Uchaguzi wa Kiteto: Taarifa mbalimbali

Status
Not open for further replies.
Pundamilia07;146641 [SIZE="4" said:
NI YAPI MANENO MUAFAKA YA KUWAAMBIA WAPIGA KURA WAKATI WAKUHITIMISHA KAMPENI ZAKO? JE UNAPASWA KUWAAMBIA UKWELI AU MANENO YA KUBABAISHA?[/SIZE]

VICTOR KIMESERA ANAISHI WAPI?

Tukianza kuulizana maswali ya nani anaishi wapi nadhani itakuwa tunaelekea Kenya na kwingine kwenye ukabila .....
 

Mtanzania yeyote mwenye akili timamu aliyeshiriki kupiga kura katika uchaguzi uliofanyika jana Kiteto na pia alipata nafasi ya kusikia kashfa mbali mbali za BoT, mikataba ya madini, mikataba ya rada, ununuzi wa magari ya jeshi na helikopta n.k. na bado akaipigia kura CCM basi akili yake ina walakini wa aina fulani. Halafu huyu huyu analalamika kwamba mashule hayana madawati na walimu, barabara mbovu, ajira hakuna, hospitali hazina madawa wala vitanda, umeme bei mbaya, gharama za maisha zimeongezeka sana, upatikanaji maji safi ni shida pamoja na kashfa zote alizosikia bado hakuona umuhimu wa kubadilisha kura yake!

Vyama vya upinzani navyo lazima vijiangalie. Watanzani wengi tumesema tungependa kuona vyama hivyo vinaunga, maana umoja ni nguvu na utengani ni udhaifu. Kuna muda wa kutosha kati ya sasa na uchaguzi wa 2010 wa kuunda chama kimoja chenye nguvu cha kuishinda CCM. Sikilizeni maoni ya wananchi mfanye kweli. Ubinafsi hautawafikisha popote, CCM katika miaka miwili tangu uchaguzi wa mwaka 2005 haijafanya chochote cha kustahili kupata hata kura moja achilia mbali kushinda kiti hicho cha Kiteto. Katika kipindi chote hicho waligubikwa na kashfa nzito ambazo zinaingamiza Tanzania na kufanya maisha ya Watanzania walio wengi kuwa magumu zaidi.

Kama hakukuwa na mizengwe katika uchaguzi huo wa Kiteto na bado upinzani ukashindwa kuchukua kiti hicho, basi ni wakati muafaka wa upinzani kupanga mikakati mipya ikiwa ni pamoja na la kuunda chama kimoja chenye nguvu kitachowaunganisha wapinzani wote kabla ya uchaguzi wa 2010.
 
Hili ndilo linaogopesha hapa!

..unajua kuogopa ni vyema lakini hakuna msaada sana!

..laiti kama wenye macho wangeona hili linakuja,and believe me liko njiani!

..mi wala siogopi,nasikitika tu! africa seem to have its unique ways of falling into violence!

..ni kama historia ya europe inajirudia africa!
 

Kama ulisoma comments za watu kwenye website ya bbc wakati wa fujo za Kenya, hili ndilo exactly watu wengi walisema kuhusu kinachotegemewa kutokea Afrika. Nasikitika sana kila mara ninapokubaliana na Ngabu kuwa waafrika ndivyo tulivyo.
 

MZEE MWANAKIJIJI,
HUO NI MTAZAMO WAKO KWANI KILA MTU ANA UWEZO WAKE WA KUFIKIRI NA KUJENGA TASWIRA YA KILE ANACHOKIAMINI.

MUHIMU KATIKA MAANDIKO YANGU NI UJUMBE ULIOPO, KAMA NIMETUMIA KIPAZA SAUTI AU VINGINEVYO THAT'S NOTHING, TUJADILI HALI HALISI ILI HISTORIA IWEZE KUTUHUKUMU KWA YALE YA KWELI.

USIOGOPE KUSEMA UKWELI LABDA WEWE NDIYE UNAESUBIRIWA KUVUNJA 'UKUTA WA BERLIN'
 
Vipi kama pesa ya wizi ndiyo inatumika kulisha na kuendesha familia?


Kushindwa kwa upinzani mie naamini kabisa ni SERA ndizo zinawashinda kuzitumia ,hawa wapinzani wamekua kama CCM kuamuka tu siku za uchaguzi na kuanza kupaa na madege angani huku wakisahau kua CCM wamejijenga toka zama zile hivyo kupaa kwa kipindi cha miezi kadhaa kubadirisha kilichojengeka vichwani kwa miaka kadhaa ni ngumu.

Na ili ubadirishe kilichokwisha jengeka kichwani ni lazima umu shawishi mtu husika kwa matendo mfano tu baada ya kumalizika kwa uchaguzi ule mkuu wangejikita zaidi ktk maendeleo ya jamii mfano kwa hizo harambee na kutafuta wadhamini kuwapelekea huduma wananchi ya maji/umeme

kufanya harambee kuwajengea watu wanaoenda maili kadhaa kutafuta disipensari .

kufanya ma harambee na kutafuta wadhamini kujenga vyuo vikuu vya kutosha na vitu vingine vya namna hiyo.

Hapo wananchi watakua wameona nini maana ya upinzani na nini kinafanya na hapo ndipo kitakua kimejikita vichwani mwa wananchi.

Unajua kuna fomula moja ukitaka kushindana na mtetea taji unatakiwa uweke mikakati ya kumshinda kwelikweli hata asipate feva yoyote ambayo anaweza pata.

Huku kuja kuuza sera dakika za majeruhi tena kwa maneno matupu si njia muafaka Je tutaamini vipi hizo sera kama sio za kiulaghai?? Je wapinzani wapewe tu kwa vile wanaongea maneno matamu?? Je wewe unaweza kuamini mtu kwa maneno yake tu??

Wapinzani wabadirishe jinsi ya kupeperusha bendera vinginevyo ndiyo kama hayo ya kiteto na ya Mrema mwaka 1995.

Huwezi kutumia wizi wa watu wachache ukasema ni chama ,chama sio physical entity ambacho kinaweza iba kitu.

Mfano ktk familia ya watu 8 mmoja kati yao anaweza akawa mjinga lakini huwezi sema familia ile ni jinga.

Failure ya tanzania sio ya CCM as CCM ila ya familia nzima yani watanzania.

Wapinzani wangapi wametulaghai wakati ule kwamba wao ni wema wamekimbia ccm maana ni chama kibaya leo hii NDIO viongozi na wafuasi wazuri wa CCM Je tutafahamu vipi huyu ni mlaghai,huyu ni propaganda ,huyu ni mtafuta madaraka??? kwa maneno matupu?? lahasha.

Haya mambo ya kuibua skendo si hoja kabisa ya kumfanya mtu apewe madaraka,kwani skendo hizi zimeanza kuibuliwa na wapinzani mbona mbunge wa CCM kama sikosei ni Mzee ndakaya ama kingunge ameibua skendo ngapi amefukuzisha mawaziri wangapi??

Kawaida ya mnafiki hua anakumonita tu ndg Kitila sehemu utapokesea ili ukumalize lakini mara kwa bahati mbaya juhudi za namna hii hua hazifanikiwi
 
Ushindi wa CCM kiteto umeshakubalika na Chadema. What next? Ukweli vyama vya upinzani havijajijenga vijijini na pia wapiga kura wa leo hawajali sera bali hela wanazopokea wakati wa uchaguzi. CCM hizo zimejaa. Bado uwezekano wa kushinda hapo baadaye upo katika kujenga vyama kwenye msingi wa yote, vijijini. Wakazi wa mijini Tanzania hawazidi 30% na hao pia ni rahisi kufikiwa, kwa kutumia mbinu za soko, 70% iliyoko vijini ndio mtaji mkuu wa CCM na huko ndiko upinzani uelekeze nguvu yao. Niliwahi kwenda kutembelea jamaa zangu kijijini, katika mazungumzo kuhusu siasa na upinzani, mzee mmoja aliniuliza swali moja "una baba wangapi?" akimaanisha kwao CCM ni kama baba katika taifa letu na hakuna haja ya upinzani. Nilitambua ugumu wa kubadirisha fikira kwanibado 'partenal' thinking ndiy inayotawala. Labda ni ule msemo wa 'zimwi likujualo halikuli ukakwisha' ndio unaofuatwa na wapiga kura wetu.
 
Tukianza kuulizana maswali ya nani anaishi wapi nadhani itakuwa tunaelekea Kenya na kwingine kwenye ukabila .....

PAMOJA NA KUKWEPA KUJIBU SWALI LAKINI UKWELI NI KUWA MESSAGE IMEFIKA, UNAPOSEMA ...msiwacgaue hao wanaokaa Oysterbay, Masaki na Mikocheni...UNATAKA KUWAAMBIA NINI WAPIGA KURA WAKO WAKATI UNAMNADI MGOMBEA AMBAYE UMEKUJA NAE KUTOKA DAR? TUELIMISHANE, TUJIKOSOE, TUREKEBISHE. WAPIGA KURA WANASIKIA NA WANAELEWA NA NDIO WENYE UAMUZI WA MWISHO.
 
Huu ni ukweli ingawa nina wasiwasi kuwa mapinduzi yakimalizika Chadema na vyama vya siasa basi kanda ya ziwa yote itakuwa imeuzwa kwa sinclair na wenzake. Sad but true
..usiwe na wasi,

..nani alisema kwamba wakati wa mapinduzi watu "hawanywi" wala "kula"? infact wanahitaji hivyo bila kukosa ili wawe na nguvu ya kusonga mbele!
 
Tatizo lililopo ni kwamba about 80% of Tanzania population wanaishi vijijini amabako ni vigumu kuwaelimisha wananchi, kwa sababu zifuatazo
  1. Watanzania wengi hawana Elimu, Hivyo hawawezi kuchanganua Mambo ambayo serikali inawafanyia
  2. Inaitajika resources nyingi sana kuweza kuwaeleza wananchi hali halisi ya Tanzania
  3. Watanzania wengi hawatumii mtandao ambayo ndo njia rahisi ya kufikisha ujumbe.
  4. Jamii ya Tanzania haiko huru hata kidogo, watu wanapiga kura kwa sababu mjomba ni CCM au baba alikuwa CUF basi naye anaenda huko
Kwa mfano sasa hivi tunapika kelele kuhusu swala la Tanesco, lakini kumbuka CCM wanajua wananchi walio wengi haswa wa vijijini hawawezi kuwaelewa kwa sababu hawautumii huo umeme, kwahiyo haina tatizo kwao.
Utaongelea maji, Kumbua vijini maji watu wanachota mitoni hivyo hawajali hata kidogo mambo yenu ya maji.
Kama mtagundua ndo maana CCM haifanyi mambo ya Maendeleo, kwa sababu inajua ikifanya hivyo ndo mwanzo wa kupoteza kura, wananchi wote watajua gharama za Umeme, maji barabara na n.k

Hapa nadhani kunaitajika Strategy za Hali ya juu sana kuweza kuwakomboa wananchi Jamani.
 

Hii bado ni speculation mkuu na hakuna ambaye anajua ni kwani zaidi ya nusu ya watu waliojiandikisha kupiga kura "hawakupiga kura". Hata hivyo ccm wanapongezwa kwa "ushindi wao hapa na kwa "kuwagalagaza" wapinzani.

Asante
 
Wapinzani wamejitahidi wameshindwa.

Kidumu chama hiki eeh! aah! samahani nimesahau kidogo
Eti! Hiki chama ambacho Waziri wake Mkuu wa zamani MH Lowassa amegushi na kuiba kupitia mkataba wa RDC na hadi leo anaendele kuiba mamilioni?
Aaah! nimeshindwa kukisema, sijui ni WAOEMU??.

ahh! nimekumbuka SISIEMU.

Kidumu chama cha SISIEMU!!!!!!!

Sasa ni muda wa kukaa chini na kujiuliza kwa nini wameshindwa?
Mwaka 2010 wafanye nini ili washinde?
Kwa nini watu wengi wameshindwa kujitokeza kupiga kura?
Wafanye nini ili kila mpiga kura aweze kupiga kura?
Kwa nini askari wa FFU waliletwa kwa mlima?
Uwepo wa FFU umeathiri nini?
FFU wanatisha au ni tumaini la wanyonge?
Raia wa kawaida anajisikiaje mbele ya mtutu wa Bunduki?
Nini maoni ya watu walioacha kwenda kupiga kura?
Nini ni udhaifu wa SISIEMU?
Wapinzani watumieje udhaifu wa SISIEMU kwa manufaa yao?
nk.
 

Sasa wewe hebu tuelezee katika kipindi cha miaka miwili tangu uchaguzi wa 2005, CCM imegubikwa na kashfa nzito nzito zinazotangwa kila kukicha katika magazeti, redio na TV hivyo kila mpiga kura wa Kiteto ama alisoma au kusikia kashfa hizo. Sasa kama bado aliona kuna umuhimu wa kuipigia kura CCM, basi kuna kasoro fulani maana unaipigia kura CCM kwa kipi hasa walichokifanya kinachostahili kuwapa kura? 😕
 


Kitila,
Give me a break! Hivi unataka kuniambia kuwa Mzee Kimesera anakubalika kuliko mgombea wa CCM?

If you believe in this, I think even Alsaaf will admire you!


Kama kawaida wewe Kitila ni mmoja ya wachezaji waliopo uwanjani, waamuzi ambao ni wananchi wa Kiteto wameshatoa uamuzi wa mwisho juu ya pambano lililokuwepo. Sisi watazamaji na wachambuzi tumeona kuwa mchezaji aliyewekwa kufunga magoli hakuwa na uwezo, sasa unataka kusema kufikirika kunatoka wapi? Accept challenges kwa lengo la kurekebisha mambo. Kwa hili la mgombea wa CHADEMA kuna kasoro nyingi za kiuteuzi ambazo CHADEMA kwa makusudi kabisa hawakutaka kuzifanyia kazi ambazo mizizi yake ni ubwanyenye tu. Tunahitaji opposition yenye nguvu na isiyogubikwa na utata otherwise you will never grow.
 
Kuna mambo yaliyotokea Kiteto ambayo yatawafanya mashabiki wa CCM wainamishe vichwa kwa aibu. Tunawapongeza kwa "ushindi" kwani hata bao la Maradona lilihesabiwa na watu walishangilia..
 

NAOMBA UELEWE KUWA WANANCHI WA KITETO WALIKUWA WANAMCHAGUA MBUNGE ATAKAYE WAWAKILISHA BUNGENI, HIZO KASHFA UNAZOZISEMA WANAZIFAHAMU SANA TU.
WALICHOFANYA NI KUMCHAGUA MTU AMBAYE ATAWAWAKILISHA VEMA BUNGENI NA SI VINGINEVYO. KUMBUKA WANANCHI WA KITETO SI MBUMBUMBU KAMA UNAVYODHANI.

MZEE WANGU KIMESERA WANAKITETO WALISHAMKATAA SIKU NYINGI TU NA ALIKWENDA KWENYE UCHAGUZI AKIJUA KABISA HUKUMU YAKE ILISHAPITISHWA SIKU NYINGI.

KAMA NILIVYOSEMA HAPO AWALI KIMESERA
WAS NOT THE BEST CANDIDATE BUT JUST A CANDIDATE.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…