BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,165
Huo ni mwanzo tu wa kuporomoka kwa uchumi kama hakutakuwa na maamuzi muafaka ya kuondoa sheria kandamizi dhidi ya Wakulima, Wafanyabishara na Wafanyakazi basi anguko la uchumi litaendelea kwa kasi ya kutisha.
Hayo yamefichuka leo baada ya hotuba ya Mh Rais Samia Suluhu alipokuwa anawahutubia Wafanyakazi wa Tanzania kwenye kilele cha siku ya wafanyakazi Duniani
Ameitaja Corona kama sababu kubwa ya kuanguka kwa uchumi wa Nchi yetu , ambapo amewaomba wafanyakazi kuvumilia hadi mwakani ili kuongezwa mshahara baada ya Uchumi wa nchi kuporomoka kutoka 6.9% hadi 4.7%
Ikumbukwe kwamba kwa miaka mingi viongozi wa Tanzania wakiwemo Rais wa zamani pamoja na Mawaziri kadhaa mmojawapo akiwa Mwigulu Nchemba hawakuamini uwepo wa corona wala athari zake .