Napendekeza tufanye mazungumzo na wewe nikuhoji kuhusu ulichoandika tuone utavumilia kwa muda gani kutetea hoja zako. Sidhani kama umeshakutana na maswali ninayouliza mimi.
Mzee Mwanakijiji,
Unamuuliza Mohamed Said atavumilia muda gani kutetea hoja zake.
Mohamed Said anakula na kulala JF bado masiku machache afikishe mwezi humu hakuna yeyote humu pamoja na wewe ambaye anaweza kukaa mwezi kwenye uzi kutetea hoja zake.
Mohamed Said anafundisha ndiyo tofauti yake na nyie.
Ritz,
Huyu Mwanakijiji nimemwekea mambo yalotokea baina yangu
na CCM Dodoma kuhusu Abdulwahid Sykes, Waislam na historia
ya uhuru.
Nimemwekea na rejea.
Badala ya kuchukulia kutoka pale tukanogesha chembelecho Zomba
anakuja na viroja.
Kama hajiwezi si aungane na wenzake wanishambulie?
Angalau labda...
sawa; kwenye ukurasa wa ngapi wa kitabu cha kivukoni panaposema nyerere alisema amepigania uhuru peke yake; na ni ukurasa gani unasema nyerere alisema aandikwe yeye peke yake tu na si wengine. Unaweza ukaweka na nukuu yake.
Hapa tuingie kwenye Filosofia kidogo. Wote hao uliwataja walipaswa kumjua? Maana unavyozungumza ni kana kwamba wao walipaswa kumjua. Lakini kwanini walitakiwa kumjua? Je hawa wote walimjua kila mtu mashuhuri jijini Dar? Lakini jambo jingine ambalo binafsi silioni kwanini umelifanya kuwa la muhimu sana; kama Nyerere alikuwa hajulikani mahali ambapo hakuzaliwa au kuishi ujana ulitarajia ajulikane vipi?
Maana wote hao uliowataja unafikiri walikuwa wanajulikana sehemu nyingine za Tanzania? Ukienda Tanga tu hapo utakuta kuwa baadhi ya hao uliowataja hawajulikani kabisa wakati huo au hata ukienda Songea, au Morogoro. Sasa kutokujulikana kwao ni kosa lao, ni jambo baya, au ni kukosa umashuhuri?
Unavyoandika unaashiria (imply) kuwa Nyerere kutojulikana kwa hawa basi hakuwa mashuhuri; swali liinaweza kuulizwa kinyume chake je wao walikuwa wanajulikana kwa Nyerere kabla hajaja Dar-es-Salaam? Jibu ni kuwa la hasha! Vinginevyo akiwa Makerere angeshawajua na badala yake alikuja kuwasikia tu kutoka kwa watu wengine. Je kwa vile Nyerere alikuwa hawajui ina maana hawakuwa maarufu Dar?
Hoja hii ya Nyerere kutokujulikana kwa baadhi ya wazee - maana ushahidi upo kuwa baadhi yao tayari walimjua kabla ya 1953 haina nguvu na kwa kweli ni mojawapo ya hoja dhaifu. Kutokumjua mtu kabla hujakutana naye si jambo la kujisifia na kujulikana siyo sifa kwani katika maisha watu wanajua na wengine hawajulikani. Kwa mfano, unafikiri wote wote Tanzania wanakujua wewe? Na unaweza ukaamini wewe ni maarufu kweli kumbe wanaokujua ni wale tu WALIOPASWA kukujua. Na hilo ni kweli kwa kila mtu.
Nyerere kutokujulikana Dar - kama unavyodai - siyo jambo la fedheha wala la kuonesha kuwa hakuwa maarufu. Inaonesha tu kuwa hawakuwa na nanafasi ya kukuutanishwa na kuthibitisha kuwa Nyerere alikuwa ni maarufu kweli ndio maana Sykes na Kasela Bantu wote walijitahidi kumtambulisha Nyerere kwa wazee hawa au - unaweza kuwaangalia kwa kona nyingine - ni wazee hawa waliotambulishwa kwa Nyerere kwani alikuwa hawajui japo waliamini wao ni maarufu zaidi. Na kuonesha nani alikuwa maarufu baina yao jibu ni jepesi.
Kwanini nasema Nyerere alikuwa maarufu zaidi kuliko wazee wa Dar ni kwa sababu moja - alikuwa ni maarufu zaidi kwa Tanganyika kuliko wazee wa Dar. Wao walikuwa maarufu mjini kwao Nyerere umaarufu wake ulivuka mipaka ya mji. Na historia imeshuhudia hivyo na ndio maana hata leo ukienda kuwauliza wazee wengine nje ya Dar hakuna anayemkumbuka Mshume, Sheikh Ameir na hata kina Sykes!
lakini waulize kama wanamkumbuka Nyerere....
Napendekeza tufanye mazungumzo na wewe nikuhoji kuhusu ulichoandika tuone utavumilia kwa muda gani kutetea hoja zako. Sidhani kama umeshakutana na maswali ninayouliza mimi.
Si kweli, wewe unachotaka ni kusema tu hutaki kutetea hoja zako, hutaki kujibu unachoulizwa. Hata hivyo ninaelewa sababu nini.Sijibu kwa kuwa maswali yenu mengine yanachusha hayamtii mtu hamu ya kuandika.
Ritz,
WildCard,
Hii hapa picha nimekuleta kulia kwa Nyerere ndiyo mweka hazina wa TANU Idd Faiz.
Hapo wanamuaga Nyerere kwenda UNO.
Huyo mwanamke peke yake ni Bibi Titi Mohamed, cha kuchekesha hao wote hawamo katika waasisi wa TANU.
Kusoma hujui hata picha huoni.
[/B]Inaonekana akili yako imekataa kabisa kukubali ukweli wa kihistoria. Nyerere hakushirikishwa na wazee wa Dar katika mapambano; alishaanza yeye mwenyewe nje ya Dar. Wazee wa Dar-es-Salaam walimhitaji Nyerere zaidi kuliko yeye alivyowahitaji wao. Hakuna kati ya wazee wote wa Dar aliyekuwa maarufu Tanganyika kuliko Nyerere. None. Siyo John Rupia, siyo Dr. Kyaruzi wala Sykes. Nyerere alikuwa maarufu zaidi na siyo maarufu tu alikuwa ameonesha uwezo zaidi wa kupambana na wakoloni kuliko wengine wote waliomtangulia.
Si kweli, wewe unachotaka ni kusema tu hutaki kutetea hoja zako, hutaki kujibu unachoulizwa. Hata hivyo ninaelewa sababu nini.
Umezoea kukalisha watu kitako na kuwasimulia huku wakisema tawire baba, wengine swadakta n.k.
Nikupe mfano mwingine wa maandiko yako maana mimi nimechoka kufikiri ninatumia kalamu yako mwenyewe kukufungua.
Mwanakijiji aliuliza swali kuwa je, wazulu walikuja Tanganyika wakiwa waislam? Jibu lako ni ndio.
Huo si ukweli! umepotosha.
Mzee Said, hapa hatupo kusikia unatumabia nini au unatutajia majina ya watu na picha zao. la hasha ustadhi! hapa ni hoja kwa hoja na wewe unajua hivyo lakini utakubali vipi mauzo ya kitabu toleo la 3 yadode?
Yaani utuambie kuwa Tanganyika imeundwa na Narung'ombe, Tandamti, mchikichini na kipata na makao makuu yake ni Gerezani nasi tuitikie tawire! real! Ibn Samtungo! Kwa jiografia hiyo kuna sababu za kulaumu NECTA kweli!
MM,
Kuna wakati historia hii ilikuwa haipo.
Sasa hali imebadilika sana.
Mshume Kiyate ni maarufu sana.
Uliza.
NAPENDA nieleze kisa hiki cha kusisimua cha marehemu Mshume Kiyate kama nilivyoelezwa na mzee wangu Ahmed Rashad Ali, kisa ambacho yeye alihadithiwa na Mwalimu Julius Nyerere kwa kinywa chake mwenyewe. Ahmed Rashad anasema siku aliyosikia kisa hiki yeye alikuwa pamoja na Dossa Aziz na Lucy Lameck.
Baada ya Mwalimu Nyerere kumaliza kutoa msimamo wake wakawa sasa wamekaa wanapiga gumzo huku wakinywa vinywaji na Mwalimu alikuwa mtu hodari sana wa kustawisha baraza. Waliokuwa karibu na Nyerere wanamjua kwa sifa hii.
Mwalimu Nyerere alianza kuhadithia kisa chake na Mshume Kiyate. Haifahamiki hasa ni lini Nyerere alijuana na Mzee Mshume lakini huenda ilikuwa hata kabla ya kuaisiswa kwa TANU siku zile za TAA Nyerere alipokuwa nakwenda ofisini kwa Abdulwahid Sykes pale Kariakoo sokoni ambako Abdulwahid alikuwa Market Master.
Nyerere alianza kukihadithia kisa chake na Mzee Mshume kwa kusema kuwa siku moja wakati wa kudai uhuru alikuwa anatoka nyumbani kwake Magomeni Majumba Sita kwa miguu kuelekea Kariakoo ili kupata mahitaji yake lakini katika safari hiyo mfukoni mwake alikuwa hana hata senti moja.
Akiwa njiani karibu na sehemu inayoitwa Mwembe Togwa (hapa kwa leo ni pale Fire makutano na Morogoro Road na Barabara ya Umoja wa Mataifa)Mwalimu alikutana na Mzee Mshume Kiyate.
Mwalimu Julius Nyerere akamfahamisha Mzee Mshume kuwa alikuwa anakwenda sokoni Kariakoo lakini hana fedha za kununulia mahitaji yake.
Mzee Mshume Kiyate aliingiza mkono katika koti lake akatoa shilingi mia mbili na kumpa Nyerere. Ukitaka kujua thamani ya fedha hiyo kwa wakati ule, naitoshe kujua kwamba ilimgharimu mtu shilingi mia tano tu kujenga nyumba ya vyumba sita katika eneo la Kariakoo.
Kutokana na hali hii Mzee Mshume aliona itakuwa ni kumtaabisha Nyerere bila sababu ikiwa atakuwa anashughulika na kuwatafutia wanawe chakula na wakati huohuo akiwa na jukumu la kufanya kazi za TANU.
Hapo ndipo Mzee Mshume alipojitolea kuihudumia nyumba ya Mwalimu Julius Nyerere. Kila asubuhi Landrover ya TANU inapiga breki Karikaoo sokoni pale na Mzee Mshume ananunua mahitaji yote ya siku anamkabidhi dreva wa TANU jina lake Said lakini watu wakampachika jina wakimwita TANU. Said TANU anachukua vitu vile anapeleka vile Magomeni Majumba Sita kwa Mama Maria.
Mzee Mshume alifanya hivyo hadi uhuru ulipopatikana
Baada ya uhuru Mwalimu Nyerere sasa akiwa Waziri Mkuu alimwomba Mzee Mshume aache kumnunulia chakula lakini Mze Mshume alikataa na badala yake akamtafadhalisha Mwalimu Nyerere aendelee kupokea chakula chake na kile ambacho kinatolewa na serikali kwake yeye, kama mkuu wa nchi alimuomba Mwalimu awakirimu wageni wake. Mwalimu Julius Nyerere alikiita kisa hiki ‘the TANU spirit' – yaani moyo wa TANU – akieleza mapenzi na moyo waliokuwanao wana TANU wakati ule wa kudai uhuru.
Kisa hiki kwa mara ya kwanza kabisa kilihadithiwa hadharani na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa wakati ule marehemu Ditopile Mzuzuri Mkiwaona kada wa Chama Cha Mapinduzi.
Ditopile alikieleza kisa hiki kama alivyokieleza Mwalimu Nyerere kwa Ahmed Rashad na Lucy Lameck kwa nia ya kuonyesha moyo wa TANU na mchango wa wazalendo katika kupigania uhuru wa Tanganyika. Kisa hiki kwa Dossa hakikuwa kipya. Dossa akimjua Nyerere nje ndani.
Kwa bahati mbaya waandishi wa magazeti wakapotosha kisa kizima. Badala ya kutoa umuhimu kwa moyo wa ukarimu wa Mzee Mshume na kumueleza kama mzalendo aliyejitolea katika kupigania uhuru, magazeti yakageuza maneno ya Ditopile kuwa masimango dhidi ya Mwalimu Nyerere. Kwa ajili hii nafasi ambayo ingeliweza kutumiwa ili kueleza umuhimu wa Mzee Mshume na historia ya TANU ikapotezwa.
Mzee Mshume kwa niaba ya wazee wa TANU alipanda jukwaani na kumvisha Nyerere kilemba kama ishara ya kumuunga mkono.
Hakuna picha aliyopiga Nyerere kati ya mwaka 1955 na 1961 ambayo Mzee Mshume asiweko ndani yake. Mzee Mshume alikuwa mstari wa mbele katika harakati za uhuru na kumuunga mkono Nyerere kwa kila jambo kwa hali mali.
Nimesoma Ilm ya mnakasha, hutoi silaha zote kwa wakati mmoja!!hapo kwenye red wagala ndio mnaponichosha
umesema sio kweli,haya lete ukweli wewe
nyinyi ndo wapotoshaji na waongo
Nimesoma Ilm ya mnakasha, hutoi silaha zote kwa wakati mmoja!!
Soma vizuri na kwa fikra pana nilivyoandika halafu jiulize kwa sentesi yangu fupi je, sikujua kuwa ninapaswa kusema nini!
Zamani sisi tukitega ndege kwa karai na punje mbili za mahindi, ndege akiingia unavuta kamba!
sikuhizi mnatumia ipod! ok
umesahau kumwambia hata matonya (R.I.P) alikuwa omba omba maarufu sana hapa tanzania pengine kuliko hata baadhi ya viongozi waliopata kushika nyadhifa mbalimbali za kitaifa..historia isiyokuwepo siyo historia
......................................................
Ndio maarufu lakini ni umaarufu wa nini? Mtu yeyote anaweza kuwa maarufu lakini ukijiuliza utaona kuwa ni maarufu kwa nani? Unadhani ukienda Mbeya hata mjini u kiuliza Mshume Kiyate watu wanamjua. Kama ni maarufu miiongoni mwa Waislamu (kitu ambacho naamini unamaamisha) utasema umefanikiwa sana? Lakini umeangalia ni umaarufu gani unasema alikuwa nao?
...........................
Mzee wetu kawapaka vibaya UDINI wazee wake hawa akidhani anammaliza na kulipiza kisasi kwa Mwalimu. Anawagawa pia Waislam kwa kuwaita wengine ni "WAISLAM wa BAKWATA" kwa kuwa walimuunga mkono Mwalimu katika utawala wake na kupambana wazi na UDINI wa watu kama Sheikh Amir.
Mzee wetu Mohamed hatabadilika kwa kuwa alikwisha yaandika haya. Muhimu ni kuwa naye karibu tu asiendelee kuwavuruga vijana wadogo wa Kiislam ambao wana muda mrefu wa kuishi kuliko yeye. Mtu msomi wa kiwango chake hawezi kufikiria watu kugawana vyeo na madaraka kwa uwiano wa DINI, kugawana fursa za ELIMU kwa kuzingatia DINI, historia ya NCHI iandikwe kwa kuzingatia DINI za wahusika. Hatutaishia hapo tu.
Tuendelee kuijenga TANZANIA hii hivi tulivyo. Muislam anamuoa Mkristo au kinyume chake; Tunachaguana kwenye UONGOZI wa NCHI kwa sifa binafsi ya mtu sio dini yake.
Ah! Ritz, hiyo post inajitosheleza. Isome tena. Yapo matatizo yanayochangiwa na UISLAM hasa upande wa ELIMU. Kwa kuna Muislam wa kiwango chenu cha elimu halioni hili huyo ni MDINI wa kutupwa. Ni mfiaDINI. Hatufai.Mbona ueleweki wewe kila siku unaandika humu JF tatizo la Waislam ni Uislam wenyewe saizi unamlalamikia Mohamed Said.
historia isiyokuwepo siyo historia
Ndio maarufu lakini ni umaarufu wa nini? Mtu yeyote anaweza kuwa maarufu lakini ukijiuliza utaona kuwa ni maarufu kwa nani? Unadhani ukienda Mbeya hata mjini u kiuliza Mshume Kiyate watu wanamjua. Kama ni maarufu miiongoni mwa Waislamu (kitu ambacho naamini unamaamisha) utasema umefanikiwa sana? Lakini umeangalia ni umaarufu gani unasema alikuwa nao?
Ngoja nitoe mfano kwenye maandishi yako mwenyewe. Unaanza simulizi lako kuhusu Mshume Kiyate kwa kusema hivi:
Sasa tufikirie kidogo: Huyu Nyerere mwenye chuki dhidi ya Waislamu na ambaye hakutaka wenzie walioshiri naye katika harakati za uhuru wajulikane anasimulia kisa hiki. Na anaye msimulia siyo Askofu wa Kikatoliki bali mmoja wa wazee wako - Ahmed Rashid Ali.
Unaendelea na kusema:
Haya ni maneno yako. Unachosema hapa ni kuwa hadi mwaka 1965 ambapo kisa hiki kinadaiwa kutokea Nyerere alikuwa na uhusiano mzuri tu na angalau mmoja wazee wako Ahmed Rashid Ali. Siyo uhusiano mzuri tu.. unasema walikuwa "wakinywa vinywaji" tena wapi.. nyumbai kwake. Dossa, mzee Rashid wako nyumbani kwa Mwalimu na kunywa naye chai; na hii ni mwaka 1965! Siyo maneno yangu haya ni ya kwako. Unaendelea tena:
Wanafunzi wako hapa kina Ritz nikiwauliza hapa mara moja Nyerere na Mshume Kiyate walifahamiana lini na wapi kwa haraka watasema "ofisini kwa Abdulwahid Sykes pale Kariakoo". Lakini ukweli ni kuwa hujui walifahamiana vipi na lini. Umeandika hisia zako kwa kusema "lakini huenda" ikawa mahali pale. Lakini hiyo ni hisia yako tu haina msingi wowote katika ukweli. Haya tuendelee
Unataka watu wenye akili timamu waamini kuwa Nyerere kaondoka nyumbani kwake kwenda Kariakoo kununua kitu sokoni bila kitu mfukoni. Siijui vizuri Dar-es-Salaam hasa eneo la "Majumba Sita" nitaulize nieleweshe tu uhusiano wake na ile "Majumba Sita" ya kule Kipawa. Hii Majumba Sita ya Magomeni ni ipi ili angalau niweze kufikiria umbali maana ile ya Kipawa ni mbali sana kuliko ya Magomeni. Sasa Nyerere anaondoka nyumbani kwake kwenda sokoni bila kitu mfukoni. Na haya ni maneno yake - uliyosimuliwa. Hadithi hadithi.. tuendelee
Tukubaliane na weewe tu kuwa kati ya watu wote katika siku hiyo isiyo na jina Nyerere anautana na Mshume Kiyate. Sawa nasibu inaweza kutokea haya tuendelee.
Na wapo watu wanaamini hili simulizi; Mshume katoa karibu nusu ya gharama ya kujenga nyumba kampa Nyerere kwenda sokoni! koh koho koh... utamu njoo...
Pamoja na utamu wote wa simulizi hili na kwa kweli linagusa moyo tatizo ni kuwa Mama Maria Nyerere yupo hai. Yeye peke yake anaweza kuelezea kwa kirefu hili na kukupa ushahidi zaidi wa msaada wa Mshume. Hujawahi kumtafuta, hujawahi kumuuliza na hata kutaka kujua kumbukumbu alizonazo kuhusiana na hali ngumu ya maisha. Tunatakiwa tukubali tu...
Nyerere alikuwa na chuki na Waislamu; hadi hapa inaonekana kuwa hadi kupata uhuru hawakuwa na tatizo lolote. Na kwa vile unasema Ahmed Rashad Ali alisimuliwa kisa hiki na Baba wa Taifa mwaka 1965 akipata "vinywaji" na kina Dossa ni wazi kuwa hadi mwaka 1965 bado kulikuwepo na Waislamu wengi tu - miongoni in mzee wako Ahmed Rashad... walikuwa na nafasi nzito tu serikalini. Kukumbusha tu umetuambia kuwa Bw. Ali alikuwa Katibu Mkuu Msaidizi Idara ya Habari!
Lakini unaendelea na kusema:
Sasa hapa unaingiza ile kanuni yako; unawanukuu wale marehemu ambao huwezi kuwahoji. Marehemu Ditopile alikipata wapi kisa hiki. Tukumbuke kuwa kulikuwa na watu watatu tu ambao walikuwa wanafahamu kisa hiki. Mzee wako Rashad, Dossa Aziz na Lucy Lameck. Hivyo, Ditopile atakuwa amesimuliwa. Na nani?
Lakini pia unasahau kitu kimoja muhimu kwenye communication jinsi habari inavyobadilishwa kwa kadiri kinavyopitishwa kwa watu. Lucy Lameck alikuwa ni mtu pekee wa kukuhakikishia kisa hiki ili ulinganishe na ulichosikia toka kwa mzee wako. Lakini kwa miaka yote uliyoandika kitabu chako hukujaribu kwenda kuuliza toka kwa Lucy Lameck yeye anakumbuka vipi kisa hiki. Hukufanya hivyo Bana Said... yawezekana kwa sababu alikuwa Mkristu? au kwa vile ni mwanamke ushahidi wake hauaminiki sana? Tuendelee...
Magazeti yalisema nini na ni magazeti gani? Historia inadai uyataje matoleo na kile walichokisema angalau tujue jinsi gani waligeuza hicho kisa.
Lakini katika kuonesha jinsi ambavyo unaandika bila kufikiria sana unachosema unadai hivi (na bahati mbaya kina Ritz wataamini maskini)
Sasa hili linadai ukweli. Kweli kuna watu wanakusoma hapa na wanaamini kuwa Nyerere hakupiga picha yoyote kati ya 1955 na 1961 ambapo mzee Mshume hakuwemo ndani? Picha hii ni ya Nyerere na Machifu na ilichukuliwa 1961...
sasa simulizi lako ndivyo lilivyo. Lakini lote limeanza kwa simulizi la mtu mmoja tu ambaye peke yake umemuamini na sisi wengine wote tunatakiwa tuamini. Sina shaka hata kidogo Mshume Kiyate alikuwa na mchango wake lakini alikuwa na mchango kuliko Nyerere? Alifanya zaidi ya Nyerere? Ushahidi wako mwenyewe unaonesha Nyerere hakumsahau na hakutaka watu wasahau...
Inaitwa Spirit of TANU...
Leo unasema Nyerere alitaka watu wasahuliwe; yeye ambaye amekumbusha majina yao. Kwa ufupi, usingejua alichofanya Mshume kwa Nyerere kama Nyerere mwenyewe asingesimulia! Ungejuaje? Hata mzee wako Rashad asingeweza kujua. Kumbe ni Nyerere kamrudisha mzee Mshume kwenye historia. Siyo mzee Rashad, Siyo Kitwana Kondo, siyo Dossa Aziz. Wewe mwenyewe unaposimulia kisa hiki inabidi utoe shukrani kwa Nyerere kwa kuwa mwaminifu na muungwana wa kukiri.
Angekuwa na Makuu Nyerere asingesimulia hili. Asingeheshimu mchango wa wazee hawa asingetaja miaka minne baadaye.
Mzee Said nikikuuliza ukiondoa hilo simulizi la Nyerere kumhusu rafiki yake ambalo leo linadumu na kunogesha mazungumzo yako ni kitu gani kingene ambacho mzee Mshume alikifanya na kupata umaarufu katika TANU. Mchango wake mwingine wa "hali na mali" ni upi? Sasa siulizi hili kwa sababu nadharau bali nataka kuonesha tu kuwa umaarufu wa Mshume umetokana na Nyerere na si vinginevyo. Kabla ya kukutana na Nyerere umesema alikuwa maarufu; kwenye mambo gani? kwenye siasa? au kwa kuwa mchuuza samaki?