Ufugaji wa kisasa wa Nyuki: Faida, Utaalam na Masoko

Ufugaji wa kisasa wa Nyuki: Faida, Utaalam na Masoko

Kuna njia mbalimbali za kuwavutia nyuki waweze kuinhabit mizinga mipya. Njia kubwa kabisa na ya kisasa ambayo mimi huwa natumia ni matumizi ya nta (wax sheets). Hapa huwa naweka wax sheets kwenye vibao vya ndani ya mizinga yangu na harufu yake huwavutia nyuki na kuwafanya waingie kwenye mzinga. Njia nyingine ambayo pia husaidia nyuki waingie kwenye mzinga ni matumizi ya majani ya mchai chai (unapaka kidogo sehemu ya mlango wa mzinga na ndani ya mzinga). Pia unaweza tumia "majani ya kufukuzia mbu" na kuyasmear ndani ya mzinga, harufu yake inavutia sana nyuki.

Kama unakuwa na mzinga mingi na ufugaji wa kisasa, ukipata makundi kwenye mzinga michache unaweza kufanya colony division na kumultiply makundi yako kwenye mizinga mingine. Mfano, kama una mizinga kumi na umepata nyuki kwenye mitano, colony division itakusaidia kupata makundi kwenye mizinga mitano liliyobaki ndani ya muda mfupi. Hii njia inahitaji utaalam kidogo ila ni rahisi na haina gharama.

alan unafanyaje ili nyuki waweze kuinhabit mzinga mpya?
 
Asante sana kwa maelezo hapa ni kujipanga tu.
Mama Joe,

Katikati ya heka kumi unaweza kabisa kuweka mzinga na kufuga nyuki. Kitaalam inashauriwa mradi wa ufugaji nyuki uwe umbali wa kuanzia mita 100 na kuendelea (hii sana sana ni kwa nyuki wanaouma), nyuki wasio uma hawana shida unaweza kuwafuga hata kwenye nyumba yako unayoishi.
 
Nyuki wasiouma unaweza ukawatega pia kama nyuki wanaouma. Mizinga inayotumika katika ufugaji wa aina hizi za nyuki ni tofauti. Kuna watu huwa wanauza kundi la nyuki wadogo na mzinga wake wa kisasa Tshs 100,000/-. Wengine huuza kundi la nyuki wadogo na mzinga wa kienyeji kati ya Tshs 60,000 - 80,000. Kama utahitaji naweza kuunganisha na baadhi ya watu wanaofanya biashara hiyo.

Asante je hao nyuki wasiouma wanapatikana wapi
 
Nyuki wasiouma unaweza ukawatega pia kama nyuki wanaouma. Mizinga inayotumika katika ufugaji wa aina hizi za nyuki ni tofauti. Kuna watu huwa wanauza kundi la nyuki wadogo na mzinga wake wa kisasa Tshs 100,000/-. Wengine huuza kundi la nyuki wadogo na mzinga wa kienyeji kati ya Tshs 60,000 - 80,000. Kama utahitaji naweza kuunganisha na baadhi ya watu wanaofanya biashara hiyo.
Asante kwa elimu unayotupa.

Kwenye mti mmoja wa mu-embe mkubwa unaweza kuweka mizinga mingapi ili kupata maximum output.
 
Wadau naomba msaada ni wapi jijini Dar-es-salaam naweza kupata ushauri kuhusu Ufugaji wa nyuki kwa kutumia njia za kisasa. nina shamba nje ya jiji ambalo nataka nifanye shughuli hiyo. Asante!

Nipigie 0784176678/0757176678/0715176678 nitakuunganisha na mtaalamu aliyenianzishia mimi huo mradi hapa Dar.In case i don't pick up- i'll return your call same day when free.
 
Mimi nimeanza mradi kama huo hapa Dar.Nipigie nitakuunganisha nitakupa maelezo mafupi na kukuunganisha na mtaalamu wa mambo hayo.0784176678/0757176678,0715176678
 
Ndugu,

Idadi ya mizinga inayoweza kukaa kwenye mti mmoja wa muembe mmoja hutegemea sana ukubwa wa mti husika. Ouput ya mazao ya nyuki haitegemei mti mmoja tu, nyuki wanauwezo wa kutembea zaidi ya kilometa tatu toka kwenye mzinga wao hivyo output ya mazao ya nyuki itategema sana plant density na bee fodder plants zilizopo kwenye eneo nyuki watakaloweza kwenda.

Swali kwako: Hiyo mzinga yako unategemea kuitundika muda wote wa ufugaji?

Kama utalenga ufugaji mkubwa, ningekushauri utundikaji wa mizinga kwenye miti ufanyike wakati wa kutega makundi tu. Na siku 45 baada ya kupata kundi la nyuki kwenye mzinga unashusha mzinga wako kwenye jukwaa. Njia hii ni nzuri na inarahisisha sana ukaguzi wa mzinga yako na itakupunguzia gharama za kuwa na watu wengi wa kupanda kwenye miti.

Tazama picha nilizoambatanisha hapa za mzinga iliyotundikwa na mfano wa mzinga iliyo kwenye jukwaa.

Asante kwa elimu unayotupa.

Kwenye mti mmoja wa mu-embe mkubwa unaweza kuweka mizinga mingapi ili kupata maximum output.
 

Attachments

  • nyuki 1.jpg
    nyuki 1.jpg
    118 KB · Views: 486
  • nyuki 2.jpg
    nyuki 2.jpg
    152.8 KB · Views: 1,166
  • nyuki 3.JPG
    nyuki 3.JPG
    1.6 MB · Views: 506
  • nyuki 4.JPG
    nyuki 4.JPG
    999 KB · Views: 480
Ninataka kujikita rasmi kwenye ujasirimali ambao hautakua na risk kubwa. Nimefikiri Ufugaji wa Nyuki unaweza kuwa na tija kwa sababu hawahitaji chanjo, maji, umeme, ni kuweka mzinga na kwenda tu kuvuna kila inapojaa.

Ni nani mwenye taarifa kuhusu mradi kama huu?

- Ni wapi hasa kunafaa kwa ufugaji? nawezafuga vizuri mikoa ya pwani?
- risk zake ni zipi?
- soko lake likoje?
Kama bado una interest nipigie 0784176678/0757176678/0715176678 nikuunganishe na aliyenianzishia mradi huo hapa Dar karibuni.Utapata maelezo ya kutosha.
 
UFUGAJI WA NYUKI
Eneo linalofaa

SIFA ZIFAAZO KWA MAENEO YA KUFUGIA NYUKI (MANZUKI)
Eneo lifaalo kwa shughuli za ufugaji nyuki ni lazima liwe na sifa zifuatazo: Eneo la shamba la nyuki ni lazima liwe ni salama kwa mizinga, mazao yake, mifugo, binadamu, na mahali ambapo maadui wa nyuki hawapo au wanaweza kudhibitiwa(Ili kuwa na ufanisi mzuri, nyumba hii inafaa kujengwa nje kidogo ya makazi ya watu, Kusiwe na mifugo karibu, Iwe sehemu ambayo watoto hawawezi kufika, Isiwe karibu na njia ambayo watu wanapita mara kwa mara.)

(iv) Kivuli cha kadri na kinga ya upepo ili kuwapunguzia nyuki kazi kubwa ya ubebaji maji kwa ajili ya kupunguza joto. Inafaa kufugia nyuki ndani ya nyumba iliyoandaliwa kwa ajili ya ufugaji wa nyuki(bee-house)

Mawasiliano ya barabara ni muhimu yawepo ili kurahisisha uhudumiaji wa makundi ya nyuki pamoja na mazao yake hadi kufikia sokoni.

Mavuno
Baada ya kujenga nyumba, kuweka mizinga na nyuki kuingia, unaweza kuvuna kwa mara ya kwanza baada ya miezi mitatu. Utaweza kupata mavuno mazuri endapo utavuna kabla nyuki na wadudu wengine hawajaanza kula asali.
Ni muhimu kuhakikisha kuwa wadudu waharibifu kama vile sisimizi, mende na wengineo wanadhibitiwa ili kutokuathiri uzalishaji wa asali. Hakikisha unavuna kitaalamu ili kuepuka upotevu wa asali. Endapo nyuki wametunzwa vizuri na kwenye mazingira mazuri, unaweza kuvuna asali mara tatu kwa mwaka. Katika mzinga mpya nyuki wana uwezo wa kutengeneza masega kwa siku tatu na kuanza uzalishaji wa asali.
Ni nini umuhimu wa asali
• Asali inatumika kama chakula
• Inatumika kama tiba ya magonjwa mbalimbali
• Hutumika kutibu majeraha
• Ni chanzo kizuri cha kipato
• Hutumika katika kutengeneza dawa za binadamu
*Asali inaweza kuhifadhiwa kwa miaka mingi sana bila kuharibika. Hii inatokana na wingi wa dawa maalum iliyo nayo inayofanya isiharibike.
MAGONJWA YANAYOTIBIWA KWA
MATUMIZZI YA ASALI.
1. Ugonjwa wa viungo/maumivu na uvimbe.
2. Kukatika kwa nywele.
3. Ukungu wa miguu.
4. Maambukizo kwenye kibofu cha mkojo.
5. Maumivu ya jino.
6. Helemu (Cholestral).
7. Ugumba
8. Mchafuko wa tumbo.
9. Ugonjwa wa moyo
10. Shinikizo la damu.
11. Kinga ya mwili.
12. Ukosefu wa nguvu za kiumbe.
13. Flu.
14. Umri wa kuishi.
15. Chunusi.
16. Kuumwa na wadudu (kwa washawasha) wenye sumu.
17. Madhara ya ngozi.
18. Kupungua kwa uzito.
19. Saratani.
20. Uchovu mwilini.
22. Harufu mwilini.
23. Kupungua kwa usikivu.

Bidhaa zinazotokana na asali
Kuna aina nyingi ya bidhaa zinatokana na asali, kwa kutengenezwa na nyuki wenyewe na nyingine zikitengenezwa na binadamu kutokana na tafiti mbalimbali. Miongoni mwa bidhaa hizo ni:
• Asali yenyewe
• Royal jelly : Hii ni aina ya maziwa yanayotengenezwa na nyuki, ambayo hutumika kama tiba.
• Gundi: Hii hutumika kutengeneza bidhaa za aina mbalimbali kulingana na mahitaji ya mtumiaji.
• Nta: hutumika kutengenezea mishu maa, kulainisha nyuzi, kutengeneza dawa ya viatu, mafuta ya kupaka, pamoja na dawa ya ngozi.






UFUGAJI WA NYUKI.

Eneo linalofaa

SIFA ZIFAAZO KWA MAENEO YA KUFUGIA NYUKI (MANZUKI)
Eneo lifaalo kwa shughuli za ufugaji nyuki ni lazima liwe na sifa zifuatazo:
<>Ø<>Ø


SHAMBA LA NYUKI.


MZINGA WA KISASA WA NYUKI
 
Muwe mnaweka apa Wazi na Wengine wanafaidi sio kunufaishana Uko Peke Yenu.
 
Ni kweli ziko asali nzito na nyepesi, amber, nyeupe na nyeusi. Uzito au rangi za asali kwa kiwango kikubwa huchangiwa na aina ya maua ambayo nyuki huchukua mchozo wa kutengenezea asali. Mfano asali ya maeneo mengi ya Tabora ni nyeusi wakati ile ya Singida maeneo ya Sanjaranda na Itigi ni amber ilhali ile ya Dodoma ni nyeupe na ina machicha kama barafu.

Aina ya nyuki wanaofungwa zaidi katika maeneo ya Kitropiki na Tanzania ikiwemo ni Apis Mellifera mbao tuliowengi tunawafahamu kama nyuki wakubwa. Hawa nyuki ni wakali na wana mwiba unaotumika kujihami. Tofauti na nyuki wadogo ambao ni wapole na asali yake inatumika zaidi kama dawa

Ufugaji wa Nyuki ni kazi ya kudumu lakini uvunaji wa mazao ya nyuki hufanyika kwa misimu. Iko mikoa nchini mwetu ambayo huwa na misimu miwili kwa mwaka; Msimu mdogo na msimu mkubwa. Maranyingi asali inayopatikana katika msimu mdogo huwa ni ya masega ambayo hayajakomaa. Ninaweza kukushauri kwenye hili pale utakapo kuwa umeisha amua wapi utaweka mizinga. La muhimu ni kujua msimu wa maua unaanza lini. Hii itakusaidia kupata nyuki-wakaaji hii itakuhakikishia masega kujenjwa katika muda mfupi.

Watanzania wengi wanapenda asali ya amber. Ili kisayansi asali ya Dark-Blue ina virutubisho vingi zaidi. Mkoa wa Kigoma unaibuka kama chanzo cha asali nzuri na bora. Ninaposema bora namaanisha ulinaji unaozingatia kanuni bora, ukamuaji unaojali usafi na upakiaji katika vifaa safi na bila kuongeza kitu chochote (adulteration)

Iko mizinga ya aina mbalimbali na hivyo bei tofauti tofauti. Kwa maelezo ya kina nitumie email ekimasha@jamiiforums.com

Aina ya mzinga inaushawishi katika ubora na kiwango cha asali inayopatikana. Majibu zaidi ya swali hili nitayaandaa au nitakupatia vitabu vyenye vipimo ambavyo vitakupanua uelewa kwenye suala hili.

Miti na maua yanayotoa mchozo ni muhimu sana. Lakini pia chanzo cha maji lazima kipatikane katika eneo la mzingo usiozidi ekari tano

Sikumbuki vizuri. Nitauliza

Soko la Jumla litakulipa lakini si vizuri sana kama kupaki kwenye chupa na kusambaza katika Min and Supermarkets. Pia unaweza kufanya direct home delivery. Soko la Jumla liko kwa wapakiaji wa Dar (Honey Packers) ambao wengine hufuata moja kwa moja kutoka huko mikoani.

Mimi ni muumini wa soko la ndani. Hii inatokana na ugumu na vikwazo vingi vilivyoko katika soko la nje na mwisho wa siku profit-margin ni ndogo sana. Soko la ndani ni kubwa mno ndo maana bado supermarkets zetu zimejazwa na asali kutoka Brazil, india na China.



Thanks Mkuu Ericus Kimasha, asante kwa maelezo yako mazuri. Unadhani ni kwanini nyuki wadogo wanatumika kama dawa na si wakubwa? au ni kwa sababu ya uhaba wa upatikanaji wa asali yake? naomba msaada Mkuu!
 
Last edited by a moderator:
Habari zenu wadau. Niliomba mtuambaye amesha wahi kufanya biashara hii ya asali ama uvunaji anisaidie kunipa ushauri na kuielekeza unafaidikaje na biashara hii
 
Wewe unataka kuanza fuga nyuki au tayari unayo mizinga?biashara ya nyuki kwa kutumia mizinga ya kisasa,inaweza kujipatia mpaka 1 million kwa mwaka kwa mzinga mmoja.nyuki ana mahitaji ya madawa wala chakula toka kwa mfugaji,soko lipo wazi ndani na nje ya Tanzania.ni PM kama utataka makundi ya nyuki(tunazalisha) au maelezo zaidi.
 
Wakuu,
Unaweza kuni PM Namba yako ya Simu ili uwe added kwenye WhatsApp Group ya wadau wanaojihusisha na wenye interest ya Ufugaji wa Nyuki na Biashara ya Asali Kiujumla..
Utapata fursa ya kipekee kujifunza mambo mbalimbali kupitia Kuuliza maswali na kupata majibu..
Ahsanteni..
 
FBY 2013 Jukwaa hili ndipo mahali sahihi pa kujifuzia, tafadhali weka nondo zako hapa tuanze tuition.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom