Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

 
na hayo maradhi lazima yatokomezwe, la sivyo yale ya Burundi na Rwanda au korea yatatufikia.
 
Sheikh Farid, ahlan wahsalan muungwana.
Sina chuki na wzn kwasababu nikiwachukia lazima nianzie katika familia yetu.
Ninachofanya ni kujibu yale ambayo wznz wamekuwa wanasema miaka nenda rudi.
Wakatuita Makafir ndiyo maana tukakubali na ndio maana ya hiyo cc, kwamba ukitoka bara ''hilo chogo la kuja,kaafir huyo'' Wakatuita wanyonyanyaji, wakasema sisi wezi tunawaibia na kila aina ya fitna.

Leo Watanganyika wanaweka kila kitu mubashir mnaona ni chuki au matusi. Chuki kaanza nani?
Pili, muungano wa Nyerere ulikuwa wa Pan Afrika na ukichagizwa na nguvu ya pamoja kudhibiti madhara ya cold war pia.

Nia ilikuwa kuendelea kwa pamoja tukijisahihisha hadi kuridhiana.
Wznz wakageuza kuwa ni mradi, kila wakitaka jambo tishio tunavunja muungano.
Sasa hivi Watanganyika wanasema wala hamna haja ya kusema ondokeni tu! hata kuaga msiage mtume twitter mkishateremka Malindi.

Sasa yanazuka madai ya kugawana. Kwamba watu wagawane kisichokuwepo. Wewe una sh 24 mwenzako 1498 halafu unataka mgawane sawa. Hata hizo 24 hukuziweka katika mchango. Unadai nini kama si upungufu wa fikra.
Hatutazuia begi la mznz, lakini hakuna atakayeondoka na kingine! njia nyeupeee

Kuhusu utegemezi, ah ndugu yangu si tumeweka kila mnachotegemea?
Jana tu mumeomba mkatupe ngano bara maana hamna eneo, huo si uetegemezi.
Unaposoma bure wakati mwenzako analipa mkopo, huo si utegemezi

Nadhani ujibu kwa nukta moja hadi nyingine ukionyesha wapi si utegemezi, vinginevyo Yericko kasema mtoto aliyebebwa ana viwembe sasa ni wakati tumtue atembee mwenyewe.
 
Yericko Nyerere,

Wanaukumbi ndiyo wataamua, wapi nimeleta matusi na kejeli naona "mipini" imekuchanganya sana nionyeshe wapi nimekutukana? kwa faida ya Wanaukumbi nashindilia Mpini mwingine halafu utasema matusi.

Nakujuza kuwa mzee wetu Shehe Issa Bin Amir amefariki 26 januari 1953 akiwa na umri wa miaka 107!
Wanaukumbi nadhani mnajionea wenyewe hapa anatujuza kuwa huyo Sheikh Issa amefariki mwaka 1953 hapa chini baada ya kufa akafufuka...waalahi bayana zako ndiyo zinakutukanisha na mimi siwezi kukaa kimya umekutana na kichwa cha madrassa mnywa Gahawa, haha haa aaa Shariff gombesugu, upo Alhy Baabu soma chini hapa.

Sheikh Issa Bin Amir amefariki mwaka 1953 halafu alifanya mkutano na Nyerere mwaka 1954...ha ha haaa
gombesugu, Jasusi, Kadogoo,
 
Last edited by a moderator:
Ukiwa mbinafsi na mbora mimi kamwe huwezi kuandika historia ya nchi inayohusu makabila zaidi ya 120 na inayohusi imani zaidi ya tano nchini!

Utabaki na kikundi cha wanafiki na wafitini tu ndio wataokuunga mkono!

"Kikundi cha wanafiki na wafitini" ha ha haa...mnafiki ni wewe unaoyejinasibisha na baba ambae si wako halafu unajifanya mjanja, ntakupa kisa kimoja ndani ya Quran kuna bwana mmoja alikuwa anaitwa Walid bin Mughira huyu mzee Mughira alikuwa anapesa sana na kipindi hicho mtoto wa kiume mkubwa ndio alikuwa anarithi mali sasa huyu mzee Mughira jongoo lilikuwa halipandi mtungi mama yake Walid akapiga mahesabu akafikiria nani atarithi mali ya mzee Mughira ikabidi akazae nje ya ndoa ndio akapatikana Walid bin Mughira lakini kumbe walid sio mtoto wa mzee Mughira na hilo swala walid alikuwa halijui,walid alikuwa nimfanya biashara mkubwa sana pale Makka kwasababu alirithi mali ya mzee Mughira basi siku moja akawa anapita nje ya nyumba ya mtume Mohamad(s.a.w)anasoma suratul kalam akasikiliza ikafika sehemu mwenyezi mungu anamwambia mtume usimti mtu mwenye kuapa apa hovyo,mtu mwenye kujiona,mtu muongo ilipofika pale inaposema baada ya hayo yote mtu mwenyewe ni wa nje ya ndoa,baada ya yote Walid akiangalia sifa zote zilizo tajwa anazo ila hiyo moja ndio ikamtatiza,ikabidi amtafute mama yake amuulize Muhamad nimemsikia anasoma Quran sifazote alizozitaja ninazo ila moja tu ndio sijamuelewa mama yake akamuuliza ni ipi akamwambia amesema mimi mtoto wa nje ya ndoa mama yake akamwambiani kweli wala hajakosea akamueleza issue yote ilivyo kuwa ikabidi walid awe mpole, na ndio maana uislamu umepinga mtu kujinasibisha na baba ambae si wake ahsante tuendelee na munakash.cc Mohamed Said,Ritz Gombesugu,Big Show
 
JokaKuu!
Ninachofahamu mimi kutoka kwako ni kuwa unajaribu kuwaonyesha wana ukumbi hasara za Muungano kwa Watanganyika na athari zake mbaya ikiwemo ukwamishaji wa "maendeleo" ya Mtanganyika kama vile Kusini.

Umetuonyesha huko nyuma pia kuwa upo mstari wa mbele katika kuwazindusha Watanganyika kuhusu hasara wanazozipata kutokana na Muungano.Ulitufahamisha vilevile kuwa Watanganyika wamechelewa katika kuzidai haki zao zinazohodhiwa na Muungano.

Unaweza kutuelezea ni sababu zipi unafikiria zilimchelewesha Mtanganyika kuzinduka katika kudai haki yake?
Ni matumaini yangu kuwa kuelewa kwa Mtanganyika wapi alijikwaa kutakuja kumsaidia sana mbeleni.
*Si lazima JokaKuu yoyote anaweza kujimwaga na kutupatia tathmini yake.
 
na hayo maradhi lazima yatokomezwe, la sivyo yale ya Burundi na Rwanda au korea yatatufikia.

Nashukuru Zumbe; Sielewi mtu utakavyowadanganya wale wazee pale stendi Mlalo, au Bumbuli kuwa Nyerere hakuwa lolote katika kuikomboa nchi toka kwa wakoloni. Eti mkombozi wa kweli alikuwa mtu mwingine na huyo ndiye baba halisi wa taifa, ndiye aliyeunda TANU, nk. Labda vizazi vinavyokuja. Lakini kama ni wale wazee wa kisambaa wa kule Kwemakame, hawatakusikiliza. Ushahidi umesheni kuwa waliishi kama watanganyika na kila mtu na dini yake. Familia ni nyingi wazazi ni dini tofauti na watoto, kwa hii EFFORT ya DIVIDE AND MISRULE umefikia wakati wa kila mmoja kuwa mwangalifu sana. Siku zote wadanganyifu huwa wana maneno matamu. Ujinga walionao ni pale wanaposhindwa kujua kuwa zikianza risasi mtaani, hata binti/baba yake yatampata.
 
Zumbe mkuu, kuna watu walipinga ukoloni hadharani. Kuna kitu kinaitwa kodi ya Mbiru, wapare wanakifahamu sana ukisoma historia. Tena kiliwahi kuwa na tamthilia RTD nyakati hizo.
Hayo hayasemwi yanasemwa ya familia moja iliyokuja kuikomboaTanganyika.

Wickama, tena hao waliokuja kuikomboa Tanganyika ni hao hao walikuja na Wajerumani wapigane dhidi ya Watanganyika.
Leo tunaambiwa huko bara watu walikuwa wamelala usingizi wa pono, wakitafuna dodo na ng'ongo kama si kugigina vibanda meno na mahiza! Jamani.

Hizo pesa za matawi hazisemwi kwasababu ukizisema si Nyerere alikuwa katibu Tabora!! Sasa hapo utakuwa umeondoa maana nzima ya Nyerere kufundishwa siasa alipokuja Dar na kukutana na wakombozi.

Utakuwa umeondoa maana halisi ya Nyerere kuwa na mchango maana yeye aliletwa na wamishenari kufundisha, tena si mkatoliki?

Kwahiyo naomba msiongelee mambo ya matawi, mtatia maji katika wine! chonde chonde waungwana acheni ngano iumuke wanaomeza wameze.
 
Mbona kwangu inafunguka picha hiyo Nyerere na Ally Sykes mwaka 1958

Hata mimi kwangu haifunguki. Ila kuna notification kuwa THE ADMINISTRATOR MAY HAVE REMOVED THE CONTENT au kama hivyo. Huenda ndio censorship tena au watarekebisha, kwa vile wanauliza kama unadhani ni vyema!!!!
 

Jasusi,

Kwanza niliweka nia nikuwekee hapa ukukmbini watu wote kutoka Tanzania waliopitia Carleton University lakin nimepata ushauri toka kwa wengi nisiweke hapa lakin kama utapenda naweza nikaku PM wote uangalie kama Huyo Anna yupo.

Lakin unapoandika kitu hakikisha kuwa una yakini nacho kama mimi ninavyoyakinisha. Kumbuka kuwa enzi hizo ili mtu aende CHUO KIKUU ilimpasa kwanza amalize Form four na kisha aende form six na kisha apite JKT. au apitie Adult chances ambazo nina hakika yeye hajapita huko.Sa

Sasa hebu dadavua kidogo kuwa je aifanikiwa kupata maksi za kutosha kwenda form six. je alisoma skuli gani na JKT alipitia wapi kama huu msema kweli?

Nitakuongezea moja hapo yule mtoto wake uliyesema alikwenda Airforce China. Je unajua kuwa alikuwa form four akaenda kusomea kozi ya urubani ambazo colifications zake zilihitaji form six. Na wote aliokuwa nao walikuwa form six yeye pekee ndio alikuwa form four? Na alikuja baada e alishindwa masomo hayo. Je nae alipitishwa kinamna hiyo au ... Je nalo hili unalikataa?

Kwa kuwa najua mengi sana kwa sababu nilikuwa karibu na familia hiyo nilipokuwa Tz. napenda kukwambia Nyerere alipenda sana vijana wake wasome lakin ...

Nilichokubainishia hapa alipenda watoto wa wengine wapite njia sahihi yeye wake walipita njia za mkato japo wengi hawakufanikiwa kufika. Ndio maana tunasema hakuwa mwadilifu.

Kuhusu PhD yangu isikutie khofu kwani nimeipata kihalali kabisa toka Mtendeni skuli Dar, Tambaza, Ilboru, JKT Ruvu, UDSM(Tz). Carleton Univ(Can), Na Sofia Univ (Jpn).tafuta tu jina la Dr Hamza Yousuf Al-Naamaniy


Tuendelee na mnakasha kwani tutaingilia siri za ndani za familia hii ambazo si vizuri kuzianika hapa.

Pole sana


 


Nguruvi; Umegusa kitu sikuwahi kukiwaza hivi kama Julius Nyerere baba yake angekuwa kafika hapa nchini kama mamluki wa kijerumani kuja kuwatwanga wakina Kimweri kule Lushoto, kisha na huu Ukatoliki wake!!! Aiseeeeeeee, PANGECHIMBIKA Ndugu yangu
 
afanaleki, tena wale wazee ukiwaletea uongo kama huu wa MS walahi watakutemea mate yaliyojaa ugoro mdomoni,
 
Too late Mohamed, hoja iliyokuwepo mbele yetu ni kuwa Nyerere kwa ''udhalimu'' wake alimfukuza Sheikh Amir bila sababu. Ukaenda mbele na kumhusisha na EAMWS pale tulipouliza inawezekanaje Nyerere aamke asubuhi na kumchukia mtu aliyefanya naye kazi miaka mingi. Hakuna maelezo mengine zaidi ya kusema ukataili wa mwalimu dhidi ya wazee wako.

Leo unataka kueleza kisa baada ya kujulikana kuwa Sheikh alikuwa Msaliti.
Labda tuanzie na kwanini alikataa nafasi alizopewa na kwanini alijificha na kuendeleza siasa za pembeni.

Kuhusu Sheikh Amir kuwa Walii hilo halina tabu kama wapo walioamua kumpa hishma hiyo.
Lakini pia kuna jambo hapa, sasa kama alipewa hishma hiyo na wafuasi wake kwa taratibu za imani yao, Iweje basi wawepo watu wa kuhoji u-saint wa Nyerere anaotaka kupewa na watu wa imani yake?
Hakuna double standard kwa mtazamo wa haraka tu.

Mwisho, Sheikh kuitwa mnafiki na msaliti si tusi, kama lingekuwa tusi linalowaumiza basi msingezunguka duniani mkimsema Nyerere kuhusu viarago na pesa za vitoweo.

Kama lingekuwa linaumiza basi msingemvunjia hishma kwa kusema Laanatullah kila anapotajwa, wala asingeitwa habithi, baradhuli, mnafiki n.k.

Kwanini udhani kuwa sheik Amir anastahili hishma kuliko Nyerere wote wakiwa wanadamu, wazee na familia zao?

Hapa ndipo nasema kila siku lazima watu waangalie nyuma, pembeni na mbele.
Kurushia watu mawe ukiwa katika nyumba ya glasi si jambo jema.

Kila mzee wetu aliyepigania nchi hii na apewe heshima.
Tuache uchochezi usio na maarifa

Hii inaitwa fitna al maarifa kama anavyosema ndugu yangu Gombesugu.
Tuache haya tuangalie jamii inakwenda wapi, inahitaji nini, tufanye nini kwa pamoja na si kwa chuki na kubaguana.
 
Nguruvi; Umegusa kitu sikuwahi kukiwaza hivi kama Julius Nyerere baba yake angekuwa kafika hapa nchini kama mamluki wa kijerumani kuja kuwatwanga wakina Kimweri kule Lushoto, kisha na huu Ukatoliki wake!!! Aiseeeeeeee, PANGECHIMBIKA Ndugu yangu
Kimweri alimzuia nyerere na timu yake kupanda milima ya Lushoto akidhani ni mamluki wa wakolini, wake zake kimweri ndo walienda kuondoa mawe bara barani ili nyerere aweze kupita.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…