Uchambuzi; Usafiri wa ndege ni salama kuliko usafiri mwingine wowote, ajali ya precision lawama kwa waokoaji. Hongera rubani

Uchambuzi; Usafiri wa ndege ni salama kuliko usafiri mwingine wowote, ajali ya precision lawama kwa waokoaji. Hongera rubani

Zipo wanapona wengi tu! Tatizo kubwa watu kutokupatiwa msaada baada ya kupaa na parachute!

Ebu waza mtu hajawahi kubembea hata kwenye bembea Leo asavaivu angani pasipo msaada!
Kama ukitaka kunielewa vyema panda ghorofani chungulia chini ukiweza kumudu hofu Basi unaweza savaivu angani japo msaada ni lazima
...Ndege za Abiria hazibebi Pachute Mkuu! Acha kuchapia ![emoji57][emoji57]
 
Kweri hii dunia usi mzalau mtu, ndege na abiria wake ina okolewa na wavuvi na mitumbwi hii ajari imenifundisha kitu kikubwa sana.
 
Halafu kwenye kutangaza idadi ya watu walio hesabiwa kwenye sensa ya watu na makazi, tunatumia chopa!!

Bila shaka ni Tanzania pekee ndiyo tunafanya hivi.
Mi nimesema uhalisia! Uokoaji ni janga kubwa sana
 
Aisee sisi bado tunaishi zama zetu hili tukio limenishangaza nikawaza kama hapo karibu hali ni hii, ingekuwa katikati si ndio basi tena.
Ukweli sisi bado sana, nasema bado sana matukio, majanga ya kibinadamu yanayotokea yanaonyesha how we're, yaani janga linatokea mamlaka zinasubiri kutoa taarifa, yaani hapo ndipo wanaona kuna jambo muhimu.

Toka MV. Bukoba nk inaonyesha giza tulilonalo, sasa ngoja issues za kisiasa uone nini serikali inafanya!.
 
Hivi hao watu 26 waliookolewa vipi yani, mlango ulifunguliwa au?
 
Mbona watu mnang'ang'ania parachute wakati kuna mambo ya maana kayaandika?

Kwa ujumla mleta Uzi amezungumzia zoezi la uokoaji yaani usalama kwa abiria. Hata kama sehemu nyengine ameteleza ila kiitifaki inabidi wachangiaji wajikite kwenye zoezi la uokoaji hususani kwa hili tukio la leo. Lakini watu wanajifanya ujuaji mwingi na kuacha kujadili hoja ya msingi.
 
...Ndege za Abiria hazibebi Parachute ndugu!
Zitaongeza TU Uzito. Ile Ndege kubwa kuliko Zote inayoweza kubeba Abiria Mpaka 450 hauwezi kubeba Tena Parachute 450 za Abiria! ZitaongezUzito TU!
Sababu si uzito tu. Kuna sababu zaidi ya hiyo, kubwa zaidi ni design ya ndege za kiraia.
 
Mbona watu mnang'ang'ania parachute wakati kuna mambo ya maana kayaandika?

Kwa ujumla mleta Uzi amezungumzia zoezi la uokoaji yaani usalama kwa abiria. Hata kama sehemu nyengine ameteleza ila kiitifaki inabidi wachangiaji wajikite kwenye zoezi la uokoaji hususani kwa hili tukio la leo. Lakini watu wanajifanya ujuaji mwingi na kuacha kujadili hoja ya msingi.
Ndo watu wetu tuwazoee tu!
 
...Ndege za Abiria hazibebi Parachute ndugu!
Zitaongeza TU Uzito. Ile Ndege kubwa kuliko Zote inayoweza kubeba Abiria Mpaka 450 hauwezi kubeba Tena Parachute 450 za Abiria! ZitaongezUzito TU!
Sijaelewa! Hiyo ndege ya kubeba abiria 450 ndo kubwa kuliko zote hapa duniani au unasema ndio kubwa kuliko zote hapa Tanzania?
 
Katika masomo ambayo niliishia njiani ilikuwa kusomea urubani wa ndege!

Ndege ni chombo cha usafiri kinachoongoza kwa usalama kuliko vyombo vingine!

Ukubwa wa ajali ya ndege hutegemea na uzembe wa mamlaka zingine saidizi!

Ndege ina injini zaidi moja, mfano zilizopo Tanzania nyingi zina injini tatu!
Injini moja ikifeli haizuii ndege kutua kwa kutumia injini nyingine kwa dharula!

Ajali ya precision air huko Bukoba, Rubani kafanya kazi yake kwa usahihi kabisa!

Ndege inapoaanza safari huhifadhi oksjeni ya kutosha kulingana na ukubwa wa ndege!
Hewa hiyo ndiyo hutumika na abiria wawapo angani hadi wafikapo safari!

Ndege inapowashwa ndipo mitambo ya hali ya hewa kwenye ndege nayo hufanya kazi!
Ndege ikizimwa hata hewa hukosekana inakuwa sawa na chupa iliyofungwa!

Hivyo kama ndege hutegemea Hali ya hewa kupaa na kutua maana yake kazi ya rubani ni kuhakikisha anaipaisha au kuitua kulingana na Hali!
Tukio la precision linampa pongezi kubwa rubani kwamba baada ya hali kuwa mbaya!

Jambo la kwanza ilikuwa kuangalia yuko umbali gani kutoka ardhini! Karibu au mbali

Kama angekuwa juu sana na hali ikawa mbaya kutokana na hitilafu za chombo kuna namna nyingine ya kuokoa abiria

Lakini kama yuko mbali na chombo ni kizima lakini shida ni mawasiliano Basi hupaswa kutua uwanja uliyokaribu au kurudi!

Shida ni hapo akiwa karibu na ardhini halafu hali ya hewa iwe mbaya ambayo kuendelea na safari angani haiwezekani na mawasiliano ni mabovu!

Njia pekee ya rubani katika hali hiyo ni kupunguza risk! Yaani kuhakikisha anaitua ndege porini, jangwani au ziwani/baharini!

Rubani wa precision alifanikiwa sana kutua ndege salama! Shida yoyote ambayo huhatarisha uhai katika mazingira hayo ni ukosefu wa huduma saidizi! (Poor rescue team with modern technology)

Kama nilivyosema hapo awali ndege hutegemea hewa iliyotoka nayo ili watu wapumue!
Sasa ikitua baharini kama hakujapasuliwa kioo hewa haipiti watu ni rahisi kuzimia (faint)

Pia wanaowahi kuja kuokoa wakizibua vibaya maji huingia na watu hukanyagana kutokana na kutaka kuokolewa haraka!

Tukio la precision rubani kafanya kazi yake. Vyema! Mengine ni uzembe wa rescue team!

Wavuvi wamefanya wanachoweza kujitolea! Uzembe ni kwa mamlaka za uokoaji!

Kwa ajali za kuruka na parachute bado abiria wanaweza toka wote kwenye Ndege angani! Lakini huku duniani wakaenda kutua juu ya mbuga ya wanyama kama hakuna msaada watakufa hata juu ya mchongoma!

Usafiri wa ndege ni salama angani! Kuna rubani namba moja, rubani namba mbili, Technician Fundi rubani namba tatu usalama ni mkubwa kwa waongozaji hata mmoja akilala.

Matatizo yapo huku chini duniani namna ya uokoaji!

Na baada ya kugundua hili ni tatizo maboresho ya kizazi cha ndege kuelea kinafanyiwa kazi, ili hata ndege ikifa angani yenyewe nzima nzima iwe na parachute la kuelea taratibu, na ikitua baharini iweze pia kuelea kama meli!!

Lakini kwa sasa tatizo kubwa ni uokoaji kwa wakati! Vifo vingi ni uzembe kwa waokoaji!
Iyo ndege ya precision ilikuwa ninya brand gan ?
 
Sasa ueleze unavyoelewa mkuu mbon unakua km uneducated kwanini hupingi kwa kutoa hoja zako unazoona zina mashiko, unapopinga bila kueleza chochote wewe ndio unaonekana hujui kitu ila unajibaraghuza tu hapa na wewe uonekane unajua kumbe empty tu
Kupoteza muda kuwaelekeza watu wapumbavu mfano wako ni matumizi mabaya ya muda
 
Dark humor

WhatsApp Image 2022-11-06 at 10.44.45 AM.jpeg
 
Kupoteza muda kuwaelekeza watu wapumbavu mfano wako ni matumizi mabaya ya muda
Asante, mjinga mmoja wewe unaejifanya unajua kila kitu kumbe kichwani ni ZERO
 
Tungejikita kwenye ishu nzima ya kujadili namna ya uokoaji ..
Ninachoishangaa hii nchi, Kila kitu ni kichekesho, mpka sahv hakuna takwimu ya kueleweka ya abiria waliokuwa wamepanda ndege..

Ndege kuvutwa na wavuvi Tena kwa kamba, 🤣🤣🤣🤣
.
 
Back
Top Bottom