Uchaguzi wa Kiteto: Taarifa mbalimbali

Uchaguzi wa Kiteto: Taarifa mbalimbali

Status
Not open for further replies.
Nawashangaa CHADEMA ,hivi wanafahamu maana ya upinzani ,hebu waulize mawakili kwanini mshitakiwa anatakiwa akatae kosa alilolifanya na kwa hali yoyote alikatae na alipinge.
CHADEMA kama chama cha upinzani kilitakiwa kisitoe kauli ya kuyakubali matokeo , kwani hiyo ni sumu ya kuwaua wateja wake ,kwa vyovyote vile ingelikataa kushindwa na kuweka kuwa uchaguzi ulikuwa na mizengwe na makosa kibao , automatic wafuasi wake wangelijisikia na kutembea kifua mbele kuwa uchaguzi na ushindi wa CCM una mashaka.
Lakini leo mfuasi wa Chadema na upinzani kwa ujumla hana mdomo mbele ya CCM maana wakubwa wamishasema na kukubali kushindwa ,wandugu hapa hakuna mashindano ya mpira au ngumi hapa ni mashindano ya SIASA ,hivyo unachotakiwa ni kupinga tu hata kama una uhakika ni kweli CCM imeshinda hutakiwi kabisa kusifu na hivyo hivyo ,Upinzani hautakiwi kuisifu Serikali wala kiongozi wake kwa kitu chochote ,maana unatakiwa utafute kosa lolote na hapo udidimize ,na kama hakuna kosa basi propaganda inabidi ichomekewe. Na hiyo ndio siasa.
Nikiwauliza UPINZANI na haswa Chadema ambao naamini walipewa kipau mbele na wenzao hivi mchakato wa upigaji kura Hapo KIteto haukuwa na kasoro hata moja kuanzia mwanzo hadi utangazwaji wake , na kubwa zaidi wakuu wake kucharangwa Mapanga na sime pamoja na bisibisi..........Vipi mnasema au mnakubali kuwa mmeshindwa kwa tamko la mwanzo tu mnabwaga manyanga na kukubali kuwa CCM ndio washindi halali wa Kiteto.
Siwezi kusema mengi lakini naona nimefahamika ,iwe mwiko kusifu Chama Tawala kwa lolote lile ,kila wanachokifanya basi kitafutiwe kosa ,kitungiwe kosa na kutembezwa kwa wananchi ,msikubali kabisa kuingia katika mitego ya kusifu utawala ,mtapoteza nguvu ya upinzani ,ndugu zanguni ulaya chama cha upinzani kuisifu serikali ni mwiko ,maana alieko serikalini akionekana kusalimiana na demu tu basi inakuwa ishu katika mambo ya kisiasa ,vipi hapa ambapo watu wamepigwa na kuchomwa sime mnarudi na kusema uchaguzi mmeshindwa ,inaonekana bado viongozi wa Upinzani wanajipendekeza kwa CCM ,wacheni mara moja au wapisheni watu wenye usongo na nchi yao ,Vipi mnaisifu Serikali iliyojaa ubadhirifu ,hawa hawafai kusifiwa hata chembe ni kupondwa tu kwa kila wanachokifanya.
 
Mtanganyika,


U have real sent a STRONG message,

Wapinzani ninyi ni ndugu zetu, ni watanzania wenzetu, watanzania wengi wanawapenda sana, they are looking for alternatives.

Lakini acheni kuwa siku zote kwenye short term plan, THINK BIG.

Historia haiko upande wenu... hili lazima mulitambue.

1. NCCR-MAGEUZI waliwa-let down Watanzania 1995 kwa masumbwi kule Tanga
2. CUF waliwa-let down Watanzania 2000 na 2005 (kumbuka matusi yalimwagwa siku za mwisho za kampeni za Uchaguzi)
3. CHADEMA ya 1995 iliwa-let down Watanzania kwa kutoweka mgombea Uraisi wakati ndio kipindi CHADEMA, hadi leo CHADEMA ya 1995 haijarudi tena.
 
Mkuu haya mafao hulipwa kwa pande zote mbili, sio wabunge wa CCM tu, kama kuna tatizo kwenye hili, basi tungesikia wabunge wa opposition wakikataa hela na mashangingi, wabunge wetu ni lazima walipwe vizuri ili kuwaepusha kuingia taamaa za kurubuniwa na mafisadi.

Naona umetoka nje. Kumlipa mtu vizuri sio chanzo cha ufanisi wa kazi na mifano kamili ni Bunge la Tanzania, Mawaziri, BOT na TRA.

Mpaka sasa taasisi zenye kuongoza kwa ufisadi Tanzania ni zenye kulipa vizuri.

Baada ya kusema hayo narudia kuwa ushabiki wa Simba na Yanga mmeuingiza kwenye siasa.
 
Nimeshawai kusema huko zamani sana CHADEMA inatumia system ya mwenda wazimu, nikasema CUF will never ever win general election. Leo nasema tena, CHADEMA will never run Tanzania hata kwa dakika moja kama wataendelea kutumia 1960s tacticts. Why did i said that?

Mwaka 2007 katikati nilitoa wito kwa Zitto na John Mnyika kuandaa solid strategy ndani ya chama chao na kuachana na hii system ya zimali moto. Nikasema kinachoicost CHADEMA sio bad policy zao, ila ni Mh. Mbowe na wenzie. Hawa watu wana run 1961 campain in 2008 then una expect kushinda.

Nilisema few things can be done kuongeza nguvu ndani ya upinzani, nitarudia the same thing. Kwanza kabisa upinzani unaitaji stategic plan ya long term na sio zimali moto strategy waliyotumia kwenda kiteto. Pili, upinzani unatakiwa uachane kabisa na kufocus sana na kampeni za urais, bali inabidi wa create grassroot movement kuanzia shina hadi shina, kata hadi kata, tarafa hadi tarafa, wilaya hadi wilaya then mkoa hadi mkoa. Hii movement itabainisha ni nini policy za upinzani, hii movement not only itawausisha wananchi moja kwa moja na siasa, bali itaweza kuinvolve kwenye maswala ya kijamiii, kiuchumi na kisiasa kwenye center point hizo za uchumi wa nchi

Upinzani inabidi wawe na msemaji mkuu na waache hizi habari za kila mtu kwenda kwenye media na kufungua mdomo wake kwa opinion zake. Kama upinzani watatumia grassroot movement then tutaongeza namba ya viongozi wa upinzani kwenye serikali za mitaa, tutaongeza namba ya upinzani kwenye bunge then tunaweza kuomba kubadili katiba which is the center point.

Watanzania sio wajinga, watanzania hawana idea upinzani ni nini, wanaogopa madhara yaliotokea nchi jirani yasitokee Tanzania, hivyo ni jukumu la upinzani kurestore trustee ya Watanzania. Kutumia startegy ya kwenda kwenye campain kwa helikopta i think is rediculous, sababu who cares kuhusu helicopter? People want to know ni jinsi gani watapata maji, ni jinsi gani watoto wao watapata elimu, ni jinsi gani watapata tiba pindi wanapoihitaji. So, i don't understand why upinzani don't get it.

Unajua nini maana ya mjumbe wa nyumba kumi? That is a grassroot movement, kwamba CCM wamesogeza msaidizi wao katika kila nyumba kumi. sasa kusubiri week mbili kabla ya uchaguzi ndio mnamchukua Zitto, Dr Slaa na wengine i guess ni kuwachosha wabunge hawa.


Mkuu nakubaliana na wewe kabisa....mimi baada ya uchaguzi 2005 pia niliwahi kumtumia Mbowe email ya kumpa ushauri kama huohuo ulivyosema hapo juu...nilimwambia kwamba kushindwa kwao iwe changamoto na kinachotakiwa wawe na mikakati ya kufika kila pembe ya Tanzania na cha maana zaidi watengeneze mkakati mzito ambao wataweza kuchambua jinsi gani ya kuongeza idadi ya wanachama na pia jinsi ya kuwapata watanzania mahiri wanaoweza kugombea nafasi za ubunge. Lakini mpaka leo hii sijaona kama kuna cha maana kimefanyika...sasa imebaki miaka 2 tu. Utashangaa ikifika 2010 watakapoanza kukurupuka. Yaani sasa wangekuwa wanahakikisha kuwatafuta watu wa kukaa kila jimbo la uchaguzi na kuwaandaa vyema kabisa.

Mambo ya helikopta waache kabisa....ni uharibifu wa pesa...ingia kijijini panda punda, ngamia na baiskeli na fanyeni kazi sasa tena wakati mwingine si lazima mfanye ma mikutano makubwa...pita kila kitongoji...tengenezeni mahandishi rahisi yenye kuvutia na kushawishi wananchi ili waweze kuelewa vizuri....mkishafanya hivyo nyinyi CHADEMA tutaweza kusema kwamba sasa mnaonyesha ukomavu na mko kwenye mapambano ya kweli.

"Tusisifie kikosi cha zimamoto kwa kuwa kimeweza kuzima moto uliotokea kwenye jengo fulani ila tuwasifie kwamba wameweza kuchukua tahadhari zote za kuelimisha watu ikiwa ni pamoja na kuandaa mikakati ya kuzuia moto usitokee"

Sasa CHADEMA achana na mambo ya zimamoto...weka mikakati mahiri...siyo mambo ya kurukaruka kama digidigi hapa....
 
Sasa mapendekezo yangu... ni kwamba wanaCHADEMA kazeni boot safari bado ndefu... Mzee Mwanakijiji, Mpaka kieleweke, Mwafrika wa Kike, Kitila, John Mnyika, Zitto, Slaa etc... endeleeni badilisheni gear, wekeni gear kubwa...

wenzako wamejaribu...!!!
 
Matokeo ya Kiteto: CHADEMA yaduwaa

na Mwandishi Wetu
Tanzania Daima~Sauti ya Watu

MATOKEO ya uchaguzi mdogo wa ubunge katika Jimbo la Kiteto yaliyompa ushindi wa asilimia 57 mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Benedict ole Nangoro, yanaonekana dhahiri kukichanganya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Kuchanganyikiwa kwa CHADEMA, chama ambacho viongozi wake wakuu walikuwa na matumaini makubwa ya kuibuka na ushindi wa kishindo, yanatajwa kuwa yamesababishwa na kubainika kwa ukweli kwamba watu waliopiga kura ni asilimia 47 tu ya watu wote waliokuwa wamesajiliwa kwa ajili ya uchaguzi katika jimbo zima.

Kupungua huko kwa wapiga kura kumewafanya viongozi na makada hao kuingiwa na hofu kuwa ushindi huo wa CCM kwa kiwango kikubwa unatokana na kufanyika kwa jitihada za chini kwa chini za kununua shahada za wapiga kura ambao walikuwa wakionyesha mwelekeo wa kukikataa chama hicho tawala.

Wasiwasi huo tayari umeifanya CHADEMA itangaze rasmi kuyakataa matokeo ya uchaguzi huo mdogo wa ubunge, ambao umefanyika kutokana na kufariki dunia kwa aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Benedict Lusurutia.

Katika kuonyesha namna wanavyopinga ushindi huo wa CCM, viongozi wa CHADEMA na mgombea wake, Victor Kimesera, aliyevuna asilimia 41 ya kura zilizopigwa, hawakutokea katika hafla ya kutangaza matokeo hayo, licha ya kusubiriwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuanzia saa 5:00 asubuhi hadi takriban saa 11:45 jioni jana.

Kushindwa kwa wapinzani katika uchaguzi huo, kunazidi kuifanya kambi hiyo ishindwe kuweka rekodi iliyowekwa kwa mara ya mwisho na John Cheyo, aliyeshinda uchaguzi mdogo wa ubunge wa Magu, mkoani Mwanza miaka 10 iliyopita.

Akizungumza muda mfupi baada ya NEC kutangaza matokeo hayo rasmi, Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA, Freeman Mbowe, alisema kuwa chama chake kimedhamiria kwenda mahakamani kupinga ushindi huo wa CCM ambao alisema umepatikana katika misingi ya hila na udanganyifu.

Takwimu zilizotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) jana jioni baada ya kuchelewesha kutangaza matokeo hayo kwa takriban siku nzima, zinaonyesha kuwa Nangoro alishinda kwa kupata kura 21,506, huku Kimesera akifuatia kwa kupata kura 12,561.

Mgombea wa Chama cha Sauti ya Umma (SAU), Mashaka Fundi, aliambulia kura 300 wakati yule wa PPT-Maendeleo, Juma Saidi, ambaye alitangaza awali kumuunga mkono mwenzake wa CHADEMA alipata kura 110.

Takwimu hizo za NEC zinaonyesha kuwa kati ya wapiga kura 74,629 walioandikishwa katika daftari hilo mwaka 2005 ni watu 35,261 tu walijitokeza kupiga kura hiyo juzi, idadi ambayo kwa kiwango kikubwa ndiyo iliyoishtua CHADEMA.

Kwa upande mwingine, matokeo hayo ya NEC yanaonyesha kwamba, kura halali zilizohesabiwa katika uchaguzi huo zilikuwa ni 34,477, wakati zilizoharibika zikiwa ni kura 784.

Akizungumza baada ya kutangaza matokeo hayo, msimamizi wa uchaguzi huo, Faustime Kang’ombe, alisema kuwa, kujitokeza kwa watu wachache kupiga kura kunatokana na wengi wao kuwa mashambani wakati huu, wakiendelea na shughuli za kilimo.

Kwa upande wake, Mbowe alisema kuwa, pamoja na hujuma hizo, kitendo cha Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Henry Shekifu, ambaye ni kada wa CCM kufanya ziara na kufungua miradi ya maendeleo katika Jimbo la Kiteto wakati wa kipindi cha kampeni ni ukiukwaji mkubwa wa taratibu za uchaguzi, ambazo hazina budi kupata majibu ya kisheria.

Mbowe alisema kitendo hicho cha Shekifu ambaye ni kada wa CCM kufanya vitendo hivyo, ilikuwa ni ishara ya wazi kuwa alichokuwa akikifanya kilikuwa ni kampeni za wazi kwa mgombea wa chama hicho tawala.

Hata hivyo, kwa siku kadhaa sasa, Shekifu ambaye alikuwa mbunge hadi mwaka 2005, alikana kufanya kampeni kuisaidia CCM, kwa kusema kuwa ziara alizokuwa anazifanya ni za kawaida kwa yeye kama mkuu wa mkoa.

Alisema kuwa hakuna sheria inayomzuia yeye kutembelea eneo lolote la mkoa wake na kuwa hakufanya hivyo wakati huu kwa lengo la kumpigia kampeni aliyekuwa mgombea wa CCM bali kuhimiza maendeleo.

Kwa muda mrefu jana asubuhi, Mbowe alikuwa na kazi nzito ya kuwazuia wafuasi wa chama hicho wa maeneo yote ya Kibaya, waliokuwa wakitaka kuandamana kwenda kwenye ofisi za NEC kupinga matokeo hayo.

Vijana hao waliandaa mabango ambayo wangeyatumia katika maandamano yao lakini Mbowe aliwazuia akisema kuwa hakuna busara yoyote katika kufanya maandamano katika mazingira ambayo yalikuwepo jana mjini hapa.

“Turudi Dar es Salaam na tutafungua kesi. Hakuna haja ya kuandamana, mtaumizwa na polisi bila sababu,” alisema Mbowe na akawataka vijana hao kuwa watulivu, kwani mapambano ya kusaka ushindi huo bado hayajaisha.

Hata hivyo, aliwalaumu watu ambao walikubali kuingia katika mtego wa kuuza shahada zao na kubainisha kuwa wao ndio waliosababisha matokeo hayo yawe kama yalivyo.

Alisema kuwa chama hicho kina ushahidi wa tuhuma zote ambazo wamezitoa na hivyo wana uhakika wa kushinda katika kesi watakayofungua.

Mbali ya hilo, Mbowe alisema chama chake kinatarajia kufungua kesi ya kikatiba dhidi ya Daftari la Wapiga Kura ambalo limepoteza matumaini yaliyojengeka juu yake, hasa baada ya wapinzani wao kuanza kulitumia kujinufaisha.

Alisema iwapo hatua za makusudi na za mara moja hazitachukuliwa dhidi ya udhibiti wa Daftari la Wapiga Kura, basi litakuwa ni jambo gumu kwa wagombea wa kambi ya upinzani kushinda katika uchaguzi mwingine wowote.
 
Mtatafuta kila sababu.Ooh vyama ni vingi,Ooh sera ni mbovu,strategy hakuna.Kwa Tanzania hata vyama viungane watu watachagua CCM. In short watanzania wengi ni WAJINGA SAANA, na huu ndo ukweli hata kama ni mbaya.
Watanzania tunafanya siasa kama mpira kati ya Yanga na Simba ambapo effect zake huishia kwenye ushindi.Kwenye siasa mambo yanakwenda zaidi ya ushindi. Ushindi huu unagusa Maisha ya wananchi,Mambo ya sheria,Usimamizi bora wa Serikali,Uingiaji wa mikataba,Huduma kwa wananchi nk.Bila kujua huu ushindi tunaoufurahia una uhusiano gani na UCHAFU unaoendelea nchini.Tutaendelea kufanya siasa ni mpira.
 
Hii iacheni hapa kwa muda ijadiliwe halafu iunganisheni na zile zingine za uchaguzi Kiteto. Taarifa nilizozipata hivi karibuni ni kwamba kule Kiteto asilimia 30 za kura katika vituo vya vijijini zilichelewesha na kuletwa baada ya usiku wa manane. Huko ndipo ambapo CCM ilipata zaidi ya asilimia 90 ya kura wakati ilishindwa maeneo mengine yote.Huko ndipo idadi ya wapiga kura ilizidi asilimia 70 wakati ambapo maeneo mengine yote idadi ya wapiga kura ni wastani wa 47%. Ile ile staili ya Kibaka Kibaki wa Kenya ya kusubiria matokeo ya maeneo ya wapinzani wako, na kuitumia Tume ya Uchaguzi kuongeza matokeo kiasi kikubwa maeneo yaliyobaki na kujitangazia ushindi. Tujadili

Asha
 
Hii iacheni hapa kwa muda ijadiliwe halafu iunganisheni na zile zingine za uchaguzi Kiteto. Taarifa nilizozipata hivi karibuni ni kwamba kule Kiteto asilimia 30 za kura katika vituo vya vijijini zilichelewesha na kuletwa baada ya usiku wa manane. Huko ndipo ambapo CCM ilipata zaidi ya asilimia 90 ya kura wakati ilishindwa maeneo mengine yote.Huko ndipo idadi ya wapiga kura ilizidi asilimia 70 wakati ambapo maeneo mengine yote idadi ya wapiga kura ni wastani wa 47%. Ile ile staili ya Kibaka Kibaki wa Kenya ya kusubiria matokeo ya maeneo ya wapinzani wako, na kuitumia Tume ya Uchaguzi kuongeza matokeo kiasi kikubwa maeneo yaliyobaki na kujitangazia ushindi. Tujadili

Asha


Dear Asha , sasa baada ya haya kujiri ina maana sasa kuna ushahidi wa kutosha wa uchafu wote .Je Chadema wana mpango gani ? Wamekubali kushindwa ama wanaenda Mahakamani ? Je si wakati sasa wapinzani kupeleka hoja ama kudai katiba na Tume ya Uchaguzi iwe ya wote ?
 
Hii iacheni hapa kwa muda ijadiliwe halafu iunganisheni na zile zingine za uchaguzi Kiteto. Taarifa nilizozipata hivi karibuni ni kwamba kule Kiteto asilimia 30 za kura katika vituo vya vijijini zilichelewesha na kuletwa baada ya usiku wa manane. Huko ndipo ambapo CCM ilipata zaidi ya asilimia 90 ya kura wakati ilishindwa maeneo mengine yote.Huko ndipo idadi ya wapiga kura ilizidi asilimia 70 wakati ambapo maeneo mengine yote idadi ya wapiga kura ni wastani wa 47%. Ile ile staili ya Kibaka Kibaki wa Kenya ya kusubiria matokeo ya maeneo ya wapinzani wako, na kuitumia Tume ya Uchaguzi kuongeza matokeo kiasi kikubwa maeneo yaliyobaki na kujitangazia ushindi. Tujadili

Asha

kwani chadema hakupeleka mawakala wao huko au ilikuwaje,ninavyoelewa mimi ni kuwa kura zinaesabiwa vituoni au kama kuna utaratibu mwingine sijui.
 
Chadema wanaweza kudai mahakama itengue ubunge wa Kiteto, wakitaka wanasheria wanaweza kulitekeleza hilo kwani Bw. Mbowe ameeleza kwamba unao ushahidi wa kukiukwa kwa taratibu za uchaguzi kama vile kuwatishia wapiga kura, kununua shahada za wapiga kura, vurugu nk.
Hata hivyo kesi hiyo itatolewa hukumu 2010, wakati wa uchaguzi ujao.

Hata hivyo ni kweli Chadema wameibiwa kura? au uchaguzi umehujumiwa? sikubaliani kwamba style ya Kibaki ilitumika kwani Chadema ilitumia mawakala machachari akina Zitto, Mdee, Komu nk.

shida iliyopo ni kasumba ya wanakiteto (huenda maeneo mengi ya Tanzania) kwamba CCM ndiyo chama stahili. Kumbuka kwamba viongozi wa vijiji wanasikilizwa sana.

Vyama vya upinzani vinapaswa kuwa na mikakati ya kushida kwenye vitongiji, vijiji then ubunge na Urais.
 
Dear Asha , sasa baada ya haya kujiri ina maana sasa kuna ushahidi wa kutosha wa uchafu wote .Je Chadema wana mpango gani ? Wamekubali kushindwa ama wanaenda Mahakamani ? Je si wakati sasa wapinzani kupeleka hoja ama kudai katiba na Tume ya Uchaguzi iwe ya wote ?

Mbowe kasema wanaenda mahakamani. Lakini hujuma za CCM zilianza pale walipoiga kutumia chopa na chopa la CHADEMA likapata mushkeli pale Dodoma. Nafikiri CCM walishinda kabla ya uchaguzi kwani yule mwimba kwaya alishasema......
 
Hapo CHADEMA mmeshindwa tu na inabidi mkubali. Sisemi CCM wameshinda kwa
haki maana miaka na miaka wanafanya madudu hayo hayo ila tu pale ambapo Wapinzani wana washabiki wengi, hata CCM wafanye madudu vipi, bado Upinzani watashinda tu.

Kama jimbo liko nusunusu, hapo ndipo CCM wanapotumia kila njia na kushinda.

Nafikiri upinzani inabidi kuandaa mikakati mingine na mipya hasa kwa majimbo ya vijijini. Hii ilikuwa nafasi nzuri kweli ya upinzani kushinda Kiteto, binafsi nimeskitishwa sana na hayo matokeo maana nilitegemea uwe ndio mwanzo wa mabadiliko.

Tuanze kujiandaa sasa maana 2010 sio mbali.
 
Sina haja ya kufanya utafiti wowote. Ukweli wa jinsi CCM inavyoiangamiza nchi uko wazi na sidhani kama hizo kashfa kibao hazigusi maisha ya wananchi wa Kiteto. Vipaumbele gani tofauti walivyokuwa navyo zaidi ya kuboresha maisha yao ya kila siku!? 😕
Labda unaweza kuwa katika nafasi nzuri ya kutufahamisha vipaumbele vyao tofauti na vya Watanzania wengine.


Sadakta!!!
Wamechagua CCM ili waweze kuboresha maisha yao ya kila siku.


Hata hivyoBubu ataka kusema ninakushauri siku nyingine usikate tamaa ongeza bidii ya kufanya utafiti, vinginevyo utakuwa unapoteza wakati mwingi kwenye malumbano pasi na kufaidika
 
MOD: Nawaombeni hii muiche yenyewe kwa siku chache ijadiliwe na baadaye muinganishe pamoja na thread zingine ambazo zimeshajadili uchaguzi wa Kiteto.

Watu kadhaa mmeuliza maoni yangu kuhusu uchaguzi wa Kiteto, kabla sijaanza kujadili mtizamo wangu- someni kwanza hapa msimamo wa kina wa CHADEMA kuhusu yaliyojiri katika Uchaguzi wa Kiteto: http://www.chadema.net/tamko/2008/kiteto.php

Kwa wale mnaofahamu 'the science and art of rigging elections' mtajua kwamba uwizi katika uchaguzi haufanywi kwa njia moja, ni mkusanyiko wa njia mbalimbali ambapo kila moja inatumika kuathiri matokeo kwa maana ya kuongeza au kupunguza idadi fulani ya kura. Jumla ya mbinu zote ndizo huzaa matokeo fulani ambayo yanakuwa yamepangwa.

Nawaomba tusome kwa makini ukurasa hata ukurasa katika tamko hili la kurasa tano. Nitarejea kutoa maoni yangu

JJ
 
Tamko hili tulikujibu siku za nyuma.unganisha na ile thread.
 
MOD: Nawaombeni hii muiche yenyewe kwa siku chache ijadiliwe na baadaye muinganishe pamoja na thread zingine ambazo zimeshajadili uchaguzi wa Kiteto.

Watu kadhaa mmeuliza maoni yangu kuhusu uchaguzi wa Kiteto, kabla sijaanza kujadili mtizamo wangu- someni kwanza hapa msimamo wa kina wa CHADEMA kuhusu yaliyojiri katika Uchaguzi wa Kiteto: http://www.chadema.net/tamko/2008/kiteto.php

Kwa wale mnaofahamu 'the science and art of rigging elections' mtajua kwamba uwizi katika uchaguzi haufanywi kwa njia moja, ni mkusanyiko wa njia mbalimbali ambapo kila moja inatumika kuathiri matokeo kwa maana ya kuongeza au kupunguza idadi fulani ya kura. Jumla ya mbinu zote ndizo huzaa matokeo fulani ambayo yanakuwa yamepangwa.

Nawaomba tusome kwa makini ukurasa hata ukurasa katika tamko hili la kurasa tano. Nitarejea kutoa maoni yangu

JJ

Mr. John Mnyika

Ahsante sana kwa taarifa lakini naomba kuuuliza haya

a) Hivi ni kweli asilimia 77 ya wananchi wa kiteto hawajui kusoma na kuandika?....idadi hii mbona inaonekana kuwa kubwa sana.

b) Kama mnalalamika kwamba mambo mengi yamepindishwa mbona nasikia mlikubali kushindwa?

c) Kama tuhuma zinazoelezwa umo ni za kweli (baiskeli, kugawa cement, wakuu wa mikoa 2 kutembelea Kiteto kufanya kampeni na mwingine kutembelea miradi ya mandeleo...) sasa kwa nini msipeleke kesi mahakamani kudai uchaguzi ubatilishwe?

d) Hivi madai ya kwamba CCM imetumia takribani bilioni 1 ni ya kweli na kuna jinsi ya kuweza kuthibitisha? Kama hii ni kweli basi inabidi JF na wengine wote wanaoitakia nchi yetu mema kufanya uchunguzi wa kina na hasa kwenye chaguzi zijazo maana hii imenitisha sana kwa kweli.

e) Na mwisho Mr. Mnyika na wenzako wa CHADEMA mna mikakti ipi ya 2010 na kuendelea? Maana mambo ya kukurupuka wakati wa uchaguzi hayana maana yoyote...je unaweza kutupatia mpango mkakati wenu wa miaka 3, 5 hadi 10 ijayo? au mnavamia mambo tu...mkishapigwa chini na CCM mnaanza kutafuta visingizio kibao? Tafadhali tuelezeni tujue....

Kazi njema na naomba ujumbe wangu mfikishie mwenyekiti, Katibu Mkuu na wakurugenzi pamoja na wanachama wenu wote....

Mkiwa na mikakati kamili na njia mbadala ya kupambana na CCM mtaweza kushinda....

Mungu Ibariki Tanzania......
 
mtalii tupe link....sometimes tunaogopa kuspend mda mwingi ktk net...tuwekee link...then sema iunganishwe kama kaka GameTheory afanyavyo
 
MOD: Nawaombeni hii muiche yenyewe kwa siku chache ijadiliwe na baadaye muinganishe pamoja na thread zingine ambazo zimeshajadili uchaguzi wa Kiteto.

Watu kadhaa mmeuliza maoni yangu kuhusu uchaguzi wa Kiteto, kabla sijaanza kujadili mtizamo wangu- someni kwanza hapa msimamo wa kina wa CHADEMA kuhusu yaliyojiri katika Uchaguzi wa Kiteto: http://www.chadema.net/tamko/2008/kiteto.php

Kwa wale mnaofahamu 'the science and art of rigging elections' mtajua kwamba uwizi katika uchaguzi haufanywi kwa njia moja, ni mkusanyiko wa njia mbalimbali ambapo kila moja inatumika kuathiri matokeo kwa maana ya kuongeza au kupunguza idadi fulani ya kura. Jumla ya mbinu zote ndizo huzaa matokeo fulani ambayo yanakuwa yamepangwa.

Nawaomba tusome kwa makini ukurasa hata ukurasa katika tamko hili la kurasa tano. Nitarejea kutoa maoni yangu

JJ

Sasa tukasome nini na wewe ushatuambia "mmeibiwa" kwa njia mbalimbali.

Since when u conceaded defeat? u will always have excuses to justify u failure...
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom