Kinengunengu
JF-Expert Member
- May 3, 2021
- 1,716
- 4,375
Vitabu vya dini vinakuambia mababu na mabibi zako wote waliozaliwa kabla ya Yesu na Mtume, na hata waliozaliwa baada lakini hawakuwajua wageni hawa na dini zao kwa sababu ya umbali huko Africa watachomwa na moto wa milele na Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote, kwa kuwa hawakumjua huyo Mungu, kwa kuwa hawakupewa ufunuo wa vitabu hivyo vya dini kumjua huyo Mungu.
Unaamini hili nalo?
Kijana mbona muoga sana wa maswali ? Swali langu halina makadirio hayo,bali uhalisia.
Onyesha uwezekano wa kutokuwa na kiulizi katika suala la muumbaji. Yaani utuambie linakaa tamko gani nje ya tamko "nani ?". Ukiweza naacha huu mjadala.
Usijitoe ufahamu,suala la ithibati juu ya uwepo wa Mola muumba hili nimeshalifanya,na hukuweza kukosoa ushahidi wangu. Hili nilishalimaliza zamani. Kazi imebaki kwako kutithibitishia ya uwa Mola hayupo. Na ituambie huu ulimwengu imekuwaje ukawepo.
Lugha ina hukumu. Ndiyo maana huwezi kutumia tamko "nini ?" kama kiulizi cha kitaka kujua chanzo cha Ulimwengu au dunia imekuwaje ikawa hivi ilivyo.
Kwanini unasema Uongo ?
Nakuthibitishia tena ya kuwa Mola yupo.
Anasema Allah mtukufu :
35. Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji?
36. Au wao wameziumba mbingu na ardhi? Bali hawana na yakini. (at-Tur : 35 - 36)
Sasa kosoa huu uthibitisho kwa kujibu swali hilo.
Ufahamu wako ni Mdogo Sana kuhusu dunia tulia.Kuna nadharia za ajabu sana Africa ambazo huwezi ziona dunia ya kwanza.
Uchawi ni nini. Nani ambaye anaweza kutupa prove uchawi upo? Nani alimuona mchawi? Nani anaujua uchawi? Uchawi una nguvu gani?
Hayo Majini ni nini? Hakuna cha majini wala babu yake na majini?
Hizo ni drama za kufikirika.
Utasikia kuna majini. Ushawahi kuliona! Utasikia majini majini ni viumbe visivyoonekana kama hayaonekani umejuaje kama yapo.
Majini na uchawi ni dhana za kufikilika
Lete Proof hapa.
Hakuna cha majini wala uchawi
Njoo tukupeleke chuo cha uchawi temeke na syllabus zipo na notice zake zipo.Unasoma uchawi darasani miaka 5 kwa theory na vitendo then uganga miaka 2 unapewa degree cheti kabisaAlikuwaje! Prove.. Hakuna majini
Mzee jibi swali nililo kuuliza. Set ni makubaliano ya wana mahesabu,naongelea uhalisia mzee.
Jibu swali nililo kuuliza.
Nakupa kazi onyesha na utoe mfano wa kuwa "nini ?" ndani yake kuna "nani ?". Mimi nakuonyesha "nani ?" ndani yake kuna nini. Kwangu mimi kuna nani. Sasa onyesha kwenye nini kuna nani.
Onyesha kama mahubiri si uthibitisho. Niambie kilicho andikwa kwenye aya ni uhalisia au siyo uhalisia ?
Kisha kosoa nilicho kiandika. Ukiweza naacha mjadala na nakuwa na fikra kama zako.
Njoo tukupeleke chuo cha uchawi temeke na syllabus zipo na notice zake zipo.Unasoma uchawi darasani miaka 5 kwa theory na vitendo then uganga miaka 2 unapewa degree cheti kabisa
Baadhi wanasema kuna majini wazuri na majini wabaya, wazuri hua wanasali na kumuomba mungu na wabaya hadi ma atheist wapo
Wapo wanaodai kua kuna elimu juu ya utengenezaji wa hivyo viumbe.
Kuna siku nilisikia redioni mkufunzi akitoa somo namna ya kuita jini kwa kutamka maneno fulani hivi ya kiarabu.
Yale maneno niliyanukuu vyema nikawa naya practice maana mdau alisema unatakiwa uende njia panda usiku wa maneno kisha utamke hayo maneno
Nikiwa na tumaini kua leo ndio siku ambayo najithibitishia kua majini yapo, nikafika njia panda nikaanza kuyatamka hayo maneno kwa kuyarudia rudia zaidi ya mara 100 lakini hakukua na respond yeyote kutoka third party system
Wakati nikiendelea kutamka yale maneno nilishtukizwa na roba flani matata upande wa nyuma, mwanzo nilidhani ni ujio wa jini kumbe ni kibaka wa mtaa na alikua anapiga patrol
Aisee nilimlaumu sana yule jamaa wa redioni
Una hoja dhaifu sana. Ndiyo maana nilitaka ujadili aya,na huwa ukijaribu kujibu maswali yangu unaangukia pua,hili nakuonyesha na nilishakuonyesha tangu huko nyuma katika mijadala mingine.Aya zako ni za logical non sequitur.
Kwa sababu hazielezi "wao" ni nani, na hata kama zinazungumzia watu, watu kuumbwa kwa kitu na kutoumba ulimwengu hakumaanishi wao na ulimwengu vimbwa na Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote.
Thibitisha Mungu yupo.
Usilete aya chovu kivivu hapa.
Mimi nakwambia BMW halijateng3nezwa na James Bond 007. James Bond 007 ni character wa hadithi hayupo kiuhakisia.
Unaniketea aya inasema kwani BMW halijat3mengenezwa kwa chuma?
Logical non sequitur.
Hali ina tabia moja ya ajabu saba,huwa ina mili popote.Kwa sababu inawezekana wewe ni mfiadini uliyeamua kwamba hata ukioneshwa Mungu wako ana contradiction hutakubali.
Ukioneshwa kwamba Mungu wako hayupo, utakubali?
Au utang'ang'ania ushabiki wa ki Mujahedeen tu?
Lugha ina hukumu kijana. Hakuna lugha inakubali kiulizi cha swali "nini ?" katika jambo lenye mfumo na utaratibu maalumu.swali halitakiwi kua "nani ameweka genetic code katika DNA" bali linatakiwa kua "imewezekanaje DNA" kua coded!? na imekua coded na nini?
Onyesha nje ya nafsi na kisichokuwa na nafsi kutenda na kusanifu jambo. Tofauti yangu na yenu ni kuwa mimi naongelea uhalisia nyinyi mnaleta dhana na dhahania. Lazima muumie.swali la nani linakua sio valid maana linalenga katika kuitaja nafsi!
Thibitisha hili kwa kutoa mfano. Onyesha hilo kwa kuweka nani na nini,na nani iwe baada ya nini ? Hivi sijui kama huwa mnafikiria haya mambo,au mnajiandikia.nini ni generalisation ambayo inajumlisha nani kifupi "nani" ni swali ambalo linatakiwa kuja baada ya "nini".
Jenga hoja na kosoa,usilete tuhuma baada ya kushindwa hoja.kortini hua wanatumia neno "speculating" kuashiria kua muulizaji anauliza swali linalopelekea jibu alilonalo! yaani swali linakudirect kabisa kwenye jibu la muulizaji! ndo maana swali la "nani" sio valid!
bisha tu, mana ndo kazi yako!
Nakupa kazi hii onyesha wapi Qur'aan inajipinga yenyewe kisha nikuulize maswali,ukijibu maswali yangu nakuwa mkana Mungu.kutumia aya za kitabu chenye contradiction haina mantiki yaani ni sawa na kutumia uongo kuthibitisha uongo!
Quran inajipinga yenyewe hvyo huwezi kuitumia katika kusapoti hoja yako! hvyo hoja ni dhaifu
Unasikitisha sana,niliposema hili hamliwezi nilimaanisha.unataka mfano wa kuonesha nani ipo ndani ya nini!?
mfano huu hapa!
nyumbani kwangu nafuga kuku, paka na mbwa, pia nna watoto hapahapa kwangu! nmeacha sahani ya nyama nje nkaingia ndani baada ya nusu saa narudi nakuta vipande vya nyama havipo kumbuka hapo nje uani kuna mbwa watoto wanacheza paka na kuku pia! sasa natakiwa kujiuliza nani kachukua vipande vya nyama!? au kujiuliza nini kimechukua!?
swali la kwanza linatakiwa kua nini maana kuna variety of options ambazo ni paka mbwa watoto au kuku! nkipata jawabu kua ni watoto basi ntauliza nani!? ili kujua yupi alichukua vipisi vya nyama!
nadhani nmejaribu kukuonesha vema!
Kisicho halisi hakina maana mzee,maisha yetu yote tunaishi kuutafuta ukweli na ndiyo uhalisia huo.sio kila kitu ni uhalisia!
Hahahaha dah Hadi njaa imeisha sasaBaadhi wanasema kuna majini wazuri na majini wabaya, wazuri hua wanasali na kumuomba mungu na wabaya hadi ma atheist wapo
Wapo wanaodai kua kuna elimu juu ya utengenezaji wa hivyo viumbe.
Kuna siku nilisikia redioni mkufunzi akitoa somo namna ya kuita jini kwa kutamka maneno fulani hivi ya kiarabu.
Yale maneno niliyanukuu vyema nikawa naya practice maana mdau alisema unatakiwa uende njia panda usiku wa maneno kisha utamke hayo maneno
Nikiwa na tumaini kua leo ndio siku ambayo najithibitishia kua majini yapo, nikafika njia panda nikaanza kuyatamka hayo maneno kwa kuyarudia rudia zaidi ya mara 100 lakini hakukua na respond yeyote kutoka third party system
Wakati nikiendelea kutamka yale maneno nilishtukizwa na roba flani matata upande wa nyuma, mwanzo nilidhani ni ujio wa jini kumbe ni kibaka wa mtaa na alikua anapiga patrol
Aisee nilimlaumu sana yule jamaa wa redioni
Ni muda mrefu umepita hayo maeno siyakumbuki nacho kumbuka ni hilo tukio tuTuwekee hayo maneno uliyo ya nukuu vizuri.