Ufugaji wa Kuku aina ya Kuchi na masoko yake ndani na nje ya Tanzania

Ufugaji wa Kuku aina ya Kuchi na masoko yake ndani na nje ya Tanzania

pia hawafi kwa magonjwa kama kuku wengine. dondo ,kideri wanayasikia kwa majirani
Kwahio kwanini watu wengi waziwafuge hawa na kuwauza kama kuku wa kienyeji kwa bei ya soko la kienyeji au whats the catch..., (hawafi sana, magonjwa kwao ni ya kusikia...), naona positives tu hapo na ukiweka bei ya elfu 80 kwanini watu wasifuge wawauze hata kwa 20 ?
 
Hawa kuku wanoko Sana. Siku moja Nilikuwa naongea na simu na bosi wangu nikimweleza Kuwa siwezi kwenda kazini kwasababu tumbo limenichafuka, basi pembeni alikuwepo kuku wa Kuchi kwa sauti ya juu akasema Kama tumbo limekuchafuka meza tambara LA deki

Hahaj sio alisema UONGOOOO……!
 
Anayemhıtaji kumla hawezi kutoa elfu 80.Anayemhitaji kufuga anaweza, wale kuku ni wazıto na wanatumika na wacheza kamali kugombanishwa.Wana uwezo mkubwa wa kupgana na ukiwakuta wanapigana ni burudani.
Kwahio wanaowanunua ni kwa ajili ya mbegu na gambling (kuwapiganisha), kwahio kama mimi ninao wengi kuwauzia watu wa kupika supu sina jinsi bali kuwauza tu kama kuku wa kawaida ?

Yaani demand sio kubwa kihivyo au nimekosea
 
Mimi mbona simjui kuku wa kuchi! Mimi nilifikiri kuchi ni jogoo lolote. Mwenyewe picha ya huyo kuku atuwekee hapa.
 
Mimi mbona simjui kuku wa kuchi! Mimi nilifikiri kuchi ni jogoo lolote. Mwenyewe picha ya huyo kuku atuwekee hapa.
th


https://www.youtube.com/watch?v=T4Wext_UZZo
 
Ila nadhani hio picha hapo juu nimeitoa online nadhani imepigwa kwa karibu sana hence misleading sababu hapo anaonekana mkubwa sana (ingawa ni mkubwa ila sidhani kama ni mkubwa kihivyo)
 
Wadau naomba kuuliza bei halisi ya huyu kuku, sababu nimeona link ya 2013 huko Kenya anauzwa 2000kshs, (zaidi ya elfu 80 za kitanzania) pia nimeshakutana na watu humu wana-qoute zaidi ya laki kadhaa kwa kuku mmoja.. !!!

Sasa najiuliza kwanini huyu kuku ana bei kubwa hivi ?

  • Je ni mtamu kuliko wengine ?
  • Je ni sababu ya uadimu wake na kama ni adimu kwanini watu wengi wasijitahidi kumzalisha kama return ya investment ni kubwa kiasi hicho ?
  • Je ni kweli nikiwa nao naweza kupata mteja kwa kutoa elfu 80 au zaidi kwa kuku mmoja ?, Na huyo mteja anamfanyia nini ? ni wa mbegu, uganga au kumla mchuzi ?

Maswali mengi najiuliza bila majibu..., sababu kama kweli wateja wapo na bei ndio hio inayotajwa..., maybe am in the wrong business, niambieni na mimi niweze kufaga hawa viumbe. Ingawa my business sixth sense bado inakataa this is too good to be true.
Shilingi yetu imeporomoka, lakini haijafikia kiwango hicho. Umedanganya.
 
Shilingi yetu imeporomoka, lakini haijafikia kiwango hicho. Umedanganya.

Sorry hio ilikuwa 2013 ambapo kwa pesa ya bongo ilikuwa around 40 thousands lakini kwa sasa watu huku bongo wanawauza kuanzia kwenye elfu 80 mpaka laki na zaidi
 
Kuchi ana umri 14month

Huyu nae kwenye picha ni kuchi? Au si wote wenye shingo ndefu? Na anakomaa kwa kawaida akiwa na miezi mingapi? Sababu kusubiri mwaka na ushee ili aanze kuproduce au kumweka kwenye kikaango itakuwa ni disadvantage
 
Huyu nae kwenye picha ni kuchi? Au si wote wenye shingo ndefu? Na anakomaa kwa kawaida akiwa na miezi mingapi? Sababu kusubiri mwaka na ushee ili aanze kuproduce au kumweka kwenye kikaango itakuwa ni disadvantage

huyo ndio ni kuchi,kuchi wko wa aina tofauti.huyo sasa ndo wanaotumika kwa kupigana kule sehem za india au pakistan, kwa kizungu wanaitwa Aseel.pia kuna wale midomo mifupi ambao watu wanapenda kuwaita parrot beak aseel.tafuta kwenye google Parrot beak aseel utaona picha zao.
 
huyo ndio ni kuchi,kuchi wko wa aina tofauti.huyo sasa ndo wanaotumika kwa kupigana kule sehem za india au pakistan, kwa kizungu wanaitwa Aseel.pia kuna wale midomo mifupi ambao watu wanapenda kuwaita parrot beak aseel.tafuta kwenye google Parrot beak aseel utaona picha zao.
Okay kwahio tuseme hawa soko lao kubwa ni kwenye kuwapiganisha ? Hivi huwa wanakuwa mpaka kilo ngapi yaani tofauti ya hawa na kuku wa kawaida inaweza kuwa kilo ngapi
 
kuku wa Malawi ni hybrid nadhani ambao ni weusi na upanga mwekundu uliokolea.
kuch wazuri ni wa kienyeji hawajachanganyika na ni wakubwa sana wanataga yai moja kawaida.
na hao wa Malawi wanataga na kuatamia kawaida japo si wazuri sana kama kuku wa kienyeji pure.
Malawi na kuch wanatofautiana kwa kiwango kikubwa kuanzia umbo na tabia zao.

Nauza vifaranga vya kuchi pure vina miezi mitatu.nauza wawili kwa 40,000 .Ni pure kuchi.nipo moshi.kwa anaehitaji anipigie 0715 390738.
 
Back
Top Bottom