gombesugu,
Kwa kweli nikisoma bayana zako humu jamvini walaahi najisikia murua raha mstarehe.
Hawa ndugu zetu wanasema tusitumie neno "sisi" au "nyie" wanasema siyo uzalando wakati huo huo hao wanaotoa kauli hizo ndiyo wanaotuita sisi wafuasi wa Mohamed Said na wale wote wanaopingana na fikra za Nyerere.
Kwa maana hivyo hawa wote ambao ni Wakirsto ni wafuasi wa Nyerere. Sisi watu wa madarasa akili zetu na fikra zetu zinafanana kama machinas..ha haa haa.
Kuna jamaa mmoja humu yeye alienda mbali zaidi akasema kuwataja hao wazee wa kariakoo humu jamvini kwake ni matusi makubwa huyu huyu ndiye anatoa darsa kwa Waislam, ha ha haaa.
Kuna mwingine yeye bingwa wa tambo na majingambo anawaita wazee wetu "mwanameka" yeye anaita kukata kisu na mfupa, ha haa ha.
Karibu sana mie napata uji wa shurba na mkate wa ufuta.
Ritz,
Salaams. Wallahi,sometimes trying to keep people from getting on my last nerve,is like trying not get wet ,standing outside in a dam hurricane.
I think what most people in here fail to realize is that,History is supposed to confront people. We may not agree on everything but through positive exchanges and dialogue we share and experience of something otherworldly. Ofcourse,this may provoke emotions that we are not comfortable with.
Nafurahi Al Akhiy
Barubaru,kabainisha kiduchu uhusiano na mahaba ya dhati kwa nduguye marehemu
Bw. Julius Rweikiza.
Hata nami katika mojawapo ya bayana zangu za awali nilijaribu kutoa mifano kadhaa ya family friends zetu wengi mno hapo nyumbani hasa wenye imani ya
Kikristo,baadhi nilisoma nao mimi binafsi na wengi wao walikua ni wanataaluma wenzao Wazazi wangu. Na jinsi gani tulivyoishi nao kwa hishma na mahaba ya dhati mpaka kesho.
Tatizo tulonalo,ni kuwa baadhi ya jamaa hapa jamvini wana dhana ya kufikiri ati sisi
Wakristo na
Ukristo ndo tumekuja kuwajua na kujifunzia hapa. Pia wanajaribu kwa kila hila na juhudi iso kiasi yakuwa sisi tuna chuki,udini na hatuna uzalendo.
Kwa ufupi,mpaka sasa binafsi sijaona yakini ya shutuma/mada hii kuthibitishwa asilani. Marejeo ya topics ni mengi mno,tunakwenda nje ya mada/mnakasha bila ya maudhui yenye maana na kebehi ndo zimeshamiri.
Kuna wale nao wanaodai ati
Historian/Scholar mahiri Sheikh Mohammed Said,alipoandika vitabu/kitabu chake ati hakutumia methodology mwanana na pia hana scientific methods/evidences kuthibitisha mengi alotujuza.
Infact,what we call "
science" is actually just indoctrination into yet another completely made up account of history and physical processes.
Nami nakufuatilia bayana zako kwa utuvu japo naona nyingine hakuna majibu yake!ahaha!!
Ahsanta.