Uchaguzi mkuu ujao kufanyika mwaka 2026?

Uchaguzi mkuu ujao kufanyika mwaka 2026?

Rais Samia aliapishwa kwa mujibu wa Katiba basi lazima Katiba iheshimiwe. Ibara ya 40(4) inasema: 'Endapo Makamu wa Rais anashika kiti cha Rais kwa.mujibu wa wa ibara ya 37(5) kwa kipindi kinachopungua miaka mitatu ataruhisiwa kugombea nafasi ya Rais mara mbili,lakini kama akishika kiti kwa muda miaka mitatu au zaidi ataruhusiwa kugombea nafasi ya Rais mara moja tu' Kwa hulka ya Rais Samia hatakubali kuleta mtafaruku wa Kikatiba kwa kuwaendekeza machawa.

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Rais Samia aliapishwa kwa mujibu wa Katiba basi lazima Katiba iheshimiwe. Ibara ya 40(4) inasema: 'Endapo Makamu wa Rais anashika kiti cha Rais kwa.mujibu wa wa ibara ya 37(5) kwa kipindi kinachopungua miaka mitatu ataruhisiwa kugombea nafasi ya Rais mara mbili,lakini kama akishika kiti kwa muda miaka mitatu au zaidi ataruhusiwa kugombea nafasi ya Rais mara moja tu' Kwa hulka ya Rais Samia hatakubali kuleta mtafaruku wa Kikatiba kwa kuwaendekeza machawa.

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
Asante mkuu kwa ufafanuzi! Nchi hii ina ombwe la vijana!
 
Kikatiba ana haki ya kutawala kwa miaka 10. Akienda kama unavyosema itabaki kama miezi sita kutimia miaka kumi. Atakuwa na haki kugombea tena mwaka 2030 amalizie miezi yake sita? Hapa ni kwa sababu imebaki miezi michache. Tufanye magufuli angekufa mwaka huu. Mama angemaliza mitatu ya JPM. Kisha angeweza gombea 2025 na kufanya mitano. Jumla miaka 8. Kisheria anakuwa na hakli ya kuwa rais kwa miaka miwili tena. Anaweza gombea kuimalizia?
Haipo hivyo mkuu ,tusome katiba
 
Kama chawa mnadai anamalizia kiporo cha JPM, hivyo atakuwa na nafasi ya kugombea vipindi viwili hakuna tatizo. Ila tukubaliane tu 2025, ngoma iwekwe uwanjani kila mtu achukue fomu kinyang'anyiro cha kutafuta mgombea wa Urais ndani ya ccm kifanyike, tuone huyo mama yenu atakavyotoboa.
 
So Samia anaendeleza awamu ya JPM au hii ni awamu tofauti?
Marehemu, baada ya maisha yake kukoma, haichi awamu ya uongozi ikiendelea. Pale maisha yake yalipokoma, ndipo uongozi wake ulipokoma.

Ukishafariki, huachi Urais nyuma. Nafsi yako inapokuwa imemaliza maisha ya Dunia, basi na mamlaka yako yanakuwa yameishia pale.
 
Hapana, Mama anamalizia urais wa JPM kwanza hiyo July 2025 halafu November 2025 ndio anaanza awamu yake, ila kwa vile kwa awamu ya pili ya JPM, Mama Mama nimehudumu miaka 4, hivyo hii inahesabika ni awamu yake ya kwanza na 2025 anamalizia ya pili.
P
Katiba inasemaje Samia inatakiwa miaka kumi kwa Sasa anamalizia kijiti Cha Magufuli ye ataanza 2025 Hadi 2035.
 
Hapana, Mama anamalizia urais wa JPM kwanza hiyo July 2025 halafu November 2025 ndio anaanza awamu yake, ila kwa vile kwa awamu ya pili ya JPM, Mama Mama nimehudumu miaka 4, hivyo hii inahesabika ni awamu yake ya kwanza na 2025 anamalizia ya pili.
P
Marehemu Magufuli alipofariki hakuacha Urais nyuma.

Pascal unaniangusha. Wewe mwanasheria kabisa unasema Rais Samia anamalizia Urais wa Magufuli! Hujawahi kusoma katiba?

Nenda kwenye katiba, ukaangalie ukomo wa Urais. Katiba inatamka wazi kuwa Rais aliyepo madarakani, Urais wake utakoma endapo atafariki, atajiuzulu, atakuwa amefutuwa uwanachama wa chama chake kilichomwingiza madarakani, ataugua kwa kiwango kitakachothibitika kuwa hana uwezo wa kutekeleza majukumu yake, au Bunge likipiga kura ya kutokuwa na imani na Rais, na kisha kufanyika uchaguzi ambao utawarudisha theluthi mbili ya wabunge waliokuwepo.

Urais wake unapokoma, iwe kwa kifo, maradhi, kujiuzulu, kupigiwa kura ya kutokuwa na imani, n.k; Urais wake unakuwa umeishia pale. Hakuna anachokuwa amekiacha kwenye Urais. Katiba inaeleza tu nini kitatokea baada ya yeye aliyekuwa Rais, Urais wake kukoma. Inasema kuwa hakutakuwa na uchaguzi, badala yake aliyekuwa makamu wa Rais atakuwa Rais kumalizia kile kipindi kilichobakia kama yule aliyekoma kuwa Rais angeendelea kuwa Rais. Kwa hiyo Makamu wa Rais anamalizia kipindi kilichobakia mpaka kufikia kipindi cha uchaguzi kinachofuata. Hamalizii Urais wa mtangulizi wake, maana yule Urais wake umekoma. Anamalizia kipindi kilichobakia kufikia uchaguzi unaofuata. Na akimalizia kipindi hicho, huyo Rais atakuwa na haki ya kugombea tena kwa kipindi kimoja tu.
 
Katiba inasemaje Samia inatakiwa miaka kumi kwa Sasa anamalizia kijiti Cha Magufuli ye ataanza 2025 Hadi 2035.
No!, Miaka kumi sio lazima!, awamu ya kwanza ya Rais Samia ni miaka 4 iliyobaki ya JPM, halafu awamu yake ya pili ndio 2025 -2030 ndio ya mwisho!. Hata hiyo 2025 sio lazima awe yeye Samia!. Anaweza kuamua kupumzika ndipo tutaanza awamu ya 7.
P
 
Marehemu Magufuli alipofariki hakuacha Urais nyuma.

Pascal unaniangusha. Wewe mwanasheria kabisa unasema Rais Samia anamalizia Urais wa Magufuli! Hujawahi kusoma katiba?

Nenda kwenye katiba, ukaangalie ukomo wa Urais. Katiba inatamka wazi kuwa Rais aliyepo madarakani, Urais wake utakoma endapo atafariki, atajiuzulu, atakuwa amefutuwa uwanachama wa chama chake kilichomwingiza madarakani, ataugua kwa kiwango kitakachothibitika kuwa hana uwezo wa kutekeleza majukumu yake, au Bunge likipiga kura ya kutokuwa na imani na Rais, na kisha kufanyika uchaguzi ambao utawarudisha theluthi mbili ya wabunge waliokuwepo.

Urais wake unapokoma, iwe kwa kifo, maradhi, kujiuzulu, kupigiwa kura ya kutokuwa na imani, n.k; Urais wake unakuwa umeishia pale. Hakuna anachokuwa amekiacha kwenye Urais. Katiba inaeleza tu nini kitatokea baada ya yeye aliyekuwa Rais, Urais wake kukoma. Inasema kuwa hakutakuwa na uchaguzi, badala yake aliyekuwa makamu wa Rais atakuwa Rais kumalizia kile kipindi kilichobakia kama yule aliyekoma kuwa Rais angeendelea kuwa Rais. Kwa hiyo Makamu wa Rais anamalizia kipindi kilichobakia mpaka kufikia kipindi cha uchaguzi kinachofuata. Hamalizii Urais wa mtangulizi wake, maana yule Urais wake umekoma. Anamalizia kipindi kilichobakia kufikia uchaguzi unaofuata. Na akimalizia kipindi hicho, huyo Rais atakuwa na haki ya kugombea tena kwa kipindi kimoja tu.

PASCO anaanza kuwa influenced na Sukuma gang mentality...

Ni Sawa afe mbunge halafu mtu aseme unamalizia ubunge wa marehemu...au Mkuu wa mkoa afe iwe unamalizia ukuu wa mkoa wa marehemu...

Wafuasi wa Magufuli Wengi wanaona Urais ilikuwa 'kitu binafsi" cha Magufuli...hata unaona wanakasirika Rais akifanya maamuzi tofauti na ya Marehemu....utasema Marehemu ndo alishushwa na kupewa Urais na maelekezo yote ya Urais ...
 
Kama chawa mnadai anamalizia kiporo cha JPM, hivyo atakuwa na nafasi ya kugombea vipindi viwili hakuna tatizo. Ila tukubaliane tu 2025, ngoma iwekwe uwanjani kila mtu achukue fomu kinyang'anyiro cha kutafuta mgombea wa Urais ndani ya ccm kifanyike, tuone huyo mama yenu atakavyotoboa.
Kila chama kimejiwekea utaratibu wake wa ndani wa kupata wagombea. Utaratibu wa CCM ni mgombea urais hapingwi midterms
P
 
Back
Top Bottom