Uchaguzi wa Kiteto: Taarifa mbalimbali

Uchaguzi wa Kiteto: Taarifa mbalimbali

Status
Not open for further replies.
Unajua Mwanakiji Kuna Watu Tunao Humu Jf Lkn Akili Zao Zimeshikwa Na Mafisadi,sasa Nyie Mnaona Raha Gani Ccm Kushinda?halafu Miongoni Mwa Hao Wanaoshangilia Huo Ushindi Hata Kadi Ya Ccm Hana Sasa Si Aibu Hh,au Ndio Mnafikiri Wote Walio Hapa Jf Ni Wapinzani Wa Ccm?tuliowengi Si Wana Ccm Wala Wa Pinzani Wa Ccm,ss Tunataka Kuona Maendeleo Yanapatikana Huko Bongo.kwa Maana Nyingine Tunataka Habari Zinazowachomoa Mafisadi Katika Mashimo Yao .

Kaboka,

Wewe na wananchi wa Kiteto waliopiga kura nani anafahamu hao wagombea... wewe au wao!!!

Mbona CCM kuna sehemu haitii mguu inagombea tu kwa mazoa kama majimbo ya Karatu(Dr. Slaa), Moshi Mjini(Ndesamburo)!!! ni kwa sababu mtu yuko capable... wananchi wanafahamu kwanini wamchague nani, Kule Kiteto hawakuwa wanachagua mbunge wa Taifa walikuwa wanachagua mbunge wa Kiteto....

Upinzani kama uko makini kuna majimbo ya kukomba kwa urahisi... na ni ya Mjini, kuna jimbo kama la Kinondoni... ukiweka mtu mzuri kama Kitila lazima alambe...

Tuwe makini tusitukane wananchi!!! wananchi hao hao ndio Upinzani na CCM wanawahitaji ili wawekwe madarakani...

Ukiwa makini pia utasema CCM walikuwa nayo siku zote,,, lakini Mbowe, Zitto n.k. wamefika wakati wa uchaguzi tu...

Kuhusu idadi ya wapiga kura kuwa ndogo,,, ni muhimu kujua sasa ni kipindi cha kiangazi au la!!! si unajua wakati wa kiangazi... tena tunahamisha mifugo yetu....

Mkitaka wawe wengi, mubadilishe sheria ya uchaguzi kwamba kwenye majimbo ya wafugaji,,, uchaguzi ufanyike wakati wa nyasi za kulishia zikiwa za kutosha
 
Chadema wanapaswa kuondokana na upuuzi wa kudhani kuwaonyesha wananchi 'helikopta' ndio mvuto mkubwa wananchi wawape kura. If anything, this in itself should be reason enough to vote against them.

..halafu ccm wakafuata ujinga huo huo!

Nakubaliana na mawazo ya Mkjj. Kila uchaguzi unategemea umejipanga vipi, na ni mikakati ipi umeiweka kufanikisha azma yako ya uchaguzi. Je, unawajua vizuri wapiga kura wako? Unayajua vizuri mahitaji yao?

..tukifika huku tanzania ndio itakuwa huru!

Huwezi kwenda tu kuomba kura kwa kelele za jukwaani. Mgombea wa Chadema alishagalagazwa mara kadhaa katika jimbo hilo hilo. Je, kabla ya kumteua tena kugombea mara nyingine, walijiuliza ni sababu zipi zilizokuwa zinamfanya ashindwe; na kama walizijua, ni yapi waliyokuwa wameyafanya safari hii ili aweze kukubalika zaidi!

..watajifunza kutokana na makosa, kama wao ni wanafunzi makini lakini. mwanafunzi jeuri huwa hafaulu hata siku moja.

Chadema, kama chama inawabidi pia wakae chini ili wajitazame upya. Their top leadership may not be inspiring enough to the wananchi.

..tatizo sio top leadership pekee,bali ni leadership in chadema!

..they need leaders!
 
kuna kitu ambacho hukielewi katika siasa. Tatizo la watanzania wengi wanachagua chama wala si sera. Sisemi kama wapinzani ni bora, au CCM ni bora zaidi bali ni jambo la kujiuliza huo ushindi wa CCM kiteto hutaleta maendeleo gani? Je naweza pata jibu (quantify jibu lako). Nafikiri kabla ya kushangilia huo ushindi basi vinjari wilaya ya kiteto, kisha kwa dhati kabisa usimame kushangilia huo ushindi.


Nakubaliana nawe asilimia 100.Dae Es Salaam watch your language.Hukatazwi kushangalia CCM lakini hapa si mahala pa kufanya mambo ya muhimu kama mpira wa miguu.Siasa hizi zinagusa maisha ya watu kabisa na si kuleta kejeli za JK kuwaita wapinzani watani wa jadi .This I find it always low .Siasa si kama mnavyo taka tuelewe.Tuongee issue hii bila kuonyesha kwamba jambo la mzaha tu.Hakuna mzaha hapa maana wana siasa ndiyo wanao amaua Watanzania wa Kiteto na kwingineko waishi vipi kwa hali .Kushindwa kupo na kushinda kupo.Lakini ningalikuwa wewe nisingaliweza kushangalia ushindi ambao hata damu za watu zimemwagika , Serikali na polisi wameingilia ka ku force ushindi .Mkuu wa Mkoa Shekifu alikuwa huko muda na yule mwingine toka Iringa nk .Tunajua CCM walitaka hili jambo to foos us kwamba wanakubalika .Kama wanakubalika basi wabadilishe vipengele vya katiba na hatimaye Tume ya Uchaguzi iwe na watu wote maana wa serikali wameshindwa kuwa wakweli bali kuibeba CCM sawa na Polisi na wengine wote .

Komba kafanya vurugu za wazi kabisa hajachukuliwa hatua hata moja lakini angalifanya Slaa ama Zitto ungalisikia matangazo na kipigo na kesi Mahakamani.Bado una akili timamu unataka kuleta suhabiki ? You can do this lakini nenda kule Tazama, IPP Media, Rai nk .

Tunakubalia Chadema kushindwa lakini isiwe ushabiki wa kijinga na kutufanya kjuongea kama sisi wote ni wapuuzi no .
 
vigelegele...! ujanja ni kupata siyo kuwahi!

Kidumu chama "chetu" kitukufu!

Asanteni.
 
Yapata 40,000 awakupiga kura! wote wamepoteza kadi hati zao kupigia kura!
Ushindi wa ccm ulitegemwa maana wanaweza kuwanunua Wtz masikini hata kwa pair moja ya kanga. naweza kuwa mzito wa kuelewa, lakini nikiona gharama za kampeni za uchaguzi ni kubwa sana. Sijui kwa nini hiyo pesa hawa CCM wetu wasifanye kweli kwa kutoa huduma kwa hawa wapiga kura wasiojua hata kura zao zinawagharimu kiasi gani.
 
Bado napata shida sana kuamini kama ni kweli na kwa dhati kabisa hawa ndugu zetu wa kiteto wameichagua sisiem kwa sababu wameridhika na yale inayowafanyia,na kwa hiyo wako tayari kuendelea kuvuna yale yale ambayo wamekuwa wakiyapata. Shuda yangu inapata nguvu zaidi hasa baada ya kusikia(sijathibitisha) kuwa chadema waliongoza katika maeneo ya mijini zaidi tofauti an wenzao ccm waliowekeza zaidi bush. Kama ndivyo ilivyo, basi picha inayojitokeza hapa ni kuwa aidha ccm wamekuwa wakitoa upendeleo kwa watu wa vijiji zaidi kuliko kwa wale wa town katika kuwahudumia au hawa ndugu zangu wa town ambao nadhani hawahitaji helkopta ili kuhamasika,wana chuki binafsi na ccm.
 
Yapata 40,000 awakupiga kura! wote wamepoteza kadi hati zao kupigia kura!
Ushindi wa ccm ulitegemwa maana wanaweza kuwanunua Wtz masikini hata kwa pair moja ya kanga. naweza kuwa mzito wa kuelewa, lakini nikiona gharama za kampeni za uchaguzi ni kubwa sana. Sijui kwa nini hiyo pesa hawa CCM wetu wasifanye kweli kwa kutoa huduma kwa hawa wapiga kura wasiojua hata kura zao zinawagharimu kiasi gani.

Twatafuta malisho ya mifugo kaka!!! kipindi cha kiangazi hiki ati!!! Alafu achia yule mlinzi wako akapige kura basi!!!
 
Bado napata shida sana kuamini kama ni kweli na kwa dhati kabisa hawa ndugu zetu wa kiteto wameichagua sisiem kwa sababu wameridhika na yale inayowafanyia,na kwa hiyo wako tayari kuendelea kuvuna yale yale ambayo wamekuwa wakiyapata. Shuda yangu inapata nguvu zaidi hasa baada ya kusikia(sijathibitisha) kuwa chadema waliongoza katika maeneo ya mijini zaidi tofauti an wenzao ccm waliowekeza zaidi bush. Kama ndivyo ilivyo, basi picha inayojitokeza hapa ni kuwa aidha ccm wamekuwa wakitoa upendeleo kwa watu wa vijiji zaidi kuliko kwa wale wa town katika kuwahudumia au hawa ndugu zangu wa town ambao nadhani hawahitaji helkopta ili kuhamasika,wana chuki binafsi na ccm.


Wa town wako kama 99% ya wana JF ambao wanajua mambo .Hawajali Chama ila wanataka kuona Nchi yao inasonga mbele kwa maendeleo.Leo ukiweka kura JF naamini CCM hawataona ndani na ushahidi umeuona hata Mwema na kundi lake wakaamuwa kuwamata vijana wetu kwa sababu ambazo sizijui wala wewe .Wajanja wote wanaokataa CCM .Ukimuona mjanja anaipenda CCM jua yuko highly connected na UFISADI .
 
.Dae Es Salaam watch your language.Hukatazwi kushangalia CCM lakini hapa si mahala pa kufanya mambo ya muhimu kama mpira wa miguu.Siasa hizi zinagusa maisha ya watu kabisa na si kuleta kejeli za JK kuwaita wapinzani watani wa jadi .This I find it always low .Siasa si kama mnavyo taka tuelewe.Tuongee issue hii bila kuonyesha kwamba jambo la mzaha tu.Hakuna mzaha hapa maana wana siasa ndiyo wanao amaua Watanzania wa Kiteto na kwingineko waishi vipi kwa hali .Kushindwa kupo na kushinda kupo.Lakini ningalikuwa wewe nisingaliweza kushangalia ushindi ambao hata damu za watu zimemwagika , Serikali na polisi wameingilia ka ku force ushindi .Mkuu wa Mkoa Shekifu alikuwa huko muda na yule mwingine toka Iringa nk .Tunajua CCM walitaka hili jambo to foos us kwamba wanakubalika .Kama wanakubalika basi wabadilishe vipengele vya katiba na hatimaye Tume ya Uchaguzi iwe na watu wote maana wa serikali wameshindwa kuwa wakweli bali kuibeba CCM sawa na Polisi na wengine wote .

Komba kafanya vurugu za wazi kabisa hajachukuliwa hatua hata moja lakini angalifanya Slaa ama Zitto ungalisikia matangazo na kipigo na kesi Mahakamani.Bado una akili timamu unataka kuleta suhabiki ? You can do this lakini nenda kule Tazama, IPP Media, Rai nk .

Tunakubalia Chadema kushindwa lakini isiwe ushabiki wa kijinga na kutufanya kjuongea kama sisi wote ni wapuuzi no .
Kama kawaida yenu mmeshaanza kuchonga na lawama kibao...
 
Ama kweli mwanakijiji leo kachanganyikiwa amefikia kutoa Thanks na lile jina lake la "mwafrika wa kike" ambapo mjadala huu halijachangia kitu. teh teh teh teh

bangi zingine sijui zinamhitaji invisible aje kujibu kuwa mwanakijiji sio mwafrika wa kike?!.... anyway wewe endelea kuchonga maana naona baada ya juhudi za kushindwa kuizima JF sasa kuna new memberz kibao wamejiunga hapa JF!
 
Unajua wapinzani hawana sera hichi kibano wakizoee mpaka siku ile watakapobadirika na sera zao.
watu hatuoni kwanini wapewe CHADEMA/CUF/NCCR ambao hawafahamiki namna ya uendeshaji wao.

Maana kimantiki wapinzani hawatofautiani na CCM sasa basi kwanini ufanye majaribio ???

Mie naona udhaifu wa wapinzani ni huu mtindo wao eti kuibua uozo wa mwazako na kuufanya SERA,kuibua uozo ni vyema lakini kuufanya ndio mgongo wa kupandia ni makosa makubwa ,hii naifananisha kama mtu yule anayemtaka mwanamke kwa gia za kumuambia maovu ya mwanaume aliyenaye.Mwanaumme aliyenaye anaweza akawa muovu sana lakini wewe kupitia mgongo huo ili ufanikishe adhima yako na kama mwanamke huyo ni makini hakika hutompata.

Wapinzani kama wapo tofauti na CCM hawakuhitaji kuruka na ndege angani kupoteza fedha nyingi kwa kutangaza sera za maneno ,bali sera zao zingejitangaza zenyewe kwa kufanya hivi-

Wapinzani nendeni huko kijijini mnakoruka na madege wakati tu wa uchaguzi kafanyeni harambee/tafuteni wadhamini wapelekeni huduma ya maji,umeme.

wapinzani nendeni huko mkahamasishe watu muwaelimishe jinsi ya kufanya kilimo cha kipande kidogo na kuvuna mavuno yenye tija.

wapinzani kahamasisheni huko vijijini kwa miharambee/wadhamini watu wapate muamko wa kilimo cha kutumia matrekta.

wapinzani hamasisheni wananchi/wadhamini kujengea vyuo vikuu vingi nchini ili wananchi wapate kuelimika.
Hakika mkijitahidi hata kwa nusu ya hayo mtapata kura nyingi za tsunami ambazo hata wezi wa kura wataona aibu yenyewe na mtazipata bila jitihada zozote za kuruka na ndege angani .

Mnavyofanya saizi hamna tofauti na CCM ndio maana hatuna sababu ya kuwapa kura.


Tunawapongeza CCM kwa kushinda hicho kiti pia tunawapongeza CHADEMA kukubali matokeo. Kuvunjika kwa koleo si mwisho wa uhunzi. Kama mlivyozunguka wakati wa Zito sasa muanze mapema. Ushindi upo lakini kwa kazi na si katika sahani. Tujenge nchi yetu kwa kuongeza nguvu kwa upinzani CCM kujisahihisha ni kini macho.
 
Nashindwa kuwaelewa watu ambao bado wanaipigia kura CCM.

Baada ya maskendo yote haya,je hawa watu hawaoni?

Je ni kitu gani CCM imewafanyia?

Nimechanganyikiwa !
 
Nashindwa kuwaelewa watu ambao bado wanaipigia kura CCM.

Baada ya maskendo yote haya,je hawa watu hawaoni?

Je ni kitu gani CCM imewafanyia?

Nimechanganyikiwa !

Walioipigia kura ccm mkuu ni haki yao kikatiba kuipigia sisiemu kura na wala usishangae wala kuchanganyikiwa.
 
wapinzani nendeni huko mkahamasishe watu muwaelimishe jinsi ya kufanya kilimo cha kipande kidogo na kuvuna mavuno yenye tija..

Tunawapongeza CCM kwa kushinda hicho kiti pia tunawapongeza CHADEMA kukubali matokeo. Kuvunjika kwa koleo si mwisho wa uhunzi. Kama mlivyozunguka wakati wa Zito sasa muanze mapema. Ushindi upo lakini kwa kazi na si katika sahani. Tujenge nchi yetu kwa kuongeza nguvu kwa upinzani CCM kujisahihisha ni kini macho.
 
umaskini kwa kwenda mbele,endeleeni tuu kuwachagua ila msije hapa mnalia Buzwagi wala BOT na Richmond...miaka karibu 50 ya uhuru hakuna umeme wala maji,sanasana ni rushwa tuu na wizi,mungu awasaidie kuwaonyesha njia maana hiyo ni disease.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom