Uchawi au Majini hayapo! Nani ameshawahi kukutana na jini

Uchawi au Majini hayapo! Nani ameshawahi kukutana na jini

KItabu gani kinasema hivyo? Tupe kifungu cha kusapoti usemacho
Vitabu vya dini vinakuambia mababu na mabibi zako wote waliozaliwa kabla ya Yesu na Mtume, na hata waliozaliwa baada lakini hawakuwajua wageni hawa na dini zao kwa sababu ya umbali huko Africa watachomwa na moto wa milele na Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote, kwa kuwa hawakumjua huyo Mungu, kwa kuwa hawakupewa ufunuo wa vitabu hivyo vya dini kumjua huyo Mungu.

Unaamini hili nalo?
 
Kijana mbona muoga sana wa maswali ? Swali langu halina makadirio hayo,bali uhalisia.

Onyesha uwezekano wa kutokuwa na kiulizi katika suala la muumbaji. Yaani utuambie linakaa tamko gani nje ya tamko "nani ?". Ukiweza naacha huu mjadala.

Usijitoe ufahamu,suala la ithibati juu ya uwepo wa Mola muumba hili nimeshalifanya,na hukuweza kukosoa ushahidi wangu. Hili nilishalimaliza zamani. Kazi imebaki kwako kutithibitishia ya uwa Mola hayupo. Na ituambie huu ulimwengu imekuwaje ukawepo.

Lugha ina hukumu. Ndiyo maana huwezi kutumia tamko "nini ?" kama kiulizi cha kitaka kujua chanzo cha Ulimwengu au dunia imekuwaje ikawa hivi ilivyo.

swali halitakiwi kua "nani ameweka genetic code katika DNA" bali linatakiwa kua "imewezekanaje DNA" kua coded!? na imekua coded na nini?

swali la nani linakua sio valid maana linalenga katika kuitaja nafsi!

nini ni generalisation ambayo inajumlisha nani kifupi "nani" ni swali ambalo linatakiwa kuja baada ya "nini".

kortini hua wanatumia neno "speculating" kuashiria kua muulizaji anauliza swali linalopelekea jibu alilonalo! yaani swali linakudirect kabisa kwenye jibu la muulizaji! ndo maana swali la "nani" sio valid!

bisha tu, mana ndo kazi yako!
 
Kwanini unasema Uongo ?

Nakuthibitishia tena ya kuwa Mola yupo.

Anasema Allah mtukufu :

35. Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji?

36. Au wao wameziumba mbingu na ardhi? Bali hawana na yakini. (at-Tur : 35 - 36)

Sasa kosoa huu uthibitisho kwa kujibu swali hilo.

kutumia aya za kitabu chenye contradiction haina mantiki yaani ni sawa na kutumia uongo kuthibitisha uongo!
Quran inajipinga yenyewe hvyo huwezi kuitumia katika kusapoti hoja yako! hvyo hoja ni dhaifu
 
Kuna nadharia za ajabu sana Africa ambazo huwezi ziona dunia ya kwanza.
Uchawi ni nini. Nani ambaye anaweza kutupa prove uchawi upo? Nani alimuona mchawi? Nani anaujua uchawi? Uchawi una nguvu gani?

Hayo Majini ni nini? Hakuna cha majini wala babu yake na majini?
Hizo ni drama za kufikirika.

Utasikia kuna majini. Ushawahi kuliona! Utasikia majini majini ni viumbe visivyoonekana kama hayaonekani umejuaje kama yapo.
Majini na uchawi ni dhana za kufikilika

Lete Proof hapa.

Hakuna cha majini wala uchawi
Ufahamu wako ni Mdogo Sana kuhusu dunia tulia.
 
Alikuwaje! Prove.. Hakuna majini
Njoo tukupeleke chuo cha uchawi temeke na syllabus zipo na notice zake zipo.Unasoma uchawi darasani miaka 5 kwa theory na vitendo then uganga miaka 2 unapewa degree cheti kabisa
 
Mzee jibi swali nililo kuuliza. Set ni makubaliano ya wana mahesabu,naongelea uhalisia mzee.

Jibu swali nililo kuuliza.

Nakupa kazi onyesha na utoe mfano wa kuwa "nini ?" ndani yake kuna "nani ?". Mimi nakuonyesha "nani ?" ndani yake kuna nini. Kwangu mimi kuna nani. Sasa onyesha kwenye nini kuna nani.

unataka mfano wa kuonesha nani ipo ndani ya nini!?

mfano huu hapa!

nyumbani kwangu nafuga kuku, paka na mbwa, pia nna watoto hapahapa kwangu! nmeacha sahani ya nyama nje nkaingia ndani baada ya nusu saa narudi nakuta vipande vya nyama havipo kumbuka hapo nje uani kuna mbwa watoto wanacheza paka na kuku pia! sasa natakiwa kujiuliza nani kachukua vipande vya nyama!? au kujiuliza nini kimechukua!?

swali la kwanza linatakiwa kua nini maana kuna variety of options ambazo ni paka mbwa watoto au kuku! nkipata jawabu kua ni watoto basi ntauliza nani!? ili kujua yupi alichukua vipisi vya nyama!


nadhani nmejaribu kukuonesha vema!
 
Onyesha kama mahubiri si uthibitisho. Niambie kilicho andikwa kwenye aya ni uhalisia au siyo uhalisia ?

Kisha kosoa nilicho kiandika. Ukiweza naacha mjadala na nakuwa na fikra kama zako.

sio kila kitu ni uhalisia!
 
Njoo tukupeleke chuo cha uchawi temeke na syllabus zipo na notice zake zipo.Unasoma uchawi darasani miaka 5 kwa theory na vitendo then uganga miaka 2 unapewa degree cheti kabisa

chuo kipo temeke sehemu gani!? tupe jina la chuo!
 
Baadhi wanasema kuna majini wazuri na majini wabaya, wazuri hua wanasali na kumuomba mungu na wabaya hadi ma atheist wapo

Wapo wanaodai kua kuna elimu juu ya utengenezaji wa hivyo viumbe.

Kuna siku nilisikia redioni mkufunzi akitoa somo namna ya kuita jini kwa kutamka maneno fulani hivi ya kiarabu.

Yale maneno niliyanukuu vyema nikawa naya practice maana mdau alisema unatakiwa uende njia panda usiku wa maneno kisha utamke hayo maneno

Nikiwa na tumaini kua leo ndio siku ambayo najithibitishia kua majini yapo, nikafika njia panda nikaanza kuyatamka hayo maneno kwa kuyarudia rudia zaidi ya mara 100 lakini hakukua na respond yeyote kutoka third party system

Wakati nikiendelea kutamka yale maneno nilishtukizwa na roba flani matata upande wa nyuma, mwanzo nilidhani ni ujio wa jini kumbe ni kibaka wa mtaa na alikua anapiga patrol

Aisee nilimlaumu sana yule jamaa wa redioni

Eti "Third part system" hahahahah ujue we comedy sana
 
Aya zako ni za logical non sequitur.

Kwa sababu hazielezi "wao" ni nani, na hata kama zinazungumzia watu, watu kuumbwa kwa kitu na kutoumba ulimwengu hakumaanishi wao na ulimwengu vimbwa na Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote.

Thibitisha Mungu yupo.

Usilete aya chovu kivivu hapa.

Mimi nakwambia BMW halijateng3nezwa na James Bond 007. James Bond 007 ni character wa hadithi hayupo kiuhakisia.

Unaniketea aya inasema kwani BMW halijat3mengenezwa kwa chuma?

Logical non sequitur.
Una hoja dhaifu sana. Ndiyo maana nilitaka ujadili aya,na huwa ukijaribu kujibu maswali yangu unaangukia pua,hili nakuonyesha na nilishakuonyesha tangu huko nyuma katika mijadala mingine.

Niliwahi kukwambia ya kuwa suala la ukana Mungu hamjaanza nalo nyinyi,hili weka akilini,walikuwepo na bado watakuwepo. Aya imewajumuisha nyote wenye fikra kama hizo,ndiyo maana ikawataja wao kwa tamko la kufidisha ujumla,kiistilahi tunasema "Umuuman".

Kwahiyo hakuna logic inayoweza kukosoa. Lakini umeonyesha udhaifu mkubwa sana katika hili,sababu aya iko wazi inawauliza wakana Mungu,wanao kataa kuhusu uumbaji,na hapa ndipo ithbati ilipo.

Nilisema hivi ukiweza kukosoa hiyo aya naacha huu mjadala. Sasa kama hata hujui kama wewe ni mkana Mungu,huu mjadala haukufai. Unapoteza muda wako bure.

Kwahiyo swali langu bado liko pale pale. Nasubiri ukosoaji wako.
 
Kwa sababu inawezekana wewe ni mfiadini uliyeamua kwamba hata ukioneshwa Mungu wako ana contradiction hutakubali.

Ukioneshwa kwamba Mungu wako hayupo, utakubali?

Au utang'ang'ania ushabiki wa ki Mujahedeen tu?
Hali ina tabia moja ya ajabu saba,huwa ina mili popote.

Wewe onyesha hilo kama uone nitakataa haki au kinyume chake.

Nasubiri uonyeshe.
 
swali halitakiwi kua "nani ameweka genetic code katika DNA" bali linatakiwa kua "imewezekanaje DNA" kua coded!? na imekua coded na nini?
Lugha ina hukumu kijana. Hakuna lugha inakubali kiulizi cha swali "nini ?" katika jambo lenye mfumo na utaratibu maalumu.

Unajia nini inasimama kumaanisha nini ? Ushawahi kusoma somo la adabu za kuuliza maswali na namna ya kuuliza maswali ?

Ili uone ya kuwa swali lako ni la uongo. Tupe majibu kwa mujibu wa swali lako,kisha tuonyeshe uwezekano wa nini kufanya jambo hilo. Yaani nionyeshe hiyo nini ilivyoweza kufanya hivyo. Ukiweza kufanya hivyo naacha huu mjadala.
swali la nani linakua sio valid maana linalenga katika kuitaja nafsi!
Onyesha nje ya nafsi na kisichokuwa na nafsi kutenda na kusanifu jambo. Tofauti yangu na yenu ni kuwa mimi naongelea uhalisia nyinyi mnaleta dhana na dhahania. Lazima muumie.
nini ni generalisation ambayo inajumlisha nani kifupi "nani" ni swali ambalo linatakiwa kuja baada ya "nini".
Thibitisha hili kwa kutoa mfano. Onyesha hilo kwa kuweka nani na nini,na nani iwe baada ya nini ? Hivi sijui kama huwa mnafikiria haya mambo,au mnajiandikia.
 
kortini hua wanatumia neno "speculating" kuashiria kua muulizaji anauliza swali linalopelekea jibu alilonalo! yaani swali linakudirect kabisa kwenye jibu la muulizaji! ndo maana swali la "nani" sio valid!

bisha tu, mana ndo kazi yako!
Jenga hoja na kosoa,usilete tuhuma baada ya kushindwa hoja.
 
kutumia aya za kitabu chenye contradiction haina mantiki yaani ni sawa na kutumia uongo kuthibitisha uongo!
Quran inajipinga yenyewe hvyo huwezi kuitumia katika kusapoti hoja yako! hvyo hoja ni dhaifu
Nakupa kazi hii onyesha wapi Qur'aan inajipinga yenyewe kisha nikuulize maswali,ukijibu maswali yangu nakuwa mkana Mungu.

Hapo hap unayo yasema haya hata Qur'aan huijui. Nasubiri hizo Contradiiction unazo dai,na tuzijadili moja baada ya nyingine. Mwenzako alikimbia anaye jiita Kiranga,anaweka kisha hataki kuzijadili.
 
unataka mfano wa kuonesha nani ipo ndani ya nini!?

mfano huu hapa!

nyumbani kwangu nafuga kuku, paka na mbwa, pia nna watoto hapahapa kwangu! nmeacha sahani ya nyama nje nkaingia ndani baada ya nusu saa narudi nakuta vipande vya nyama havipo kumbuka hapo nje uani kuna mbwa watoto wanacheza paka na kuku pia! sasa natakiwa kujiuliza nani kachukua vipande vya nyama!? au kujiuliza nini kimechukua!?

swali la kwanza linatakiwa kua nini maana kuna variety of options ambazo ni paka mbwa watoto au kuku! nkipata jawabu kua ni watoto basi ntauliza nani!? ili kujua yupi alichukua vipisi vya nyama!


nadhani nmejaribu kukuonesha vema!
Unasikitisha sana,niliposema hili hamliwezi nilimaanisha.

Mfano wako hauonyeshi kwenye nini kuna nani,bali mfano wako umemili kwenye nini. Ndiyo maana umezunguka sana. Hata mimi naweza kuweka msingi wa swali katika nani mwanzi mwisho,ila naweza kuonyesha ujumla wa nani kuzalisha nini.

Nakupa mifano miwili,wa nani kuzalisha nini kwa hususia na nini kuzalisha nani kadhalika,ila swali langu ni ujumla wa nani ndani yake kuna nini,ndiyo maana nili hoji huko mwanzo mtuonyeshe tu hali wezekano au ishara tu ya nini kuweza kumiliko ufahamu na usanifu.

1. Humo ndani kuna nani ? (Nini kuna nani)

2. Kichwani mwako umeweka nini ? (Nani kuna nini)

Swali langu la msingi ni kuonyesha nini kuna nani yenye ufahamu na kuratibu mambo. Muwe mnaelewa hoja. Hili swali huwezi kujibu bali hata wakubwa zako hawawezi kujibu,mwenzako amelikikbia.
 
Baadhi wanasema kuna majini wazuri na majini wabaya, wazuri hua wanasali na kumuomba mungu na wabaya hadi ma atheist wapo

Wapo wanaodai kua kuna elimu juu ya utengenezaji wa hivyo viumbe.

Kuna siku nilisikia redioni mkufunzi akitoa somo namna ya kuita jini kwa kutamka maneno fulani hivi ya kiarabu.

Yale maneno niliyanukuu vyema nikawa naya practice maana mdau alisema unatakiwa uende njia panda usiku wa maneno kisha utamke hayo maneno

Nikiwa na tumaini kua leo ndio siku ambayo najithibitishia kua majini yapo, nikafika njia panda nikaanza kuyatamka hayo maneno kwa kuyarudia rudia zaidi ya mara 100 lakini hakukua na respond yeyote kutoka third party system

Wakati nikiendelea kutamka yale maneno nilishtukizwa na roba flani matata upande wa nyuma, mwanzo nilidhani ni ujio wa jini kumbe ni kibaka wa mtaa na alikua anapiga patrol

Aisee nilimlaumu sana yule jamaa wa redioni
Hahahaha dah Hadi njaa imeisha sasa
 
Upo mjini unasema hakuna uchawi. Nenda usukumani huko shinyanga. Ukishafika kijijini sema hakuna uchawi na hakuna mtu wa kunifanyia kitu. Utakalopata uje utuhadithie hapa
 
Back
Top Bottom