Uchaguzi wa Kiteto: Taarifa mbalimbali

Uchaguzi wa Kiteto: Taarifa mbalimbali

Status
Not open for further replies.
Mtu wa Pwani,

Binafsi sina ushabiki upande wowote na kwakuwa Zitto alikuwa na namba yangu kama mwanachama wa JF basi akaniuliza kama niko mtandaoni na naweza kuwafahamisha kinachojiri. Nikafanya kuwafahamisha kadiri alivyokuwa anani-update.

Kwa sasa nimepata ujumbe toka kwake ambapo anawashukuru wana JF kwa ushirikiano. Ujumbe unasema hivi:

"Tupo kituo cha polisi Kiteto, RPC amesafiri toka Babati kuja kufuatilia suala hili. Wamekamatwa makomandoo wawili ambao wamekiri ni toka CCM na wametokea Dar trained JKT Militias. Majina yao ni Hamis Kilindo na Keneth Mbilinyi. Keneth anayejiita mlinzi wa Pius Msekwa alikabidhiwa machine gun na mkuu wa kituo". Mwisho wa kumnukuu.

Mjumbe hauwawi sio?

UnbelievablE!!!!
 
UnbelievablE!!!!

Pius Msekwea analindwa na hao makomandoo wa mtaani ?CCM jimbo moja ndilo linataka kuua watu namna hii ?Nimesoma kwamba kuna jumla yao 30.Sasa panakalika kweli hapo Jimboni ?Polisi anawapa hao silaha ? Kwa imani ipi na makubaliano yapi ?

Kweli JK una ukaribu na wapinzani nasi tunaona .
 
Hivi mapigano haya yamesababishwa na nini?

Hili ni swali lenye thamani kubwa sana?

Hata hivyo masahihisho kidogo ni kuwa, hakuna mapigano (pande mbili kupigana) bali kuna vipigo toka kwa polisi na kikundi cha ccm kinachojiita makomandoo ambao wanashirikiana kupiga na kunyanyasa viongozi na wafuasi wa chadema huko kiteto.
 
Pius Msekwea analindwa na hao makomandoo wa mtaani ?CCM jimbo moja ndilo linataka kuua watu namna hii ?Nimesoma kwamba kuna jumla yao 30.Sasa panakalika kweli hapo Jimboni ?Polisi anawapa hao silaha ? Kwa imani ipi na makubaliano yapi ?
Kweli JK una ukaribu na wapinzani nasi tunaona .

Hapo ndo nashangaa.. Hivi kweli sheria inaruhusu polisi kumpa mtu siraha ambaye si polisi ama ambaye hajathibitishwa kama akili zake ni timamu kwa ajili ya kuitumia siraha hiyo?

Watanzania inabidi tuamuke, tujikomboe kutoka utumwa wa wakoloni weusi inabidi ufike mwisho, inabidi tupate ukombozi na uhuru wa kweli.
 
Hivi ni kitu gani kinawafanya Polisi waamini kuwa kwa kutumia nguvu wanaweza kubadili mawazo ya watu? Huyo OCD lazima atimuliwe kazi na mkuu wao wa kituo vile vile na tunataka kina Makamba na Msekwa watoke hadharani na kulaani vitendo hivyi vya kinazi, kinyama, na ambavyo hakuna maneno yoyote yanayoweza kuvihalalisha.

Hivi sasa kuna habari nyingine nafuatilia kutoka Dar ambayo ina impact kubwa zaidi na JF... Mkiona imezimika kimbilieni KLH News...
 
Mwanakijiji
Ninaanza kuamini kuwa mojawapo ya sera ua uchaguzi ya CCM ni operesheni maalumu (kama hizi).

Hivi yule bwana Cheyo wa kituo cha demokrasia (alimwagiwa mihela na serikali majuzi) ana maelezo gani kuhusu unyama huu??

Je hii haiwezi kuwa another ali hasani mwinyi?? yaani waziri wa ndani ajiuzulu? Je katiba inasemaje kuhusu jeshi la polisi?? na huu si mgogoro wa kikatiba???

Naanza kupata ujasiri badala ya uoga
 
Wahenga walisema dalili ya mvua ni mawingu,kwa yanayotokea kiteto ss hvi yana reflect picha halisi ya 2010. nimegundua kwamba wanajeshi wote waliopewa uongozi CCM ni ili waweze kutumia nafasi walizo nazo ili kupata Silaha na kuwatumia wanajeshi wenzao kushinda kwa kutumia nguvu ka alivyofanya kibaki.JAMANI DEMOCRASIA WANYOIUBIRI TANZANIA IKO WAPI?
 
Najua watu wa vyombo vya habari nyumbani bado havijamaliza kuchapa magazeti ya kesho.. tafadhali kombeni hizo picha zitoke Kesho kuonesha jinsi gani serikali yetu inajali haki za binadamu na utawala wa sheria!

Mkuu, duh, this is more than serious. Hivi tulikuwa tunawazomea ni hasa Kenya?

Mimi nafikri hao jamaa ungewatumia kama una email zao maana hata Halisi naona siku hizi kapotea kabisa hapa. Shukrani kwa kutuhabarisha. Kwa kweli demokrasia kwa sisi waafrika uhuuu!
 
Halisi yupo lakini alikuwa likizo fupi siku chache zilizopita na amerudi leo na kukutana na kasheshe nyingine ambayo anaifuatilia.
 
Hivi ni kitu gani kinawafanya Polisi waamini kuwa kwa kutumia nguvu wanaweza kubadili mawazo ya watu? Huyo OCD lazima atimuliwe kazi na mkuu wao wa kituo vile vile na tunataka kina Makamba na Msekwa watoke hadharani na kulaani vitendo hivyi vya kinazi, kinyama, na ambavyo hakuna maneno yoyote yanayoweza kuvihalalisha.

Hivi sasa kuna habari nyingine nafuatilia kutoka Dar ambayo ina impact kubwa zaidi na JF... Mkiona imezimika kimbilieni KLH News...

Ninaisubiri kwa hamu hiyo taarifa ya DAR maana kuna kila dalili itakuwa breking newz kali
 
Hiyo ya Dar.. I hope itaisha kimya kimya maana ikilipuka JF mmekwisha... inaonekana mnapata nyeti nyingi kutoka serikalini hata mambo yasiyoandikwa au waandishi hawajui. eg Kwamba Kikwete alienda Ujerumani kunywa chai na kurudi kumuwahi Bush.
 
Hiyo ya Dar.. I hope itaisha kimya kimya maana ikilipuka JF mmekwisha... inaonekana mnapata nyeti nyingi kutoka serikalini hata mambo yasiyoandikwa au waandishi hawajui. eg Kwamba Kikwete alienda Ujerumani kunywa chai na kurudi kumuwahi Bush.

kwa hiyo nao wanataka kuiripua jamboforums
ebwana kweli wameishiwa
 
Ninaisubiri kwa hamu hiyo taarifa ya DAR maana kuna kila dalili itakuwa breking newz kali

Hii ya kusema kuwa tukimbilie KLH news maana yake JF itakuwa closed. Shindwa shetani. Huna mamlaka na hichi chombo kitukufu. ukija kwa njia moja utarudi kwa njia saba. Ebenezer!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom