Ufugaji wa Nguruwe: Fahamu faida, hasara na mbinu bora za ufugaji

Ufugaji wa Nguruwe: Fahamu faida, hasara na mbinu bora za ufugaji

huu uzi sijui unakaaje kwenye jukwaa la matangazo, Moderator tusaidie kuipeleka jukwaa la uchumi humu itapotea bure!
 
Last edited by a moderator:
Hii biashara inalipa sana. Mkoa wa Iringa kuna sehemu wanaita CCM. Hapo wanalika sana. Kilo moja tsh 7,000.
 
Mkuu siyo kila kitu mpaka waje watu washuhidie wee ndo uelewe. Kama unataka ingia nawe acha uvivu huo. Mbona mnachosha?

nataka nianze kazi ndani ya mwezi ujayo maana kuna ka shamba kibaha hapo ka eka 2 nataka niangalie soko kwa dar ndo nianze nao kumi na kadhaa maana faida yak e kama sio kweli vile
 
Nguruwe watoto 20 @ 20000 = 400000
Banda la mabanzi=1,000,000
Chakula = 1,000,000
Dawa= 200000
After 1yr: Nguruwe 20 watazaa vitoto kama 160,
utachakuwa vitoto jike 100,
mama zao wote watauzwa, huku shambani kwetu nguruwe
mkubwa ni Tsh 200,000 tu, utapata 4,000,000
After 2yrs: Nguruwe 100 wanaweza kuzaa 700
Kati ya 700 chagua majike 500,(unaweza kuuza watoto dume ukanunua jike)
Year 3: Nguruwe 500 watazaa watoto 3500, chagua watoto 1500 tu
Kutoka hapo unamentein Number 1500, kila mwaka unaweza kuuza
watoto zaidi ya 3000, na nguruwe wakubwa 1500
1500*200000= Tsh 300,000,000/= kwa mwaka
Nusu ya hiyo pesa ni gharama zingine, unabaki na 150mil.
Welcome to the club

Kabla hujajitumbukiza kaone mifano, au nenda sokoine ukaonane na wataalamu.
Kila mwaka nalima Mahindi, alizeti, maboga ekari 30 kwa ajili ya chakula cha
Nguruwe tu.


nakupenda saana mpwa,
mpwa nashukuru sana kwa wazo zuri sana la biashara! wacha nikuze mtaji kwanza kwa kuanza na kilimo hapo itakapotimia mwaka 2015...

Much love to you mpwa!
 
Kudadeki huu uzi unaishi kama nyimbo za Tx Moshi William toka 2009? Nnataka kuanza huu mradi na jamaa yangu akaniambia tukawaone maafisa mifugo mi nkamwambia we nenda huko mi naamini kuna mambo ya msingi ntayapata jf ila ushauri wako wa kuwaona wataalamu wa SUA pia ntauzingatia.
 
Natambua wapo watu wengi ambao imani zao zinaruhusu wanatamani kufanya mradi wa ufugaji nguruwe wenye faida.Labda wengine wamejaribu bila mafanikio.Kwa uzoefu wangu ( refer thread yangu Mbegu nzuri ya nguruwe sasa inapatikana | JamiiForums | The Home of Great Thinkers ndivyo waweza fanya kupata mfanikio.
1. Kwanza tambua hii ni agri-business,basi kama business nyingine inahitaji usimamizi wa kutosha. Watu hudhani ukianzisha mradi na kuweka kijana wa kuwalisha basi unangojea faida tu. Ni vema ukaelewa mahitaji ya hao wanyama (chakula,usafi,malazi,tiba na jinsi ya kuzuia magonjwa) na wewe sasa ndio uwe mwalimu wa herdman wako
2.Tambua faida inatokana na aina bora ya mbegu na malezi. Nia ni kuwalea wanyama wakue kufikia uzito wa soko kwa muda mfupi.Kwa kawaida nguruwe huuzwa kwa nyama akiwa na uzito kuanzia 50kg. Shambani kwangu huuzwa kuanzia miezi 5.
3. Waangalizi(herdmen) ni watu muhimu sana kwako.Ni lazima wafundishwe vizuri na maslahi yao yaangaliwe kwa makini
4. Nguruwe akiugua atibiwe mara moja. Nguruwe ni mnyama ambae haugui kirahisi akilelewa vema unless kama kuna outbreak ya ugonjwa(kama swine fever). Mara mojamoja huugua inabidi herdman awe na uwezo wa kugundua mapema na mnyama apewe tiba mara moja. Ukiwalea vizuri muda mwingi wanahitaji chanjo tu za minyoo na ukurutu
5. Nguruwe walishwe ration(balanced feed) sio pumba tu au masalia ya jikoni. Tambua mahitaji ya chakula ya nguruwe(protein,wanga,mafuta,madini,vitamin) na hakikisha mchanganyiko unaofaa kwa umri husika wa nguruwe.Shambani kwangu chakula kikuu ni mahindi/mtama,pumba za mahindi na mpunga,mashudu ya alizeti, ambayo tunalima hapo shamba.Pia huchanganya madini (nguruwe mix) na mifupa/chokaa
6. Tambua gharama kubwa ya ufugaji ipo kwenye chakula (atleast 70%). Kwa wastani nguruwe mkubwa anahitaji 2kg/siku. Kwa hiyo kumlea nguruwe mmoja hadi miezi 6 anahitaji 240kg(miezi 2 ya kwanza huwa ananyonya)
(a) ukininunua chakula ambacho tayari kimechanganywa gharama ni kama tshs 600/kg
(b) ukinunua vyakula na kuchanya mwenyewe gharama ni kama tshs.400/kg
(c) Ukilima vyakula na kuchanganya mwenyewe gharama ni kama tshs 150-250/kg
Hizo ni gharama za wastani kwa morogoro na Dar es salaam.Utaona kama waweza kulima mazao kwa ajili ya mifugo wako gharama inapungua sana. Nguruwe hula pia vyakula vingine kama mihogo,majani,viazi vitamu,maboga etc. Angalia vyakual rahisi kwa mazingira unayofuga
Faida yako ipo kwenye kuuza nguruwe wa nyama. Wanunuzi wa mbegu sio wengi na sio consistent. Kwa hiyo itakuchukua a minimum ya miezi 6 kuanza kupata faida kutoka kwenye mradi wako.Huu ndio ukweli. Lengo ni kuuza idadi fulani ya nguruwe Kila mwezi. Kwa mfano ingalau nguruwe 20 kila mwezi.Unadhani unahitaji nguruwe wangapi kwa wakati mmoja kufanikisha hilo???
8. Soko la nguruwe ni kubwa na linazidi kukua. Walaji wengi wapo Dar es salaam. Waweza kuuza live hapo shambani au ukapeleka mwenyewe machinjioni inategemeana na soko lipo mbali kiasi gani. Nguruwe wa miezi 6 anaweza kukuingizia tshs.200,000-300,000 kutegemea na namna ulivyouza na uzito 9.Unaanzaje kufuga kibiashara? Mfano.
(a) Faida ndani ya miezi 6,na kuuza nguruwe 20 kila mwezi.
Nunua nguruwe jike wenye mimba uzao wa 2 ; wa2 mimba miezi 3;wa2 miezi 2 na wa2 mimba mwezi1,wa2 ambao ndiowamepandwa na wa2 wenye umri wa miezi 6. Nunua kwa mfugaji mwenye mbegu inayoanza kuzaa mapema. Ukinunua wa uzao wa kwanza namba inakuwa nguruwe 3 badala ya 2 kwa sababu uzao wa kwanza watoto ni wachache,6-9.Pia unahitaji dume mzuri mwenye umri wa miezi 8 au zaidi.Kwa namna hii kila mwezi nguruwe wa2(au 3) watazaa watoto sio chini ya 20. Utaanza kuuza mbegu ndani ya miezi 2.Na baada ya miezi 6 utauza nguruwe sio chini ya 20 kila mwezi kwa nyama
Nguruwe jike mwenye mimba waweza kumpata kwatshs350,000-400,000
Mauzo 4-6m kila mwezi. Neti profit itategemeana na gharamaza chakula kama nilivyo ainisha awali.
Shambani kwangu tunawaachisha watoto kunyonya wakiwa na week6 na jike hupata joto na kupandwa tena ndani ya siku 3-7. Hivyo nguruwe wetuhuzaa mara 2.5 kwa mwaka. Watoto huwauza wakiwa na miezi 2 kwa 45,000-60,000 kutegemeana uzito
(b) Kama utaanza kufuga nguruwe watoto wenye miezi 2?!
Ina maana utaanza kuuza nguruwe wa nyama baada ya miezi isiyopungua 14. Pia utahitaji kuwafanya nguruwe wako wapate mimba kwa groups ambayo inahitaji uzoefu wako na herdman. Utahitaji pia dume lenye umri wa miezi12 au zaidi. Pia kwa mtu anaeanza ufugaji inasumbua kidogo. Lakini ni nafuu kidogo interms of upfront capital though gharama za ufugaji zinaWEZA kuwa kubwa. Utahitaji kuanza nao wengi pia ili kupata faida na utahitaji kufuga muda mrefu kama nilivyoeleza hapo juu.
Kama una mpango wa muda mrefu na mtaji wa kugharamia chakula na mengineyo kwa muda mrefu,hii ni namna nzuri pia.
Kwa mtu anaetaka kufuga kibiashara,mie humshauri option 8(a) hapo juu
Shambani kwangu Morogoro kwa sasa nguruwe wa 2 au 3 wanazaa kwa mwezi. Kuanzia November nguruwe 5-7watazaa kwa mwezi.
Hope hii itawasaidia watakaopenda kujaribu hii project. Ni muhimu kutembelea mfugaji halisi kupata uzoefu kabla ya kuanza ufugaji.
NYONGEZA1
Mojawapo ya vitu watu wanakosea wakati wa kuanza ufugaji wa nguruwe ni uchaguzi wa mbegu bora.Wengi anapotembelea mtu anaefuga na kukuta nguruwe wakubwa wanapata hamasa bila kuuliza maswali muhimu yatakayomsaidia kujua kama mbegu anayoona inafaa.
Mtu anaefuga kibiashara huwa na:majike na dume(au madume kutegemea na idadi ya majike).Lengo ni kuzalisha nguruwe wa kutosha watakaokua haraka na pia kuwa na nyama nzuri(isiyo na mafuta mengi) wakati wa kuuza akiwa na miezi 6 au 7.Ni vema basi ukjua sifa za jike na Dume!
Dume:iwe mbegu inayokua haraka na kuzalisha nyama nzuri.unapochagua asiwe na ulemavu wowote na awe na matiti 12 au zaidi. Large white,duroc,hampshire na crosses zake zinafaa.Ukiweza kupata first cross za duroc au hampshire ni wazuri zaidi kuwatumia kama terminal sire(dume wa kuzalishia nguruwe wako wa mauzo)
Jike:awe kutoka mbegu zinazozaa watoto wengi na pia uwezo mzuri wa kulea watoto.Awe na matiti 12 au zaidi.ni vema kutoka kwenye crosses za largewhite na landrace.Pia saddle back na crosses zake.

Kwa leo ni hayo.nitaendelea ku-update hii thread ninapokuwa na muda kwa topic mbalimbali.Ninatambua kuna breeds nzuri zaidi kama camborough,etc.nilizoelezea hapo ni breeds unazoweza kupata kirahisi humu nchini.

mawasiliano:0789412904,simu isipopokelewa andika msg ,utapigiwa

Pia angalia Mbegu nzuri ya nguruwe sasa inapatikana | JamiiForums | The Home of Great Thinkers

HABARI ZA 2016.
NNA WATAKIA UFUGAJI WENYE MAFANIKIO WALE WOTE WALIONUFAIKA KWA NAMNA MOJA AU NYINGINE NA UZI HUU!2016 UWE MWAKA WA NEEMA KWENU!
 
Last edited:
Natambua watu wengi ambao imani zao zinaruhusu wanatamanikufanya mradi wa ufugaji nguruwe wenye faida.Labda wengine wamejaribu bilamafanikio.Kwa uzoefu wangu ( refer thread yangu:Ufugaji na kilimo unalipa sana)hivi ndivyo waweza fanya kupata mfanikio.

1. Kwanza tambua hii ni agri-business,basi kama business nyingine inahitaiiusmamizi wa kutosha. Watu hudhani ukianzisha mradi na kuweka kijana wa kuwalisha basiunangojea faida tu. Ni vema ukaelewa mahitaji ya hao wanyama vema(chakula,usafi,malazi,tiba na jinsi ya kuzuia magonjwa) na wewe sasa ndiomwalimu wa herdman wako
2.Tambua faida inatokana na aina bora ya mbegu na malezi. Nia ni kuwaleawanyama wakue kufikia uzito wa soko wa muda mfupi.Kwa kawaida nguruwe huuzwakwa nyama akiwa na uzito kuanzia 50kg. Shambani kwangu huuzwa kuanzia miezi 5.
3. Waangalizi(herdmen) n
i watu muhimu sana kwako.Ni lazima wafundishwe vizuri namaslahi yao yaangaliwe kwa makini.
4. Nguruwe akiugua atibiwe mara moja. Nguruwe ni mnyamaambae haugui kirahisi akilelewa vema unless kama kuna outbreak. Mara mojamojahuugua inabidi herdman awe na uwezo wa kugundua mapema na mnyama apewe tibamara moja. Ukiwalea vizuri muda mwingi wanahitaji chanjo tu za minyoo naukurutu
5. Nguruwe walishwe ration(balanced feed) sio pumba tu aumasalia ya jikoni. Tambua mahitaji ya chakula yanguruwe(protein,wanga,mafuta,madini,vitamin) na hakikisha mchanganyiko unaofaakwa umri wa nguruwe.Shambani kwangu chakula kikuu ni mahindi/mtama,pumba zamahindi na mpunga,mashudu ya alizeti, ambayo tunalima hapo shamba.Piahuchanganya madini (nguruwe mix) na mifupa/chokaa
6. Tambua gharama kubwa ya ufugaji ipo kwenye chakula (atleast 70%). Kwa wastani nguruwe mkubwa anahitaji 2kg/siku. Kwa hiyo kumleanguruwe mmoja hadi miezi 6 anahitaji 240kg(miezi 2 ya kwanza huwa ananyonya)
(a) ukininunuachakula ambacho tayari kimechanganywa gharama ni kama tshs 600/kg
(b) ukinunuavyakula na kuchanya mwenyewe gharama ni kama tshs.400/kg
(c) Ukilimavyakula na kuchanganya mwenyewe gharama ni kama tshs 150-250/kg
Utaona kama waweza kulima mazao kwa ajili ya mifugo wakogharama inapungua sana
7. Faida yako ipokwenye kuuza nguruwe wa nyama. Wanunuzi wa mbegu sio wengi na sio consistent. Kwa hiyo itakuchukua a minimum ya miezi 6kuanza kupata faida kutoka kwenye mradi wako.Huu ndio ukweli. Lengo ni kuuzaidadi fulani ya nguruwe Kila mwezi. Kwa mfano ingalau nguruwe 20 kila mwezi.Unadhaniunahitaji nguruwe wangapi kwa wakati mmoja kufanikisha hilo???
8. Soko la nguruwe ni kubwa na linazidi kukua. Walaji wengiwapo Dar es salaam. Waweza kuuza live hapo shambani au ukapeleka mwenyewemachinjioni inategemeana na soko lipo mbali kiasi gani. Nguruwe wa miezi 6 anawezakukuingizia tshs.200,000-300,000 kutegemea na namna ulivyouza na uzito
9.Unaanzaje kufuga kibiashara????
(a) Faida ndani ya miezi 6,na kuuza nguruwe 20kila mwezi
Nunua nguruwe jike wenye mimba uzaowa 2 ; wa2 mimba miezi 3;wa2 miezi 2 na wa2 mimba mwezi1,wa2 ambao ndiowamepandwa na wa2 wenye umri wa miezi 6. Nunua kwa mfugaji mwenye mbeguinayoanza kuzaa mapema. Ukinunua wa uzao wa kwanza namba inakuwa nguruwe 3badala ya Pia dume mzuri mwenye umri wamiezi 8au zaidi. Kwa namna hii kila mwezi nguruwe wa2(au 3) watazaa watotosio chini ya 20. Utaanza kuuza mbegu ndani ya miezi 2.Na baada ya miezi 6utauza nguruwe sio chini ya 20 kila mwezi kwa nyama!
Nguruwe jike mwenye mimba waweza kumpata kwatshs350,000-400,000
Mauzo 4-6m kila mwezi. Neti profit itategemeana na gharamaza chakula kama nilivyo ainisha awali.
Shambani kwangu tunawaachisha watoto kunyonya wakiwa na week6 na jike hupata joto na kupandwa tena ndani ya siku 3-7. Hivyo nguruwe wetuhuzaa mara 2.5 kwa mwaka.
Watoto huwauza wakiwa na miezi 2 kwa 45,000-60,000 kutegemeana uzito
(b) Kama utaanzakufuga nguruwe watoto wenye miezi 2?!
Ina maana utaanza kuuza baada ya mieziisiyopungua 10. Pia utahitaji kuwafanya nguruwe wako wapate mimba kwa groupsambayo inahitaji uzoefu wako na herdman. Utahitaji pia dume lenye umri wamiezi12 au zaidi. Pia kwa mtu anaeanza ufugaji inasumbua kidogo. Lakini ninafuu kidogo interms of upfront capital though gharama za ufugaji zinaWEZAkubwa.

Shambani kwangu kwa sasa nguruwe wa 2 au 3 wanazaa kwamwezi. Kuanzia November nguruwe 5-7watazaa kwa mwezi.
Hope hii itawasaidia watakaopenda kujaribu hii project

Mungu akubariki mkuu.
 
Ahsante sana kwa kutupa uzoefu ambao hata wanaoshinda na ma - lecturer hawapati. mkuu mm naomba nikusumbue kidogo kuhusu wastani wa gharama ya chakula kwa nguruwe mmoja toka kanazaliwa mpaka mda wa kuuza anaweza akafyonza shilingi ngapi? kama nanunua vyakula mashambani na kuchanganya mwenyewe. mana nipo mbioni kuanza haka kamradi. ukinipa wastani wa mmoja mimi nitajua kwa nguruwe wengi ni kiasi gani natanguliza shukrani mkuu
 
Back
Top Bottom