Uchawi gani umetumika kuiba hela zangu kwenye kibubu?

Duu! Pole sana ndugu. Wakati mwingine kabla ya kuanza kutumia hicho kibubu kifanyie maombi au kipeleke kwa mchungaji akakiombee. Toa na sadaka kabisa kwa ajili ya ulinzi wa vitakavyokuwa vinawekwa humo. Usihahau kutoa zaka/fungu lankumi kwa kila shilingi unayopata.
 
Kaka itabidi unipe mbinu niishinde michepuko maana kama ni hivyo umefanikiwa kumuabisha shetani...mi ananiabisha kupitia michepuko
 
Kaka itabidi unipe mbinu niishinde michepuko maana kama ni hivyo umefanikiwa kumuabisha shetani...mi ananiabisha kupitia michepuko

Utafanikiwa iwapo tu utaacha kuusikiliza mwili wako. Unyime kila unachokitamani.​

Gal 5:16-26 SUV​

Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili. Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka. Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria. Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu. Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria. Na hao walio wa Kristo Yesu wameusulibisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake. Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho. Tusijisifu bure, tukichokozana na kuhusudiana.
 
Amen mtumishi.....ngoja nianze mapambano
 
Somo la kuacha kuusikiliza mwili ndo limenishindaa apa naitaj muongozooo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ