Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Mag3,

Kwa hiyo wewe upo hapa kama mpiga debe wa familia ya Nyerere?

Idd Faiz Mafongo,

Siyo mweka hazina tu unajifanya unajua historia wakati hujui kazi alizokuwa anazifanya Mzee Faiz Mafongo ngoja nikupe darsa kidogo kuhusu huyu mzee unayemponda.

Huyu pamoja kuwa mweka hazina wa TANU vilevile aliifanyia kampeni TANU, akifuatana na Nyerere katika safari za awali za kukitangaza chama, akihutubia mikutanoni jukwaa moja na Nyerere. Na yeye na kaka yake Idd Tosiri ndiyo waliompeleka Nyerere kwa binamu yao Sheikh Mohamed Ramia wa Bagamoyo.

Idd Faiz alikwenda mpaka Tanga kutafuta pesa za kuongezea safari ya Nyerere kwenda UNO.

Mlivyokuwa na dharau mnaropoka tu ovyo eti mweka hazina nani atamuenzi.

Hayo maswali yako hayana tija unauliza ili ujifunze.

Ritz linapokuja suala la kuwataja viongozi waliopigania uhuru wetu, huwezi kuwataja watu wote walioshiriki kwa ujua wao, mara nyingi hutajwa mtu aliyekua kiongozi wa harakati hizo. hii haina maana kuwa wengine walokuwa nae bega kwa bega wamesahaulika. ona jinsi anavyo enziwa Nelson Mandela kama mpigania uhuru A kusin, inamaana hakuwa na watu walio kuwa naye katika kusaka uhuru? mbona hawatajwi? Arafat wa palestina hutajwa yeye peke yake kama vile hakuwa na wapambanaji wengine. wapo na wengine wengi sana tu ambao hutajwa peke yao mf: Jomo kenyata, lumumba na wengine. angalia raisi kikwete anapokuwa katika ziara mbalimbali hutajwa yeye peke yake kuwa ndie kasema hiki na kile hata kama hotuba kaandaliwa na mwingine. hivyo suala la kwanini huyu kasahaulika ktkt historia sio la msingi.
 
Last edited by a moderator:
Hate is taught, Love comes naturally.

Mzee Said, ninatatizwa sana na mitazamo hasi, mitazamo ya 'wao' na 'sisi'.

What kind of future do you see in Tanzania?
Hilo ni swali langu moja na nitaendelea kukuuliza swali hilo kila nipatapo nafasi, likiwa na sehemu tofauti tofauti.

Wakati unanijibu, uwe unajiuliza, what difference have you made to the youth of this nation that inspire the future you want to see. Nitakuwa nakukumbusha hili.

You must be the change you wish to see in the world.
-Gandhi

I'd rather live with a good question than a bad answer.
-Aryeh Frimer

Hilo swali umelielekeza sipo.

Sisi Waislam tumeilalamikia serikali siku nyingi kuhusu dhulma.
Serikali imetupuuza.

Hapa nilipo nipo katika juhudi ya kueleza tulikotoka na nini kilipitika
hadi tumefika hapa.

Kitu cha kufanya ni kwa serikali ikatoka ilikojificha ikakubali ukweli
kuwa tuna tatizo.

Baada ya hapo tuzungumze na kusafiana nia.
 
Bila ya kukusimulia ungenijuaje?

Hebu soma hii kutoka katika kitabu changu:

[TABLE="class: MsoNormalTable"]
[TR]
[TD] In 1954, risking his job as Market Master, little did Abdulwahid realise that a time would come when the history of the struggle would be written and his name would not be associated with that important period in the history of Tanganyika as a nation.

One can also speculate what would have been the role of Nyerere in the politics of Tanganyika if Chief Kidaha had accepted TAA’s proposal to become president of the Association in 1951; or what would have been the future of Tanganyika if Abdulwahid and the TAA inner circle had accepted Ivor Bayldon’s proposal to form a multiracial political party.

This was an obvious ploy contrived by the government to co-opt the nationalists and hence compromise their stand for majority rule.

What the government was seeking was to incorporate the TAA leadership with the traditional authorities in the Legislative Council and form what could be wrongly perceived as true representative body of authority with the Governor at the top.

This would have nipped in the bud the struggle for majority rule for the Africans of Tanganyika.

[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 601"] With such an hypothetical set up, would Nyerere had been able to form a political party of his own, either within the framework of the TAA or from any other base? Would his party build its power base first from the peasantry in his home area in Musoma, or could he have ventured to build his base from Dar es Salaam with the same Muslim support he was able to get in TANU through his acquaintance with the townsmen? [/TD]
[/TR]
[/TABLE]

Nikweli umesimulia, lakini hujawa msaada kwangu kwa mengi, msaada wako kwangu umekuwa ni 0.01% katika yale niyajuayo,

Ninaamimi katika simulizi za wazee wako wa kariakoo unaijua kwa 100% kabisa, lakini HISTORIA ya ukombozi wa nchi hii huijui, na unahitaji msaada mkubwa sana ikiwa mwili na akili yako bado vitakuwa na ushirikiano mzuri!

Karibu tujifunze histori ya nchi, sio ya wazee wako wale WALIOASI baada ya uhuru na wakakumbana na ghadhabu ya watanzania chini Mtakatifu Julius Nyerere!
 
Bila ya kukusimulia ungenijuaje?

Hebu soma hii kutoka katika kitabu changu:

[TABLE="class: MsoNormalTable"]
[TR]
[TD] In 1954, risking his job as Market Master, little did Abdulwahid realise that a time would come when the history of the struggle would be written and his name would not be associated with that important period in the history of Tanganyika as a nation.

One can also speculate what would have been the role of Nyerere in the politics of Tanganyika if Chief Kidaha had accepted TAA's proposal to become president of the Association in 1951; or what would have been the future of Tanganyika if Abdulwahid and the TAA inner circle had accepted Ivor Bayldon's proposal to form a multiracial political party.

This was an obvious ploy contrived by the government to co-opt the nationalists and hence compromise their stand for majority rule.

What the government was seeking was to incorporate the TAA leadership with the traditional authorities in the Legislative Council and form what could be wrongly perceived as true representative body of authority with the Governor at the top.

This would have nipped in the bud the struggle for majority rule for the Africans of Tanganyika.
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 601"] With such an hypothetical set up, would Nyerere had been able to form a political party of his own, either within the framework of the TAA or from any other base? Would his party build its power base first from the peasantry in his home area in Musoma, or could he have ventured to build his base from Dar es Salaam with the same Muslim support he was able to get in TANU through his acquaintance with the townsmen? [/TD]
[/TR]
[/TABLE]
Mohamed,
You and I know that a multiracial political party in those days and circumstances would not have gotten anywhere. UTP anyone? Usidharau moto ulioanzishwa na TANU bwana. Muulize Zuberi Mtemvu alipata kura ngapi 1959. Hamna cha kuspeculate hata kidogo.
 
La hasha mkuu wangu wala sijadhani umeforge; nina maana ulichosema hapo juu ni kana kwamba nakala za hizo documents ndio umetuwekea kumbe ni vichwa vya habari tu. Kama wewe unazo na zinaweza kupatikana kutoka kwako itakuwa vizuri tu na rahisi zaidi... jitihadi utupatie tunatanguliza shukrani.

Unayo hotuba ya Nyerere kuaga mwaka 1985?

Wala usihangaike kunikumbusha.
Hivi shida yote hiyo inikute kwa kutaka nini?

Nimekuelekeza nenda kwanza MNF niliwapa zote tena
miaka mingi sana iliyopita.
 
Nguruvi3,

Wewe unaponda maandishi ya Mohamed Said na kuyaita ngano yako kwako sijui tuyaitaje.

Unasema udini ulikuwepo toka kabla ya uhuru sijui umeipata wapi wewe na Nyerere sijui tumuamini nani.

Pitia tena hotuba ya Nyerere anavyowaelezea wazee wa Dar es Salaam wakati wa TANU na harakati za kupigania uhuru.

Nyerere mwenyewe anakiri fadhira za Wazee wa Dar es Salaam kuna kipindi anasema alikuwa Mkiristu peke yake lakini wanamtendea wema wewe leo unasema walikuwa wadini.

Angalia hizo picha wazee walivyokuwa na mahaba na Nyerere.
Ritz, mimi hata siku moja sikuwahi kusema wazee wetu walikuwa wadini. Kinyume chake nimekuwa natetea kuwa hawakuwa wadini ndio maana waliweza kufanya kazi across the board. Nimetolea mifano ya akina Sykes, Mshume, Rupia, Lugazia Kyaruzi, Kawawa, Chaurembo, Yufu Ngozi n.k. na mara zote nimesema wazee wetu tunawashukuru, sio tunawapongeza tu bali tunawashukuru sana!

Aliyeonyesha kuwa kulikuwa na udini ni Mohamed Said. Mohamed anasema miaka 1950 kulikuwa na radical moslems kwa maneno yake, waliotaka kumuondoa Nyerere katika uongozi wa chama kwasababu ya ukristu wake.
Tafadhali sana naomba uelewe ni Mohamed Said siyo maneno yangu.

Mohamed akaeleze kisa cha kuundwa kwa AMNUT na radicals.
Mohamed akasema kuwa bila Abdul Sykes Nyerere asingeweza kufanikiwa kwasababu kwa nyakati hizo mkristo hakukubalika. Hayo si maneno yangu ni ya Mohamed yakishadidia kuwa Mohamed aliona suala la udini kuanzia nyuma.

Hata pale ilipothibitika kuwa Kyaruzi na Mtamila waliwahi kuwa viongozi ndani ya jiji la Dar badio Mohamed ameshikilia kuwa Nyerere asingeweza kufanikiwa. Hii maana yake ni kuwa kulikuwa na udini kwa mtazamo wake

Kwa muktadha huo na ushahidi wa maneno ya Mohamed nasimama kusema kuwa Mohamed anajua udini ulikuwepo kuanzia zama hizo kwahiyo si haki kusema udini uliletwa na Nyerere.

Sijatuhumu wazee wetu, ninachofanya ni analysis ya maneno ya Mohamed na jinsi anavyo skew information.
Matokeo ya spinning ni kuwanyooshea kidole wale anaowatetea.

Mimi nimeandika kuanzia mwaka 2011 katika minakasha kuhusu maneno ya Nyerere alivyokiri.
Hata katika uzi huu nimeandika hayo kama unanisoma vizuri.
Post iliyopita nimesema kuwa Nyerere amekiri katika kitabu chake ''we must run..'' kwa kuwataja wazee.

Mimi ni miongoni mwa watu waliokariri maneno ya Nyerere hata kabla kipande hakijawekwa.
Nimekuwa napinga dhana kuwa Nyerere aliwadharau wazee hawa na nimepinga dhana kuwa wazee walimdharau yeye.
Kwahiyo hapo unafanya spinning ku-discredit maandishi yangu lakini wasomaji wananielewa nasimamia nini.

Narudia, anayejenga dhana ya wazee hawa kuwa wadini ni Mohamed Said Abdallah Salum muyukwa Samtungo.
Siyo Nguruvi3 au Nyerere. Msome Mohamed vizuri.

Ama hili la kuita ngano, hilo ninabaki nalo kwasababu kila mtu ana mtazamo wake kuhusu maandishi ya Mohamed.
Wapo wanaomeza na wapo wanaofikiri. Inategemea mtu yupo upande gani wa mtazamo.

Lakini Ritz, hivi kama si ngano wewe ulijua kuwa shirika la dini la Maknol liliwahi kutoa ticket kwa Nyerere kusafiri kwenda UNO? Mbona hilo halisemwi na Mo? Hivi unajua kanisa lilishiriki vipi kuua EAMWS? unalo jibu wewe! maana Mo hana.

Ritz, Mo anasema Nyerere alikuja Dar 1952 ukweli si huo, je hiyo si ngano?
Ninabaki kusema kuwa Mohamed ameandika ngano hii kwa kutumia majina ya watu, nyakati na matukio ambayo ni ya kweli akiwa na lengo lake lililo nje ya ukweli uliokusudiwa bali aliokusudia ili kujenga mazingira anayotaka.
Kwa mintaarafu hiyo nasoama kitabu chake tofauti na wewe, kama unaona ni maandiko matakatifu hilo ni juu yako.
Mimi naona ngano! Nitty gritty!
 
fatilien history msipelekwe pelekwe abdulwahid sykes mwaka 1948 alikua katbu wa chama cha wafanyakaz bandarin wakat huo nyerere dsm anaickia tu nyerere kaletwa kwa abdul na kasela bantu kwa kimemo pia hcho chama cha taa kimeanzshwa na baba yke abdulwahd sykes nyumban kwao jiulize taa imeanzshwa mwaka 1929 Nyerere kaingia mwaka 1953
Mbona na wewe unageuka kuwa copy and paste?
 
Mohamed,
You and I know that a multiracial political party in those days and circumstances would not have gotten anywhere. UTP anyone? Usidharau moto ulioanzishwa na TANU bwana. Muulize Zuberi Mtemvu alipata kura ngapi 1959. Hamna cha kuspeculate hata kidogo.

Jasusi,

Nilikusudia khasa ni hili.
Nyerere angeweza kuanzisha TANU Musoma?
 
Halafu wanatokea watu kama Mag3 wanataka kutia mchanga kitumbua chake, hata usingizi hawezi kuupata! Kitu ambacho yeye Mohamed Said na "cheerleader" wake (nimeona wakiitana waje kuokoa jahazi) wanashindwa kukitambua ni jinsi huu uzi unavyozidi kumuumbua na kumwacha uchi...sasa yeye mzee wa watu badala ya kuchutama anazidi tu kujifunua, duh! Tofauti na Mwanakijiji na wenine, mimi naziita hizi simulizi zake kwa jina lake, ngano...sifichi msimamo wangu.

Narudia maswali yangu na sasa nimeongeza la nane;

  1. Abdulwahid Sykes aliingia kwenye uongozi wa AA mwaka gani kwa mara ya kwanza na kwa wadhifa gani?
  2. Je mwaka 1946, Mwalimu Nyerere alipohudhuria mkutano wa AA Dar es Salaam kama katibu wa tawi la Tabora, Abdulwahid alikuwa na nafasi gani ndani ya AA?
  3. Je, Abdulwahid Sykes alihudhuria huo mkutano uliofanyika mwaka 1946 Dar es Salaam na kwa wadhifa upi ndani ya AA?
  4. Je, Abdulwahid Sykes kama alihudhuria, kwa nini idaiwe ni mwaka saba baadaye, 1953, ndio kakutana na Nyerere kwa mara ya kwanza?
  5. Je, kama mwaka 1946, Abdulwahid Sykes hakuwa na sifa wala wadhifa wa kuhudhuria huo mkutano wa AA, nani kati yake na kaka yake Mwalimu Nyerere alitangulia kwenye siasa?
  6. Je si kweli kuwa Dr. Kyaruzi, aliyefahamiana na Mwalimu Nyerere toka Makerere, ndiye aliongoza mapinduzi ndani ya AA mwaka 1950 na yeye kuchaguliwa Raisi wa kwanza wa TAA?
  7. Mkutano wa kwanza wa kuizindua AA mwaka 1929, ulifanyika nyumbani kwa nani na chini ya uongozi wa nani?
  8. Kwa nini hasa AA ilianzishwa mwaka 1929...je hiyo AA iliihusu Tanganyika peke yake? Ni wakati gani ilibidi ibadilike na kuitwa TAA na kwa sababu gani?
Nitatoa hapa nukuu kidogo kutoka kitabu cha Sanderson Beck, "Tanganyika and the British 1918-1950".


Ninchotaka kusema hapa ni kwamba Watanganyika Weusi walibaguliwa kwa rangi yao na si dini na hivyo mwamko ukawa ni kudai usawa na haki. Huu mwamko kama mnavyoona ulichelewa sana kuanza Dar es Salaam...sasa kama huu mwamko ndio udaiwe kuwa msingi wa harakati za uhuru, basi ni miaka mingi kabla ya kuzaliwa AA ya Cecil Matola akishirikiana na wazee wa Mohamed ambao kwa muono wake ni Manyema na Wazulu, wa Gerezani na Waislaam. Lakini kama tunaongelea chama kilichoasisiwa rasmi kudai uhuru na kutambulika kama chama cha siasa, ni TANU iliyozaliwa tarehe 7, Julai 1954 ikiongozwa na Mwalimu Julius Nyerere.

Kwa nini nasema hivi? Yako madai ya kipuuzi yanayoletwa na Mohamed Said kwamba AA ndiyo msingi wa kupatikana kwa uhuru nchini. Kwa nini tusianzia mwaka 1922? mwaka 1923? mwaka 1925? au mwaka 1927? Mbona tayari vyama vya kupigania maslahi ya Watanganyika vilikuwepo sehamu nyingi tu ya Tanzania hata kabla ya AA. Je ni kwa sababu mababu zake Mohamed Said walishiriki kuanzisha AA mwaka 1929 ndio wawe vinara wa harakati hizo? Mimi namtaka Mohamed Said ajibu hayo maswali yangu kwanza ili wanajamvi waweze kutambua uwongo, ghilba, chuki, uchochezi...vilivyotawala maandishi yake.

Turudi kidogo nyuma wakati wa Mjerumani...Wazulu na Manyema wanaingiaje hapa? Hebu someni hii;


Na hii pia;



Je yawezekana miaka hiyo ya nyuma hataji Mohamed Said kwa sababu mababu zake walikuwa upande wa Mkoloni Mjerumani? Jamani tumetoka mbali, tusizikubali hizi ngano za kichochezi anazoleta Mohamed katika mission yake ya kupandikiza chuki za kidini, ili iweje? Kutusambaratisha?

Tukiziita "Ngano" za Sanderson Beck nadhani tutakuwa sahihi.
 
Mbona na wewe unageuka kuwa copy and paste?

Bila ya cut and paste mengi yasingepatikana humu ukumbini.

Hebu angalia hii:

[TABLE="class: MsoNormalTable"]
[TR]
[TD] When Abdulwahid died the Ministry of Information issued a press release announcing that the President had attended the funeral of Abdulwahid Sykes.[1]

Surprisingly the press release gave few details of his government service, completely eclipsing his checkered political career.

It was an Englishman, Brendon Grimshaw, the editor of Tanganyika Standard, who published a fitting obituary to Abdulwahid describing him as: 'one of the architects of the independence movement and one of the men who helped launch President Nyerere on his political carrier...'

[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 601"] The obituary also paid glowing tribute to the family on its contribution to the political development of Tanganyika by mentioning that ‘much of the desire among Africans for a powerful political party in Tanzania came from the drive of the Sykes family'. [2]

It is said that this recognition of Abdulwahid as one of the founding fathers of the nation became a focus of attack from certain members of the TANU leadership.

They were overheard grumbling in the corridors of the TANU headquarters in Dar es Salaam that Ally and Abbas Sykes were trying to glorify their elder brother.

[/TD]
[/TR]
[/TABLE]


[1]See Press Release A/2746/68 IT/1.322 of 13 th October, 1968. East Africana, University of Dar es Salaam.
[2]Sunday News, 20 th October, 1968.
 
Hilo swali umelielekeza sipo.

Sisi Waislam tumeilalamikia serikali siku nyingi kuhusu dhulma.
Serikali imetupuuza.

Hapa nilipo nipo katika juhudi ya kueleza tulikotoka na nini kilipitika
hadi tumefika hapa.

Kitu cha kufanya ni kwa serikali ikatoka ilikojificha ikakubali ukweli
kuwa tuna tatizo.

Baada ya hapo tuzungumze na kusafiana nia.

Kwa bahati mbaya sijauliza 'nyie wIslamu'.
Nimesema ninatatizwa sana na maelezo na mijadala ya 'wao' na 'sisi'.

Nimeanza kwa kusema Mzee Said, nikaendelea kwenye swali langu.
Lakini pia, wewe sio 'waislam' wewe ni Mzee Said ninayekuuliza swali hapa. Na ninataka kujua elimu yako na 'uhanaharakati' wako unawaweka wapi vijana wa Tanzania katika utu uzima na uzee wao.

Sijataka mawazo ya waislamu. Nikitaka nitapiga simu radio Iman au radio kheri.
Nimetaka mawazo yako kama mzee, mtanzania. Sio mwislam wala mwislam wa bara wala wa pwani.

Tafadhali sana.
Kama huwezi kujibu barazani kwasabau yoyoyte ile, nijibu hata kwa PM. Nitasema nimejibiwa, na nitashukuru.
 
Jasusi,

Nilikusudia khasa ni hili.
Nyerere angeweza kuanzisha TANU Musoma?
Kwa Musoma hapana. Nitakupa sababu zake. Nyerere alikuwa nationalist. Labda enzi hizo tumwite territorial. Aliiangalia Tanganyika si kwa macho ya Umusoma, au Gerezani kama unavyofanya. Na nahisi hiyo ndiyo tofauti kubwa kati yako na Nyerere kwa sababu yeye aliiona Tanzania kwa umoja wake wakati wewe uliiangalia zaidi kupitia macho ya Gerezani.Hata ukiangalia juhudi alizofanya akiwa Makerere alijikita zaidi kushirikiana na wenzake kutafuta chombo cha kuikomboa Tanganyika. Sasa, kama Musoma ingekuwa ndiyo makao makuu ya Tanganyika, then that would have been another issue. Sijui umenielewa?
 
Tukiziita "Ngano" za Sanderson Beck nadhani tutakuwa sahihi.

[TABLE="class: MsoNormalTable"]
[TR]
[TD] When Abdulwahid died the Ministry of Information issued a press release announcing that the President had attended the funeral of Abdulwahid Sykes.[1]

Surprisingly the press release gave few details of his government service, completely eclipsing his checkered political career. It was an Englishman, Brendon Grimshaw, the editor of Tanganyika Standard, who published a fitting obituary to Abdulwahid describing him as: ‘one of the architects of the independence movement and one of the men who helped launch President Nyerere on his political carrier...'
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 601"] The obituary also paid glowing tribute to the family on its contribution to the political development of Tanganyika by mentioning that ‘much of the desire among Africans for a powerful political party in Tanzania came from the drive of the Sykes family'. [2]

It is said that this recognition of Abdulwahid as one of the founding fathers of the nation became a focus of attack from certain members of the TANU leadership.

They were overheard grumbling in the corridors of the TANU headquarters in Dar es Salaam that Ally and Abbas Sykes were trying to glorify their elder brother.
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]


[1]See Press Release A/2746/68 IT/1.322 of 13 th October, 1968. East Africana, University
of Dar es Salaam.


[2]Sunday News, 20 th October, 1968.
 
Kwa Musoma hapana. Nitakuwa sababu zake. Nyerere alikuwa nationalist. Labda enzi hizo tumwite territorial. Aliiangalia Tanganyika si kwa macho ya Umusoma, au Gerezani kama inavyofanya. Na nahisi hiyo ndiyo tofauti kubwa kati yako na Nyerere kwa sababu yeye aliiona Tanzania kwa umoja wake wakati wewe uliiangalia zaidi kupitia macho ya Gerezani.Hata ukiangalia juhudi alizofanya akiwa Makerere alijikita zaidi kushirikiana na wenzake kutafuta chombo cha kuikomboa Tanganyika. Sasa, kama Musoma ingekuwa ndiyo makao makuu ya Tanganyika, then that would have been another issue. Sijui umenielewa?

Sana nimekuelewa.

Je bila ya ''inner circle'' ya TAA na viongozi wa Dar es Salaam angeweza kupata
watu wa kumuunga mkono?

Nani angelimjulisha wa Sheikh Hassan bin Amir?
 
Jasusi, Nilikusudia khasa ni hili.
Nyerere angeweza kuanzisha TANU Musoma?
Exactly! Angekuwa mdini angefanya exactly that. Lakini tukiacha hii dhihaka yako kwa watu wa Musoma (niliwahi kukuonya kuhusu dhihaka kama hizi!), na mimi nikuulize, ilikuwaje wazee wako wa Dar es Salaam wampe usukani mtu wa Musoma? Kwami akina Abdulwahid Sykes, Dossa Aziz, Abdallah Salum muyukwa Samtungo hawakuwepo? Hivi hata kwa akili ya kawaida hujui kuwa Dar es Salaam ilikuwa ndiyo maao makuu ya utawala wa kikoloni? Nafikiri swala zuri zaidi ni hili, je, kwa kiwango gani TANU ingefanikiwa kama haingeungwa mkono na watu si wa Musoma tu bali Kilimajaro, Mwanza, Bukoba, Mbeya, Rungwe, Iringa na sehemu zote za Tanganyika? Je unajua kwamba katika muda mfupi zaidi ya asilimia 60% ya wanachama wa mwanzo wa TANU walitoka mikoa ya Ziwa?

Hilo moja lakini la pili, unayo habari kuwa kabla ya uhuru (1961) wengi wa wazee wako waliokuwa wanachama wa TANU walijiengua na kujiunga AMNUT? Unajua kuwa kama ingekuwa ni mapenzi na maamuzi ya wazee wako tusingepata uhuru tarehe 9 Desemba 1961? Unaona unavyojaribu kupotosha mambo kwa makusudio ya kupanda, kupalilia na kujenga chuki za kidini kwa sababu tu baba zako wa Gerezani walidhani uhuru ukipatikana basi kila moja atakuwa na wadhifa kama wa Raisi wa nchi. Tazama unavyomjenga Abdulwahid Sykes...kamfundisha Nyerere kuvaa, kamfundisha kuongea kiswahili, kamfundisha siasa, kampa uenyekiti wa TANU, kamwandikia hata hotuba...duh, yaani hata kama ni matusi, aibu huna?
 
nikweli umesimulia, lakini hujawa msaada kwangu kwa mengi, msaada wako kwangu umekuwa ni 0.01% katika yale niyajuayo,

ninaamimi katika simulizi za wazee wako wa kariakoo unaijua kwa 100% kabisa, lakini historia ya ukombozi wa nchi hii huijui, na unahitaji msaada mkubwa sana ikiwa mwili na akili yako bado vitakuwa na ushirikiano mzuri!

Karibu tujifunze histori ya nchi, sio ya wazee wako wale walioasi baada ya uhuru na wakakumbana na ghadhabu ya watanzania chini mtakatifu julius nyerere!
mfa maji siku zote haishi kutapa tapa,eti yericko nae anatamba sasa kumtambia moh said aende kwake kujifunza historia?historia gani sasa,umeambiwa andika basi kitabu umekosa cha kujibu,,
yaan yericko kadir muda unavozid kwenda ndivo unavozid kuonekana kwako kuwa wewe si lolote si chochote,hufaham lolote na ni kama debe tupu unaetegemea back up zisizo na tija,

ona sasa umeamua kumvisha kambarage julius utakatifu..!what a shame...!
Kambarage utakatifu autolee wapi??si huyu huyu kambarage aliezusha ya kwamba idd amini ni nduli mla nyama za watu?au mwingine si huyu??
Mmeishiwa nguvu kabisa..
 
Sana nimekuelewa.

Je bila ya ''inner circle'' ya TAA na viongozi wa Dar es Salaam angeweza kupata
watu wa kumuunga mkono?

Nani angelimjulisha wa Sheikh Hassan bin Amir?
Hakuna anayebisha juu ya "inner circle." Hata kabla hujaandika kitabu chako nilishasoma kitabu cha Judith Listowell nilipokuwa Aga Khan 1967. Ndio maana nilithamini sana uhusiano wangu na mzee Abdulwahid kwa sababu huyu nilishamsoma mchango wake. Wewe, kitabu chako, ambacho pia nimekisoma, kingekuwa na maana zaidi kwa kila Mtanzania, kama ungeelezea tu mchango wa wazee wa Gerezani bila kuingiza mambo ya udini na bila kushusha au kubeza mchango wa Mwalimu Nyerere. Nadhani wote tulio upande huu wanakubaliana na mimi kwa hilo. Lakini kwa zoezi hili unatugawa, ninyi waislamu, na sisi wakristo. Hivi utajisikiaje nikikwambia kuwa baba yangu mdogo, Suleiman Mukama, alikuwa ni muislamu, mfuasi wa Zuberi Mtemvu na mpaka anaenda kaburini hakutaka kusikia habari za TANU na Nyerere? Lakini akija nyumbani, tunaweka siasa pembeni tunaweka mbele damu yetu. Hii ndiyo Tanzania niliyokulia.
 
ungekuwa unaijua historia ya nchi hii
wala usingepata tabu ya kuandika utumbo humu jamvini
Wala usingehangaika kutafuta hotuba ya 1985 leo hii
Huna unachokijua zaidi ya kuleta uongo hapa jamvini
Kwa kweli umejifunza mengi kwa Mohamed Said
ukiangalia maandishi yako hilo lipo wazi
Huna chochote cha maana ulichoeleza kuhusu historia ya tanganyika
Umeshindwa wewe na wenzio kutuelezea hiyo historia ya 'kweli' ya tanganyika
badala yake mna kejeli na kuleta dharau juu ya kitabu cha Mohamed Said
USISAHAU KUANGALIA HAPO CHINI KWENYE RED


Nikweli umesimulia, lakini hujawa msaada kwangu kwa mengi, msaada wako kwangu umekuwa ni 0.01% katika yale niyajuayo,

Ninaamimi katika simulizi za wazee wako wa kariakoo unaijua kwa 100% kabisa, lakini HISTORIA ya ukombozi wa nchi hii huijui, na unahitaji msaada mkubwa sana ikiwa mwili na akili yako bado vitakuwa na ushirikiano mzuri!

Karibu tujifunze histori ya nchi, sio ya wazee wako wale WALIOASI baada ya uhuru na wakakumbana na ghadhabu ya watanzania chini Mtakatifu Julius Nyerere!
 
Last edited by a moderator:
Ritz linapokuja suala la kuwataja viongozi waliopigania uhuru wetu, huwezi kuwataja watu wote walioshiriki kwa ujua wao, mara nyingi hutajwa mtu aliyekua kiongozi wa harakati hizo. hii haina maana kuwa wengine walokuwa nae bega kwa bega wamesahaulika. ona jinsi anavyo enziwa Nelson Mandela kama mpigania uhuru A kusin, inamaana hakuwa na watu walio kuwa naye katika kusaka uhuru? mbona hawatajwi? Arafat wa palestina hutajwa yeye peke yake kama vile hakuwa na wapambanaji wengine. wapo na wengine wengi sana tu ambao hutajwa peke yao mf: Jomo kenyata, lumumba na wengine. angalia raisi kikwete anapokuwa katika ziara mbalimbali hutajwa yeye peke yake kuwa ndie kasema hiki na kile hata kama hotuba kaandaliwa na mwingine. hivyo suala la kwanini huyu kasahaulika ktkt historia sio la msingi.

satelite,

Ni kweli unachosema huwezi kuwataja wote lakini kuna wale muhimu lazima watajwe wewe nikikuuliza hebu nitajie wanachama 20 wa mwanzo wa TANU huwajuhi. Lakini wa Chadema au CUF unawajua.

ANC ya kina Mandela wapingania uhuru wao mbona wanajulikana na wameandikwa kwenye historia ya yao.

Walioanzisha ANC ni watu watatu ni John Dude, Pixley ka Isaka Seme, Sol Plaatie, mwaka 1912 wakati Nelson Mandela kazaliwa mwaka 1918 historia ipo wazi Mandela kaingia ANC na vijana wenzake wakati ule kina Olive Tambo.

Bahati mbaya kwetu kila kitu kafanya Nyerere wote tunaambiwa walikuwa wasaidizi wake.
 
Last edited by a moderator:
JK,

Ikiwa Maryknoll waliunga mkono harakati za kudai uhuru wa Tanganyika sawa hakuna mtu wa kupinga hilo.

Hakuna mwenye haki ya kukataa hilo.

Mie kwa kutambua hilo la yaliyojificha ndipo nikaandika kitabu.

WR Duggan na JR
Civille wameandika kitabu ''Tanzania and Nyerere,'' Maryknoll New York, Orbis Book, 1976. Atakae na asome hicho kitabu wala mimi sina haja ya kusema mengi.

Kitabu hiki kimo katika bibliografia yangu.
Nimekisoma chote.

Kitabu hiki kipo Maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.


Huo mchango wa Maryknoll unaozungumzwa hapa ukumbini umo humo.
Atakae ende akausome humo.

Lakini anaetaka kujua khasa waliochangia narudia tena waliochangia uhuru wa Tanganyika watake wasitake lazima wasome kitabu changu.

Wala si suala la udini.
Haiwezekani kutaja mchango wa Mufti Sheikh Hassan bin Amir ukaacha kutaja wanatarika wa Qaudiriyya.

Huu ndiyo ukweli wenyewe hata kama unauma.



Mohamed,
Tatizo si nani aliyechangia uhuru wa Tanzania. Tumekusoma na tumekuelewa. Tatizo ni pale unapotaka kuunganisha kuwa nyuma kwa Waislamu katika elimu na Nyerere. Tumekubaliana sote kwamba wakati tunapata uhuru wakristo walikuwa mbele katika elimu kuliko Waislamu. Hilo halina ubishi. Pia tumeona, ingawa si katika maandishi yako, kwamba Mwalimu Nyerere alitambua tatizo hilo na kuchukua hatua kwa kutaifisha shule za wamisheni ili watanzania wote wasome bila kubaguliwa dini zao. Lakini hilo sijaona popote una acknowledge. Unaendelea zaidi kuwa kwa kupiga EAMWS marufuku Nyerere alirudisha nyuma elimu ya waislamu. Kwa hiyo tatizo si nani alichangia juhudi za uhuru. Tatizo ni hizi propaganda zako kuwa leo waislamu wako nyuma kwa sababu ya Nyerere. Hapo ndipo tunapopingana. We seem to be barking at the wrong tree. Nyerere has been dead 14 years now. Has been out of power almost 30 years. Je, mbali na Kikwete kupromote mahakimu waislamu wasio na elimu ya kutosha, kumechukuliwa hatua gani kuwasaidia Waislamu wajiendeleze katika elimu? What is the end game?
 
Back
Top Bottom