeleki fedha za kujenga barabara au maji au huduma yote ya kijamii jimboni kwake, hilo litakuwaje tatizo la Gwajima?

Kama huduma za jamii kwa ujumla wake i .e maji, umeme, barabara, makazi, mipango miji, usafiri na usafirishaji, kupanda kwa gharama za maisha kwa wananchi nk nk. Ni kwa vipi hii imuhusu Josephat Gwajima?

Hebu nieleze bwana labda nitakuelewa....

Nani mwenye jukumu la kukusanya kodi na kupanga matumizi yake? Gwajima au serikali?

Gwajima ni mbunge na kazi ya mbunge generally ni kusema kwa niaba ya wananchi anaowakilisha bungeni. Kusema juu ya mahitaji yao ya kimaendeleo kijamii na kiuchumi ili serikali kupitia mifumo yake ifanye. Kama serikali haijafanya nani alaumiwe?

Mimi nadhani hapa wa kulaumiwa ni Rais Hayati John P. Magufuli na sasa Samia Suluhu Hassan na chama chenye dhamana ya serikali yaani CCM kuwa wamefeli kuleta maendeleo jimboni Kawe kwa Gwajima...!;
 
Hata katika logic ya kawaida , Mungu hataruhusu mwanamke atawale . Mungu alitaka mwanamke awe msaidizi wa mwanaume toka mwanzo wakati dunia inaumbwa .
Unajua maana ya Msaidizi Wewe? Kuwa Msaidizi Haina maana kuwa mtu mdogo Hata awe mke.Roho Mtakatifu ni Msaidizi Lakini Sio mdogo kwetu ni mkubwa kwetu soma hapo

Yohana 14:26 “Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia.”
 
Binadamu angekuwa hana tumbo angekuwa mtu mzuri sana lakini tumbo linafanya watu wathmie kila mbinu.
 
Gwajima huyu huyu😂😂😂😂😂😂.

Basi kweli Mungu katuchoka watanzania.

View attachment 2969990
Wewe nawe acha ujinga kuleta vitu vya kutengenezwa (photoshoping) kwa nia ya kudhalilisha na kutweza utu wa wengine..

Hii haikuwa halisi. Ni vitu vya kutengeneza na kubumba tu na ilifanywa na huyuhuyu ndugu yenu Paul Makonda..

Lilishafafanuliwa hili na Paul Makonda kutubu na kuomba radhi kwa ujinga wake huu..
 
Halafu kijana huyo asiye na maadili ndiye anajaribu kujilinganisha na Mzalendo Magu!!
 
Lakini maana ya msaidizi kibinadamu ni mtu anayefanya kazi ya mwingine . Nilikuwa naongelea mwanamke kama binadamu siyo Roho mtakatifu.
 
Labda ndoto hizo, ccm kuchomoka madarakani Kwa njia ya makaratasi sio rahis kivile
 
Gwajima ni msanii sanii kupita kiasi. Tuwatu twa kupepesa pepesa macho na ujanja ujanja na utapeli na kuongea harakaharaka kitapeli
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…