Uchambuzi huru: Hotuba ya Rais Samia Suluhu ya Aprili 22, 2021

Uchambuzi huru: Hotuba ya Rais Samia Suluhu ya Aprili 22, 2021

Mkuu 'Ame'
Nimefuatilia maandishi yako kwenye mada hii, na nadhani nimeelewa vizuri unachkiandika hapa; ambacho mimi ninakubaliana nacho kabisaaaaa!

Ila, usijidanganye, ukadhani viongozi tulionao wana fikra kama ulizonazo wewe; na wala usidhani kwa hali ya wananchi wa Tanzania ilivyo, unaweza ukaitegemea kuzuia chochote.
Akitokea JK mwingine sasa hivi huko CCM, usidhani kuna mtu yeyote atakayenyanyua kidole. Utaanza kuona watu wanajipanga kwenye mstari kuimba nyimbo zake na kumwonyesha yeye ni kama malaika.

Inaumiza sana.

Iwe ni kwa bahati tu, tumpate kiongozi mwenye kuyaamini haya yanayopigiwa kifua na mkuu 'Ame' na wengine kama akina 'Mkandara' na akina 'Kalamu1' - hiyo itakuwa ni bahati yetu nzuri tu na sio kwa utashi wa waTanzania..., sijui kwa nini.
Lakini mtu huyo asiwe kama Marehemu Magufuli, kwa yale mabaya yake!

Sijui tutampataje mtu wa aina hiyo. Najua wapo..., lakini hawataki kujitokeza mbele waliokoe taifa letu.
I cannot say never...Lakini tumpe mama benefit of doubt ni mapema sana kuhukumu; ila nilishajiapiza sintaondoka dunia hii kama msindikizaji ipo siku nayo yaja tena si mbali sana kama si mimi kizazi changu nchi hii haitakaa irudi kwenye ufisadi....nadhani sipo ndotoni ebu tuendelee tuone!
 
I cannot say never...Lakini tumpe mama benefit of doubt ni mapema sana kuhukumu; ila nilishajiapiza sintaondoka dunia hii kama msindikizaji ipo siku nayo yaja tena si mbali sana kama si mimi kizazi changu nchi hii haitakaa irudi kwenye ufisadi....nadhani sipo ndotoni ebu tuendelee tuone!
Basi ulishindwa kutimiza wajibu wako maana CAG katuonyesha wazi, serikali ya mwendazake ilijaa ufisadi na upigaji.

Na upigaji aliotuonyesha CAG ni just tip of the iceberg, je angekagua mamununuzi ya hizo ndege si pangechimbika?
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Kuna story moja, sijui kama ni kweli au story tu, lakini ujumbe wake ni muhimu kuuelewa.

Inamhusu waziri mmoja mkubwa wa Nigeria, nafikiri alikuwa waziri wa fedha.

Alikuwa waziri shupavu kupinga rushwa, nchi haijawahi kuona waziri shupavu kama huyo, alikuwa anasema sana kukemea rushwa.

Ikafika wakati akaanza mpaka kwenda benki za kimataifa kunegotiate hela za Nigeria zirudishwe, alikuwa hataki mchezo.

Akaenda Uswizi, akazwa anazunguka mabenki, akafanya uchunguzi kutafuta benki yenye usiri kabisa Uswizi.

Akaipata, akaenda kuonana na CEO wa benki.

Akamwambia anataka majina ya Wanaijeria wote wenye hela kwenye hiyo benki, na vyanzo vyao vya mapato.

CEO akamwambia siwezi kukupa majina hayo.

Akasema nipe majina, ukinipa nitakutafutia deal kubwa sana na serikali ya Nigeria iweke hela zake kwenye benki yako, utapata faida sana.

CEO akawmambia siwezi kukupa majina, nafuata kanuni za faragha za kibenki.

Waziri akamwambia nitatengeneza deal na serikali ya Nigeria kwamba ukiripoti hela za wizi zilizoibiwa Nigeria tutakupa kiasi fulani katika hizo hela.

CEO akakataa, akasema hawezi kuzisaliti kanuni za faragha za kibenki.

Basi yule Waziri akamwambia CEO, huyu hapa Dr. Adebayo Adedeji wa African Development Bank, ukitupa majina tutakupa deal kubwa sana la Benki ya Maendeleo ya Africa, uweke hela za mabilioni mengi sana ya ADB.

CEO akakataa kutoa majina, akasema siwezi kusaliti kanuni za faragha za kibenki.

Waziri akasema sawa, wewe ndiye niliyekutafuta.

Nimekuja na mimi nataka kuweka mamilioni ya dola yangu kwenye benki yenu, lakini kabla ya kuweka kwanza nilikuwa nakupa mtihani nione kama watu wakija kutaka majina ya wateja wenu unaweza kutoa au hutatoa.

What's my point?

Ukiwa so caught up na habari za "mabeberu this, mabeberu that" na kushikwa na theatrics za viongozi wa Afrika wanaojinadi kupigana na mabeberu, unaweza kuchotwa kirahisi na watu wanaoshirikiana na hao mabeberu.

Mtu anaweza kujitengenezea image nzuri kuwa anapingana na mabeberu, kumbe na yeye anajipandisha bei tu apige hela kubwa zaidi.

Tunatakiwa kuwa makini sana tusiingie katika mtego wa simple narratives.

Kuna mabeberu wengine weusi wenzetu Watanzania, na kuna watu wa nchi za nje wanaoweza kutusaidia kupigana na ubeberu.

Kwa hiyo tujadili mambo kwa nuance, sio kwa a broad painting brush.
Kama nilivyosema nakubalina kabisa na wewe kwa mengi ila amini nimeishi na hawa ndugu zetu, nimefanya nao kazi tangu ni kiwa kinda kabisa age ya 25 years....Linapokuja maslahi ya jamii yao na mataifa yao imeshakuwa kama ugonjwa they never count us as beneficiaries....At personal level ni watu wazuri sana honest wenye integrity ila nadhani wamekuzwa kuamini sisi hatustahili kama wao. Hata akijitahidi vipi bado hawezi kubali kuwa sawa na sisi...Hofu hii ndiyo inayowapelekea kutoamini kutoa fursa ya sisi kujitegemea hata siku moja kwakua wanajua tukishafanikiwa pengine watapunguza heshima yao.

Chamsingi ni kweli, uki negotiate vizuri wana ka ustaarabu fulani hivi kakukubali ila si kwa level ile ya kukufanya uachane kabisa na utegemezi.
 
Basi ulishindwa kutimiza wajibu wako maana CAG katuonyesha wazi, serikali ya mwendazake ilijaa ufisadi na upigaji.

Na upigaji aliotuonyesha CAG ni just tip of the iceberg, je angekagua mamununuzi ya hizo ndege si pangechimbika?
Pengine!
 
@Mkandara ,unachambua hotuba ya Mh. Rais Samia au unamuongelea mwendazake JPM!!??
Naona Magufuli nyingi zaidi ya kilichoongelewa na Mh. Rais.
Well nachambua kulingana na jinsi mnavyopeleka Mjadala huu maanake nimeona watu wengi bado wanataka kulinganisha sio tu Magufuli na Samia bali hata Viongozi walotangulia kama JK .

Nami sina budi kuweka mawazo yangu haswa pale tunapo tofautiana. Mama Samia alisema Yeye na Magufuli kitu kimoja kwa maana ya kwamba YEYE mama Samia alishiriki kikamilifu katika maandalizi ya dira na mwelekeo pamoja na kila Maamuzi ya Utekelezaji aloyafanya rais Magufuli. Muda wote walikuwa pamoja yeye ubavuni mwake. Kwa wale wanaomlaumu Magufuli basi lawama hizo hata yeye zinamhusu. Lakini wapi kiswahili cha ndani kiliwashinda kutafsiri..

Nami katika bandiko langu nikasema sioni kama wako kitu kimoja! kutokana na hotuba yake siku aloapishwa, na labda sikuongezea pia hotuba yake nyingine siku ya kupokea taarifa ya CAG. Alisistiza sana mageuzi na wala sii maboresho ya dira na mwelekeo! Wazi kabisa alichukua mkondo mwingine hivyo.safari yetu haikuwa ile ya Uchaguzi mkuu 2020 tena.

Toka pale nilimsoma tofauti kabisa na Mambo yaakaanza kwenda kushoto Kulia, mvurugano kila kona, Wanafiki nao wakajitokeza wazi Bungeni, kuna Mkuu wa Mkoa fulani huko kusini, alidiriki hata kusema picha ya rais Magufuli ishushwe hata kabla Mama Samia kuapishwa! Haya yote yametokea within 15 days baada ya Magufuli kuzikwa. I was pissed off, nikamfikiria sana Mama Janet na familia Wanajisokiaje huko waliko? I wouldn't blame her for whatever decisions she has made since!

Na Wakati yote haya yanatokea, Mama Samia anazidi ku pose na mipasho - 'Ukinizungua Tutazinguana!' Sijii ngoma zinachezwa Mitandaoni blaa blaa blaaa yaani mambo ya Mwambao na Kibaokata! Pengine huo ndio Uhuru wa Kujieleza lakini siku zote Uhuru una mipaka yake jamani..
 
Kuna story moja, sijui kama ni kweli au story tu, lakini ujumbe wake ni muhimu kuuelewa.

Inamhusu waziri mmoja mkubwa wa Nigeria, nafikiri alikuwa waziri wa fedha.

Alikuwa waziri shupavu kupinga rushwa, nchi haijawahi kuona waziri shupavu kama huyo, alikuwa anasema sana kukemea rushwa.

Ikafika wakati akaanza mpaka kwenda benki za kimataifa kunegotiate hela za Nigeria zirudishwe, alikuwa hataki mchezo.

Akaenda Uswizi, akazwa anazunguka mabenki, akafanya uchunguzi kutafuta benki yenye usiri kabisa Uswizi.

Akaipata, akaenda kuonana na CEO wa benki.

Akamwambia anataka majina ya Wanaijeria wote wenye hela kwenye hiyo benki, na vyanzo vyao vya mapato.

CEO akamwambia siwezi kukupa majina hayo.

Akasema nipe majina, ukinipa nitakutafutia deal kubwa sana na serikali ya Nigeria iweke hela zake kwenye benki yako, utapata faida sana.

CEO akawmambia siwezi kukupa majina, nafuata kanuni za faragha za kibenki.

Waziri akamwambia nitatengeneza deal na serikali ya Nigeria kwamba ukiripoti hela za wizi zilizoibiwa Nigeria tutakupa kiasi fulani katika hizo hela.

CEO akakataa, akasema hawezi kuzisaliti kanuni za faragha za kibenki.

Basi yule Waziri akamwambia CEO, huyu hapa Dr. Adebayo Adedeji wa African Development Bank, ukitupa majina tutakupa deal kubwa sana la Benki ya Maendeleo ya Africa, uweke hela za mabilioni mengi sana ya ADB.

CEO akakataa kutoa majina, akasema siwezi kusaliti kanuni za faragha za kibenki.

Waziri akasema sawa, wewe ndiye niliyekutafuta.

Nimekuja na mimi nataka kuweka mamilioni ya dola yangu kwenye benki yenu, lakini kabla ya kuweka kwanza nilikuwa nakupa mtihani nione kama watu wakija kutaka majina ya wateja wenu unaweza kutoa au hutatoa.

What's my point?

Ukiwa so caught up na habari za "mabeberu this, mabeberu that" na kushikwa na theatrics za viongozi wa Afrika wanaojinadi kupigana na mabeberu, unaweza kuchotwa kirahisi na watu wanaoshirikiana na hao mabeberu.

Mtu anaweza kujitengenezea image nzuri kuwa anapingana na mabeberu, kumbe na yeye anajipandisha bei tu apige hela kubwa zaidi.

Tunatakiwa kuwa makini sana tusiingie katika mtego wa simple narratives.

Kuna mabeberu wengine weusi wenzetu Watanzania, na kuna watu wa nchi za nje wanaoweza kutusaidia kupigana na ubeberu.

Kwa hiyo tujadili mambo kwa nuance, sio kwa a broad painting brush.
Na mm pengine natafuta nafasi hiyo...Moyo wa binadamu una siri sana...I concur!
 
Kwa rehma zake Mwenyezi Mungu ni matumaini yangu sote tutaumaliza Mwezi huu Mtukufu wa Ramadhan salama salimin na hakika yeye ndiye mwenye kurehemu riziki zetu kubwa na ndogo na hapana mwingine apaswaye kuabudiwa. Tumuombe sote atuepushe na kila lisokuwa na kheri kwetu. Ameen.

Nina hakika siku ya leo tutasikia SIFA kemkem za mafuta ya tin na zaitun zitamiminika kupamba na kusifia hotuba ya rais wa JMT Mama Samia Suluhu Hassan kwa sababu imewagusa watu wote katika mazingira tofauti katika mwelekeo mpya wa dira ya Awamu hii ya sita ikitekeleza kauli mbiu ya KAZI IENDELEE.

Mimi binafsi, niseme ukweli wangu kutoka moyoni ya kuwa sii mshabiki wa rais Mama Samia Suluhu Hassan toka hotuba yake ya kwanza alipo apishwa kama rais wa Awamu ya sita. Huu ndio ukweli wangu! Na sababu zangu ni ndogo kabisa, nilimsoma toka mwanzo mwelekeo na Dira yake Kitaifa, dira ambayo Kiitikadi, mimi sii muumini wake na hupingana na nadharia zinazofungamana zaidi na UBEPARI badala ya UJAMAA wa Mwafrika.

Hivyo unaponisoma hapa ni muhimu Uzingatie kuwa mimi ni muumini wa UJAMAA wa Mwafrika na naamini Maendeleo ya Tanzania yataletwa na WATANZANIA wenyewe badala ya WAWEKEZAJI kutoka nje. Imani ya kwamba maendeleo yetu yanahitaji kuweka masharti rahisi ili kuvutia Wawekezaji ni sawa na fikra za.Kitumwa za Mababu zetu walokubali kupewa na wakoloni Shanga na vilemba ili tupendeze huku wagenu wakiondoka na madini mali ghafi na nyara zetu za Kitaifa.

Niseme wazi kwamba binafsi yangu naiona tofauti kubwa sana baina ya Hayati rais wa awamu ya Tani John Pombe Magufuli na Mama Samia Suluhu Hassan na kwamba hawa sii kitu kimoja hata kidogo. Tofauti zinazotokana na ahadi za mabadiriko makubwa ya SERA na SHERIA ambazo Chama cha Mapinduzi na Hayati Magufuli walizitumia kupata ushindi mkubwa katika Uchaguzi wa mwaka 2020. Niseme kwa nini nasema hivi?

Haina Shqka kabisa, Hayati Magufuli alikuwa rais anayepigania maslahi ya Wananchi Wanyonge kwa maana ya Watanzania Maskini dhidi ya Wawekezaji Mabeberu tofauti kabisa na Dira na Mwelekeo wa Mama Samia anayetazama zaidi viwashwishi kwa maslahi ya WAWEKEZAJI pamoja na dhana ya UKUONGEZA UZALISHAJI wa Mazao kwa WINGI zaidi (Quantity) badala ya fikra za Magufuli kudhamiria Kuanzisha viwanda vya ndani ili Kuongeza thamani ya Mazao yetu ya Asili yalokuwa BORA zaidi (Quality).

Nimalizie tu kwa kusema, rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan awe makini sana na dhana hizi, kwani hatukuanza jana wala juzi. Tulifuata mrengo ule toka wakati wa Rais Ally Hassan Mwinyi, akaja Mh. Benjamin Mkapa na Mwishowe mstaafu Jakaya Kikwete, na kote huko nyuma tulifanya makosa mengi sana kwa dhana ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Biashara. Matokeo yake tukaunda Matabaka ya Walionacho na wasiona nacho baina ya Wainanchi wenyewe. Ndipo Ufisadi na rushwa viliposhamiri kwani hapana alotaka kubakia katika kundi la wasionacho (Maskini)

Maoni ya rais kuhusu matumizi ya mbinu za kisasa katika Kilimo, kuna hatari kubwa ya nchi yetu kurudi kutawaliwa tena Kiuchumi kutokana na ujio wa mbegu za maabara ambazo zitaondoa kabisa rutuba ya Ardhi yetu, ubora wa mbegu zetu (Organic) na kubwa zaidi kumikilisha Mashirika ya nje nguzo za Uchumi wetu Kitaifa.

Maasalaam,
- Ramadhan Kareem
Huu ni ufupisho wa hotuba na wala si uchambuzi
 
Kama wewe unaamini kuwa 1984 Nyerere aliiacha nchi kwenye hali nzuri sana kiuchumi sina neno la kukuongezea.

Isipokuwa ninachofahamu ni kuwa Nyerere alikuwa amehangaika sana kutafuta misaada na mikopo nafuu akaishia kukutana na kikwazo cha IMF. Wafadhili wakubwa hata marafiki wa Tanzania hawakuwa tayari kumpa misaada mikubwa nje ya muafaka na IMF. Yeye aligoma kabisa kusaini mkataba na IMF akaamua kung’atuka.

Nilisoma kuwa AHM alipoingia madarakani kama Rais, wadau mbalimbali na media walimuuliza Mwalimu kama atakuwa radhi mrithi wake AHM asaini mkataba na IMF kama Rais wa JMT. Akasema hana tatizo kabisa na hilo ilimuradi sio yeye!

Nyerere alijua vizuri sana masharti ya IMF kwamba yangeathiri sana legacy yake hasa mashirika ya umma yaliyokuwa yameshikilia uchumi wa taifa. Lakini alijua hakuna namna. Itabidi AHM asaini mkataba na IMF na kuutekeleza. Ilikuwa dhahiri kwamba mashirika kama TRC, ATC, TANESCO, n.k. yaliyokuwa yakiendeshwa bila ufanisi, rushwa kwa wingi, nepotism, n.k. yangetetereka na mengine kufa.

Kwa taarifa yako, ATCL bado haijafufuliwa. Kilichofanyika ni serikali kujitwisha mzigo wa kununua na kumiliki ndege angalau kuweka taswira ya uhai wa ATCL. Ndege sio kigezo cha uhai wa shirika ya ndege. Kama alivyosema Rais Mh. SSH, hatua za kufufua shirika zitachukuliwa rasmi ili kulipa uhai wa kibiashara.

Miradi mingine ya umeme, reli, n.k. bado ni miradi. Tusubiri kuona hatua zitakazochukuliwa kuikamilisha na kuiendesha kwa ufanisi. Nina hakika hata Magufuli angekuwepo isingeendeshwa “KIJAMAA” kama enzi za Nyerere. Na angethubutu kufanya hivyo angekwama mapema sana. Hata North Korea yenyewe leo hii inashiriki uchumi wa kibepari kwa kuibia sana. Makampuni ya US na Ulaya yanazalisha bidhaa huko kwa kutumia mgongo wa China kukwepa vikwazo vya UN.

Kuhusu wizi wa Magufuli nakuachia ubishane na hao waliokuambia. Sina hizo siri.
Kama ilivyo ada sitachoka kutoa darasa kwa watu wanojadili vitu kwa sababu wamesikia kwa watu wakisema ama wamesoma pahala. ATCL haijafufuka kivipi wakati shirika.lipo, ndege zinaruklshwa na marubani Waajiriwa wa ATCL! Au kufufuka mpaka uhakiki na vidole kama Wafuasi wa Yesu? Hahahaha it's joke.

Ukiachana na Vita ya Uganda, mwaka 1980 hadi 1983, Dunia nzima kulikuwa na Economic Depression yaani kulikuwa na recesssion kali sana duniani, na kwa mara ya kwanza kabisa pipa la mafuta ghafi lilifika Usd 100. Since then hatujawahi kupitia rwcession wqla hatua kama hiyo ndio maana watu wengi hawakumbuki tulikotoka. Ebu Wauulize watu, mara ya mwisho Kimbunga kupita Tz ilikuwa mwaka gani? Utashangaa majibu utapakayo pata maana watakupa mafuriko ya Jangwani.. Hahahaha

Ni wakati huo huo nchi zote maskini zilipigwa na wimbi kubwa la Kiuchumi na pengine kuwa mwisho wa nchi za Kikomunist.

Marekani yenyewe wanamshukuru Reagan mpaka kesho kwa msimamo wake kupitisha Sheria kali ya Uzalendo - Patroit act yaani Mmarekani haruhusiwi kununua nje ya nchi lakini wao wnauza nje. Pia aliwanua kwa kuuza Ngada US wakifanya Money laundy ku finance vikundi vya Sandinista huko Amerika ya Kusini. Marekani (CIA) wakinunua Cocaine kutoka Colombia na kuuza kwa cartel wa US kisha wanachukua fedha na kununua silaha ambazo wanazipeleka huko Nicaragua kusini - A Game changer!

Kwa hiyo Mwalimu aliufanya Ujamaa wetu kama vile mzazi anavyomlea mwanaye anayetambaa. Leo bro unashangaa Mwalimu kutuvika diapers na kutulisha kwa kijiko, akatse tusile nyumba tusozijua.. Mtoto kulelewa na kijiji sii vibaya lakini huwezi kumpa mchawi mwanao amlee! Hizo ni methali zenye nidjamu ya woga wa kumpoteza mwana bora afe wa jirani...sijui unanipata pata?

Kwa hiyo Magufuli asingeweza kuendesha UJAMAA wa Mwalimu na hata Ubepari wa miaka ya 60s hadi 80s sio huu wa leo. Biden hawezi kuiongoza Marekani kwa sera za Jimmy Carter. Umaskini aloukuta Nyerere sio sawa kabisa na Umaskini tulokuwa nao leo. Hivyo itachekesha sana kama Magufuli naye angejaribu kutuvika diapers na kutulisha kwa kijiko ilhali sasa hivi sisi ni midume ya kutafuta Wachumba (Soko huria) Just common sense..

Soma hiyo document niliyokuwekea hapo nchini uone jinsi nchi ilivyokuwa inatimka vumbi kwa ujenzi kipindi cha JK

Achana na hearsay

By the way ni JK ndiye aliyetuondolea aibu ya kupitia Kenya kwenda Kagerhoja hapa.ni kipanda kwa dwni la Taifa. Nimekuuliza ni vitu gani vilivyojengwa kwa fesha hizo hujanibu. Unanipa list ya vitu ambavyo hata Mkuu wa Mkoa au Halmashauri walivifanya... Wabongo bana khaaa!
 
Amechambua na kulinganisha kisha kutoa mawazo yake! Hajatumia lugha ya kuudhi, amesema anachoamini yeye! Anachoamini si lazima kiwe sahihi na si lazima tukikubali! Ni mawazo mbadala!
 
Sioni kosa kwa huo mtazamo wa Rais, hiyo dhana ya kila Rais kuja na mtazamo wake imeasisiwa na watangulizi wake, hivyo naye sio wa kwanza, japo hii tabia kwa namna fulani inachangia kuturudisha nyuma kitaifa, binafsi ningependa pawe na kitu kama succession plan kwa hawa viongozi wetu, anapomalizia mmoja ndipo aanzie mwingine.

Kuhusu kuvutia wawekezaji yupo sawa, hawa watu tunawahitaji na dollar zao watasaidia kwa namna kupunguza tatizo la ajira nchini, na kuongeza mzunguko wa pesa kwa watanzania kama anavyojinasibisha Rais, japo anatakiwa kuwa na tahadhari ahakikishe analinda maslahi yetu kama taifa.

Mfano. Alipozungumzia uchimbwaji wa madini ya Hellium yaliyopo kwenye mbuga fulani akasema Simba hawayali yale, sawa hawayali, lakini awe makini kwenye mikataba serikali yake itakayoingia na wawekezaji coz record za mikataba na wawekezaji kwa viongozi wa awamu zilizopita ni mbovu.

Mwisho kabisa unajinasibu kwa ujamaa kwa kusema wewe unaamini maendeleo ya mwafrika yataletwa na mwafrika mwenyewe, hiyo dhana kiukweli kwangu imepitwa na wakati, huu ujamaa wa mwafrika utaleta maendeleo gani bila kuwa na teknolojia, capital, na skilled man power inayohitajika? hapa unanikumbusha ile kauli ya Nyerere aliposema madini yaachwe ardhini yatachimbwa na mtanzania akiwa tayari.

Sasa kuliko kuendelea kusubiri huo utayari kwa serikali hii ya CCM ambayo imekuwa ikipigana na maadui watatu (ujinga, umaskini, maradhi) toka tupate uhuru zaidi ya miaka sitini sasa, huo utayari wa kuchimba wenyewe tutaupata lini? naona bora tuwape wazungu wachimbe, lakini tuhakikishe tunapata faida badala ya kuwaachia wazungu waondoke na faida huku viongozi wetu wakipata 10% na sisi kuachiwa mashimo.
Tatizo mabeberu huangalia maslahi yao tu!! Inabidi kuwa tafu sana kushughulika na mabeberu! Wakikuona ni mjanja wanakupigia hesabu ya kukuondoa!!
 
Basi ulishindwa kutimiza wajibu wako maana CAG katuonyesha wazi, serikali ya mwendazake ilijaa ufisadi na upigaji.

Na upigaji aliotuonyesha CAG ni just tip of the iceberg, je angekagua mamununuzi ya hizo ndege si pangechimbika?
Mimi ningeomba hizi taarifa za CAG siku moja zinyanyambuliwe vizuri ili zieleweke.

Haiingii akilini hata mara moja, matarakimu yote yale anayoyatoa kila mwaka uwe ni upigaji; halafu cha kusikitisha zaidi, kila anapomaliza kuyatangaza, na watu kuyapigia mayowe kwa muda, kila kitu kinarudi pale pale kama kawaida, kana kwamba hakuna lolote lililotokea.

Huoni yeyote akiwajibishwa, na wala juhudi za serikali kurekebisha chochote.

Mwishowe, imenibidi nihitimishe kwamba huu ni aina fulani ya usanii mtupu!
 
Mimi ningeomba hizi taarifa za CAG siku moja zinyanyambuliwe vizuri ili zieleweke.

Haiingii akilini hata mara moja, matarakimu yote yale anayoyatoa kila mwaka uwe ni upigaji; halafu cha kusikitisha zaidi, kila anapomaliza kuyatangaza, na watu kuyapigia mayowe kwa muda, kila kitu kinarudi pale pale kama kawaida, kana kwamba hakuna lolote lililotokea.

Huoni yeyote akiwajibishwa, na wala juhudi za serikali kurekebisha chochote.

Mwishowe, imenibidi nihitimishe kwamba huu ni aina fulani ya usanii mtupu!
CAG hapeleki watu mahakamani.
Yeye anafanya kazi na kuiachia serikali au Bunge vichukue hatua. sasa serikali isipochukua hatua au bunge kutochukua hatua, wa kulaumiwa siyo CAG
 
CAG hapeleki watu mahakamani.
Yeye anafanya kazi na kuiachia serikali au Bunge vichukue hatua. sasa serikali isipochukua hatua au bunge kutochukua hatua, wa kulaumiwa siyo CAG
Naelewa vyema, kwamba sio kazi ya CAG kupeleka watu mahakamani, lakini si kuna vyombo stahiki?

Mimi sijamlaumu CAG; sijui ni vipi umenielewa hivyo!
 
Ndugu yangu, kwa wazungu hicho kinachoitwa "diplomasia ya uchumi" kinamaanisha wewe kutoa malighafi ziende kwao na wewe uwe mpokezi wa "finished products" kutoka kwao ikiwemo mitumba.
Tuwe makini sana na ufunguaji milango ya kukaribisha wawekezaji kwani wengi ni WAPORAJI na wajengaji wa kwao. KAMWE HATUTAENDELEZWA NA WAWEKEZAJI.

#TANZANIAISNOTFORSALE!
Mkuu,nakubaliana nawe.Lakini,hao wazungu hawawezi kutulazimisha.Tunahiari kukubali au kukataa.Katika diplomasia ya uchumi sisi kama nchi lazima tuzingatie "the so called win-win situation." Tunategemeana.
 
Nimependa hapo kwa wanyonge. Hivi huwa wanamaanisha nn hasa wanaposema wanyonge? Au ni hao mama na baba lishe wanaowalisha wananchi wetu uchafu kwa kuvunja sheria za nchi? Jpm kwangu mm ni the most divisive president ever kwa Tanzania. Kizazi cha akina makonda, sabaya etc walikuwa juu ya sheria enzi za jpm why? Jpm hajawahi kuwa rais wa wanyonge alikuwa rais wa kikundi fulani na wale brain washed aliokuwa anawagawia pesa barabarani.

Mama Samia yuko exposed na part of ipi kwa kuwa amefanya kazi kwenye NGOs kubwa Znz kwa zaidi ya 20 yrs kama sikosei. Yule mwingine im sorry ila ushamba wake umetucost sana kama nchi kwa kweli.
Kuwa exposed ina maana gani kwako na ushamba ni nini?!
 
Unapochambua hoja za kisiasa unatazama Uhalisia wa Sera zinazotazamiwa kuongoza DIRA na MWELEKEO wa Taifa Katika muda husika! Huhitaji kuandika gazeti au vipengele vya hotuba ilichukua masaa matatu kuelezea. Binafsi yangu, hotuba nzima sikuona jipya ambalo Mkapa na Kikwete hawakufanya. Kwa ujumla JK kwa nia nzuri kabisa alitoa nafuu ya kodi kwa Wawekezaji wa nje miaka mitano bila kulipa. zana na vitendea kazi za Ujenzi na Uendeshaji bure, vibali vya kazi vikatoka kama uyoga lakini matokeo yake Ufisadi ulikuwa mkubwa. Nini najaribu kujenga hapa? Ni kwamba Maendeleo ya Tanzania yataletwa na Watanzania wenyewe.

Serikali zote za Ulaya na Amerika zimeweza kutokana na pato la Kodi kwa kuwezesha raia wao. Ubepari ni mfumo ulotangulia kabla ya soko huria ambao msingi wake ulikuwa CHUMA NJE leta Mafanikio yako nyumbani. Na ndio Utajiri wa nchi hizo ulipoanzia. Sisi kama Mabepari tutachuma wapi na kuleta nyumbani. Aidha mfumo ulofuata baada ya wao kujenga viwanda ni Soko huria! Yaani wamepanua sasa soko lao na mahitaji waweze kuuza bidhaa zao mahala popote Duniani. Sisi tutauza wapi ikiwa hatuna viwanda vyetu wenyewe? Atakaye jenga Kiwanda Tanzania atasaidia Ajira na huyo raia ndiye atakuwa mlipa kodi wakati Mwekezaji akipeleka mavuno yake kwao Ulaya. Tumewaona kina Acacia na Symbion, je bado hatujapata somo?
Jamani Mchina ajenge bandari ya Bagamoyo kweli? Kama tumeweza.kujenga Hydro sisi wenyewe tunashindwa kipi kujenga Bandari? Let people pay tax hili sii swala la Hiyari bali mandatory na halihitaji ku negotiate. Je, ikiwa rais ana bishara zake nani ataweza kuzungumza naye kuhusu kodi? Tuwaache TRA wafanye kazi zao kiutaalam. Hukulipa.kodi miaka 5 au 10 iliyopita, ni nafuu zipi zitamfanya aanze kulipa kodi kesho? Just common sense haihitaji digrii..
Nasikia uchungu sana nikisoma uzi huu...yale machozi na zile kanga watanzania walizokuwa wanazitandika barabarani walizimaanisha...hata km JPM hakuwapa shilingi....maana kupata kiongozi mzalendo km JPM nimajaliwa na sasa kaondoka what next, business as usual ama?!
Nikiwaza viongozi waliokuwa majasiri km JPM hawakulast nabaki kuwa na maswali mengi sana..

ukiangalia alivyopigwa vita na baadhi ya watanzania...huku watu wengi huko nje wakimsifu wazungu kwa weusi..maswali yananizidi..
Tatizo ni sisi wanyewe watanzania tunasobotage power/maendeleo kwa mgongo wa mabepari kwa shule na degrees walizotumezesha au ni nini?!
Hapa namkumbuka Bob Marley alisema halaumu kwanini hakuenda shule maana angekuwa ignorant..na yet akawa maarufu kwa nyimbo zake za kupinga ubepari na mwisho wake wote tunaujua

vitu vingine haviihitaji rocket science jamani

Sokoine alisema ili usinyanyasike jitahidi ulime kwa bidii ukiwa na chakula chako hakuna atakae kunyanyasa...there is no free lunch jamani...tunaomba viongozi walikuwepo madarakani kwa Sasa mfanyemaamuzi yatakayo tukomboa kutoka kwenye umaskini...uwekezaji uwe wenye tija huku tukijikita kwenye mikakati yakujikomboa wenyewe....mkoloni alituacha kwa jembe la mkono na baadhi bado kilimo nihicho cha msimu..sitaki kuamini km hatuna wataalamu wakilimo wakutosha...hatuna uwezo kufungua viwanda vidogo km vya akina Tanga Fresh,katani,pamba tutengeneze nguo zetu,ngozi - viatu etc

Kuhusu mbegu jamani tuwe waangalifu GMO sio kabisa nadhani tumenusurika kwa Corona sababu ya lishe yetu..,tukiruhusu hizo mbegu zao..I believe ni one big trap..the next pandemic itakuwa balaa..nawakilisha maoni yangu

tusitukanane watanzania tupendane tujibu hoja kwa hoja hamna alikuwa zaidi ya mwingine wote tunajitahidi kujenga nchi yetu,tuwe kitu kimoja maana Mungu wetu ni mmoja

Mungu atubariki Watanzania wote
Mungu mbariki Raisi wetu
 
Mkuu,nakubaliana nawe.Lakini,hao wazungu hawawezi kutulazimisha.Tunahiari kukubali au kukataa.Katika diplomasia ya uchumi sisi kama nchi lazima tuzingatie "the so called win-win situation." Tunategemeana.
Mkuu hili neno 'win- win situation' ni mtego tu inategemea wewe utalielewaje.

Wakati wa JK tuliambiwa ni win win situation. Aki define Ukitaka kula lazima nawe uliwe.. Enzi ya JPM kuna wengine wanasema TUTA-wafukuza Wawekezaji! Hii kutangulizi TUTA wakati hao Wawekezaji bado wapo imna wanazidi kuingia ilinipa wasiwasi kutoka ndani zaidi kuliko nje. Leo tunasikia Tutalegeza masharti ya Uwekezaji...yale yaleeee
 
Kuna story moja, sijui kama ni kweli au story tu, lakini ujumbe wake ni muhimu kuuelewa.

Inamhusu waziri mmoja mkubwa wa Nigeria, nafikiri alikuwa waziri wa fedha.

Alikuwa waziri shupavu kupinga rushwa, nchi haijawahi kuona waziri shupavu kama huyo, alikuwa anasema sana kukemea rushwa.

Ikafika wakati akaanza mpaka kwenda benki za kimataifa kunegotiate hela za Nigeria zirudishwe, alikuwa hataki mchezo.

Akaenda Uswizi, akazwa anazunguka mabenki, akafanya uchunguzi kutafuta benki yenye usiri kabisa Uswizi.

Akaipata, akaenda kuonana na CEO wa benki.

Akamwambia anataka majina ya Wanaijeria wote wenye hela kwenye hiyo benki, na vyanzo vyao vya mapato.

CEO akamwambia siwezi kukupa majina hayo.

Akasema nipe majina, ukinipa nitakutafutia deal kubwa sana na serikali ya Nigeria iweke hela zake kwenye benki yako, utapata faida sana.

CEO akawmambia siwezi kukupa majina, nafuata kanuni za faragha za kibenki.

Waziri akamwambia nitatengeneza deal na serikali ya Nigeria kwamba ukiripoti hela za wizi zilizoibiwa Nigeria tutakupa kiasi fulani katika hizo hela.

CEO akakataa, akasema hawezi kuzisaliti kanuni za faragha za kibenki.

Basi yule Waziri akamwambia CEO, huyu hapa Dr. Adebayo Adedeji wa African Development Bank, ukitupa majina tutakupa deal kubwa sana la Benki ya Maendeleo ya Africa, uweke hela za mabilioni mengi sana ya ADB.

CEO akakataa kutoa majina, akasema siwezi kusaliti kanuni za faragha za kibenki.

Waziri akasema sawa, wewe ndiye niliyekutafuta.

Nimekuja na mimi nataka kuweka mamilioni ya dola yangu kwenye benki yenu, lakini kabla ya kuweka kwanza nilikuwa nakupa mtihani nione kama watu wakija kutaka majina ya wateja wenu unaweza kutoa au hutatoa.

What's my point?

Ukiwa so caught up na habari za "mabeberu this, mabeberu that" na kushikwa na theatrics za viongozi wa Afrika wanaojinadi kupigana na mabeberu, unaweza kuchotwa kirahisi na watu wanaoshirikiana na hao mabeberu.

Mtu anaweza kujitengenezea image nzuri kuwa anapingana na mabeberu, kumbe na yeye anajipandisha bei tu apige hela kubwa zaidi.

Tunatakiwa kuwa makini sana tusiingie katika mtego wa simple narratives.

Kuna mabeberu wengine weusi wenzetu Watanzania, na kuna watu wa nchi za nje wanaoweza kutusaidia kupigana na ubeberu.

Kwa hiyo tujadili mambo kwa nuance, sio kwa a broad painting brush.
Daaah Uzuri hiyo ni hadithi japo inafikirisha! Ukweli unabakia Ukisha umwa na nyoka kuogopa majani yakikugusa sii kosa! Tembea sehemu za wazi zaidi kulizo zenye kiza na majani..
 
Back
Top Bottom