Ndugu yangu ni ngumu sana kutafuta wapi umweke Mohamed Said.Unatakiwa kumfahamu kabla ya kumchukulia dhamana.
Hakika kama humuopopi MS kuna tatizo. Huyu ni mtu anayeweza kusimama na kuhadithia kuwa maziwa ya ng'ombe yanatoka katika mafenesi na si ngombe hundreds times.
FYI Mohamed is a master mind behind the turmoil seen recently.
He is a gifted story teller with incendiary power.
Ni kwasababu ulizosema tumekuwa na MS mara kadhaa tukitaka kurekebisha pale palipopinda. MS hakubali hilo kwasababu ya madai kuwa anatoa mada Ulaya. Kila tukimtaka ataoe maelezo ya ziada ima anshindwa au anapindisha ukweli na wakati mwingine anakimbia kama si kutoka nje ya swali, hoja au mada.
Hivi ninavyokuambia kuna hoja na maswali lukuki aliyoshindwa kuyajibu, kuyatetea au kutolea maelezo japo kwa fikra. Silaha kubwa ya majaliano aliyo nayo ni kuandika sana na kualikwa ulaya.Mtamwambia nini ninyi wamatumbi!
Badala ya kuwashambulia wanaotaka record ziwe straight ungemshauri MS asimame kidete kutetea hoja zake kwa mantiki. Nadhani umesoma na kuona contradictions nyingi kwa MS mwenyewe na ya mwisho ni hiyo niliyoweka akakana maneno yake achilia mbali wale anaowasemea kumkana bila yeye kujielewaMkuu, Malumbano haya yanatija sana kwasababu moja kubwa. Kuzuia upotoshaji kwa vizazi vijavyo, kuzuia maafa yatokanayo na upotoshaji na kuzuia ongezeko la wapotoshaji duniani.
Niseme kwa nafsi yangu ambayo nina hakika wengi ndipo wanaposimamia. Alichokiandika Mohamed ni historia ya matukio ambayo yalikuwepo. Kleist Syke alikuwepo, Abdul Sykes alikuwepo n.k. Hakuna anayekataa uwepo wa baadhi ya matukio hayo kwasababu historia haiumbwi inajiumba.
Lakini basi hivi tukubali tu kuwa Rais wa kwanza wa AA ni K.Sykes alimyemkabidhi mtoto wake A.Sykes TAA halafu TANU! Kupitia malumbano haya wengi wamejua huo ni uongo, uzushi na uzandiki mzuri tu.
Kwa mfano huo mmoja katika ya mamia unataka tukae chini na kumeza tu! Please tuonee huruma nduguzo.
Akili zetu tutazitumia wapi na lini!!Ndugu yangu kupitia JF na mnakasha huu Mohamed has been brought to his knee by admitting mistakes, accepting facts and most important he has purge and expunge some of his rhetoric and toxic materials.
FYI hii si mara ya kwanza kuwa na mnakasha na MS na kila mara wasomaji wameongezeka. Maana yake si kuwa wanamsoma MS, wapo waliomsoma na sasa wanatazama upya kurasa walizosoma.
Wapo wenye maswali ambayo kupitia mjadala wanapata ufahamu wa sehemu ya pili.
Muhimu sana ajenda, nia na dhamira ya Mohamed sasa vipo wazi kuliko wakati mwingine wowote.
Ngano ni masimulizi matamu ya kusadikika yanayotumia mazingira na yasiyoweza kuthibitika, kuthibitishwa, kutetewa au kujitetea zaidi ya ujumbe wake kumfanya msikiliza ayafurahie.Kwanza tumshukuru sana mzee wako kwa uzalendo wake wa kulitumikia taifa hili hata pale alipoweka maisha ya watoto wake kama wewe on the line.
Huyu ni one too many katika wale tunawaowaongelea na kuwatetea.
Hakika kupitia yeye na wenzake sote tupo huru tena kama taifa.
Maelezo haya yanatusadia kututetea pale tunaposema harakati za uhuru zilizagaa nchi nzima na si Tandamti, Kidogo chekundu au Narung'ombe kama MS anavyouaminisha ulimwengu.
Lakini pia unatutetea ya kuwa wazalendo kama baba yako hawakufanya hayo kama wakristo,waislam au Wanyamwezi.
Hapa ndipo tunapoachana sana na MS kwa kutaka kuibadili hsitoria, kufifisha heshima za watu na kukweza watu bila sababu.
Baba yako alifanya hayo kwa faida yako wewe na sisi sote bila kujali kabila, dini, Umanyema au Unubi.
Ndivyo malefu ya watu walivyofanya kote nchini.Ni tusi kubwa kwa watu kama baba yako pale tunaposikia kuwa kama si wazulu, wamanyema na wanubi tusingepata uhuru.
Baba yako hajaeleza fadhila zake kwa Nyerere, yeye amebaki kuwa rafiki wa Nyerere.
Leo tunaambiwa Nyerere alikwenda sokoni bila kujua kuwa anapaswa kuwa na fedha na wewe unataka tuamini tu kwasababu imeandikwa.
Tunachosem ni kuwa wazalendo wapewe heshima zao kama Watanganyika na si kwasbabu ni Wazulu, Wamanyema au Wanubi. Wazalendo waheshimiwe kwa mchango wao na si kwa imani zao kama ilivyokusudiwa kutugawa kutoka kwa MS.
Na yaandikwe ya kweli si kuficha baadhi, kusingizia, kuzua au kuweka maneno midomoni mwa marehem kwasababu tu hawawezi kujitetea.
Sijui kama baba yako au wewe mnadai nafasi pekee katika taifa hili kwasababu tu mzee ali risk kutoa vifaa vya sauti.
Sijui kama mna madai ya kwanini ninyi hamjapewa uwaziri n.k. kwasababu tu ya historia.
Na wala sijui kuwa mnaonewa na kudhulumiwa kwasababu ya historia ya mzee wako.
Kama sivyo, kwanini MS atake hayo yatokee? Kwamba yeye anapaswa kuwa waziri kwasababu babu yake aliongoza mgomo wa bandari!Nikushukuru kwa kutambua kuwa kuna ya ukweli na ya uongo.
Nadhani mimi na wengine hatuna tatizo na yale ya ukweli, tatizo letu lipo katika yale ya uongo.
Tupo hapa kurekebisha yale yenye mapungufu, but we don't have the right partner.
Sisi tunasimamia ukweli, MS anasimamia agenda yake so we don't have the common ground.
May be it's time you reach MS and convince him to join us regardless of our social differences for the betterment of this nation.Please let him understand that bigotry, hatred, incendiary comments, fallacy and the likes are contrary to Islamic teaching, they're inhumane and ''toxic asset'' we can pass on to next generation.
Huo mstari wa mwisho niliokazia, hapo ndipo MS asipokubaliana nawe.
Agenda yake ni kudhalilisha jamii nyingine na kuleta mifarakano, vipi akubali marekebisho yatokayo huko.
Ameandika kitabu ku-attack wakristo sasa atakubali vipi maoni ya watu wenye imani tofauti na yeye.
Nimalizie kwa kusema tatizo ni MS si wale wanaotaka kuweka record straight!