Ufugaji wa Kuku wa Kisasa: Fahamu Mbinu, Faida, Changamoto na Masoko

Ufugaji wa Kuku wa Kisasa: Fahamu Mbinu, Faida, Changamoto na Masoko

emma250,
Asante kwa maswali yako mazuri. Kwakifupi ni kwamba, moshi unawaathiri vifaranga kama ambayo huwaathiri binaadamu
kitu cha msingi unapaswa kuhakikisha kuwa yale majiko yanakolezwa nje ya chumba cha vifaranga yakishakolea vyema yanayaingizwa ndani hivyo yanakuwa hayana tena moshi lakini pia ni muhimu kuhakikisha kuwa unapata mkaa mzuri maana mikaa mingine inakuwa na matatizo ya kutoa moshi.

Majiko 4 yanatosha kwa kuku hao 1000. Vilevile unapaswa uwe na vyumba viwili tofauti vya kuwalelea vifaranga hao kila chaumba kibebe vifaranga 500 na baada ya mwezi mmoja wawekwe kwenye vyumba 4 tofauti kila chumba kikibeba kuku 250. Nyumba itakayotosha kuku hao 1000 inatakiwa iwe yenye ukubwa wa 15m kwa 8m, kisha utaigawa katika vyumba vinne vilivyo sawa.

Ukifuga kwa kufuata kanuni na misingi ya ufugaji bora vifo vinakuwa ni 5%. Ingawa bado inalipa kibiashara hata vifo vikifika 10% ya kuku wote walioagizwa. Vifo zaidi ya asilimia kumi ni ishara ya kukosa umakini katika uleaji na utunzaji wa vifaranga na hivyo kupunguza faida. Kama utafuata ushauri kutoka kwa mtaam aliyesomea taaluma ya mifugo bila shaka utafanya vizuri katika ufugaji wako wa kuku na hata faida ufugaji itaonekana.

Katika uleaji wa vifaranga huwa tunatengeneza chumba maalum kwa ajili ya kulelea vifaranga hasa katika zile wiki tatu za mwanzo ambapo vifaranga wanahitaji joto kwa kiasi kikubwa ili kuwakinga dhidi ya baridi. Chumba hicho huitwa brooder. Brooder inaweza kutengenezwa kwa sealing board inayojikunja au chumba cha kawaida kinaweza kutumika kama brooder isipokuwa zile kona za chumba zitapaswa kuondolewe kwa kutengeneza vibao maalum ambavyo vitaondoa kona, ukiwasiliana na mafundi selemala watakusaidia.

Bei ya trai moja ya mayai kwa sasa ni tsh 7500 kwa jumla na tsh 9000 kwa bei ya rejareja, itategemea pia na mahali ulipo.

Asante.

Aman
Asante kwa kunipa mwanga,

Nimeambiwa taa ya chemli unaweza ikatumika kwenye brooder kama source ya joto, je ni Kweli?

Kama nikweli unashauri taa ngapi kwa vifaranga 1000?

Unaweza ukarecommend suppliers wazuri wa vifaranga wa mayai hapa dar?
 
Aman
Asante kwa kunipa mwanga,

Nimeambiwa taa ya chemli unaweza ikatumika kwenye brooder kama source ya joto, je ni Kweli?

Kama nikweli unashauri taa ngapi kwa vifaranga 1000?

Unaweza ukarecommend suppliers wazuri wa vifaranga wa mayai hapa dar?

emma250,
Supplier wazuri wa vifaranga wa mayai kwa Dsm na Kibaha ni mkuza, interchicks, na taasisi ya elimu kibaha. Na kwa kuku wa nyama Broiler Amadori Euro poultry Ltd.

Kuhusu kutumia taa za kandili au chemli kama source ya joto kwa vifaranga ingawa huwa inapendekezwa lakini sikushauri kwani kwani utafiti umeonyesha kuwa ufanisi wake katika kuleta joto ni mdogo sana hivyo hatari ya vifaranga kufa ni mkubwa sana. Labda kama zitatumika aina flani hivi za taa zinaitwa karabai sema tu huleta hasara kwenye upande wa matumizi ya mafuta.
 
emma250,
Supplier wazuri wa vifaranga wa mayai kwa Dsm na Kibaha ni mkuza, interchicks, na taasisi ya elimu kibaha. Na kwa kuku wa nyama Broiler Amadori Euro poultry Ltd.

Kuhusu kutumia taa za kandili au chemli kama source ya joto kwa vifaranga ingawa huwa inapendekezwa lakini sikushauri kwani kwani utafiti umeonyesha kuwa ufanisi wake katika kuleta joto ni mdogo sana hivyo hatari ya vifaranga kufa ni mkubwa sana. Labda kama zitatumika aina flani hivi za taa zinaitwa karabai sema tu huleta hasara kwenye upande wa matumizi ya mafuta.

Aman

Asante kwa majibu yako,

Hv kwa sehemu kama dar yenye joto kuna haja ya kuwapa vifaranga source nyingine ya joto kwa mchana?
 
Aman

Asante kwa majibu yako,

Hv kwa sehemu kama dar yenye joto kuna haja ya kuwapa vifaranga source nyingine ya joto kwa mchana?

emma250,
Kama joto litakuwa jingi hakutakuwa na haja ya kuwapa joto la ziada lakini ni muhimu kutazama mwenendo wa vifaranga hao, kama joto litakuwa la kutosha vifaranga watatawanyika chumba kizima bila kubanana, ukiona hali hii hunahaja ya kuwawekea joto la ziada lakini wakati wa asubuhi na usiku ni muhimu sana kuwawekea joto kutokana na hali ya baridi inayokuwepo wakati huo.
 
emma250,
Kama joto litakuwa jingi hakutakuwa na haja ya kuwapa joto la ziada lakini ni muhimu kutazama mwenendo wa vifaranga hao, kama joto litakuwa la kutosha vifaranga watatawanyika chumba kizima bila kubanana, ukiona hali hii hunahaja ya kuwawekea joto la ziada lakini wakati wa asubuhi na usiku ni muhimu sana kuwawekea joto kutokana na hali ya baridi inayokuwepo wakati huo.

Shukran mkuu, nntakutafuta nikuwa na maswali mengine
 
Naombeni msaada wa dawa bora ya mafua ya kuku na macho kuvimba sana na kutoa vitu vyeupe...hii ni kwa kuku na bata mzinga.Asanteni
 
Englishlady,
Ok nimekupata bibie, kwa chakula hupaswi kupima kwa gram moja moja isipokuwa inatakiwa kujua kwamba kuku mmoja anakula gram ngapi kwa siku kisha unazidisha mara idadi ya kuku utapata jumla ya gram ambazo kuku atakula kwa siku then utabadilisha gram kwenda kwenye kilogram.

Kwa mfano kifaranga mmoja wiki ya kwanza kwa siku atahitaji grm 12.Ukiwa na vifaranga 100 ile wiki ya kwanza kila siku watahitaji gram 1200 sawa na kilo 1.2. Kilo 1.2 ni rahisi kuipima. Sijui kama nitakuwa nimekuridhisha.


kuku wangu wanaanamia, wemanaharisha brown na nyekundu, nimeenda dukani nimeambiwa ni coccidiosis nikapewa ampolium, kuku wamekufa wengi sana wamekaribia 70 sasa, nimechanganuikiwa. dk mwingine akanitajia dawa nyingine, nimenunua kn kila asubuhi kwa siku tatu naokota kuku 24, 22. msaada tafadhali kuku ndio kwanza wana wiki saba.
 
Aman Ng'oma naomba mawasiliano yako simu, kuku wangu wamekufa karibu 100, kwa ugonjwa wa mapafu na ndui licha ya kua niliwachanja nashndwa kujua nlikosea wapi
 
kuku wangu wanaanamia, wemanaharisha brown na nyekundu, nimeenda dukani nimeambiwa ni coccidiosis nikapewa ampolium, kuku wamekufa wengi sana wamekaribia 70 sasa, nimechanganuikiwa. dk mwingine akanitajia dawa nyingine, nimenunua kn kila asubuhi kwa siku tatu naokota kuku 24, 22. msaada tafadhali kuku ndio kwanza wana wiki saba.
Pole sana Englishlady,
Ndio maana nilisema toka awali kuwa kupata kile kitabu changu ni muhimu sana tatizo hizi lisinge tokea. Prevention ingefanyika toka mapema na kwamba kuku wangeendelea tu vizuri. Sasa ili kukusaidia vizuri ulitakiwa kutoa dalili zingine ambazo kuku wako wanaonyesha.Mfano kuku wagonjwa wanaonekanaje,mabawa yao yanakuwaje,wao wenyewe kwa ujumla wakoje?Pia ungeshituka mapema ungenipigia hata kabla hujakimbilia sehemu nyingine ungeokoa kuku wako.
Hebu sasa nipe haraka haraka hizo dalili zingine ili nikuambie tatizo na kisha nikupe ufumbuzi wa uhakika.
 
Aman Ng'oma naomba mawasiliano yako simu, kuku wangu wamekufa karibu 100, kwa ugonjwa wa mapafu na ndui licha ya kua niliwachanja nashndwa kujua nlikosea wapi

msungupendigwite;
Ugonjwa wa mapafu ya kuku!!,labda ni Infectious Coryza, hebu toa dalili zote ambazo wanaonyesha hao kuku wako ili nikuambie ni ugonjwa gani
 
Mkuu hongera sana kwa kazi ya kutuelimisha, nimekuwa nikikufuatilia toka mwanzo mpaka sasa. naomba msahada wako katika haya
1.Kitabu chako kwa Dodoma kinaweza patikana maduka yapi?
2. Naomba fomla ya kutengeneza chakula cha broiler kwani naexpirience ghalama ktk kununua chakula.
3.ningependa kujua kama kunashida yoyote kufuga broiler, layers na chotara katika eneo moja ila kwa mabanda tofauti?
natanguliza shukranI
 
Habari ya asubuhi Jamani.Samahani Nina Kuku wa kienyeji wakubwa baadhi wanataga Na wengine wameatamia. Sasa Leo ninaona katika kinyesi chao kuna mchanganyiko wa rangi nyeupe kama mtindi. Je, hili ni tatizo gani Na tiba yake ni nini?
 
Mimi nina banda la kuchukua kuku mianne(400) ningependa kupata maelekezo.nahitaji kufuga kuku wa nyama
ningependa ukanitumia contact zako tuwasiliane
 
Pia ninauza majogoo kwa bei nafuu 3500 tsh karibu,
Mimi nina banda la kuchukua kuku mianne(400) ningependa kupata maelekezo.nahitaji kufuga kuku wa nyama
ningependa ukanitumia contact zako tuwasiliane
 
Kwa wafuatiliaji wote wa uzi huu,
Wakati mwingine nakabiliwa na majukumu kidogo hivyo nakosa nafasi ya kuingia humu ndani,kwa wote wenye dharura tuwasiliane kwa mawasiliano yangu hapo chini ili kupata msaada zaidi
Aman Ng'oma,


A Livestock Based Project Consultant,

P.O BOX 1989,
Dodoma,
Tanzania.
Tel +255(0)767989713, +255(0)715989713,
+255(0)786989713
E-mail: amanngoma@gmail.com
 
Kwa wale wanaohitaji vifaranga vya kuku wa nyama (Broilers) inbox me
 
Back
Top Bottom