Uchawi au Majini hayapo! Nani ameshawahi kukutana na jini

We jamaa Mzushi tu

mchawi gani unatumia hadi whatsapp, profile picha umemuweka morison mzee wa kukera akiwa amepiga uzi mpya??

Nakupa task tumia uchawi wako fanya uweze kuipata namba yangu ya whatsapp niliyotumia kuangalia profile yako, ukiweza hilo tunafunga huu uzi na rasmi naanza kuamini uchawi
 

unasema lugha inahukumu!? katika comments zangu pitia nimekupa mfano ulio wazi!

halafu hua ukiulizwa swali ukashindwa kujibu hua unasema "swali ni la uongo" huu ujinga alikufundisha nani!? yaani mtu yoyote atakushangaa sana eti swali la uongo! unataka istilahi za kuuliza maswali usilete konakona istilahi pekee ya swali ni lijibiwe ! sasa ww unataka kuuliza maswali katika mtindo elekezi wa majibu yako!

na nnadhani ukiendelea na huu upuuzi utakosasifa ya kuingia mjadala na mimi! maana kazi ya kujadiliana na wewe itakua sawa nakumkanda mbwa kizazi
 

una uthibitisho gan Quran siijui!? au kila mtu anaekwambia Quran si sahihi ni Quran haijui!? hii inathibitisha ni namna gani umekariri! umekaririshwa kila mkosoaji ni haijui Quran!

pole sana
 

tumia akili yako vizuri hyo mifano haiendani na nini na nani!

mfano wa kwanza umehoji uwepo wa nabi kwenye nini pasi na kujua uwepo wa kitu husika ila umekipa nafsi moja kwa moja! je kama humo ndani kuna kitabu!?

mfano wako wa pili unauliza kichwani mwako umeweka nini hili ni swali ambalo linakuleta kwenye nnachokisema umehoji kichwani nimeweka nini nakujibu kichwani nna mawazo ya mtu! swali linalofata ni huyo mtu ni nani! na mawazo gani juu ya huyo mtu!


ukishindwa kunielewa hapa hutakuja kunielewa tena!
 

haya kuna hii hapa kati ya dunia na mbingu kipi kilianza!?

hapa anasema

29. Yeye ndiye aliye kuumbieni vyote vilivyomo katika ardhi. Tena akazielekea mbingu, na akazifanya mbingu saba. Naye ndiye Mjuzi wa kila kitu. (2:29)

yaan kua alianza na ardhi kisha akazigeukia mbingu ndo akaziumba( kifupi imeanza ardhi ikafata mbingu)


halafu huku tena anasema

Are you the harder to create, or is the heaven that He built?
He raised the height thereof and ordered it;
and He has made dark the night thereof, and He brought forth the morn thereof.
And after that, He spread out the earth. -- Sura 79:27-30


hapa ameanzia mbingu halafu akamalizia ardhi!

vipi hiyo sio contradiction!? au tuendelee na zingine!?
 

54. Hakika Mola Mlezi wenu ni Mwenyezi Mungu aliye ziumba mbingu na ardhi katika siku sita. Kisha akatawala juu ya Kiti cha Enzi. Huufunika usiku kwa mchana, ufuatao upesi upesi. Na jua, na mwezi, na nyota zinazo tumika kwa amri yake. Fahamuni! Kuumba na amri ni zake. Ametukuka kabisa Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa viumbe vyote.
(7:54)

hyo inasema kua dunia imetengenezwa kwa siku 6.

halafu huku anasema hivi pia!


9. Sema: Hivyo nyinyi mnamkataa aliye umba ardhi katika siku mbili, na mnamfanyia washirika? Huyu ndiye Mola Mlezi wa walimwengu wote. 9


10. Na akaweka humo milima juu yake, na akabarikia humo na akakadiria humo chakula chake katika siku nne. Haya ni sawa kabisa kwa wanao uliza. 10


11. Kisha akazielekea mbingu, na zilikuwa moshi, akaziambia hizo na ardhi: Njooni, kwa khiari au kwa nguvu! Vyote viwili vikasema: Tumekuja nasi ni wat'iifu. 11


12. Basi akazifanya mbingu saba kwa siku mbili, na akazipangia kila mbingu mambo yake. Na tukaipamba mbingu ya chini kwa mataa na kwa ulinzi. Hichi ndicho kipimo cha Mwenyezi Mungu Mwenye Kujua. (41:9-12)

tukizichambua hizi aya ukijumlisha siku 2 za kuumba ardhi, halafu 4 za kuumba milima na kuweka chakula, halafu 2 zingine za kutengeneza mbingu, yaani 2+4+2=8 sasa hapa hyo quran huoni inajipinga!? yaan inasema mungu kaumba katika siku 6 ila katika kuelezea process zimekuja siku 8[emoji16][emoji16][emoji16] bado mnataka kuniambia kitabu kama hiki kimekamilika!?
 
Sasa huko dunia ya ngapi sijui si ndo wanatengeneza movies kama Game of Thrones?!? Unadhani mawazo yale wanatoa wapi kama hawaujui uchawi?!! Wazungu hao mnaowasifia nao wanga tu!!
 
Upo mjini unasema hakuna uchawi. Nenda usukumani huko shinyanga. Ukishafika kijijini sema hakuna uchawi na hakuna mtu wa kunifanyia kitu. Utakalopata uje utuhadithie hapa
Nimeshafika mpaka Gamboshi!

Na Usukumani nimeshatembea sana tu.

Kote huko nilikopita nishawaambia hakuna uchawi: kama upo, na waniroge ili kunitolea mfano.

Lakini huyu hapa bado nipo nikisema hakuna uchawi.

Na mimi si Msukuma robo, nusu, wala shombe.

Mimi ni Msukuma kwelikweli. Kwenye pande zote mbili za ukoo ni Wasukuma kurudi nyuma vizazi na vizazi.

Narudia tena. Uchawi haupo. Kama upo, yeyote yule aliye mchawi aniroge.
 
una uthibitisho gan Quran siijui!? au kila mtu anaekwambia Quran si sahihi ni Quran haijui!? hii inathibitisha ni namna gani umekariri! umekaririshwa kila mkosoaji ni haijui Quran!

pole sana
Kusema Qur'aan inajipinga yenyewe ni uthibitisho wa kuwa Qur'aan huijui. Qur'aan haijipingi.

Nimekupa kazi kijana,onyesha kujipinga kwa Qur'aan kisha nikuulize maswali,ukijibu hayo maswali,mimi naifuta hii ID,na wewe utakuwa shahidi.

Qur'aan huijui,sasa thibitisha kama Qur'aan unaijua.
 
Hali ina tabia moja ya ajabu saba,huwa ina mili popote.

Wewe onyesha hilo kama uone nitakataa haki au kinyume chake.

Nasubiri uonyeshe.
Sasa hapo umekubali au umekataa?

Unakubali kutumia kipimo cha mantiki katika kuamua ukweli na uongo?
 
Sasa hapo umekubali au umekataa?

Unakubali kutumia kipimo cha mantiki katika kuamua ukweli na uongo?
Mantiki uwezo huo haina,nilisha kuonyesha hilo zaidi ya mara moja.

Weka uhalisia,ndiyo humaliza kila kitu.
 
Bora na wewr umeona hili.

Nimemueleza mara kadhaa, analeta ubishi tu.

Ni kama vile anaanza na jibu lake, halafu anauliza swali linalolenga hilo jibu.
 
Mantiki uwezo huo haina,nilisha kuonyesha hilo zaidi ya mara moja.

Weka uhalisia,ndiyo humaliza kila kitu.
Unaelewa kwamba hata haya maandishi uliyotumia kuandika "mantiki uwezo huo haina" yametumia mantiki?

Yani, huwezi kuikwepa mantiki, mpaka unapotaka kuiponda mantiki, inakubidi utumie mantiki.

Unaelewa kwamba bila mantiki hoja zako za kusema Mungu yupo zinavunjika?

Unaelewa kwamba ukiiponda mantiki unafungua mlango wa kuleta fake news yoyote ile hapa?
 
tumia akili yako vizuri hyo mifano haiendani na nini na nani!

mfano wa kwanza umehoji uwepo wa nabi kwenye nini pasi na kujua uwepo wa kitu husika ila umekipa nafsi moja kwa moja! je kama humo ndani kuna kitabu!?
Onyesha utofauti wa nilicho kionyesha mimi na ulichokifanya wewe katika mfano wako,zaidi ya kuweka uhusiano wa nini na nani tu.

Kama nimekipa nafsi,niambie ni nafsi ya ngapi hiyo ? Unawaza na kufikiri kwa kutumia nini ?
mfano wako wa pili unauliza kichwani mwako umeweka nini hili ni swali ambalo linakuleta kwenye nnachokisema umehoji kichwani nimeweka nini nakujibu kichwani nna mawazo ya mtu! swali linalofata ni huyo mtu ni nani! na mawazo gani juu ya huyo mtu!
Sasa kama unakubali hili,katika mfano huu wa pili unakataa lile la mfano wa kwanza,kwa kigezo cha nafsi hapa kuna tofauti gani ?
ukishindwa kunielewa hapa hutakuja kunielewa tena!
Bado hujaonyesha tofauti ya ulicho kiandika wewe na mfano nilio utoa,na bado hujajibu swali langu la kuonyesha uwezo wa "nini ?" kuratibu mambo na kusanifu na kuwa na malengo. Hili swali mnalikimbia nyote. Sababu hatulei ujinga,hili swali mpaka mlijibu.
 
Bora na wewr umeona hili.

Nimemueleza mara kadhaa, analeta ubishi tu.

Ni kama vile anaanza na jibu lake, halafu anauliza swali linalolenga hilo jibu.
Tatizo hamjibu swali langu,la kuonyesha uwezo wa "nini ?" kuratibu na kusanifu mambo,mnakimbia hili swali.

Mfano wake wa nini kuzaa nani ni utungaji wa sentensi tu kama ilivyo kumuweka nini ndani ya nani. Hili rahisi sana.

Hoja yangu,ni kwanini na kwa vipi nini iweze kutenda jambo na kusanifu mambo ? Onyesheni uwezekano wa hilo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…