Uchambuzi: Huruma ya rais Samia imeondoa mateso ya watoto shuleni siku hizi

Uchambuzi: Huruma ya rais Samia imeondoa mateso ya watoto shuleni siku hizi

BWANKU M BWANKU

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2019
Posts
377
Reaction score
435
UCHAMBUZI- HURUMA YA RAIS SAMIA, ILIVYOONDOA MATESO YA WATOTO SHULE SHIKIZI.

Na Bwanku M Bwanku.

Leo Ijumaa Februari 25, 2022 kwenye Gazeti la TANZANIA LEO Ukurasa wa 6 nimechambua uamuzi wa Serikali ya Rais Samia kutoa Bilioni 60 kujenga madarasa 3,000 kwenye Vituo Shikizi 970 na kuwaondolea Wanafunzi mateso makali waliyokuwa wanakutana nayo kwa ubovu na uhaba wa miundombinu ya Vituo hivyo kama uhaba wa madarasa hali iliyopelekea watoto kwa muda mrefu kusomea kwenye miti, matope na nyasi.

Shule Shikizi ni vituo vya kutoa elimu kwa wanafunzi wa elimu ya awali mpaka darasa la pili ambao wanakabiliwa na jiografia mbaya kuelekea kwenye shule mama za Msingi. Shule hizi ni saidizi za shule mama za Msingi. Kuna kata, mtaa ama tarafa ina shule lakini kuna wanafunzi wanaishi mbali sana na shule hizo mama, kwahiyo Serikali ikaona ni vema kujenga Vituo hivi Shikizi kwaajili ya wanafunzi wadogo wapate elimu wakiwa karibu na makazi yao halafu wakishakuwa wakubwa kidogo kwa maana wakishafika darasa la 3 hutoka kwenye vituo hivyo Shikizi na kuendelea sasa na Shule Mama za Msingi.

Kuingia kwa Rais Samia alikerwa na hali mbaya ya mateso ya wanafunzi kusomea kwenye mazingira magumu kwenye vituo hivi na hivyo kuamua kutokea hizo Bilioni 60 kujenga madarasa ya kisasa kabisa ili watoto wasomee pazuri na kuondoa kero hiyo ya miaka kwa miaka. Pata NAKALA ya Gazeti hili sasa ili uone mageuzi makubwa aliyoyafanya Rais Samia kwenye Vituo hivi Shikizi kwa muda wake mfupi tu wa miezi 11.

IMG-20220225-WA0014.jpg


ortamisemi~p~CYGd_Nrtlvh~1.jpg
 
Kweli aiseee, watoto walikuwa wanasomea kwenye hatari sana. Sasahivi kila sehemu nchi nzima ukipita watoto wanasomea madarasa ya kishua sana sana. Ashukuliwe Rais Samia. Mama Samia ana huruma sana na nawaambia tutafika nae mbali sana. Nchi inakimbia, inafunguka sana siku hizi
 
Acheni ufala:-----hao watoto wazazi wao ni walipa kodi pia wa taifa hili.

Rais anaongoza wananchi kuwapelekea maendeleo na ni wajibu wake wa kikatiba.

Hatukuchagua rais kwajili ya kutugawia huruma.

Hii nchi ina wananchi wengi wapumbavu sana ukiwemo wewe mtoa mada.
 
Baada ya msoto wa kukosa mahali pazuri pakusomea watakapohitimu masomo yao wanarudi tena kuungana na wenzao kwenye msoto wa mitaani na huruma za mama zinakuwa zimeishia hapo.
 
Kweli aiseee, watoto walikuwa wanasomea kwenye hatari sana. Sasahivi kila sehemu nchi nzima ukipita watoto wanasomea madarasa ya kishua sana sana. Ashukuliwe Rais Samia. Mama Samia ana huruma sana na nawaambia tutafika nae mbali sana. Nchi inakimbia, inafunguka sana siku hizi
Kwamba huruma ya SSH... ebu acheni kauli za kujidharaulisha!!
 
Acheni ufala:-----hao watoto wazazi wao ni walipa kodi pia wa taifa hili.

Rais anaongoza wananchi kuwapelekea maendeleo na ni wajibu wake wa kikatiba.

Hatukuchagua rais kwajili ya kutugawia huruma.

Hii nchi ina wananchi wengi wapumbavu sana ukiwemo wewe mtoa mada.
Pole sana habari umeuumiza mtima wako.
 
Habari imekaa kiudhalilishaji sana.
Na inaonesha kumuabudu mtu mmoja ambaye huruma yake na moods zake ndo zinaendesha taifa. This should not the case. We need stronger institutions not stronger persons!
Aibu sana!
Kujikomba kwa mwenye madaraka ndio sifa yetu.
 
Africa kuendelea itachukua karne nyingine hata mia. Imagine miaka zaidi ya 60 ya uhuru bado tunadili na uhaba wa madawati, madarasa, barabara mbovu, umeme, maji, dawa, vituo vya afya.

Inafikia mahali jambo kama hili la kawaida kabisa nalo linakuwa habari. Kama mambo kama haya hayaistui akili yako na kukuacha na maswali tambua ukombozi wa kifikra au kiuchumi hauko karibu kama unavyodhani. Bado tuna safari ndefu sana. SANA.
 
Acheni ufala:-----hao watoto wazazi wao ni walipa kodi pia wa taifa hili.

Rais anaongoza wananchi kuwapelekea maendeleo na ni wajibu wake wa kikatiba.

Hatukuchagua rais kwajili ya kutugawia huruma.

Hii nchi ina wananchi wengi wapumbavu sana ukiwemo wewe mtoa mada.
Acha kulalamika,utapata presha bure.
 
Baada ya msoto wa kukosa mahali pazuri pakusomea watakapohitimu masomo yao wanarudi tena kuungana na wenzao kwenye msoto wa mitaani na huruma za mama zinakuwa zimeishia hapo.
Hakuna msoto wa mitaani,wawaekezaji wanakuja,kwa viwanda,biashara,utalii,madini nk,zote ni ajira,watapata ajira.
 
Africa kuendelea itachukua karne nyingine hata mia. Imagine miaka zaidi ya 60 ya uhuru bado tunadili na uhaba wa madawati, madarasa, barabara mbovu, umeme, maji, dawa, vituo vya afya.

Inafikia mahali jambo kama hili la kawaida kabisa nalo linakuwa habari. Kama mambo kama haya hayaistui akili yako na kukuacha na maswali tambua ukombozi wa kifikra au kiuchumi hauko karibu kama unavyodhani. Bado tuna safari ndefu sana. SANA.
Ni kutokana ongezeko la watu.Afadhali sisi tunadili na uhaba wa madawati,madarasa,barabara,umeme,maji dawa,vituo vya afya nk.Hao wengine wanadili na vita,wanawaza vita,silaha makombora,mabomu ,Bunduki wanadili na kkuwana tu,Mrusi anamvamia Ukraine,Amerika na wengine NATO,nk
 
Daaa huyu angejuwa watoto hawana walimu asingeandika huuu upupu
Angejua ni wajibu wa kiongozi kufanya hivyo asingepiga vigeregere
Angejua ni Kodi yake asingeshangilia

Haya nakupa angalizo hebu njoo hapa Arusha mjini uone idadi ya watoto na walimu
 
Africa kuendelea itachukua karne nyingine hata mia. Imagine miaka zaidi ya 60 ya uhuru bado tunadili na uhaba wa madawati, madarasa, barabara mbovu, umeme, maji, dawa, vituo vya afya.

Inafikia mahali jambo kama hili la kawaida kabisa nalo linakuwa habari. Kama mambo kama haya hayaistui akili yako na kukuacha na maswali tambua ukombozi wa kifikra au kiuchumi hauko karibu kama unavyodhani. Bado tuna safari ndefu sana. SANA.
Bora mara mia yule dogo wa Mtwara alomlima mwalimu mkuu barua akafanye yake kwa uhuru kuliko kujifanya kusoma bila kuelimika.
Wanaojiita wasomi wengi hawana elimu yoyote ya kujua vipaumbele vya mwananchi mmoja mmoja.
Nakubaliana na wewe. Inatia aibu na hasira kwamba hadi Rais atoe maelekezo ndo kitu kifanyike. So watu wapo makazini lakini wanakula mishahara ya bure wakiendelea kusikilizia moods za Rais!
Ipo siku tutampata tena Rais mwenye instant mood swings (bipolar) na itakuwa hatari zaidi.
 
Back
Top Bottom