Nguruvi,
Siwezi kukunyima starehe yako. Hapo ndipo unapopaweza.
Kwa hakika nakutaja sana kwa sababu you make my mojo working.
Unaweza kunijibu kwa lugha yoyote ili muradi hunitukani.
Lakini nilikuuliza wewe nani akujuaye? Unaweza kujidhihirisha kama Mohamed?
Hukunijibu, Lakini si lazima unijibu.
Hata ukikaa kimya kwangu ni jibu tosha.
Ukitaka kuyafikia makamu yangu uandike. Nisingeandika ningekuwa mti kati ya miti porini.
Na wala si lazima niandike ulichoandika. Nina hakika nikikuonyesha nilichoandika hutaweza kuuliza au kuhoji maana ni mambo yanayohusu maisha yako leo hii siyo simulizi.
Hivi unaweza kuhoji chochote kuhusu Limbic System na impact ya psychological trauma inayoyosababishwa na malezi mabaya! Kwanza tu nikisoma maandishi yako kwangi ni sehemu ya study. Unajua Grandiosity na inferiority complex zinavyofanya compliment each other.Unaweza kuchangia lolote kuhusu manic syndrome au schizophrenia.
Siyo lazima mtu aandike kisicho cha kweli ilimradi tu kaandika. Kuandika kwenye heshima ni kule kunakoleta fikra na mtazamo mpya. Kwanini niandike kuwa commonwealth ni mjumuiko wa mataifa yenye mfumokristo nikifahamu huo ni uongo mzuri tu?
Kwanini niudanganye umma kuwa Nigeria ndiyo nchi yenye waislam wengi duniani.
Kwanini niandike kitu nisichoweza kukitetea na pengine kunidhalilisha kama takwimu ulizotoa?
Umeanza ngano yako kuwaondoa wapiganaji kwa kutumia dini, ukabaki na waislam.
Nao umeanza kuwagawa kwa kutumia makabila Wazulu na wamanyema na sasa umezama kabisa katika Umanyema kama ambavyo nina nukuu za kutosha kuthibitisha hayo.
Kuwa maarufu hakuhitaji kuandika. Osale Otango, Osama, Budia, Ngweso au makundi kama Sandinista,Red brigade, Alqaeda au Hakhan si maaurfu eti kwasababu wameandika ni maarufu kwa sababu zao kama ulivyo maarufu kwa kufarakanisha Watanzania.Wewe ni maarufu kwa wasio na uwezo wa kuchambua maandishi yako.
Kwa watu wenye akil,i Mohamed Said, ni mchochezi, mzushi na muongo.
Umeandika ngano kwa kutumia majina bila kuwa na tafiti.
Kama moja ya tafiti ni hiyo ya takwimu nitaomba dunia ifute somo hilo.
Mohamed umaarufu wako uko wapi wakati unakimbia hoja lukuki.
Kututajia majina ya akina Tatu Said, Mwanameka n.k. haitusaidi kitu kwasababu majina tu hayatoshi kufanya unachosema kuwa kweli.
Kuwasingizia marehemu kwa maandishi ni kinyume cha maadili ya kiroho na Uislam.
Simama na tetea hoja zako. Umekimbia maswali na hoja za wanajamvi kama akina Mag3, Mwanakijiji, Platozoom n.k.
sasa umaarufu wako ni kuhusu nini. Lakini hapa hatupo kuonyesha umaarufu,tunatumia akili zetu kukueleza kuwa si kweli kuwa Sykes alianzisha AA na si kweli kuwa Sykes alimfundisha siasa Nyerere.
Tutakuwa hatuzitendi haki akili zetu tutakapokubali kuwa sheikh Chaurembo aliandika hotuba na Nyerere mwenye Master msomi na Mwalim aibebe kama ilivyo hadi UNO kuisoma. Real!
Kushindwa kwako kuthibitisha tuhuma kama za hotuba ya Nyerere kuhusu Sykes alipoaga ni ushahidi mzuri sana kuwa umejifungia chumbani, ukatumia majina ya watu na matukio kuandika tamthilia hii tamu.
Nakishukuru chuo kikuu cha DSM kutofikiria hadithi hii kama sehemu ya mtaala wa wanafunzi maana mwanafunzi anapaswa kupewa elimu na wala si chuki, udini na ukabila.
Ni tusi kumfundisha mwanafunzi kuwa bila Wazulu na Wamanyema uhuru wa Tanganyika ungekuwa mashakani.
Ni dhalili kumlisha mwanafunzi takwimu za kiwango chako tutegemee mwanafunzi huyo alisaidie taifa katika utafiti.
Kwa ufupi jitihada zako za kuandika ngano ili zijenge mazingira ya kufarakanisha watu sasa zi wazi.
Pengine tofauti baina yako na Ilunga ni namna ya kufikia hadhira.
Tupo hapa kuwaonyesha wanajamvi mbinu zako za kujenga mazingira ya kusema watu fulani wanaonewa huku ukijua ukweli kuwa uonevu ni zao la kujionea.Unashinda kuwapigia watu hadithi badala ya kuwaambia wapeleke watoto shule, wawasaidie homework, kuwajengea kujiamini na kwamba sky is the llimit. Wewe unawafanya wajiskie dhalili, watu wa kiwango duni na kwamba wakibadili majina yao basi maisha yatanyooka wakiwa vitandani.
Kibaya zaidi ni jinsi unavyowafanya vijana hasa wa kiislam kuamini kuwa mafanikio yao yanaambatana na majina na wala si jithad. Kwamba jihad iwe kutafuta nani kafanya nini na wala si wao wanafanya nini katika maisha yao.
Unafanya hivyo ukijua wao hawatahoji kuwa wewe ni zao la mfumo kristo na kwamba ni ALUMNI wa st Joseph Catholic school. Unawadanganya waandamane kwenda kumuwekea dhamana Ponda na wala si kwenda maktaba.
Mohamed, sifa ya uislam ni ukweli na haki. Maandiko yako yanaacha maswali mengi kuliko majibu na ni vema ukasema historia uandikayo ni ya wazee wako wa Narung'ombe wala si Tanganyika. Ukitaja Tanganyika umetualika na hapo hakuna favor or fear, just facts on the table.