Uchawi au Majini hayapo! Nani ameshawahi kukutana na jini

Uchawi au Majini hayapo! Nani ameshawahi kukutana na jini

Research zipo za aina nyingi.
Hata mambo ya kiroho yana research zake.Ni mpaka uwe na elimu hio.
Upo sahihi but research ya haya hapa,ni tuna transform into modern with accurate achievement /targets.
Ndio maana wataalamu wengi wapo based na SYMPATHIC MAGES./involuntarily sympathetic order s.
 
nlichojifunza kutoka kwako ni kua uko tayari kukana kwa kila kitu! mpaka hapa umeshakosa sifa za kujibizana na mimi! kazi ya kua unacheza mdundo wa singeli kwa ku dab! nmekuachia wewe mwenyewe!

aya zinajieleza vizuri tu ila unakuja na maelezo yako ya namna ya kuielewa wakati hizo aya ziko clear zinasema nini!
Sasa kosoa nilichokiandika kwa hoja acha kulalama,aya imetumia tamko ka wakati ulio pita kwa ardhi kisha kwa ujinga wako una dai Mbingu ndiyo imeanza.

Sasa nakuuliza swali rahisi sana kwa kipi au lipi limekufanya useme mbingu ndiyo zimeanza wakati Allah ameonyesha wazi hapo.

Imaamu Shawkaniy alisema ukiona Qur'aan unahisi inajipinga kwanza ituhumi akili yako na elimu yako kuwa ndogo juu ya hilo.

Nambie wewe sasa tamko "ame...." ni la wakati uliopo au ujao ?

Kisha rejea Tafsiri za Qur'aan ukasome.
 
54. Hakika Mola Mlezi wenu ni Mwenyezi Mungu aliye ziumba mbingu na ardhi katika siku sita. Kisha akatawala juu ya Kiti cha Enzi. Huufunika usiku kwa mchana, ufuatao upesi upesi. Na jua, na mwezi, na nyota zinazo tumika kwa amri yake. Fahamuni! Kuumba na amri ni zake. Ametukuka kabisa Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa viumbe vyote.
(7:54)

hyo inasema kua dunia imetengenezwa kwa siku 6.

halafu huku anasema hivi pia!


9. Sema: Hivyo nyinyi mnamkataa aliye umba ardhi katika siku mbili, na mnamfanyia washirika? Huyu ndiye Mola Mlezi wa walimwengu wote. 9


10. Na akaweka humo milima juu yake, na akabarikia humo na akakadiria humo chakula chake katika siku nne. Haya ni sawa kabisa kwa wanao uliza. 10


11. Kisha akazielekea mbingu, na zilikuwa moshi, akaziambia hizo na ardhi: Njooni, kwa khiari au kwa nguvu! Vyote viwili vikasema: Tumekuja nasi ni wat'iifu. 11


12. Basi akazifanya mbingu saba kwa siku mbili, na akazipangia kila mbingu mambo yake. Na tukaipamba mbingu ya chini kwa mataa na kwa ulinzi. Hichi ndicho kipimo cha Mwenyezi Mungu Mwenye Kujua. (41:9-12)

tukizichambua hizi aya ukijumlisha siku 2 za kuumba ardhi, halafu 4 za kuumba milima na kuweka chakula, halafu 2 zingine za kutengeneza mbingu, yaani 2+4+2=8 sasa hapa hyo quran huoni inajipinga!? yaan inasema mungu kaumba katika siku 6 ila katika kuelezea process zimekuja siku 8[emoji16][emoji16][emoji16] bado mnataka kuniambia kitabu kama hiki kimekamilika!?
Hili nalo ni dogo sana. Hapo umeshondwa wewe kuelewa,katika sura ya 41, Allah ametumia tamko "katika" siku nne,kwa maana mbili za mwanzo na mbili za upambaji jumla ni nne na zile mbili jumla sita. Hajasema "kwa siku nne" bali "katika siku nne".

Lakini hili lina mifano mingi sana katika lugha,ndiyo maana hakuna kitabu sahihi wala fasaha zaidi kushinda Qur'aan. Nikisema "Nimetoka dar kwenda Moro ndani ya siku kumi na mpaka Arusha ndani ya siku kumi na tano". Hapo jumla zinakuwa siku 25 au 15 ?
 
We jamaa Mzushi tu

mchawi gani unatumia hadi whatsapp, profile picha umemuweka morison mzee wa kukera akiwa amepiga uzi mpya??

Nakupa task tumia uchawi wako fanya uweze kuipata namba yangu ya whatsapp niliyotumia kuangalia profile yako, ukiweza hilo tunafunga huu uzi na rasmi naanza kuamini uchawi
Sidhani kama hauamini uchawi kwa sababu hujawahi kuona matukio au mambo yenye kuhusishwa na uchawi kama ambavyo unataka huyo jamaa aitambue namba yako. Wewe hauamini uchawi kwa sababu una msimamo wa kupinga uwepo wa uchawi na ndio maana mambo yote yenye kuhusishwa na uchawi unapinga kwa sababu msimamo wako ni kwamba uchawi hakuna.
 
Kama hujui chochote kuhusu ulimwengu wa roho unapoteza mda wako bure kuwaza juu ya hayo mambo.

Nakushauri endelea na maisha ya kawaida kwenye ulimwengu huu wa damu na nyama.
 
Upo sahihi but research ya haya hapa,ni tuna transform into modern with accurate achievement /targets.
Ndio maana wataalamu wengi wapo based na SYMPATHIC MAGES./involuntarily sympathetic order s.
Huwezi base kwenye instrument moja kupimia object zingine.
Kipimo cha uchawi kinaitwa ICDs indicator,hii ni kwa waliosomea uchawi vyuoni
 
Umeandika kama umekatwa kichwa.

Wachawi wapo, nimeshawaona kwa macho wakiwa wanawanga usiku.

Majini yapo pia, ni viumbe wasioonekana kwa macho ya kawaida.

Ukiona haujakutana na mambo ya giza basi ujue wewe hauna tija wala umuhimu.

Wachawi na mashetani huwa wanashughulika na watu wenye vipawa na nyota zinazowaka.

Mungu akikujalia vipawa lazima nguvu za giza zikuandame kwa kasi ya ajabu.

Na Mungu anaruhusu hayo ili ujitambue kiroho. Ukishajitambua, vita inakuwa nyepesi.
Mkuu hayo majini wewe ushawahi kuyaona?
 
Haya jibu nini/kipi/nani aliecode/kilichocode DNA zetu?
Naomba ufuatilie jibu langu kimantiki na kuondoa ushabiki wa kidini.

Sijajua jibu la nini kime cide DNA, lakini jibu lake si Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote.

Katika kutafuta jibu, kuna njia nyingi. Njia moja inaitwa "elimination method".

Ukiambiwa, mji mkuu wa Chad, Central Africa ni Washington DC iliyopo Marekani, ukijua kwamba mji mkuu wa nchi ni lazima uwe ndani ya nchi hiyo, na Washington DC ipo Marekani, si Chad, utajua kwamba, Washington DC si mji mkuu wa Chad, hata kabla hujajua mji mkuu wa Chad ni mji gani. Hapi unaweza ku eliminate Washington DC kama mji mkuu wa Chad. Unaondoa jibubla Washington DC, unatafuta jibu la kweli.

Sasa, hata kabla ya kujua jibu la mji mkuu wa Chad ni mji gani, unakuwa ushajua jibu sahihi si Washington DC.

Ukiambiwa kwamba, binti ambaye leo ana miaka mitano, ni mama mzazi wa mwanamme mwenye miaka 60 leo, na wewe unajua mama mzazi ni kazima awe mkubwa kuliko mtoto wake, unaweza kujua kwamba, huyu binti wa miaka mitano hawezi kuwa mama mzazi wa huyu mwanamme mwenye miaka 60. K3a sababu mama yake mzazi huyu mwanamme mwenye miaka 60 hawezi kuwa na miaka michache kuliko hiyo sitini.

Hizi habari mbili za mji mkuu wa Chad kuwa Washington DC, na mama wa mwanamme mwenye miaka 60 kuwa binti wa miaka 5 zina contradiction.

Washington DC kuwa Marekani haiwezi kuwa mji mkuu wa Chad, kwa sababu ina contradict kanuni kwamba mji mkuu wa nchi ni lazima uwe ndani ya nchi hiyo.

Kwa hiyo nikikua Washington DC haupo Chad tu, najua hauwezi kuwa mji mkuu wa Chad, hata kabla sijajua mji mkuu wa Chad ni mji gani.

Vivyo hivyo, nikishajua tu kwamba binti wa miaka 5 ni mdogo kuliko mwanamme wa miaka 60, nitajua kwamba huyu binti hawezi kuwa mama mzazi wa mwanamme mwenye miaka 60. Kwa sababu huyu binti wa miaka 5 kuwa mama mzazi wa mwanamme mwenye miaka 60 kuna contradict kanuni kwamba, mama mzazi wa mtu anatakiwa kuwa mkubwa kuliko huyo mtoto, mama anatakiwa kuwa kazaliwa kabla ya mtoto.

Hapo tunaona kwamba, mtu hahitaji kujua jibu sahihi ili kujua kwamba jibu fulani si sahihi. Na kwamba, katika kutafuta jibu sahihi, tunaweza kuondoa majibubfulani kwamba si ya sahihi.

Kuhusu suala la DNA, bado watu wanatafuta jibu sahihi.

Lakini, kama tunavyoweza kusema Washington DC si mji mkuu wa Chad, au binti wa miaka 5 hawezi kuwa mama mzazi wa mwanamme mwenye miaka 60, tunaweza pia kusema Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hawezi kuwa designer wa DNA.

Kwa sababu.

DNA ina mapungufu. Ikipigwa na radiatio ninafanya mutations zinazosababisha magonjwa. Mungu mwenye uwezo wote ujuzi wote na upendo wote surely angekuwa designer wa DNA angefanya DNA ya viumbe wake anaowapenda iwe much better than this.

The other objectionnis a general versionnof this argument.

1. Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayuko compatible na ulimwengu unaoruhusu mabaya. Yuko mutually exclusive na ulimwengu unaoruhusu mabaya.

2. Maana yake, huwezi kuwa na ulimwengu unaoruhusu mabaya kutokea, halafu hapo hapo Mungu huyu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote akawepo. Maana yake, Mungu huyo akiwepo, ulimwengu unaoruhusu mabaya hauwezi kuwepo, na ulimwengu unaoruhusu mabaya ukiwepo, Mungubhuyo hayupo.

3. Ulimwengu unaoruhusu mabaya upo. Ndiyo huu tunaoishi ndani yake. Una magonjwa, majanga ya kiasili, matetemekonya ardhi, mafuriko, vita, ujambazi, etc.

4. Hivyo, Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na uoendo wote hayupo.
 
Kuna kipindi shuleni walikua wanakuja wanamazingaumbwe tunatoa ela wanafanya show ...ebu niambie kile kiini macho kinachotufanya tuone yale mauza uza ni nini.alafu unasema ety uchawi ni africa tuh ebu google uone huyo mtu anayesemekana ni mchawi kuliko wote kuwai kuishi ni mzungu au muafrica
Mkuu,

Nikuulize swali.

Karata tatu ni uchawi?
 
Hii si kweli sababu tamko "nani ?" ni kiulizi kwa kile chenye ufahamu na nini ni kinyume chake (au tunasema kwa Hayawani).

Sasa jifunze kutumia maneno vizuri.
Nikiuliza nini kimefanyabuwepo hapa duniani, kama jibu ni wazazi wako kukuzaa, jibu la kilichosababisha kuwepo kwako duniani ninwazazi wako kukuzaa lipo ndani ya swali la nini.

Ukiuliza "nani kaweka jani la muembe mlangoni mwangu", kamanjani limewekwa na upepo, swali lako la nani linakuwa ni swali potofu.

Ukiuliza "nini kimeweka jani la muembe mlangoni mwangu" swali liki more inclusive. Kama jani limewekwa na mtu jibu la mtu lipo ndani ya swali la nini.

Kama jani limewekwa na upepo, swali la nini liko inclusive. Utaambiwa jani limewekwa na uoepo.

Sasa wewe umekuta jani liko mlangoni mwako, badala ya kuulika nini kimeweka jani hapo, jani limefikaje ( kwa sababu swali la nani liko specific kwa mtu/ chenye nafsi, upepi hauna nafsi na swali hilo halitakuwa inclusive). Badalanya kuuliza nini k8meleta jani mlangoninkwako, unaukiza nani kaleta jani.

Huoni kama jani limeletwa na upepo swali la nani ni swali la makosa?
 
Ngoja nikusaidie jambo moja. Nilicho kiona kwako ni kuwa, huujui Uchawi ni nini lakini ajabu unaupinga. Hapa ndipo huwa nawaona akili zenu hazifanyi kazi.

Nanukuu :

Katika kamusi maarufu ya Kiarabu iitwayo "Lisanul Arab", muandishi anafasiri tamko "Uchawi" kama ifuatavyo "Neno Uchawi kwa kiarabu "As-Sihr", maana yake ni kitendo cha kujikurubisha kwa Shetani (wa kijini) na kwa msaada wake. Akasema tena "Uchawi ni kulibadilisha jambo mbali na uhakika wake,nalo ni kuwadhihirishia watu jambo lisilo la kweli wakaliona kuwa ni la kweli"

Ama Swahaba mtukufu Ibn Abbas (Allah amridhi),anasema " Ni kuidhihirisha batili katika sura ya haki"

Ama katika Kamusi ya dini,Uchawi kama alivyo fasiri Mwanachuoni mkubwa Fakhrudinn ar-Razi anasema "Ni kila jambo lililo fichika sababu zake,linalo tokeza kwa sababu zisizo za kawaida na ndani yake kuna hadaa (udanganyifu)"

Uchawi unajulikana kwa sababu nyingi sana,hasa kwa masharti ambayo ukiyapima huoni uhusiano wa moja kwa moja na huwa ni magumu. Mathalani ukiambiwa uende njia panda upasue nazi kisha usigeuke nyuma na mfano wa hayo.

Huyu muongo na alikuwa hajui nini UCHAWI.

Uchawi unajulikana na unatofautishwa kabisa bila shida yoyote.

Wazee wetu mambo mengi sana walikuwa wanayafanya pasi na elimu ya hakika kabisa,sababu laiti kama wangejua historia ya Uchawi basi hayo ya Wazungu wasingeona uchawi. Uchawi umegawanyika sehemu mbili,na wa mwanzo kuwa na elimu ya Uchawi ni majini,na majini walikuwa wanawafundisha watu,rejea habari za Mfalme Suleyman,aina ya pili ya uchawi ni ule uchawi ambao walikuja nao Malaika wawili wakashuka nao kule Baabil (Babeli),wanazuoni wanasema Uchawi huu ni ule wa kuwafarakanisha wapenda nao yaani mke na mume,na ule wanao fundisha Mashetani ndiyo unao husu mambo mengine kama vile mauaji na mfano wake.

Kwa anaye jua Sayansi na misingi yake hawezi kudai Uchawi ni Sayansi au kulinganisha viwili hivi.

Suala jua kupatwa au mwezi kupatwa,sisi wengine tunajua pasi na kutegemea tabiri za Kisayansi,ambazo zimemili katika ubahatishaji,mimi najua kabisa ya kupatwa kwa jua hakutoi nje ya tarehe fulani miaka yote kadhalika kupatwa kwa mwezi.

Kwahiyo hizi elimu zilikuwepo tangu na tangu na Mtume wetu aliwafundisha maswahaba na nini cha kufanya pindi jua linapo patwa au mwezi na nini maana ya viwili hivyo.
Wewe una define uongo mmoja kwa kutumia uongo mwingine.

Unaweza kuthibitisha shetani yupo?
 
Wanaweza wakaja na kisingizio kwamba jini halipigiki picha!

Waumini wa uchawi wana visingizio vingi!
Picha wakiweka utajuaje hii ni ya jinibm kweli na hawajaokota tu kwenye some obscure Turkish horror TV series?
 
Nakumbuka tukiwa shule kuna vile viemolo sijui vimbilikimo,,,vilikuwa vinaonekana alfajiri.Nilikuwaga najua ndiyo majini/wachawi wenyewe.Kipo kisa kimoja tuu ambacho jirani yetu kijijini mchawi alishindwa kutoka tukamkuta yupo kibambazani yupo uchi wa mnyama aisee,,,,daah! Japo alikuwa mashallah vijana walimtandika bakora hatari.Mimi alinivutia umbo lake,,,yaani pissi kali alafu mweusi.....
 
Wewe mtoa mada unataka "proof" kwamba majini yapo? Je, wewe unaweza kutupa ushahidi kwamba unayo akili? Hiyo akili yako iko wapi? Je, ya kwako (kama unayo) ni timamu?

Sio kila kitu kisichoonekana hakipo.
 
Picha wakiweka utajuaje hii ni ya jinibm kweli na hawajaokota tu kwenye some obscure Turkish horror TV series?
Ndo hapo sasa!

Wanaweza kweli kuweka picha yoyote tu ile na kudai ni picha ya jini.
 
Nikiuliza nini kimefanyabuwepo hapa duniani, kama jibu ni wazazi wako kukuzaa, jibu la kilichosababisha kuwepo kwako duniani ninwazazi wako kukuzaa lipo ndani ya swali la nini.
Swali hili si sahihi bali ni swali la uongo. Nini haingii kwa nani,ndiyo maana ukijibu ni wazazi,tutatuuliza wazazi ni nini au wazazi ni kina nani ?

Swali sahihi ni nani amefanya wewe ukawepo hapa duniani ?

Nini hakina uwezo wa kuratibu mambo wala kuumba.
Ukiuliza "nani kaweka jani la muembe mlangoni mwangu", kamanjani limewekwa na upepo, swali lako la nani linakuwa ni swali potofu.
Swali langu linakuwa sahihi sababu,nani inaingia kwenye upepo na upepo ni katika kiumbe kinacho amrishwa na kutii na Allah mtukufu.

Allah anasema kuhusu Upepo :

22. Na tunazipeleka pepo za kupandishia, na tunateremsha kutoka mbinguni maji, kisha tukakunywesheni maji hayo. Wala si nyinyi mnayo yaweka.(al-Hijri :22)

Akasema tena


57. Na Yeye ndiye anaye peleka pepo (za kuvuma) kuwa ni bishara kabla ya kufika rehema yake. Hata hizo pepo zinapo beba mawingu mazito tunayachunga mpaka kwenye nchi iliyo kufa. Kisha tunateremsha kwayo maji, ndio kama hivyo tukatolesha kila aina ya matunda. Basi hali kadhaalika tunavyo wafufua wafu, ili mpate kukumbuka. (al-'Araf : 57)

Akasena tena Allah mtukufu :

12. Na Suleiman tuliufanya upepo umtumikie. Safari yake ya asubuhi ni mwendo wa mwezi mmoja, na safari yake ya jioni ni mwendo wa mwezi mmoja. Na tukamyayushia chemchem ya shaba. Na katika majini walikuwako walio kuwa wakifanya kazi mbele yake kwa idhini ya Mola wake Mlezi. Na kila anaye jitenga na amri yetu katika wao, tunamwonjesha adhabu ya Moto unao waka. (sabaa : 12)

Ndiyo maana kwenye upepo nani anakaa.
Kama jani limewekwa na upepo, swali la nini liko inclusive. Utaambiwa jani limewekwa na uoepo.
Kwenye Upepo anaingia nani. Nikisema nani ameweka jani,nikajibu Upepo jibu hili ni sahihi na swali kadhalika sahihi.

Ila ukauliza nini kimeweka hapa hilo jani ? Swali hili la uongo sababu hakuna nini chenye uwezo wa kuweka kitu mahala fulani.
Sasa wewe umekuta jani liko mlangoni mwako, badala ya kuulika nini kimeweka jani hapo, jani limefikaje ( kwa sababu swali la nani liko specific kwa mtu/ chenye nafsi, upepi hauna nafsi na swali hilo halitakuwa inclusive). Badalanya kuuliza nini k8meleta jani mlangoninkwako, unaukiza nani kaleta jani.
Swali sahihi ni nani ?!
Huoni kama jani limeletwa na upepo swali la nani ni swali la makosa?
Upepo ni kiumbe mzee,kama nilivyo kuonyesha huko juu.
 
Wewe una define uongo mmoja kwa kutumia uongo mwingine.

Unaweza kuthibitisha shetani yupo?
Kwanza onyesha huo uongo wa kwanza na uongo wa pili.

Naweza kuthibitisha ya kuwa Shetani yupo.

Unaweza kuthibitisha ya kuwa Shetani hayupo na umejuaje ?
 
Back
Top Bottom