Nguruvi3, mwanakijiji na wengine.
Mtakuwa hamjawatendea haki waTanzania wenzenu kama mtaishia hapa hapa kubishana na kupongezana bila kukusanya haya mawazo yenu na kuyaweka katika kitabu ambacho kinaweza tumiwa na vizazi vingi vingi kupingana na Al Akhiy MS ambaye ametujuza mengi.
Nawanaswihi tumieni busara nanyi kuandika kitabu chenu na tutakuwa tayari kabisa kuwapa support kwa hali na mali ili vizazi vya sasa na vijavyo viweze pata historia sahihi ya uhuru wa Tanganyika.
watendeeni haki watanzania.
Amiin Rabilaalmiin..gombesugu, The Great Thinker, hiyo mipini yako ni "Mubashar" umetutajia wazee wetu umewaka Hadhwarani umenikumbusha mbali kuna wazee wengi umewataja nimewaona takuwa mchoyo wa Fadhwila nisipo kupongeza. Umetaja Baadhwi ya mitaa yetu sisi wanywa Gahawa wa Stanley Street, Mbaruku Street, New Street, Manyema Street, Chura Street, Udoe Street, Mkunguni Street, Raha Street, Narung'ombe Street, Congo Street, Mchikichi Street, Livingstone Street, Msimbazi Street, Uhuru Street, Kipata Street, Lindi Street, Somali Street, Kariakoo Street, Tandamti Street, Pemba Street, Muhonda Street, Nyamwezi Street, Swahili Street....nimechoka kutaja maeneo ya wanywa gahawa. Kuna mzee mmoja anaitwa Idd Mtingwa, marehemu nadhani ni baba ya Rukia Mtingwa wa Voda huyu mzee alikuwa rafiki kipenzi wa marehemu mzee alikuwa afisa wa ubalozi wa Tanzania nchini Marekani. Mwenyezi Mungu hawape rehema hawa wazee wazalendo waliotangulia mbele ya haki.
Mwl, mpaka anaingia kabulini, hakuacha kuililia Nbc bank.Jee, alimpuuza chaguo lake Mzee Mkapa baada ya kuuza mashirika yote ya umma likiwemo NBC? au alifurahia kazi nzuri aliyofanya Rais wake?
From a reliable source nimeambiwa,bila John Rupia,safari ya Nyerere UNO,ilishaota majani-i have in my posession breakdown nzima ya huo mchango-haifai kuwekwa hapa-cause heads will roll. Nyerere kutokuandika kitabu amefanya jema-ingebidi aandike uongo kuwahifadi watu
Mzee Ms,
Son...
Itakuwa vyema kama utaweka hiyo michango.
Hapa tuko katika kuiweka wazi historia ya uhuru na itapendeza kama wale
walochangia watajulikana huenda ipo siku wataenziwa.
TAA hadi TANU kuna wafadhili wa kudumu ambao wanajulikana na wapo wale
ambao walijitahidi kutoka kila ilipobidi.
Ni vyema hawa wote wakatambulika.
Ama hilo la Nyerere kutoandika kitabu halina uhusiano na azma yake ati anawahifadhi
baadhi ya watu.
Hii si kweli wala haingii katika mantiki.
Nimeona umeweka ''kabati la fedha'' tena isomwe.
Ngoja nikufahamishe.
Abdu Sykes alikuwa na kituo cha kuuza mafuta (filling station) pale Ilala Kitchwele Street
mkabala na ofisi ya Mkuu wa Wilaya.
Kituo hiki kipo hadi leo hii mahali palepale.
Sasa kinapofungwa kituo mauzo ya siku yalikuwa yanapelekwa nyumbani kwake Stanley
Street na hapo ndipo hizo fedha zinatiwa katika hilo kabati la Bi. Mwamvua.
Sasa inapotakikana fedha ofisi ya TANU ndipo hilo kabati hufunguliwa.
Gombesugu,
Kumbe na wewe umo huvumi tu.
Umenipeleka mbali sana.
Shariff Attas mara ya mwisho kumuona ilikuwa Eid Fitr 1990 mimi na Kleist Abdulwahid Sykes
tulikwenda kufuturu nyumbani kwake asubuhi baada ya sala ya Eid.
Alitupa kisa kizuri sana kati yake na Nyerere pale Sokoni Kariakoo ofisini kwa Abdu Sykes.
Kisa ambacho kila mtu akikisikia atapata simanzi.
Nilifika kijiji cha Blantyre nje kidogo ya Glasgow, Scotland.
Hapa ndipo alipozaliwa David Livingstone na kijiji hiki chote kimefanywa kuwa makumbusho yake.
Nilifanya kipindi na BBC Swahili Service ''Barua Kutoka Glasgow'' kuhusu kijiji hiki na Mkuu wa BBC
Swahili Service siku zile Mzee Neville Helms alikipenda sana.
Hapa Dar es Salaam Mtaa wa Lumumba kuna kijana ana collection ya picha nyingi sana za watu
maarufu walioishi katika huu mwambao wa pwani.
Mimi nina hakika hakuna mtu Afrika Mashariki hii amekusanya picha kama hizo.
Nimeona hata picha ya Al Manzil na wanachama wake nk.
Nguruvi3, mwanakijiji na wengine.
Mtakuwa hamjawatendea haki waTanzania wenzenu kama mtaishia hapa hapa kubishana na kupongezana bila kukusanya haya mawazo yenu na kuyaweka katika kitabu ambacho kinaweza tumiwa na vizazi vingi vingi kupingana na Al Akhiy MS ambaye ametujuza mengi.
Nawanaswihi tumieni busara nanyi kuandika kitabu chenu na tutakuwa tayari kabisa kuwapa support kwa hali na mali ili vizazi vya sasa na vijavyo viweze pata historia sahihi ya uhuru wa Tanganyika.
watendeeni haki watanzania.
Mohamed, tunachotaka kujua ni namna WML ilivyofanya shughuli zake katika nchi ya mfumo kristu.
Hata kama WML na Rukara hawapo sasa lakini hatuzuiwi kuangazia uwepo wao nchini na utendaji kazi zao Katika nchi ya mfumo kristu, tena unathibitisha kabisa kuwa serikali (yamfumo kristu) ilitoa baraka zake
Mohamed, watu wana kiu. Tafadhali tulizungumze hili.WML Walifukuzwa nchini au ilikuwaje wakafunga ofisi?
Mkuu JokaKuu hili ndilo nalisema kila siku. Nashukuru labda lugha yako itaeleweka.Ritz,
..Prof.Maghembe alikuwa waziri wa elimu, kwa hiyo hizo takwimu alizotoa zinatosheleza. unachoweza ku-argue kutokea hapo ni conclusions alizotoa.
..kwa mtizamo wangu Prof.Jumanne Maghembe ni kama vile ametoa majibu kwa madai ya Prof.Malima, Prof.Njozi, na Mzee Kitwana Kondo.
..Prof.Malima alidai tatizo fitina na kutokuwepo kwa utaratibu wa namba za mtihani. sasa Prof.Maghembe amekuja kubainisha kwamba tatizo ni UTORO wa wanafunzi.
..mimi sisemi kwamba Uislamu ni tatizo, ila nasema Waislamu ni waathirika wa mazingira ya kijamii/social na kiuchumi/economic yanayopelekea utoro wa wanafunzi ktk mikoa ya Pwani.
..inawezekana shule ni mbaya, inawezekana wazazi hawana uwezo ni masikini, au pengine hakuna mwamko, huenda kuna mila na tamaduni mbaya etc etc. ushauri wangu ni kwamba tuangalie kila kitu, na tusiweke udini mbele, bali tuongozwe na UMOJA wetu kama WATANZANIA.cc: gombesugu, Nguruvi3, Kadogoo, Ami, Son of Alaska, THE BIG SHOW
Barubaru, mbona unapata taabu kuuelewa huu mnakasha unahusu nini, kinchogomba si Mohamed kuandika historia ya wazee wake, hapana, ni namna anavyowahadaa wananchi kwa madai ya kipuuzi yasiyo na ukweli wowote...hata hivyo naomba kwa niaba ya hao wengine usiowataja nikutake uzingatie mambo matatu muhimu;Nguruvi3, mwanakijiji na wengine.
Mtakuwa hamjawatendea haki waTanzania wenzenu kama mtaishia hapa hapa kubishana na kupongezana bila kukusanya haya mawazo yenu na kuyaweka katika kitabu ambacho kinaweza tumiwa na vizazi vingi vingi kupingana na Al Akhiy MS ambaye ametujuza mengi.
Nawanaswihi tumieni busara nanyi kuandika kitabu chenu na tutakuwa tayari kabisa kuwapa support kwa hali na mali ili vizazi vya sasa na vijavyo viweze pata historia sahihi ya uhuru wa Tanganyika.
watendeeni haki watanzania.
gombesugu, maadamu umeamua na wewe kuingia kwenye mkumbo huo huo wa kuwatazama waliokuwa Watanganyika katika misingi ya wao na sisi katika harakati za uhuru, naomba nikukumbushe jambo moja muhimu...huko unakoita mikoani ndiko walipoishi zaidi ya asilimia 98% ya wananchi milioni nane. Kwa idadi ya wakazi wa Dar es Salaam wakati huo, unaweza kuwataja hadi vichanga, hutaweza kufikia idadi ya wakazi wa kadistrict kamoja tu ka Mwanza. Heri mfungue thread mahsusi mtajiane majina yote yale tangia Arab Street, Kichwele, Ring Street, Main Avenue hadi mtaa wa Unter Den Akazien.Gombesugu said:Tafadhali jamaa na nyie kutoka mikoani, kipata fursa tusaidiane japo kiduchu kutaja baadhi ya majina yalosahaulika. Nachelelea baadae tusijemlaumu Sheikh Mohammed Said kuwa ati kapendelea mno Wazee wake na vinyozi wa Kipata na Mkunguni!? Nashauri tukishamaliza mnakasha huu,nasisi soote kwa pamoja tukusanye makabrasha yetu humu na kuandika rasmi "Marekebisho ya Historia ya Tanganyika kutoka JF".
Usidharau usichokijua. Hivi kweli leo Mag3 na Nguruvi waunganishe nguvu zao waandikie kitabu patakalika kweli hapa jamvini?Barubaru:
Nakuhakikishia hawawezi kuandika kitabu hawa! wanahofia kije kuwa kichekesho!
Usidharau usichokijua. Hivi kweli leo Mag3 na Nguruvi waunganishe nguvu zao waandikie kitabu patakalika kweli hapa jamvini?
Mohamed, hawa WML walipewa kibali na nani, walikuwa wanashughulikia nini, walikuwa wanajamii gani wanayoihudumia?
Je, walifukuzwa au waliondoka wenyewe?
Mzee Ms,
Kabati la fedha hufunguliwa katika mahitaji ya tanu tu?
Je? na akitaka kuagiza mzigo mpya wa mafuta inakuwaje?
Au kisima kilikuwa kikitoa mafuta muda wote bila kujazwa tena?
Mag3, kwahakika wengi sana wamesema na wamerudia kuwa Mohamed akaiamua kutaja majina ya wajukuu, vilembwe na vining'inia toka miaka waarabu wanaingia Mzizima, wala hakuna atakaye nyanyua mdomo.Mag3;6109922]Barubaru, mbona unapata taabu kuuelewa huu mnakasha unahusu nini, kinchogomba si Mohamed kuandika historia ya wazee wake, hapana, ni namna anavyowahadaa wananchi kwa madai ya kipuuzi yasiyo na ukweli wowote...
Sasa Mohame unawezaje kuwa na taarifa za world church council usijue kinachotokea hapo ukumbini mwa nyumba yako!Nguruvi,
Sina taarifa za ndani za WML.
Jasusi,
Hata Shigongo kila siku anaandika vitabu waambie hao jamaa zako waandike kitapata soko sana Kanisani na kwenye vigango lakini siyo kwa Watanzania.
Hao waandishi wako kuna mmoja yeye anasema wazi kabisa kuwataja hao wazee wenu wa Kariakoo kwake ni matusi makubwa.
Bahati nzuri kitabu chenu kitakuwa kimejaa wasomi watupu hakuna mmoja hata mwenye akili za madrasa, mnywa gahawa, washinda vibarazani, kina mwanameka.
Jasusi, jikusanyeni wote muandike hapo kweli humu jamvini hapatakalika lakini kwa Watanzania ndiyo itakuwa mtihani na kituko kusoma hizo ngano.