Ufugaji wa kisasa wa Nyuki: Faida, Utaalam na Masoko

Ufugaji wa kisasa wa Nyuki: Faida, Utaalam na Masoko

Hii njia inakuwa applied hata kwa nyuki wasiouma?

Nyuki wasio uma mara nyingi ni njia ya kwanza, deswarming na ya tatu, yaani mzinga wao ukikosa usalama basi wanahama. Ni ngumu sana kuhamia ktk mizinga ya kisasa. Wapo vijana wanaweza kuwahamisha toka makoloni yao ya asili mpaka kwenye mizinga ya kisasa. Uzuri wa hawa nyuki unaweza kukaa nao sebuleni na ukala na kunywa nao !!!!!!
 
Nyuki walikuwepo kabla ya alizeti kuenea nchini kwetu, na kuna sehemu alizeti hakuna na nyuki wapo na wana asali bomba. Cha msingi sana kuwe na maua umbali usio pungua 4km kutoka kwenye mzinga. Nje ya umbali huo nyuki hupotea njia ya kurudia kwao. Kumbuka pollination theory.

Hakuna kipimo rasmi, ila mzinga ukiwa juu kama mita moja na kuendelea juu ni bora zaidi, hasa kwa usalama. Kuna wadudu,wanyama wadogo, maji pia yanaweza kuozesha. Kumbuka pia nyuki hukaa mashimoni !!! Maji ni muhimu sana ili wasitumie muda mwingi kutafuta maji. Ukiwa na kisima chenye maji na kiko wazi itakuwa vizuri, sio kisima kina kina kirefu, nyuki hawezi ingia huko kuteka maji, ndio maana wanapendekeza bwawa/ponds kwa sababu maji yako at ground level.

Mavuno hutegemea chakula na majira ktk eneo husika. Kuna sehemu wanavuna mara mbili kwa mwaka, may na november kama Iringa. sehemu nyingine mara moja, na kwingine hakuna kuvuna. Factor kubwa ni uwingi wa chakula na majira ya mwaka. Kukiwa na baridi na maua hakuna nyuki nao hawawezi kuwa na asali. Kwa hiyo waweza ona kwamba jibu la swali lako haliwezi kuwa sawa kwa kila sehemu. Kama msosi ni mwingi, ndani ya miezi mitano kitu kinajibu.

Asante sana mkuu Malila.
Kuna post hapo juu nimeuliza pia kuhusu nyuki wasiouma, labda unaweza kueleza kidogo management yake.
Pia ungeongezea ni aina gani ya mimea ipandwe kuzunguka eneo husika hasa kama eneo ni zaidi ya eka 40
 
Asante sana mkuu Malila.
Kuna post hapo juu nimeuliza pia kuhusu nyuki wasiouma, labda unaweza kueleza kidogo management yake.
Pia ungeongezea ni aina gani ya mimea ipandwe kuzunguka eneo husika hasa kama eneo ni zaidi ya eka 40

tatizo ni kwamba wengi wanafuga bila kuwa na malengo ya mbali sawa na soko, sasa sijui nkupe data ukiwa ktk kundi gani. Ngoja nikupe kwa ujumla.

Kama unataka shamba lako litoe asali bora zaidi, kaa mbali na mashamba makubwa ambayo yanatumia dawa za kilimo. Ukiweza kupata eneo lenye miti ya asili zaidi ni vizuri kwa sababu miti ya asili mzunguko wa maua kwa mwaka unajulikana kwa kila sehemu, hivyo ni rahisi kujua ratiba ya uvunaji. Kuna miti inayotunza maji sana, kama mivengi, otesha sana, sababu ya kutunza eneo lako. Miti ya kizungu si mizuri sana, hasa eucalyptus na pines, pine zinaua miti mingine na eucalyptus zinakausha ardhi.

Kama unataka kuwa na apiary nzuri na salama, kuzunguka eneo hili otesha mkonge/katani. Mkonge ukishona vizuri huzuia moto, na wanyama wakubwa hawawezi kupita kuingia ktk eneo lako. Hitimisho, panda miti yote ya asili inayotoa maua mapema kwa mzunguko unaojulikana,ambayo ni rafiki wa mazingira. Weka firebreak kuzunguka eneo lako.

Kama utapanda mimea mingine, basi kilimo chako kiwe organic. Nyuki wanataka chavua basi ili wafanye vitu vyao.
 
Wapendwa Great thinkers.

Ninakiu kubwa sana ya kufanya ufugaji nyuki na ufugaji wa kuku (wa kienyeji au mchanganyiko yani chotara) . Natamani kupata mtu tutakaeshirikana nae kwa mradi huu. Mimi sina pesa ila ni eneo kubwa sana maeneo ya Kilindi ukielekea Njia ya Turiani.

Wana JF natumaini mtanishauri na kunipa wazo hatimae nitimize ndoto yangu..
 
Asigwa,

Kwa wastani, super box moja (box la mzinga wa kisasa linalovunwa) linaweza toa lita 10 - 15. Hivyo kujibu swali lako, kutegemea na hali ya hewa na super boxes zilizopo katika mzinga wako ndio zitaamua kiwango cha asali utakachovuna kwa mwaka. Kukupa mfano, shambani kwangu ambapo ni mkoa jirani na Dar, huwa tunavuna lita 30 - 60 kwa mwaka kwa mzinga mmoja.

Kuhusu swala lako la pili, huo ndio tunaita ufugaji wa kisasa. Unaweza kupanda miti kama mlonge (moringa oleifera) ambayo inakuwa haraka, inavumilia ukame na inatoa maua mengi na mara nyingi kwa mwaka. Pia kilimo cha bustani au mazao kama alizeti na mbaazi kwa mzunguko yatakusaidia sana kuwa na mavuno mara nyingi na mengi kwa mwaka.

Mkuu nina mswali mawili matatu mkuu...

Mzinga huo wa commercial unaweza kutoa lita ngapi kwa mwaka?? hasa ukizingatia kuwa uvunaji hufanyika mara mbili..

Je kama utapata eneo na ukaandaa kabisa bustani ya maua na maji ya kutosha je itaongeza uzalishaji wa asali???
 
TIQO,

Katika ufugaji nyuki wa kisasa, ukaguzi wa mizinga yako ni muhimu sana ili kujua maendeleo ya kundi na kuweza kupanga muda muafaka wa kuvuna asali yako. Kiashiria kikuu cha asali iliyo tayari kuvunwa ni utando mweupe kwenye sega lililo na asali. Kwa mazoea, wafugaji wengi huishia kuvuna sali mara moja kwa mwaka kila baada ya mavuno ya mazao ya kilimo. Hiyo pia ni sawa ingawaje inaweza kukukosesha mavuno ya asali na muda mwingine nyuki kula asali. Ushauri wangu kwako ni kuwa na ratiba nzuri ya ukaguzi wa mzinga na kupanga ratiba yako ya uvunaji kulingana na maendeleo ya mzinga, na sio lazima uvune mizinga yote kwa wakati mmoja.

Mkuu ni muda gani muafaka wa kulina asali? au miezi ipi? au kipi kiashiria sasa ni muda muafaka wa kulina asali?
 
Mzee wa Manzese,

Kuna jamaa wanaitwa THE HIVE LIMITED wamefungua ofisi yao Dar es Salaam maeneo ya Victoria (Jengo la Green Acres).

Wana vifaa vizuri sana vya ufugaji nyuki wa kisasa ikiwemo mizinga ya kisasa (langstroth hives), honey extractors, mavazi ya nyuki, smokers na vingine vingi. Pia wanatoa mafunzo ya ufugaji nyuki wa kisasa kama package ya Kit watakayokuuzia na wana soko la uhakika la asali yako yote utakayozalisha popote Tanzania.

Tembelea group website yao hapa chini:

The Hive Limited

Pia, nimeambatanisha kipeperushi chao kwa ajili ya kuona vifaa vyao na mawasiliano yao. Nafikiri nimetoa mwanga kidogo.

Shukrani na kila la kheri.


Hii biashara ni nzuri sana je wapi naweza kipata mizinga kwa bei nafuu
 

Attachments

Tafuta pesa ya kuwekeza kwenye hiyo miradi.Tafuta hati miliki ya hilo shamba lako kisha nenda benki,watakupa mkopo kwa dhamana ya shamba lako.
 
Asante sana kwa maelezo mazuri, ukisema ufugaji au shamba viwe mbali na watu unamaanisha umbali gani? Ndani ya shamba eka 10 kwa mfano katikati naweza kuweka mizinga au hapo bado watapata usumbufu?
Mzee wa Manzese,

Kuna jamaa wanaitwa THE HIVE LIMITED wamefungua ofisi yao Dar es Salaam maeneo ya Victoria (Jengo la Green Acres).

Wana vifaa vizuri sana vya ufugaji nyuki wa kisasa ikiwemo mizinga ya kisasa (langstroth hives), honey extractors, mavazi ya nyuki, smokers na vingine vingi. Pia wanatoa mafunzo ya ufugaji nyuki wa kisasa kama package ya Kit watakayokuuzia na wana soko la uhakika la asali yako yote utakayozalisha popote Tanzania.

Tembelea group website yao hapa chini:

The Hive Limited

Pia, nimeambatanisha kipeperushi chao kwa ajili ya kuona vifaa vyao na mawasiliano yao. Nafikiri nimetoa mwanga kidogo.

Shukrani na kila la kheri.
 
Hapa kipele kimepata mkunaji. Amani kwako allan
 
Last edited by a moderator:
Asante kwa ushauri Mbunda. Ninayo hati niliyopewa na kijiji je inatosha?
 
Last edited by a moderator:
Bei ikoje unauza sh.ngapi per litre mkuu unapouza jumla...
 
Mama Joe,

Katikati ya heka kumi unaweza kabisa kuweka mzinga na kufuga nyuki. Kitaalam inashauriwa mradi wa ufugaji nyuki uwe umbali wa kuanzia mita 100 na kuendelea (hii sana sana ni kwa nyuki wanaouma), nyuki wasio uma hawana shida unaweza kuwafuga hata kwenye nyumba yako unayoishi.

Asante sana kwa maelezo mazuri, ukisema ufugaji au shamba viwe mbali na watu unamaanisha umbali gani? Ndani ya shamba eka 10 kwa mfano katikati naweza kuweka mizinga au hapo bado watapata usumbufu?
 
Back
Top Bottom