Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar


Nguruvi,
Sina ujuzi wala makamo ya kumjibia kitu Mzee Jumbe.
 
Mwaka 1974 Nyerere aliwatwisha Chuo Cha Kivukoni jukumu la kuandika historia ya TANU.

Chuo hiki kilianzishwa kama shule ya kuwasomesha makada wa TANU katika mambo ya itikadi, propaganda na uhamasishaji umma wakiiga mfano wa Ruskin College ya Uingereza.

Cha kushangaza wale ambao aliofanya nao harakati za kutafuta uhuru kina Abdulwahid, mweka hazina wa TANU Idd Faiz Mafongo, Baraza la Wazee wa TANU liliundwa Makao Makuu ambalo lilikuwa na wajumbe 170 pamoja na kamati yake ambayo Mwenyekiti wake alikuwa Sheikh Suleiman Takadir.

Hawa wote hawatambuliki hawamo kwenye historia ya TANU ya Kivukoni lakini cha kushangaza Nyerere wakati anaaga kwenye hotuba yake nafsi ilimsuta ikabidi hawataje.
 

Ami uko vizuri huyu jamaa asikutishe endelea kumpigilia misumari hata kama ameambiwa akupuuze hiyo haiwezi kuwa hoja kumbe nguruvi kuna watu wana mcontrol nyuma yake huyu mtu ni dhaifu.
 
Kwa yeyote ambaye amezama kwenye historia ya TANU naomba anifahamishe sababu iliyowapelekea Baghdelleh na Makange kwenda jela.
 
Mohamed Said;6019051]Nguruvi,Nikitoa maana haitakuwa na tija si kwako wala kwa watazamaji.Mimi Insha Allah nakuwekea hapa vipi mfumokristo unavyofanya kazi.
Wanajamvi hapa ndipo kila siku tunasema wakati mwingine watu wanajadili kitu bila kujua wanajadili nini. Mohamed anafahamu wazi kuwa hana definition ya maana kuhusu ndeno mfumokristo na ile aliyokuwa nayo akiitoa haiwiani hata kidogo na madai yake. Amejitahidi kukwepa hoja hiyo muhimu akijua kuwa jibu lake linaweza kumaliza mjadala kabla haujaanza. Ametuwekea mfumo unavyofanya kazi ingawa hatujui mfumo ni nini.

Kwa taarifa ya wasomaji muasisi wa neno mfumokristo ni Mohamed. Neno hilo kwavile halina definition limetumika na watu na kupoteza maana nzima hata pale ambapo kuna hoja ya maana. Jokakuu amenikumbusha kauli yangu miaka miwili niliyoandika hapa kuwa tatizo siyo hoja ni watu wanaoibeba hoja. Tumeona mwenzetu Mdondoaji akijenga hoja na kumnukuu Rais Jumbe wakati huo, tumemuuliza ufafanuzi wa kauli ile kuhusu ''serikali kama haina dini kwanini inamshirikiano na Vatican'' ameshindwa kuitete. Haya ndio matokeo ya kubeba kitu kizima kabla ya kukiangalia upside down.

Pamoja na kukwepa hoja ya definition ya Mohamed Said, hebu tuangalie kule alikokimbilia akidhani ataweza kutuondoa katika hoja. Hata hivyo wanajamvi waelewe kuwa Mohamed hana definition ya mfumokristo ana maelezo.
Kwa maneno mengine Mohamed anajua gari linavyokwenda lakini hawezi kueleza gari ni kitu gani.

Tuendelee hapa. Ni mwinyi huyo huyo alikuwa sehemu ya serikali ya Nyerere ambayo muslims walikuwa agitated na against.

Mo anasema waislam walikuwa raia wa daraja la tatu. Hakueleza daraja la kwanza na la pili akina nani.
Hii imewekwa kwanza kujenga hasira kwa msomaji kabla hajalishwa habari inayokusudiwa.
Under such a politicalclimate President Mwinyi could not augur well with a Christian dominated cabinet and the civil service as the bureaucrats in these institutions deep intheir hearts resented a Muslim head of state
Mohamed hakueleza Mwinyi aliwezaje kuwa rais katika serikali iliyokuwa dominated na Christians.
Je alitokea msituni au aliingia madarakani kwa njia za deomkrasi ndani ya mfumo ule ule wa Christian dominated government.

Lakini anapopotosha zaidi ni pale anaposema uwezo wa mwinyi ulififishwa na baraza la mawaziri lililokuwa limetawaliwa na Christians.
Sote tunajua kuwa baraza la mawaziri linachaguliwa na Rais na Rais huyo huo ana uwezo wa kumuondoa waziri asiyekubaliana naye.
Ilikuwaje yeye akaishi katika mazingira hayo magumu akiwa na uwezo wote kama Rais?Na je aliwezaje kumuondoa naibu waziri mkuu Mrema katika hali kama anayoisema?Soon opposition to Mwinyi's rulewithin his cabinet and ruling party, CCM surfaced into the open.[/QUOTE]
 
Na kwa mantiki hiyo si Kikwete!

Nguruvi,

Angalia nini kimepita hadi Abdu akapewa
medali na Kikwete.

Kikwete asingeweza kuzuia historia ya Abdu
hasa baada ya watu kujakujua nini Abdu
kafanya kwa Nyerere mwenyewe na nini Abdu
kafanya katika TAA na TANU.

Ikiwa Prof. Haroub Othman hakumjua Abdu vipi
Mwinyi atamjua?
 
[/QUOTE]

Nguruvi,
Unasubiri ''definition'' sawa wako watakaokupa.

Tusubiri ''definition'' kwa wanajamvi kisha tutaendelea Insha Allah.
 
Nguruvi,
Sina ujuzi wala makamo ya kumjibia kitu Mzee Jumbe.
Soma vizuri ndugu yangu, naona kama umechanganyikiwa kidogo. Nimeandika mara 2 kuwa swali la Jumbe si lako ni la Mdondoaji. Wewe umedandia tu hoja za kitoto za Ami.
Mzee Said niliposema ''ukioga na watoto mtoni hutakati'' nilikuwa na maana kuwa wao watavuruga maji kwa michezo yao ya kitoto na wewe mtu mzima utatoka ukiwa na matope kama unavyotoka sasa.
 
Nguruvi,
Unasubiri ''defination'' sawa wako watakaokupa.Tusubiri ''defination'' kwa wanajamvi kisha tutaendelea Insha Allah.
Kwenye definition nshamaliza, huna. Nipo katika bandiko lako nimejibu hoja zako. Hii ni njia yako ya kukwepa hoja tushaizoea
 
Napenda huu munakasha Mohamed Said anatoa darsa wanajibu cha kushangaza Mohamed Said haulizi mtu kitu chochote kuhusu historia.

Tuendelee...
 
.[/COLOR][/FONT]Kabla ya uteuzi wa Mwinyi, Mohamed alipaswa kuwaeleza wasomaji Prof Malima alikuwa na nyadhifa gani wakati wa Nyerere.

Tungalie sehemu ya pili....


asante Nguruvi3 nahakika hapo hawezi kujibu hata hoja moja.

Na hivyo basi nakuja na conclusion kuwa maandishi ya MS ni HISTOHISIA
 

Jokakuu,

Hapo kwenye RED unaweza kuorodhesha angalau baadhi ya madai ya haki za Waislamu? natanguliza shukrani kwako kwa kukiri tatizo na huu ni mwanzo mzuri! hata kama hatuna uwezo wa kuleta mabadiliko lakini kukiri kuwa kuna tatizo ni sehemu ya utatuzi!
 
Napenda huu munakasha Mohamed Said anatoa darsa wanajibu cha kushangaza Mohamed Said haulizi mtu kitu chochote kuhusu historia.

Tuendelee...

wewe nawe kwa kukurupuka kama unausingizi kanawe miguu ulale.

Hapa MS ndio mtuhumiwa wa uchochezi kupitia NGANO na HISTOHISIA zake.. Kwahyo anatakiwa a'prove maandishi yake.
 
Basi mimi kila nikimuona Nguruvi3 humu ndani huwa najikuta tu naimba
Nguruvi3 Bomaye!,
Nguruvi3 Bomaye!
As Congolese Chanted in Lingala when Mohamed Ali entered the ring during the Rumble in the Jungle fight against George Foreman in 1974

Mkuu Nguruvi naona wapambe wanajipanga kurusha taulo kati
 
Last edited by a moderator:
wewe nawe kwa kukurupuka kama unausingizi kanawe miguu ulale.

Hapa MS ndio mtuhumiwa wa uchochezi kupitia NGANO na HISTOHISIA zake.. Kwahyo anatakiwa a'prove maandishi yake.

Wewe nakushauri ungekuwa msomaji tu huna unalolijua humu wewe ni futuhi wetu humu ukumbini unatupa burudani.
 
M Si kweli. Umeficha ukweli hapa. John Garang alikuwa mwanafunzi wa UDSM. Alirejea kama Alumni wa UDSM ambaye wakati huo alikuwa katika conflict na alishakuwa mwanasiasa.
Ni sawa na wewe Mohamed ''mtafiti na Mwanadishi'' utakaporejea St Joseph Catholic school Dar es Salaam, shule ina kila sababu ya kukupokea kama ALUMNI wao. Kwahiyo si suala la Christians kuwa wengi. Ni suala la weledi. Mwaka jana wanasheria wakuu wa serikali za Uganda, Kenya na Tanzania walikuwa Alumni wa UDSM faculty of Law. Hivi leo Museven akirudi UDSM atakuwa anarudi kama Mkristo au Alumni! OMG! Yarabi!

Wole Soyinka alipokuja UDSM hivi karibuni, mimi nilikwenda kumsililiza. Alikuwa na wenyeji wake akina Shivji. Ukumbi wa Nkrumah ulijaa si kwasababu Wole ni mkristo bali tunu ya kile alichopaswa kukieleza. Lazima ukubali kuwa katika maeneo ya UDSM ile ni sehemu ya Academic na hivyo mtu yoyote husikilizwa bila kujali ana itikadi gani kisiasa au kiimani. Ndivyo ambavyo Chuo kikuu kimoja cha Marekani kilikubali kumkarabisha Ahmadinajade licha ya kwamba serikali haikupendelea. Chuo kikuu ni academic arena siyo mahali pa kueneza unfounded allegation, mahali pa kuangalia nani kavaa msala mkubwa mkubwa nani ana msuli ay tarabushi inayong'ara. You ought to know this Mohamed! No excuse1 you ought to know this Mzee.
The academic staff as well as students went out of their way to potray Garang as a "true son of Africa", and a crusader against Muslim hegemony in Sudan. And Garang cherished every moment of it.
Ukienda chuo kikuu leo wapo wanaomuona Ahmadinajade shujaa, wapo wanaomuona Ghadafi shujaa na wapo wanaopingana na hoja hiyo. Hiyo ndio maana ya kuwa na intellectual discourse na different opinion.
Kwa wale wa zamani UDSM ilikuwa ''centre for academic intelligence'' katika Afirika. Wote unaowasikia akina Olive Tambo, Tabo Mbeki, Yaser Arafat, Kahama n.k walikuwa hawaishi kutembelea UDSM kupata different opinion. Si kila mtu alikubaliana nao lakini hata kwa kutokubaliana hiyo ni sehemu ya academics na ndivyo chuo kinavyopaswa kuwa.

Hebu tembelea pale Kennedy institution uone jinsi watu wanavyocharurana kwa hoja. Utadhani si Waamerika.
Chuo kikuu ni sehemu ya fikra chem chem na huliangalia jambo kutoka angle zote. Si sehemu watu wanakaa katika mkeka kusikia hadithi bila kuhoji au wanapohoji maandishi na mitazamo kwa njia tofauti wanakuwa wamekufuru achilia mbali kuwa wajinga.

The ten percent Muslims at Dar es Salaam University did not even dare pose a single question to Garang much as it was evident that Garang was fighting an anti-Muslim war in the name of war of liberation.
Umepataje ten percent. Takwimu zako za Christian vs Muslims ambazo pia zinaonyesha Christians vs non muslims zinaonyesha uwiano wa 20:80. Vipi umefikia 10%.
Lakini muhimu hapa ni kuwa kama hawakuwa na maswali je walipaswa kuuliza tu kwasababu ni waislam. Na pia ulitumika utaratibu gani wa ku-sideline waislam ambao unaweza kutueleza zaidi ya 10 %. Ni vema ueleze ili watu wajue hii ''systemic discrimination'' ilifanyika vipi. Vinginevyo hoja yako haina mashiko na wala haisimami yenyewe bila neno muslims au Christians. Ni hoja mfu. Mohamed, Yaser Arafat nao wanapata msaada wa serikali ya Tanzania kwa kutumia kigezo gani. Unakumbuka serikali ya Nyerere ilivunja uhusiano na Israel kwa sababu ya Palestina.
Tanzania inaunga mkono POLISARIO na ilismama kidete hadi China ikapewa hadhi UN sasa huko nako unasemaje?

Kambi za wakimbizi wa Msumbiji zilikuwa hapa Tanzania. Mreno ni mkatoliki kweli kweli sasa kwanini serikali ya Christian ilipiga vita wakristo wa ureno.
Kambi za akina ANC, PAC zilikuwepo hapa. Wote akina Mbeki, Khama n.k waliungwa mkono na Tanzania kupambana na mifumo ya utawala ambao ni wa kikristo pengine zaidi ya waislam. Hoja kwamba Garang alipewa mapokezi kwasababu ni mkristo is too low.

Unafahamu kuwa Henry Kissinger kutoka mfumo wa kikristo kwa maana yako aliwahi kupingwa na wanafunzi wa chuo kikuu.
Mzee Said hoja za namna hii next time ukifanya review ya vitabu na paper zako ziondoe maana hazina mashiko wala fikra
Untypical trait of journalist and researcher the least to say!
 

Nguruvi,
Niwie radhi kwa "kudandia."

Ingawa ningefurahi kama usingetumia neno hilo kwangu.
 

Nguruvi,
Hakuna tatizo.

Kila jambo lina tafsiri yake kutokana na mtu linavyokugusa.
Nimeeleza yangu nawe umeeleza upande wako.
 
Nguruvi,
Unasubiri ''defination'' sawa wako watakaokupa.

Tusubiri ''defination'' kwa wanajamvi kisha tutaendelea Insha Allah.
Kwenye definition nshamaliza, huna. Nipo katika bandiko lako nimejibu hoja zako. Hii ni njia yako ya kukwepa hoja

Nguruvi,
Sipo hapa kujibu maswali yako kama unavyotaka.

Wakati mwingine hupenda wengine wakujibu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…