Ni wazo zuri jaribu sana kuzingatia
i. Bidhaa zinazohitajika kwa sana mahali hapo
ii. Huyo dogo ana uzoefu wa kusimamia biashara?
iii. Je nidhamu ya fedha anayo?
iv. Biashara na ndugu siku zote asilimia za kuendelea ni ndogo sana ivyo uwe unafuatilia kwa karibu sana
v. Pia kuna bidhaa ambazo zinapigwa vita kuuzwa kwenye maduka ya vipodozi jaribu kuzingatia ilo pia
vi. Pia isajili biashara yako (Jina la biashara-BRELA)
vii. Pia mtoa huduma awe na kauli nzuri kwa wateja
viii. Pia jaribu kuwa na mpango kazi hili ukuongoze katika biashara yako
Hayo ni machache tu ya kuzingatia na mengine wadau watakuja nayo
Karibu sana