Uchaguzi wa Kiteto: Taarifa mbalimbali

Uchaguzi wa Kiteto: Taarifa mbalimbali

Status
Not open for further replies.
baada ya tamaa ya fisi kuona kuwa mkono wa binaadamu utaanguka wapinzani waliona kuwa CCM ambayo kwa sasa ina kazi kubwa ya kujisafisha na kujipanga itapoteza jimbo la kiteto.

wakawa na tamaa ya kuwa CCM itaanguka tu, wakaenda kwa majigambo na kedi, wakajiamini kupita kiasi.

magazeti yakanadi hapa JF kina Mkjj na wenziwe wakajilabu vya kutosha kuwa kipindi hiki wapinzani watatoa somo ambalo CCM hawatalisahau.

lakini baada ya kuona kinyume wazee wetu wamenywea hakuna breaking news wala cha nn kimya utadhani hakuna uchaguzi.


kilichobaki ni kusubiri matetezi ya ndugu zetu wapinzani.

wapinzani jee umoja wao utadumu?

jee watasoma alama za nyakati au watasubiri huruma ya wananchi bila ya jasho?

hivi ni kweli wananchi ni wajinga wakikichagua CCM ?


lini hii jeuri ya kuwadharau wananchi itakoma kwa wananchi?


lengo la CCM ni kuhakikisha bunge la 2010 kuwe hakuna wapinzani bungeni isipokuwa wapemba tena na huko tutagawana nusu kwa nusu.


tutawafunza kuwa jeuri si maungwana na siasa si lelemama

Hii kiboko!
Yaani kura 1000 walizopishana ndio za "KUGARAGAZWA"? Ingekuwa kura 10000 je ungesemaje?
Hata hivyo hongereni kwa ushindi, tuchape kazi tujenge taifa, uchaguzi ushaisha.
 
Ndio nasema hoja zetu nyingi zimejengwa katika misingi ya hisia kiasi kwamba inakuwa vigumu sana kutoa counter-argument. Angalau kwa habari ambazo tulikuwa tunasoma kwenye magazeti tunajua hili sio kweli. Sio kweli kwa sababu huyu mgombea wa CCM alikuwa hawezi kabisa kuongea na ilifika mahala akipanda jukwaani wananchi wanamzomea. Siku za mwisho za kampeni ilibidi viongozi wa CCM waache kumsimamisha jukwaani ili kuepuka aibu ya kuzomewa. Kwa hiyo kimsingi wananchi wale wamechagua chama zaidi kuliko mgombea. Hii pia inajibu hoja ya Kasheshe.

Tunatambua sana kwamba hii biashara ya kujenga chama mbadala haitakuwa rahisi maana tunapambana na chama ambacho kimejijengea sura ya unchi kwa muda mrefu kwa juhudi zetu sote. Sasa tunachotarajia kutoka kwa colleagues kama JF members sio kejeli bali kutiwa moyo ili tuendelee na mapambano. Ndiyo CHADEMA wameshindwa Kiteto; lakini tutakuwa naive kukataa ukweli kwamba walipambana na juhudi hizo zinajionyesha katika idadi ya kura walizopata. Ni kweli pia kwamba lazima CHADEMA na upinzani kwa ujumla wajipange vizuri zaidi kwa ajili ya chaguzi zijazo na pengine kubadilisha mbinu na tunashukuru kwa wale wanaotoa mchango wa namna ya kuisadia CHADEMA ijipange. Tunapokea vijembe vya watu kama akina Mtu wa Pwani maana hawa tunajua ni watani zetu. But I don't expect other JF analysts to be simplistic and in their analysis in their attribution of CHADEMA's failure in Kiteto.

Kitila,

Historia iko upande wa CHADEMA na sidhani kama huu ni wakati wa kukata tamaa. Uchaguzi umefanyika na ccm wametangazwa washindi na hakuna mtu atakayekumbuka alichofanya Komba na Msekwa.

Hili lilikuwa jaribio zuri na hongera CHADEMA kwa kazi nzuri.
 
WAKUU KITILA NA LUNYUNGU,
WITH DUE RESPECT, PAMOJA NA MAPENZI MLIYONAYO KWA CHADEMA TUKUBALIANE KUWA MZEE KIMESERA HAKUWA MGOMBEA BORA KUTOKA KATIKA KAMBI YA UPINZANI, ALIKUWA NI 'BORA MGOMBEA'. KILICHOFANYIKA KUMTEUA MZEE KIMESERA SIYO OVERSIGHT, BALI INAONYESHA SIASA ZA UBWANYENYE ZILIVYOSHEHENI NDANI YA CHADEMA. WATU KADHAA WAMEKUWA WANALIONA HILI NA WANAJARIBU KULISEMA FROM TIME TO TIME LAKINI INAONEKA KUVUNJA BARRIERS ZILIZOPO ZA UBWANYENYE NDANI YA CHADEMA NI SAWASAWA NA KUJIFUNGULIA MLANGO WA KUTOKA NJE. YANAHITAJIKA MAPINDUZI YA KWELI NDANI YA CHADEMA LAKINI JE, NANI YUKO TAYARI KUMFUNGA PAKA KENGELE? MWENYEKITI MBOWE HAWEZI KULETA MAPINDUZI YA KWELI NDANI YA CHADEMA KWA SABABU YEYE ANATOKA NA MFUMO WA MABWANYENYE.
KIPINDI HIKI TULICHONACHO NI WAKATI MUAFAKA KWA CHADEMA KUJIIMARISHA KIUONGOZI NA KUTOA SURA YA KUWA NI CHAMA CHA WANANCHI ZAIDI YA WANACHAMA HII ITASAIDIA KUONDOA UBWANYENYE NDANI YA CHAMA.

Nilidhani mapinduzi yanatakiwa yafanywe ndani ya ccm ili nchi isiendelee kuuzwa kama ilivyo sasa?
 
I agree. Picha ambayo naanza kuipata ni kwamba kuna mambo ambayo sisi tunafikri ni matatizo wananchi wa kawaida hawaoni kama ni shida. Kwa mfano, hili swala la ufisadi sidhani kama watanzania wa maeneo ya Kiteto na kwingineko wanafikiri ni matatizo yanayowahusu. Yaani hawawezi kuoanisha kabisa kati ya shida walizo nazo na wizi wa pesa za serikali unaofanywa na CCM. Vinginevyo isingewezekana waichague CCM au kumshangilia Lowasa kwa kiwango tulichoona. Hapa ndipo nitakubaliana na Einstein kwamba "Siasa ni Ngumu Kuliko Fizikia"!

..nadhani unakumbuka ulipokuwa ukibadilishana mawazo na jamaa wa kijiji[au kutoka huko]ulipokuwa unarudi nyumbani likizo. what you learned in those days,still applies todate! ujinga ni mwingi. na dawa ya ujinga si propaganda[unaumwa malaria,unahitaji dawa yake na si panadol ya kupunguza maumivu]ni elimu na habari!

..sasa,huku sisi[na mola jaalia tuna ka-elimu kidogo]tuna elimishwa kila leo na habari ziko upenuni tu! wao wala hawana habari. unafikiri huwa wanayaona hayo majumba ya mbezi beach na hizo vogue au mark x kama mimi nawe?

..kazi ngumu! vyama vingine[ccm kando]vitahitaji kufanya kazi na kupiga fitna sawia, ili viweze kupata angalau "maji ya kunywa" achilia mbali hicho "chakula".

..na kwa wale wasiofahamu,hata ingekuwa chadema,wasingekubali jimbo liende kwa ccm kirahisi!hata wao wangetumia mbinu zote walizonazo chini ya mvungu kushinda. ila ustaarabu umeonekana katika kukubali mapema,kupitia tanzania daima ofcourse!
 
WAKUU KITILA NA LUNYUNGU,
WITH DUE RESPECT, PAMOJA NA MAPENZI MLIYONAYO KWA CHADEMA TUKUBALIANE KUWA MZEE KIMESERA HAKUWA MGOMBEA BORA KUTOKA KATIKA KAMBI YA UPINZANI, ALIKUWA NI 'BORA MGOMBEA'. KILICHOFANYIKA KUMTEUA MZEE KIMESERA SIYO OVERSIGHT, BALI INAONYESHA SIASA ZA UBWANYENYE ZILIVYOSHEHENI NDANI YA CHADEMA. WATU KADHAA WAMEKUWA WANALIONA HILI NA WANAJARIBU KULISEMA FROM TIME TO TIME LAKINI INAONEKA KUVUNJA BARRIERS ZILIZOPO ZA UBWANYENYE NDANI YA CHADEMA NI SAWASAWA NA KUJIFUNGULIA MLANGO WA KUTOKA NJE. YANAHITAJIKA MAPINDUZI YA KWELI NDANI YA CHADEMA LAKINI JE, NANI YUKO TAYARI KUMFUNGA PAKA KENGELE? MWENYEKITI MBOWE HAWEZI KULETA MAPINDUZI YA KWELI NDANI YA CHADEMA KWA SABABU YEYE ANATOKA NA MFUMO WA MABWANYENYE.
KIPINDI HIKI TULICHONACHO NI WAKATI MUAFAKA KWA CHADEMA KUJIIMARISHA KIUONGOZI NA KUTOA SURA YA KUWA NI CHAMA CHA WANANCHI ZAIDI YA WANACHAMA HII ITASAIDIA KUONDOA UBWANYENYE NDANI YA CHAMA.

Mzee Pundamilia, katika netiquette kuandika kwa herufi kubwa tupu maana yake ni "kushout" kwa maana ya kupiga kelele. Sidhani kama hilo ni kusudio lako kwani ulichosema ni muhimu mno na ni hoja inayohitaji kujibiwa lakini kwa vile unapiga kelele basi reaction ya kwanza ya wasomaji kama mimi ni "negative" (ni kama mtu anakuambia jambo la maana huku anakubwakia sikioni). Ila hoja yako ni hoja nzito ila haiwi nzito kwa vile umepiga kelele, bali kutokana na mantiki ndani yake.
 
Wewe watukane wazee wako tu.. wakichagua chadema/wapinzani ndio wanakuwa werevu?

Mafisadi aliwachagua nani? Basi naona tuamue moja kuchagua mafisadi na kuacha kulalamika kuwa wametuibia sijui Buzwagi/Richmond/EPA etc au kutibu kansa yetu all-together..kwa kuwafurusha kwa kura zetu..

Tuamue moja, sio kuwa vigeugeu..We can't have both..
 
..nadhani unakumbuka ulipokuwa ukibadilishana mawazo na jamaa wa kijiji[au kutoka huko]ulipokuwa unarudi nyumbani likizo. what you learned in those days,still applies todate! ujinga ni mwingi. na dawa ya ujinga si propaganda[unaumwa malaria,unahitaji dawa yake na si panadol ya kupunguza maumivu]ni elimu na habari!

..sasa,huku sisi[na mola jaalia tuna ka-elimu kidogo]tuna elimishwa kila leo na habari ziko upenuni tu! wao wala hawana habari. unafikiri huwa wanayaona hayo majumba ya mbezi beach na hizo vogue au mark x kama mimi nawe?

..kazi ngumu! vyama vingine[ccm kando]vitahitaji kufanya kazi na kupiga fitna sawia, ili viweze kupata angalau "maji ya kunywa" achilia mbali hicho "chakula".

..na kwa wale wasiofahamu,hata ingekuwa chadema,wasingekubali jimbo liende kwa ccm kirahisi!hata wao wangetumia mbinu zote walizonazo chini ya mvungu kushinda. ila ustaarabu umeonekana katika kukubali mapema,kupitia tanzania daima ofcourse!

Mabadiliko ya kweli hayaji bila kuwa na mazingira muafaka ya kufanya watu wakataka mabadiliko kwa gharama yoyote ile. Kwa sasa sisiemu wanatengeneza hayo mazingira kwa kufilisi nchi na kutajirisha watu mia moja (sera ya Kikwete).

Baada ya muda, kanga na kofia havitamnunua mtu ambaye hana chakula cha mwezi mzima!
 
Ama kweli mwanakijiji leo kachanganyikiwa amefikia kutoa Thanks na lile jina lake la "mwafrika wa kike" ambapo mjadala huu halijachangia kitu. teh teh teh teh

Chadema inabidi wampoze Mwanakijiji kama kweli anatumia majina tofauti humu kwenye JF kuipigia debe chadema, makala yake kwenye Tanzania Daima, redio yake KLH NEWS na hasa makala maalum alioyowandikia wana Kiteto vyote havikufanya kazi.

Mbowe muongeze mshahara anapigana sana kijana huyu usijekumkosa na kuna member kasema hana kibali cha kutoka na kuingia Marekani, wana chadema wamfanyie utaratibu wa kupati vibali halali vya kuishi ili 2010 awasaidie kwenye Ground au kuzunguuka nae kwenye Helkopta, Naamini ni mpiganaji mzuri anzisheni mchango wa Mwanakijiji kuliko kumtumia tu bila kujali hali yake na mazingira yanayomkabili.

Mwanakijiji.

Usirudi nyuma ndio siasa.
 
Hata wewe mkuu? Nilitegemea uwe critical kidogo kwa jinsi ninavyokujua. Yaani wewe kweli unaamini wapinzani wameshindwa kwa sababu ya sera? Hujiuliza ni kwa nini wananchi wameandamana maelefu kwa maelfu na kumshangilia sana Lowasa wakati sisi hapa wote tumekuwa tukimuona Lowasa ndio kiongozi wa ufisadi nchini mwetu? Hebu tulia kidogo, achana na ushabiki cheap na ujiulize zaidi, najua kabisa kwa jinsi ninavyokujua unaweza kufanya bora zaidi ya hapo!

Hii argument muhimu sana, inahitaji thread ya kujitegemea.
Tuendelee na mjadala!
 
Tatizo si la wananchi mimi naamini kabisa kuwa wananchi hawaichagui CCM ,hilo ni jambo ambalo nina uhakika nalo kabisa.
Ila Nilisema zamani hivi vyama vya upinzani viwachane na mambo ya kupiga kura ,waelekeze majeshi kwenye Katiba ya Nchi na tume ya Uchaguzi ,halafu mambo hayo yakishakuwekwa sawa basi hata mkuu wa Chama kama anatumika kuiunganishia CCM itakuwa vigumu kwani hata wapiga kura wanaonekana kusononeka ni kwa namna gani wameshindwa ,ukweli mchozo upo ndani ya tume ya Uchaguzi hakuna jengine haiwezekani CCM wakamate mpini na wapinzani wamekamata makali halafu mushangae kwa nini CCM hakukatika mikono itakuwa miujiza mikubwa sana.
Vyama vya upinzani vigomee kabisa kushiriki katika chaguzi hizi za sasa ,wadai tume au marekebisho ya Tume ,tume hii inayotoka katika mfumo wa Chama kimoja ikataliwe kwa nguvu zote na kuanzia ni kuwacha kushiriki katika chaguzi hizi ambazo hata upinzani ukipata mbunge inakuwa hakuna nguvu ya kudhibiti harakati za Chama Tawala ,hivyo sababu ya kudai tume huru inayoshirikisha wadau wote ianzie katika hizi chaguzi zinazoibuka kabla ya kukaribia Uchaguzi mkuu ,leo Serikali ambayo inaongozwa na Chama Tawala CCM inasema tume haina matatizo ,katiba haina haja ya kufanyiwa marekebisho ,Serikali inajifanya kama haina habari kuwa sasa Tanzania ipo katika mfumo wa vyama vingi na kila kitu chake ni lazima kifanyiwe ukarabati ili kukidhi haja ya kuwepo kwa vyama vingi katika Taifa la Tanzania.
Serikali kusema kila kitu ni sawa na hakina matata wala matatizo ni kujibebesha msalaba ambao utaipeleka nchi pahala pabaya , kila kitu kitakuwa sawa na kitakuwa hakina usumbufu wala mazonge kama kitakarabatiwa na kujulikana kuwa kimepatika na kutungwa katika mfumo wa vyama vingi ,hakuna mtu atakuja kulalama na kupiga makelele ,atakaeshindwa atakuwa hana sababu zaidi ya kushindwa katika mbinu za kampeni
Lakini leo hata ufanye kampeni za aina gani basi bado utakuja kupigwa mueleka na harakati na mikakati ya tume iliko chini ya Chama kimoja ,hata wananchi wote wachague mgombea kutoka upinzani bado tume itatekeleza mkakati wa kuhakikisha Chama chao kinabaki na kunyakua ubunge au uwakilishi na hata Uraisi ,kama mnakumbuka Zanzibari kule Karume alisema hata watu wote wasipomchagua basi kura yake na ya mkewe inatosha kumfikisha Ikulu ,hapa utapata kuona kuwa mikakati ya tume hizi za sasa si kuona uchaguzi unafanywa kwa kuzingatia matakwa ya wananchi bali mkakati ni kuhakikisha kwa njia yeyote ile mgombea kutoka chama chao anabaki kuwa mshindi liwalo na liwe.
 
.....

Mbowe muongeze mshahara anapigana sana kijana huyu usijekumkosa na kuna member kasema hana kibali cha kutoka na kuingia Marekani, wana chadema wamfanyie utaratibu wa kupati vibali

Sijui hili la kutoka na kuingia marekani linahusiana vipi na kinachoendelea hapa. Viroja huwa havishindani na hoja!?!
 
I agree. Picha ambayo naanza kuipata ni kwamba kuna mambo ambayo sisi tunafikri ni matatizo wananchi wa kawaida hawaoni kama ni shida. Kwa mfano, hili swala la ufisadi sidhani kama watanzania wa maeneo ya Kiteto na kwingineko wanafikiri ni matatizo yanayowahusu. Yaani hawawezi kuoanisha kabisa kati ya shida walizo nazo na wizi wa pesa za serikali unaofanywa na CCM. Vinginevyo isingewezekana waichague CCM au kumshangilia Lowasa kwa kiwango tulichoona. Hapa ndipo nitakubaliana na Einstein kwamba "Siasa ni Ngumu Kuliko Fizikia"!

Huwezi kutumia wizi wa watu wachache ukasema ni chama ,chama sio physical entity ambacho kinaweza iba kitu.

Mfano ktk familia ya watu 8 mmoja kati yao anaweza akawa mjinga lakini huwezi sema familia ile ni jinga.

Failure ya tanzania sio ya CCM as CCM ila ya familia nzima yani watanzania.

Wapinzani wangapi wametulaghai wakati ule kwamba wao ni wema wamekimbia ccm maana ni chama kibaya leo hii NDIO viongozi na wafuasi wazuri wa CCM Je tutafahamu vipi huyu ni mlaghai,huyu ni propaganda ,huyu ni mtafuta madaraka??? kwa maneno matupu?? lahasha.

Haya mambo ya kuibua skendo si hoja kabisa ya kumfanya mtu apewe madaraka,kwani skendo hizi zimeanza kuibuliwa na wapinzani mbona mbunge wa CCM kama sikosei ni Mzee ndakaya ama kingunge ameibua skendo ngapi amefukuzisha mawaziri wangapi??

Kawaida ya mnafiki hua anakumonita tu ndg Kitila sehemu utapokesea ili ukumalize lakini mara kwa bahati mbaya juhudi za namna hii hua hazifanikiwi
 
Huwezi kutumia wizi wa watu wachache ukasema ni chama ,chama sio physical entity ambacho kinaweza iba kitu.

Mfano ktk familia ya watu 8 mmoja kati yao anaweza akawa mjinga lakini huwezi sema familia ile ni jinga.

.......

Vipi kama pesa ya wizi ndiyo inatumika kulisha na kuendesha familia?
 
Sijui hili la kutoka na kuingia marekani linahusiana vipi na kinachoendelea hapa. Viroja huwa havishindani na hoja!?!
Mwafrika wa Kike.
Hoja hii nilimpa mwanakjj naona wewe umekuja kujibu unanifanya niamini kuwa wewe ndio Mwanakijiji. kwani sikukutaja umekuja kujibu.
 
Mwafrika wa Kike.
Hoja hii nilimpa mwanakjj naona wewe umekuja kujibu unanifanya niamini kuwa wewe ndio Mwanakijiji. kwani sikukutaja umekuja kujibu.

Nani alikuambia kuwa kuna sheria hapa JF ya kuzuia watu kujibu au kuchangia hoja ?
 
Mabadiliko ya kweli hayaji bila kuwa na mazingira muafaka ya kufanya watu wakataka mabadiliko kwa gharama yoyote ile. Kwa sasa sisiemu wanatengeneza hayo mazingira kwa kufilisi nchi na kutajirisha watu mia moja (sera ya Kikwete).

..huwezi kufilisi nchi na kutajirisha watu[hata kama wachache]at the same time! unawachimbia kaburi tu!

Baada ya muda, kanga na kofia havitamnunua mtu ambaye hana chakula cha mwezi mzima!

..baada ya muda hakutakuwa na hizi kofia wala kanga!kutakuwa na mapanga na mikuki!
 
Kiteto kuweka historia leo

na Joseph Zablon
Tanzania Daima~Sauti ya Watu





...Mbowe alisema wakati umefika kwa wananchi wa Kiteto kupigana na umaskini na kuachana na ushabiki wa vyama kwa vile CCM kimekuwa chama cha matajiri walioko Dar es Salaam na katika miji mingine mikubwa.

“Kwa maana hiyo nawaomba wananchi wa Kiteto kutumia nafasi yenu kesho (leo) kufanya mapinduzi katika maisha yenu, kuchagua upinzani kupitia mgombea wetu Kimesera,”alisema Mbowe.


...“CCM ina wenyewe, ni wale wanaoishi Oysterbay, Masaki na Mikocheni na si ninyi mlioko huku vijijini, mmekuwa mkitumiwa kwa ajili ya kupiga kura,” alisema.


Kabla ya Chadema kufanya mkutano huo, CCM ilifanya mkutano wake wa kuhitimisha kampeni kaktika Shule ya Msingi Kibaya.

Katika mkutano huo, Makamu Mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa, alimnadi kwa mara ya mwisho mgombea wa chama hicho, Benedict ole Nyangolo, kwa kuwataka wapiga kura wa jimbo hilo kumpigia kura za ndiyo.

Msekwa aliwataka wana Kiteto kutochagua mgombea mwingine kwa sababu hawezi kuwaletea maendeleo.

NI YAPI MANENO MUAFAKA YA KUWAAMBIA WAPIGA KURA WAKATI WAKUHITIMISHA KAMPENI ZAKO? JE UNAPASWA KUWAAMBIA UKWELI AU MANENO YA KUBABAISHA?

VICTOR KIMESERA ANAISHI WAPI?
 
..hata chadema ili kishinde kinahitaji mapinduzi!muulize kitila[simaanishi yeye chadema!]!

Huu ni ukweli ingawa nina wasiwasi kuwa mapinduzi yakimalizika Chadema na vyama vya siasa basi kanda ya ziwa yote itakuwa imeuzwa kwa sinclair na wenzake. Sad but true
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom