Uchumi wa Tanzania Waporomoka kutoka 6.9% hadi 4.7% kutokana na Corona

Uchumi wa Tanzania Waporomoka kutoka 6.9% hadi 4.7% kutokana na Corona

Hayo yamefichuka leo baada ya hotuba ya Mh Rais Samia Suluhu alipokuwa anawahutubia Wafanyakazi wa Tanzania kwenye kilele cha siku ya wafanyakazi Duniani

Ameitaja Corona kama sababu kubwa ya kuanguka kwa uchumi wa Nchi yetu , ambapo amewaomba wafanyakazi kuvumilia hadi mwakani ili kuongezwa mshahara baada ya Uchumi wa nchi kuporomoka kutoka 6.9% hadi 4.7%

Ikumbukwe kwamba kwa miaka mingi viongozi wa Tanzania wakiwemo Rais wa zamani pamoja na Mawaziri kadhaa mmojawapo akiwa Mwigulu Nchemba hawakuamini uwepo wa corona wala athari zake .
Aibu yao wenyewe. You can fool some people some time but you can't fool all the people all the time
 
Uchumi wetu umeshuka kimyakimya bila hata kuambiwia, tungeambiwa Wala tusingeomba piza Wala baga kwenye mei mosi. Lakini shujaa amejitokeza adharani kwa kutumia maneno ya kiungwana kutuambia Hali ya uchumi si nzuri kwa Sasa.

Lakini pia uchumi kushuka si shida Kama ambavyo tulizoe kuaminishwa kuwa uchumi unakua, uchumi umeshuka kwa matatizo yaliyoikumba Dunia. Kwanini tulikuwa tunadanganywa?

Kama kwa Sasa tupo 4.8% from 6.7% mana yake tulipaswa kuambiwa kwa muda mrefu ili tujiandae ila haikuwa hivyo.

Sasa nijukumu letu wananchi kuipokea taarifa hii nakujipanga upya namna yakuiishi kwenye uchumi huu mpya uliokuja ambao yamkini ndio ulioondoa fedha kwenye mzunguko nakutusababishia makasiriko ya mara kwa mara.

Huu ndio ukweli na ukweli siku zote hauhitaji kurudiwa rudiwa.....
Mbona rais kawaambia leo kwenye mei mosi unataka uambiwe na Nani?

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
 
Acha kujitoa ufaham, huu uchumi wetu kipindi cha jiwe tulikua tunapigwa changa la macho , hata leo kama angekuwepo lažima angesema uchumi unakua , huu uchumi Wa kati hauna uhalisia wowote na maisha Ya watu , Sasa kuna maana Gani Ya kujiita tajili wakati huna pesa

😂 😂 😂, yaani nawonea huruma sana!
ni hivi uchumi wa NCHI ukipanda ama ukishuka kwako hauna direct impact kwa sababu wewe kama wewe haufanyiwi comparison na sehem yoyote duniani! yaani serikali inaweza kusema uchumi umeshuka lakini bado kuna watu wakawa matajiri mbaya!

- wewe kitu kinachokusu direct kinaitwa (PPP), sasa serikali ikitoa tamko kuhusu PPP unaweza kua worried lakini sio sana, kama wewe unategemea uchumi wako in Tsh basi wewe suala la uchumi kupanda na kushuka halikuhusu, if unategemea USD kwenye mauzo au kununua ambapo kuna impact ndan ya nchi yako basi wewe kwako ni halali kusema uchumi kwako umeshuka kwa sababu your dealing with economy ambayo hauna control nayo

- wewe kama unadeal na Tsh maisha yako yote basi, uchumi kupanda na kushuka haukuhusu kwa sababu serikali inaweza kutoa amri ya kuchapisha Tsh mda wowote inaotaka na haina pungufu ya Tsh na haiwezi kua na pungufu! nadhan umeelewa sasa
 
Umeshuka vipi tena si tulikubaliana umepanda na Sasa tupo uchumi wa Kati?....I
 
MATAGA bana!🤣 Kwa hiyo uchumi ukitetereka mwananchi haumii?

we unaumia wap wakati hauna msaada wowote katika GDP? unauza nje ya nchi? hapana! una dollars umeweka nje ya nchi? Hapana! sasa wewe uchumi wa nchi haukuhusu mpaka apo
 
Umeshuka vipi tena so tulikubaliana umepanda na Sasa tupo uchumi wa Kati?

kwahio na marekani nao hawapo uchumi wa juu kwa sababu uchumi wao umesinyaa? ivi mtaacha kuiba pombe ya mbowe lini
 
Shida ya kushuka kwa uchumi inaweza kutambulika kwa uwezo wa serikali kutekeleza majukumu yake, kupitia kiasi cha bajeti ya nchi kinachopitishwa, huathiri wafanya biashara na wawekezaji ambao kimsingi ndio chanzo cha mzunguko wa pesa, kisha wananchi.
Kushuka kwa uchumi wa Tanzania ni kutokana na kunyanganya wafanya biashara pesa zao.
Wafanya bishara wamekimbia wamefunga biashara zao Tanzania.
Manji yuko wapi?
Mbowe. Nae kasema yuko Dubai, south Africa na Usa. Mna tegemea na huko mta pata kodi?
 
Umeshuka vipi tena si tulikubaliana umepanda na Sasa tupo uchumi wa Kati?....I
Kilichoshuka ni kasi ya ukuaji wa uchumi, sio lile daraja la nchi kutambulika kama ipo uchumi wa chini wa kati...

Hii si mara ya kwanza Rais SSH kutamka hivyo, ni kama mara ya tatu na amekuwa akibainisha athari hizo ni matokeo ya COVID-19 na wahanga ni takribani nchi zote...
 
Back
Top Bottom