Uchambuzi huru: Hotuba ya Rais Samia Suluhu ya Aprili 22, 2021

Uchambuzi huru: Hotuba ya Rais Samia Suluhu ya Aprili 22, 2021

Kwa rehma zake Mwenyezi Mungu ni matumaini yangu sote tutaumaliza Mwezi huu Mtukufu wa Ramadhan salama salimin na hakika yeye ndiye mwenye kurehemu riziki zetu kubwa na ndogo na hapana mwingine apaswaye kuabudiwa. Tumuombe sote atuepushe na kila lisokuwa na kheri kwetu. Ameen.

Nina hakika siku ya leo tutasikia SIFA kemkem za mafuta ya tin na zaitun zitamiminika kupamba na kusifia hotuba ya rais wa JMT Mama Samia Suluhu Hassan kwa sababu imewagusa watu wote katika mazingira tofauti katika mwelekeo mpya wa dira ya Awamu hii ya sita ikitekeleza kauli mbiu ya KAZI IENDELEE.

Mimi binafsi, niseme ukweli wangu kutoka moyoni ya kuwa sii mshabiki wa rais Mama Samia Suluhu Hassan toka hotuba yake ya kwanza alipo apishwa kama rais wa Awamu ya sita. Huu ndio ukweli wangu! Na sababu zangu ni ndogo kabisa, nilimsoma toka mwanzo mwelekeo na Dira yake Kitaifa, dira ambayo Kiitikadi, mimi sii muumini wake na hupingana na nadharia zinazofungamana zaidi na UBEPARI badala ya UJAMAA wa Mwafrika.

Hivyo unaponisoma hapa ni muhimu Uzingatie kuwa mimi ni muumini wa UJAMAA wa Mwafrika na naamini Maendeleo ya Tanzania yataletwa na WATANZANIA wenyewe badala ya WAWEKEZAJI kutoka nje. Imani ya kwamba maendeleo yetu yanahitaji kuweka masharti rahisi ili kuvutia Wawekezaji ni sawa na fikra za.Kitumwa za Mababu zetu walokubali kupewa na wakoloni Shanga na vilemba ili tupendeze huku wagenu wakiondoka na madini mali ghafi na nyara zetu za Kitaifa.

Niseme wazi kwamba binafsi yangu naiona tofauti kubwa sana baina ya Hayati rais wa awamu ya Tani John Pombe Magufuli na Mama Samia Suluhu Hassan na kwamba hawa sii kitu kimoja hata kidogo. Tofauti zinazotokana na ahadi za mabadiriko makubwa ya SERA na SHERIA ambazo Chama cha Mapinduzi na Hayati Magufuli walizitumia kupata ushindi mkubwa katika Uchaguzi wa mwaka 2020. Niseme kwa nini nasema hivi?

Haina Shqka kabisa, Hayati Magufuli alikuwa rais anayepigania maslahi ya Wananchi Wanyonge kwa maana ya Watanzania Maskini dhidi ya Wawekezaji Mabeberu tofauti kabisa na Dira na Mwelekeo wa Mama Samia anayetazama zaidi viwashwishi kwa maslahi ya WAWEKEZAJI pamoja na dhana ya UKUONGEZA UZALISHAJI wa Mazao kwa WINGI zaidi (Quantity) badala ya fikra za Magufuli kudhamiria Kuanzisha viwanda vya ndani ili Kuongeza thamani ya Mazao yetu ya Asili yalokuwa BORA zaidi (Quality).

Nimalizie tu kwa kusema, rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan awe makini sana na dhana hizi, kwani hatukuanza jana wala juzi. Tulifuata mrengo ule toka wakati wa Rais Ally Hassan Mwinyi, akaja Mh. Benjamin Mkapa na Mwishowe mstaafu Jakaya Kikwete, na kote huko nyuma tulifanya makosa mengi sana kwa dhana ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Biashara. Matokeo yake tukaunda Matabaka ya Walionacho na wasiona nacho baina ya Wainanchi wenyewe. Ndipo Ufisadi na rushwa viliposhamiri kwani hapana alotaka kubakia katika kundi la wasionacho (Maskini)

Maoni ya rais kuhusu matumizi ya mbinu za kisasa katika Kilimo, kuna hatari kubwa ya nchi yetu kurudi kutawaliwa tena Kiuchumi kutokana na ujio wa mbegu za maabara ambazo zitaondoa kabisa rutuba ya Ardhi yetu, ubora wa mbegu zetu (Organic) na kubwa zaidi kumikilisha Mashirika ya nje nguzo za Uchumi wetu Kitaifa.

Maasalaam,
- Ramadhan Kareem
Mkuu umepotea sana sana. Kwa nini? Au vijana wa sasa na mada zao za ki-Yanga na Simba zinakukwaza? Umetoa hoja nzuri sana sana. Tanzania itajengwa na watanzania na siyo wawekezaji kutoka nje. Hawa wanaoitwa wawekezaji wengi siyo watu wazuri. Mimi hofu yangu ni kuwa mheshimiwa Samia ameanza kuonyesha atawapigia magoti kitu ambacho ni hatari sana.
 
Kama hujui miradi aliyoifanya Kikwete basi utakuwa hufuatilii nchi hii inatoka wapi inakwenda wapi!

Ni ajabu kuuliza swali eti Kikwete alijenga kitu gani haswa? —Ina maana kuunganisha nguvu ya umma kujenga shule za kata na maabara nchi nzima unaona ni kitu kidogo?, Kuunganisha mikoa ya nchi hii kwa mtandao wa barabara za lami unaona siyo kitu?, Kutandaza mkongo wa Taifa kwa ajili ya Internet unaona ni kitu kidogo?, Kujenga Hospitali ya Mloganzila, Benjamin Mkapa huko Dodoma unaona siyo kitu?, Madaraja ya Malagarasi, Uwanja wa Ndege Terminal 3, Kutandaza mabomba ya gesi kutoka Mtwara unaona siyo kitu?, Barabara za Mwendokasi Dar unaona siyo kitu?, Ukarabati wa viwanja vikubwa vya ndege almost nchi nzima unaona siyo kitu? , Ujenzi wa Zahanati za Kata nchi nzima unaona siyo kitu?, Kusambaza umeme kupitia vijji vya REA unaona siyo kitu?, au Unadhani REA ilianza na Magufuli?, Ujenzi wa Nyumba za Maaskari nchi nzima huoni kuwa ni kitu?, Ujenzi wa Kituo cha kisasa cha kutibu moyo (JK Heart Institute) siyo kitu?, Vivuko vingi alivyonunua mfano kivuko cha MV Magogoni, na vibgine vingi tu unaona siyo kitu?, Miradi ya Maji kama vile kutoka Ruvu kupitia Bunju unaona siyo kitu?, Mieadi ya Umeme ya Kinyerezi 1 na 2 unaona siyo kitu?, Ujenzi wa chuo kikuu cha UDOM unaona siyo kitu?, Kutoa ajira kwa wingi, kupandisha kima cha chini, kupandisha watu madaraja kila mwaka kwa mujibu wa mikataba ya kazi wewe unaona hiyo siyo kitu?

Na miradi mingine mingi mingi tu ambayo siwezi kuiorodhesha hapa!
Kikwete alifanya miradi mikubwa sana lakini hakututia deni kubwa kama ambalo Magufuli katuingiza.

Unamletaje Zitto katika huu mjadala? —Kuhusu deni la Taifa kuwa kubwa sana kipindi cha Magufuli siyo habari ya Zitto baki ni fact!
Kwa hiyo miradi yote hiyo ilikuwa mikopo sio? Yaani zile shule za kata na zahanati ambazo Wananchi walijitolea kujenga kwa nguvu kumbr nyie mmekula hela mkidai ni hesabu ya mikopo? Mkuu stick to the question, sijasema JK hakufanya kitu isipokuwa maswali yenu jui ya ongezeko la deni nilitolea maelezi ambayo binafsi yangu ukiniuliza sioni kitu hata kimoja kilichodtahili kukopa feeha nje. Kazi kubwa ya Serikali ni kujenga miundombinu na binafsi sikuiona. Barabara za Dar labda lkn Dar Arusha ilikuwa mbovu, Dar - Mwanza ilikuwa.mbovu na finyu. Dar - Mbeya usiseme. Ajali kukicha. Kuna takwimu za mwaka 2008 ( kama sikosei) tulifikia vifo 20,000 kwa mwaka! Vingi Kuliko hata Ukimwi..samahani lakini..
 
Bora wakongwe mrudi maana mmewaachia jukwaa makuwadi wa siasa hadi kuna kera. Binafsi ninamuombea SSH aongoze yeye nchi hata kama atakosea kuliko kujikuta "wafulani" wanaongoza kwa mlango wa nyuma.
Kikwete is on the steering wheel now. For me this is a sad news.
 
Unakataa Umangungo wakati rais wako wa sasa kasema ukimpigia kura au usipompigia kura CCM itashinda tu?

Kama unataka kuchukua ownership ya nchi, hilo ni jambo zuri. Ondoa utawala wa CCM. Weka utawala bora zaidi.

CCM imeoza, na sioni chama cha kuiondoa.

Naomba uelewe kitu kimoja, mimi sipo hapa kutetea wawekezaji wakandamizi.

Naelewa ubaya wa wawekezaji wakandamizi. Nimefanya kazi Wall St. kwenye kitovu cha wapigaji hela wa dunia.

Kwa hiyo, naelewa madhara ya uwekezaji usio na regulation ya serikali.

Tatizo langu ni hii simple narrative ya us against them, kuwaita watu mabeberu bila distinction, kuweka uwajibikaji wa matatizo yetu kwa mabeberu wakati hao wanaoitwa mabeberu hawawezi kuingia Tanzania bila msaada wa viongozi wa Tanzania, na general anti western propaganda ambayo haina nuance, inaishia kuwa kama ile methali ya Kiswahili ya "Baniani mbaya, kiatu chake dawa".

Moja ya ujinga wa narrative hii ni kuachana na western investment na kukumbatia white elephant projects zinazokuwa funded na Wachina.

Bila kujua au kukubali kwamba the Chinese are not better and possibly even worse.
Tunakubaliana kwa vingi nakutofautiana kwa machache katika haya...Ila it doesnt matter kama ni Chines au westerns long as tunashindwa ku bargain na kufikia winwin situation ambayo haiji bila wenye ujuzi na taaluma kuchukua haya majukumu.

Tatizo ni sote kugeuka kuwa waimba chorus tu bila kuwa na critical and analytical mind hasa kwa ile cadre inayohotajika kusimama imara dhidi ya wengi ambao hawakupata nafasi ya kujua lugha ile mataifa makubwa wanaiongea.

Infact hakuna free lunch duniani na hakuna atakaye kuletea share yako kwenye silver plate na wala si kwakupiga makelele mengi ndiyo utawatisha wapigaji...Let us be responsible, wewe na mimi kwa faida ya nchi yetu na vizazi vyetu
 
Kwa hiyo miradi yote hiyo ilikuwa mikopo sio? Yaani zile shule za kata na zahanati ambazo Wananchi walijitolea kujenga kwa nguvu kumbr nyie mmekula hela mkidai ni hesabu ya mikopo? Mkuu stick to the question, sijasema JK hakufanya kitu isipokuwa maswali yenu jui ya ongezeko la deni nilitolea maelezi ambayo binafsi yangu ukiniuliza sioni kitu hata kimoja kilichodtahili kukopa feeha nje. Kazi kubwa ya Serikali ni kujenga miundombinu na binafsi sikuiona. Barabara za Dar labda lkn Dar Arusha ilikuwa mbovu, Dar - Mwanza ilikuwa.mbovu na finyu. Dar - Mbeya usiseme. Ajali kukicha. Kuna takwimu za mwaka 2008 ( kama sikosei) tulifikia vifo 20,000 kwa mwaka! Vingi Kuliko hata Ukimwi..samahani lakini..
Unaposema Dar-Mwanza ilikuwa mbovu una maana gani?, Yote ilikuwa mbovu au kuna vipande vilikuwa vibovu?

Unaposema Dar-Mbeya ilikuwa mbovu, uba maana kuwa kutoka Dar hadi Iringa ilikuwa mbovu?

Naona Unageneralize sana mzee bila kuwa na facts

Wakati wa JK ujenzi wa hizo barabara alisisimamia Magufuli huyohuyo unayemsifu na ndizo zilizimfanya akajulikana zaidi na kupendwa na watu kwa jinsi alivyopiga kazi kwenye hayo mabarabara.

Ajali zilichochewa na mambo mengi ikiwemo kutotii ile sheria ya spidi 50
Ajali hazikupungua kipibdi cha Magufuli eti kwa kuwa yeye Alizibomoa hizo barabara na kuzijenga upya bali ninkwa kuwa aligeuza faini za barabarani dili yaani chanzo cha mapato, kwa hiyo tochi za matrafiki zikawa kila pahala
 
Mkuu umepotea sana sana. Kwa nini? Au vijana wa sasa na mada zao za ki-Yanga na Simba zinakukwaza? Umetoa hoja nzuri sana sana. Tanzania itajengwa na watanzania na siyo wawekezaji kutoka nje. Hawa wanaoitwa wawekezaji wengi siyo watu wazuri. Mimi hofu yangu ni kuwa mheshimiwa Samia ameanza kuonyesha atawapigia magoti kitu ambacho ni hatari sana.
Kusema kweli nilisepa kutokana na vijana hawa wa Dotkom maanake kwanza hawana adabu. Haqajui.kujenga hoja kazi yao matusi tu. Unaandika hoja anarudi na matusi unashindwa kujua imetoka wapi halfu hugundua athari za hizi ni athari na hulka zitokanazo na Unazi.

Mzee mzima nikaona isiwe taabu, nijikate mapema maanake nikianza nami matusi kuna wanangu na wajukuu humu halafu watasema duuuh Babu yetu vipi tena. Huwa napitia mara moja moja kuwasoma.
 
Unaposema Dar-Mwanza ilikuwa mbovu una maana gani?, Yote ilikuwa mbovu au kuna vipande vilikuwa vibovu?

Unaposema Dar-Mbeya ilikuwa mbovu, uba maana kuwa kutoka Dar hadi Iringa ilikuwa mbovu?

Naona Unageneralize sana mzee bila kuwa na facts

Ujenzi wa hizo barabara alisisimamia Magufuli huyohuyo unayemsifu na ndizo zilizimfanya akajulikana zaidi na kupendwa na watu kwa jinsi alivyopiga kazi kwenye hayo mabarabara.

Ajali zilichochewa na mambo mengi ikiwemo kutotii ile sheria ya spidi 50
Ajali hazikupungua kipibdi cha Magufuli eti kwa kuwa yeye Alizibomoa hizo barabara na kuzijenga upya bali ninkwa kuwa aligeuza faini za barabarani dili yaani chanzo cha mapato, kwa hiyo tochi za matrafiki zikawa kila pahala
Mkuu hakuna kitu kizima nusu nusu aidha ni kibovu au kizima. Nyumba yenye nyufa na inayovuja maji ya mvua, huwezi kusema sio mbovu ila kuna sehemu ndio mbaya.

Kifupi huwezi kulinganisha kabisa wakati wa JK na Magufuli unless unataka kuleta Unazi wa Simba na Yanga. Anyway, naishia hapa naona tunatoka nje ya mada..
 
Hapo palikuwa na upungufu binafsi wa mhusika. Naweza pia kusema JPM hakuwa na itikadi rasmi inayoeleweka na badala yake alichokuwa anafanya ni maono na misukumo yake binafsi.
Nini maana ya Itikadi na unaitafsiri kwa sera na falsafa zipi?
 
Mkuu hakuna kitu kizima nusu nusu aidha ni kibovu au kizima. Nyumba yenye nyufa na inayovuja maji ya mvua, huwezi kusema sio mbovu ila kuna sehemu ndio mbaya.

Kifupi huwezi kulinganisha kabisa wakati wa JK na Magufuli unless unataka kuleta Unazi wa Simba na Yanga. Anyway, naishia hapa naona tunatoka nje ya mada..
Duh kweli wewe kiboko

Kwa hiyo wewe falsafa yako ni kuwa mtu akijenga Barabara ya lami nzuuri Dar mpaka Shinyanga, kwako hiyo siyo mali kitu mpaka tu hiyo ingekuwa imefika Mwanza?

Hoja yako ni Muflisi kwa sababu, nchi haiwezi kujengwa na Mtu mmoja, Akija rais mwingine atamalizia Shinyanga Mwanza

By the way, Kikwete alijenga mtandao wa lami wa kuunganisha mikoa yote TZ bara, alibakisha mikoa Sita tu ikiwemo Manyara na Kigoma. Na huyohuyo Magufuli wako ndiye aliyesimamia ujenzi huo!. Sasa wewe unakuja kuona yule aliyemalizia hiyo mikoa Sita eti kafanya kazi kubwa kuliko aliyejenga ya mikoa 20. Logic yako ya ajabu kweli hapa.

Ninaweza kukuwekea document hapa iliyoandaliwa na Waziri Magufuli mwaka 2015 akionyesha Mafanikio ya miradi ya Ujenzi wa serikali ya Kikwete kuanzia 2005 hadi 2015 uone Jinsi Yule Mkwere alivyofanya mambo makubwa kwenye sekta ya Ujenzi, na ameondoka madarakani huku mirwdi mingine akiwa aneshaitafutia fedha, ameishaifanyia upembuzi yakinifu na mingine ikiwa inaendelea na Ujenzi, Magufuli kama rais kaikuta inaendelea. Sasa kukamilika kwa miradi hiyo kipindi cha Magufuli haimaanishi kuwa yeye ndo kahustle kuiplan na kuitafutia Funding!. No!

Mkandara soma huu uzi hapa chini!, Download document nzina niliyiattach kwenye huo uzi uone miradi aliyoacha JK amekamilisha, aliyoacha ameifanyia upembuzi yakinifu na aliyoacha inajengwa

 
Duh kweli wewe kiboko

Kwa hiyo wewe falsafa yako ni kuwa mtu akijenga Barabara ya lami nzuuri Dar mpaka Shinyanga, kwako hiyo siyo mali kitu mpaka tu hiyo ingekuwa imefika Mwanza?

Hoja yao ni Muflisi kwa sababu, nchi haiwezi kujengwa na Mtu mmoja, Akija rais mwingine atamalizia Shinyanga Mwanza

By the way, Kikwete alijenga mtandao wa lami wa kuunganisha mikoa yote TZ bara, alibakisha mikoa Sita tu ikiwemo Manyara na Kigoma. Na huyohuyo Magufuli wako ndiye aliyesimamia ujenzi huo!. Sasa wewe unakuja kuona yule aliyemalizia hiyo mikoa Sita eti kafanya kazi kubwa kuliko aliyejenga ya mikoa 20. Logic yako ya ajabu kweli hapa.

Ninaweza kukuwekea document hapa iliyoandaliwa na Waziri Magufuli mwaka 2015 akionyesha Mafanikio ya miradi ya Ujenzi wa serikali ya Kikwete kuanzia 2005 hadi 2015 uone Jinsi Yule Mkwere alivyofanya mambo makubwa kwenye sekta ya Ujenzi, na ameondoka madarakani huku mirwdi mingine akiwa aneshaitafutia fedha, ameishaifanyia upembuzi yakinifu na mingine ikiwa inaendelea na Ujenzi, Magufuli kama rais kaikuta inaendelea. Sasa kukamilika kwa miradi hiyo kipindi cha Magufuli haimaanishi kuwa yeye ndo kahustle kuiplan na kuitafutia Funding!. No
Mkuu nimesafiri njia zote hizo, ilifikia kwenda Mwanza tunazungukia Kenya. Mbeya safari karibu 24 hrs, Arusha karibu siku nzima ukifika hoi. Sasa hivo vipande vipande mnavyotaka kusema ni vipi. Unatoka Dar hujafika Chalinze pale Mlandizi mashimo halafu umnatuambiwa fedha za Mkopo! Ilifika watu walikuwa qanapanda ndege haijalishi kiasi gani nsio.maana bei za ticket za ndege zilirushwa. Makampuni mengi ya nje yakaingia qalipoona firsa hizi. Dar - Mwanza ilikuwa ghali kuliko uruke kutoka Chicago kwenda New York hahahaha! watu haqakujali kwa sababu michongo ya kuibia Seeikali ilikuwa wanjewanje.. Acheni maslhala kama sii Magufuli naapa kwa Mungu, CCM isingerudi Madarakani 2015 ..
 
Tatizo.lenu nyote ni kutosoma Katiba na Sheria. Kama Sheria ya Mitandao imepitishwa na Bunge, mlitegemea yeye aachie tu watu wafanye wanavyotaka kwa sababu mnataka kutukana? Upinzani walitakiwa kupigania sheria hiyo iondolewe lakini badala ya kuipinga Sheria, wao wakapingana na Utekelezaji wa sheria na rais ilihali Sheria ipo Kikatiba. Huoni kama Uzwazwa huo, mimi nitapigana na Sera za Uwekezaji sina tatizo na Mama Samia. Akichukua mkondo wa Magufuli nitampa support zangu 100% lakini hili la Wachina sijui wajenge Bandari, wapewe Masharti rahisi waje kuwekeza? Hell no China kuna mapori kibao wakawekeze kwao, sisi tutaenda kununua huko huko Porini walikowekeza..
@Mkandara ,unachambua hotuba ya Mh. Rais Samia au unamuongelea mwendazake JPM!!??
Naona Magufuli nyingi zaidi ya kilichoongelewa na Mh. Rais.
 
Mkuu nimesafiri njia zote hizo, ilifikia kwenda Mwanza tunazungukia Kenya. Mbeya safari karibu 24 hrs, Arusha karibu siku nzima ukifika hoi. Sasa hivo vipande vipande mnavyotaka kusema ni vipi. Unatoka Dar hujafika Chalinze pale Mlandizi mashimo halafu umnatuambiwa fedha za Mkopo! Ilifika watu walikuwa qanapanda ndege haijalishi kiasi gani nsio.maana bei za ticket za ndege zilirushwa. Makampuni mengi ya nje yakaingia qalipoona firsa hizi. Dar - Mwanza ilikuwa ghali kuliko uruke kutoka Chicago kwenda New York hahahaha! watu haqakujali kwa sababu michongo ya kuibia Seeikali ilikuwa wanjewanje.. Acheni maslhala kama sii Magufuli naapa kwa Mungu, CCM isingerudi Madarakani 2015 ..
Soma hiyo document niliyokuwekea hapo nchini uone jinsi nchi ilivyokuwa inatimka vumbi kwa ujenzi kipindi cha JK

Achana na hearsay

By the way ni JK ndiye aliyetuondolea aibu ya kupitia Kenya kwenda Kagera
 
  • Thanks
Reactions: Pep
Wewe kwanza tengeneza internet yako, halafu tengeneza maandishi yako, uache internet ya mabeberu na herufi za mabeberu.

Halafu tuite huko kwenye internet yako ambayo haijatumia teknolojia ya mabeberu tujadili hoja zako za kijima.

Hapo angalau nitakuona uko serious.

Lakini maadam bado unatumia internet ya mabeberu na herufi zao, mimi nakuona mnafiki tu ukiwakataa mabeberu kwa misingi uliyoiandika hapa.

Ama mnafiki, ama mjinga.

Inawezekana kabisa mnafiki mjinga.
Aaah kubabake [emoji23][emoji23]
 
Sasa kama Nyerere alishindwa umewahi kujiuliza alishindwaje wakati nchi ina viwanda, ndege zake, miradi ya Uzalishaji Umeme n.k lakini toka Mwinyi hadi JK hatukuwa na ndege hata moja ikiruka? Hatukuwa na kiwanda zaidi ya Mengi na Bakhresa yaani miaka 30 tuna matajiri wawili wenye viwanda vikubwa nchi nzima wengine wote Matapeli. ATC, Reli ya kati, reli ya Kasikazini vimekufa barabara zote za vumbi isipokuwa Dar. Au umesahau list ya Mafisadi Papa aloisoma Mengi. Nikukumbushe kitu hivi Magufuli kawezaje kurudisha uhai wa vitu vyote kwa kutumia zaidi pato la kodi zetu? Kuna watu wanasema Magufuli aliiba sana fedha. Ebu waulizeni hizo fedha kaziweka benki gani ya ndani au nje? Au kazikwa nazo! Bila shaka hawana jibu..

Kama wewe unaamini kuwa 1984 Nyerere aliiacha nchi kwenye hali nzuri sana kiuchumi sina neno la kukuongezea.

Isipokuwa ninachofahamu ni kuwa Nyerere alikuwa amehangaika sana kutafuta misaada na mikopo nafuu akaishia kukutana na kikwazo cha IMF. Wafadhili wakubwa hata marafiki wa Tanzania hawakuwa tayari kumpa misaada mikubwa nje ya muafaka na IMF. Yeye aligoma kabisa kusaini mkataba na IMF akaamua kung’atuka.

Nilisoma kuwa AHM alipoingia madarakani kama Rais, wadau mbalimbali na media walimuuliza Mwalimu kama atakuwa radhi mrithi wake AHM asaini mkataba na IMF kama Rais wa JMT. Akasema hana tatizo kabisa na hilo ilimuradi sio yeye!

Nyerere alijua vizuri sana masharti ya IMF kwamba yangeathiri sana legacy yake hasa mashirika ya umma yaliyokuwa yameshikilia uchumi wa taifa. Lakini alijua hakuna namna. Itabidi AHM asaini mkataba na IMF na kuutekeleza. Ilikuwa dhahiri kwamba mashirika kama TRC, ATC, TANESCO, n.k. yaliyokuwa yakiendeshwa bila ufanisi, rushwa kwa wingi, nepotism, n.k. yangetetereka na mengine kufa.

Kwa taarifa yako, ATCL bado haijafufuliwa. Kilichofanyika ni serikali kujitwisha mzigo wa kununua na kumiliki ndege angalau kuweka taswira ya uhai wa ATCL. Ndege sio kigezo cha uhai wa shirika ya ndege. Kama alivyosema Rais Mh. SSH, hatua za kufufua shirika zitachukuliwa rasmi ili kulipa uhai wa kibiashara.

Miradi mingine ya umeme, reli, n.k. bado ni miradi. Tusubiri kuona hatua zitakazochukuliwa kuikamilisha na kuiendesha kwa ufanisi. Nina hakika hata Magufuli angekuwepo isingeendeshwa “KIJAMAA” kama enzi za Nyerere. Na angethubutu kufanya hivyo angekwama mapema sana. Hata North Korea yenyewe leo hii inashiriki uchumi wa kibepari kwa kuibia sana. Makampuni ya US na Ulaya yanazalisha bidhaa huko kwa kutumia mgongo wa China kukwepa vikwazo vya UN.

Kuhusu wizi wa Magufuli nakuachia ubishane na hao waliokuambia. Sina hizo siri.
 
Tunakubaliana kwa vingi nakitofautiana kwa machache katika haya...Ila it doesnt matter kama ni Chines au weatern long as tunashindwa ku bargain na kufikia winwon situation ambayo haiji bila wenye ujuzi ba taaluma kuchukua haya majukumu.

Tatizo ni sote kugeuka kuqa waimba chorus tu bila kuwa na critical and analytical mind haya kwa ile cadre inayohotajika kusimama imara dhidi ya wengi ambao hawakupata nafasi ya kujua lugha ile mataifa makubwa wanaiongea.

Infact hakuna free lunch duniani na hakuna atalaye kuletea share yako kwenye silver plate na wala si kwakyoiga makelele mengi ndiyo utawatisha wapigaji...Let us be responsible, wewe na mimi kwa faida ya nchi yetu na vizazi vyetu
Kuna story moja, sijui kama ni kweli au story tu, lakini ujumbe wake ni muhimu kuuelewa.

Inamhusu waziri mmoja mkubwa wa Nigeria, nafikiri alikuwa waziri wa fedha.

Alikuwa waziri shupavu kupinga rushwa, nchi haijawahi kuona waziri shupavu kama huyo, alikuwa anasema sana kukemea rushwa.

Ikafika wakati akaanza mpaka kwenda benki za kimataifa kunegotiate hela za Nigeria zirudishwe, alikuwa hataki mchezo.

Akaenda Uswizi, akazwa anazunguka mabenki, akafanya uchunguzi kutafuta benki yenye usiri kabisa Uswizi.

Akaipata, akaenda kuonana na CEO wa benki.

Akamwambia anataka majina ya Wanaijeria wote wenye hela kwenye hiyo benki, na vyanzo vyao vya mapato.

CEO akamwambia siwezi kukupa majina hayo.

Akasema nipe majina, ukinipa nitakutafutia deal kubwa sana na serikali ya Nigeria iweke hela zake kwenye benki yako, utapata faida sana.

CEO akawmambia siwezi kukupa majina, nafuata kanuni za faragha za kibenki.

Waziri akamwambia nitatengeneza deal na serikali ya Nigeria kwamba ukiripoti hela za wizi zilizoibiwa Nigeria tutakupa kiasi fulani katika hizo hela.

CEO akakataa, akasema hawezi kuzisaliti kanuni za faragha za kibenki.

Basi yule Waziri akamwambia CEO, huyu hapa Dr. Adebayo Adedeji wa African Development Bank, ukitupa majina tutakupa deal kubwa sana la Benki ya Maendeleo ya Africa, uweke hela za mabilioni mengi sana ya ADB.

CEO akakataa kutoa majina, akasema siwezi kusaliti kanuni za faragha za kibenki.

Waziri akasema sawa, wewe ndiye niliyekutafuta.

Nimekuja na mimi nataka kuweka mamilioni ya dola yangu kwenye benki yenu, lakini kabla ya kuweka kwanza nilikuwa nakupa mtihani nione kama watu wakija kutaka majina ya wateja wenu unaweza kutoa au hutatoa.

What's my point?

Ukiwa so caught up na habari za "mabeberu this, mabeberu that" na kushikwa na theatrics za viongozi wa Afrika wanaojinadi kupigana na mabeberu, unaweza kuchotwa kirahisi na watu wanaoshirikiana na hao mabeberu.

Mtu anaweza kujitengenezea image nzuri kuwa anapingana na mabeberu, kumbe na yeye anajipandisha bei tu apige hela kubwa zaidi.

Tunatakiwa kuwa makini sana tusiingie katika mtego wa simple narratives.

Kuna mabeberu wengine weusi wenzetu Watanzania, na kuna watu wa nchi za nje wanaoweza kutusaidia kupigana na ubeberu.

Kwa hiyo tujadili mambo kwa nuance, sio kwa a broad painting brush.
 
Naamini kabisa hii transition itatupa mwelekeo kama nchi, msije mkampoteza Mh. Kwa tamaa za miradi binafsi, hili hatutalikubali please and please come rain come sunshine....
Mkuu 'Ame'
Nimefuatilia maandishi yako kwenye mada hii, na nadhani nimeelewa vizuri unachkiandika hapa; ambacho mimi ninakubaliana nacho kabisaaaaa!

Ila, usijidanganye, ukadhani viongozi tulionao wana fikra kama ulizonazo wewe; na wala usidhani kwa hali ya wananchi wa Tanzania ilivyo, unaweza ukaitegemea kuzuia chochote.
Akitokea JK mwingine sasa hivi huko CCM, usidhani kuna mtu yeyote atakayenyanyua kidole. Utaanza kuona watu wanajipanga kwenye mstari kuimba nyimbo zake na kumwonyesha yeye ni kama malaika.

Inaumiza sana.

Iwe ni kwa bahati tu, tumpate kiongozi mwenye kuyaamini haya yanayopigiwa kifua na mkuu 'Ame' na wengine kama akina 'Mkandara' na akina 'Kalamu1' - hiyo itakuwa ni bahati yetu nzuri tu na sio kwa utashi wa waTanzania..., sijui kwa nini.
Lakini mtu huyo asiwe kama Marehemu Magufuli, kwa yale mabaya yake!

Sijui tutampataje mtu wa aina hiyo. Najua wapo..., lakini hawataki kujitokeza mbele waliokoe taifa letu.
 
katika miaka ya 90 Cgina ilikuwa na tenda ya kununua skrepa za computer za jeshi (USA). Waamerika hawakutambua kuwa wao walikuwa wanaenda kuzusambaratisha na kuiba siri za teknoljia kutoka hard drve. Walikujatambua wachina wameishaiba siri nyingi.

Dah [emoji23][emoji23][emoji23]

Kweli tumechelewa sana ndugu zangu
 
Kama hujui miradi aliyoifanya Kikwete basi utakuwa hufuatilii nchi hii inatoka wapi inakwenda wapi!

Ni ajabu kuuliza swali eti Kikwete alijenga kitu gani haswa? —Ina maana kuunganisha nguvu ya umma kujenga shule za kata na maabara nchi nzima unaona ni kitu kidogo?, Kuunganisha mikoa ya nchi hii kwa mtandao wa barabara za lami unaona siyo kitu?, Kutandaza mkongo wa Taifa kwa ajili ya Internet unaona ni kitu kidogo?, Kujenga Hospitali ya Mloganzila, Benjamin Mkapa huko Dodoma unaona siyo kitu?, Madaraja ya Malagarasi, Uwanja wa Ndege Terminal 3, Kutandaza mabomba ya gesi kutoka Mtwara unaona siyo kitu?, Barabara za Mwendokasi Dar unaona siyo kitu?, Ukarabati wa viwanja vikubwa vya ndege almost nchi nzima unaona siyo kitu? , Ujenzi wa Zahanati za Kata nchi nzima unaona siyo kitu?, Kusambaza umeme kupitia vijji vya REA unaona siyo kitu?, au Unadhani REA ilianza na Magufuli?, Ujenzi wa Nyumba za Maaskari nchi nzima huoni kuwa ni kitu?, Ujenzi wa Kituo cha kisasa cha kutibu moyo (JK Heart Institute) siyo kitu?, Vivuko vingi alivyonunua mfano kivuko cha MV Magogoni, na vibgine vingi tu unaona siyo kitu?, Miradi ya Maji kama vile kutoka Ruvu kupitia Bunju unaona siyo kitu?, Mieadi ya Umeme ya Kinyerezi 1 na 2 unaona siyo kitu?, Ujenzi wa chuo kikuu cha UDOM unaona siyo kitu?, Kutoa ajira kwa wingi, kupandisha kima cha chini, kupandisha watu madaraja kila mwaka kwa mujibu wa mikataba ya kazi wewe unaona hiyo siyo kitu?

Na miradi mingine mingi mingi tu ambayo siwezi kuiorodhesha hapa!
Kikwete alifanya miradi mikubwa sana lakini hakututia deni kubwa kama ambalo Magufuli katuingiza.

Unamletaje Zitto katika huu mjadala? —Kuhusu deni la Taifa kuwa kubwa sana kipindi cha Magufuli siyo habari ya Zitto baki ni fact!
Naam [emoji1544][emoji1544]
 
Back
Top Bottom